Kumbukumbu 29 – NEN & JCB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Kumbukumbu 29:1-29

Kufanya Upya Agano

129:1 Law 7:38; Kut 3:1; Kum 5:2-3Haya ndiyo maneno ya Agano Bwana aliyomwagiza Mose kufanya na Waisraeli huko Moabu, kuwa nyongeza ya Agano alilofanya nao huko Horebu.

229:2 Kut 19:4Mose akawaita Waisraeli wote akawaambia:

Macho yenu yameona yale yote Bwana aliyofanya kwa Mfalme Farao huko Misri, kwa maafisa wake wote na kwa nchi yake yote. 329:3 Kum 4:34; 7:19Kwa macho yenu wenyewe mliona yale majaribu makubwa, ishara zile za miujiza na maajabu makubwa. 429:4 Isa 6:10; 32:3; 48:8; Yer 5:21; Eze 12:2; Mt 13:15; Rum 11:8; Efe 4:18; Mdo 28:26-27; Za 13:3; 19:8; Yn 8:43; Efe 1:18; 2The 2:11Lakini mpaka leo Bwana hajawapa akili ya kuelewa au macho yanayoona au masikio yanayosikia. 529:5 Kum 8:2-4Kwa muda wa miaka arobaini niliyowaongoza jangwani, nguo zenu hazikuchakaa, wala viatu miguuni mwenu. 629:6 Law 10:9; Kum 8:4; Kut 16:12; Neh 9:15; Za 78:24Hamkula mkate na hamkunywa divai wala kileo chochote. Nilifanya hivi ili mpate kujua kuwa mimi ndimi Bwana Mungu wenu.

729:7 Hes 21:25-26; 21:21-24, 33-35; Kum 2:26–3:11Wakati mlipofika mahali hapa, Sihoni mfalme wa Heshboni na Ogu mfalme wa Bashani walikuja kupigana dhidi yetu, lakini tuliwashinda. 829:8 Za 78:55; 135:12; 136:22; Hes 32:33; Kum 3:12-13Tuliichukua nchi yao na kuwapa Wareubeni, Wagadi na nusu ya kabila la Manase kama urithi wao.

929:9 Kum 4:6; Yos 1:7; Kut 19:5; Za 25:10; 103:18; 2Nya 31:21; 1Fal 2:3; Yos 1:8Fuateni kwa bidii masharti ya Agano hili, ili kwamba mweze kustawi katika kila kitu mnachofanya. 10Ninyi nyote leo mnasimama mbele za Bwana Mungu wenu; mkiwa viongozi na wakuu wenu, wazee na maafisa wenu, na wanaume wengine wote wa Israeli, 1129:11 Yos 9:21, 23, 27; 1Nya 20:3pamoja na watoto wenu, wake zenu na pia wageni waishio katika kambi zenu wanaowapasulia kuni na kuwachotea maji. 12Mnasimama hapa ili kufanya Agano na Bwana Mungu wenu, Agano ambalo Mungu analifanya nanyi siku hii ya leo na kulitia muhuri kwa kiapo, 1329:13 Mwa 6:18; Kut 6:7; 19:6; Mwa 17:7kuwathibitisha ninyi siku hii ya leo kama taifa lake, ili aweze kuwa Mungu wenu kama alivyowaahidi na kama alivyowaapia baba zenu Abrahamu, Isaki na Yakobo. 1429:14 Kut 19:5; Isa 59:21; Yer 31:31; 32:40; 50:5; Eze 16:62; 37:26; Ebr 8:7-8Ninafanya Agano hili pamoja na kiapo chake, sio na ninyi tu 1529:15 Mwa 6:18; Mdo 2:39mnaosimama hapa na sisi leo mbele za Bwana Mungu wetu, bali pia pamoja na wale ambao hawapo hapa leo.

16Ninyi wenyewe mnajua jinsi tulivyoishi nchini Misri na jinsi tulivyopita katikati ya nchi mpaka tukafika hapa. 1729:17 Kut 20:23; Kum 4:28; 28:36Mliona miongoni mwao vinyago vyao vya kuchukiza na sanamu za miti na mawe, za fedha na dhahabu. 1829:18 Kum 13:6; 11:16; Ebr 12:15Hakikisheni kwamba hakuna mwanaume au mwanamke, ukoo au kabila miongoni mwenu leo ambalo moyo wake utamwacha Bwana Mungu wetu, kwenda kuabudu miungu ya mataifa hayo. Hakikisheni hakuna mzizi miongoni mwenu unaotoa sumu chungu ya namna hii.

1929:19 Za 72:17; Isa 65:16; Za 36:2; 14:1; Hes 15:39; Yer 7:24; Ay 15:16; 34:7; Efe 4:19Wakati mtu wa namna hii asikiapo maneno ya kiapo hiki, hujibariki mwenyewe na kisha hufikiri, “Nitakuwa salama, hata kama nikiendelea kuifuata njia yangu mwenyewe.” Hili litaleta maafa juu ya nchi iliyonyeshewa sawasawa na nchi kame. 2029:20 Kut 23:21; 34:4; Eze 23:25; Sef 1:18; Za 74:1; 79:5; 80:4; Eze 36:5; 2Fal 13:23; 14:27; Ufu 3:5; Kut 32:33Bwana kamwe hatakuwa radhi kumsamehe, ghadhabu na wivu wa Mungu vitawaka dhidi ya mtu huyo. Laana zote zilizoandikwa katika kitabu hiki zitamwangukia na Bwana atafuta jina lake chini ya mbingu. 2129:21 Kum 28:61; 32:23; Eze 7:26; Mt 24:51Bwana atamtwaa peke yake kutoka makabila ya Israeli kwa maangamizo, kulingana na laana zote za Agano zilizoandikwa kwenye Kitabu hiki cha Sheria.

2229:22 Yer 19:8; 49:17; 50:13Watoto wako watakaofuata baada yako katika vizazi vya baadaye na wageni ambao watakuja kutoka nchi za mbali, wataona maafa, yaliyoipata nchi na magonjwa ambayo Bwana aliyaleta juu yake. 2329:23 Isa 1:7; 6:11; 9:18; 64:10; Yer 12:11; 44:2; 6; Mik 5:11; Mwa 13:10; Eze 47:11; Mwa 19:24-25; Sef 2:9; Mt 10:15; Rum 9:29; Mwa 14:8; Yer 17:6Nchi yote itakuwa jaa linaloungua la chumvi na kiberiti: hakutakuwa kilichopandwa, hakutakuwa kinachochipua, wala hakutakuwa mimea inayoota juu yake. Itakuwa kama maangamizo ya Sodoma na Gomora, Adma na Seboimu, ambazo Bwana aliangamiza kwa hasira kali. 2429:24 1Fal 9:6; 2Nya 36:19; Yer 16:10; 22:8-9; 52:13Mataifa yote yatauliza: “Kwa nini Bwana amefanya hivi juu ya nchi hii? Kwa nini hasira hii kali ikawaka?”

2529:25 2Fal 17:23; 2Nya 36:21Na jibu litakuwa: “Ni kwa sababu watu hawa waliacha Agano la Bwana, Mungu wa baba zao, Agano alilofanya nao wakati alipowatoa katika nchi ya Misri. 26Walienda zao na kuabudu miungu mingine na kuisujudia, miungu wasioijua, miungu ambayo Mungu hakuwapa. 2729:27 Kum 28:15; Dan 9:11-14Kwa hiyo hasira ya Bwana ikawaka dhidi ya nchi hii, hivyo Mungu akaleta juu yake laana zote zilizoandikwa katika kitabu hiki. 2829:28 Za 7:11; 1Fal 14:15; 2Nya 7:20; Za 9:6; 52:5; Mit 2:22; Yer 12:14; 31:28; 42:10; Eze 19:12Katika hasira kali na katika ghadhabu kuu Bwana aliwangʼoa kutoka nchi yao na kuwasukumia katika nchi nyingine, kama ilivyo sasa.”

2929:29 Mdo 1:7; Yn 5:39; Mdo 17:11; 2Tim 3:16; Ay 11:6; 7; Mit 3:32; Yer 23:18; Amo 3:7; Za 19:7; Lk 16:29; 2Tim 3:16; Mdo 17; 11Mambo ya siri ni ya Bwana Mungu wetu, bali yaliyofunuliwa ni yetu na watoto wetu milele, ili tuweze kuyafanya maneno yote ya sheria hii.

Japanese Contemporary Bible

申命記 29:1-29

29

モアブでの契約

1神である主がホレブ山(シナイ山)でイスラエル人と結ばれた契約を、モーセがもう一度語ったのは、モアブ平原においてでした。 2-3モーセはすべての民を集めて言いました。「皆さんは、主がエジプトで王とその国民に下された大きな災害と、驚くべき奇跡とを目の当たりにしました。 4それなのに、今までまるで悟らず、見る目も聞く耳も持ちませんでした。 5荒野を放浪した四十年間を振り返ってみなさい。その間、衣服は古びず、履き物もすり切れなかったではありませんか。 6主は、あなたがたが定住して、パンを作る麦を植えたり、ぶどう酒や強い酒を作るぶどうの木を育てたりするのをお許しになりませんでした。それは、あなたがたの世話をしてきたのがあなたがたの神、主であることをわからせるためです。

7ここへ来た時、ヘシュボンの王シホンとバシャンの王オグが戦いをしかけてきました。私たちは彼らを打ち破り、 8その領地を、ルベン族とガド族とマナセの半部族に与えました。 9ですから、この契約を守りなさい。あなたがたのすることがみな、栄えるためです。

10族長も、国民も、裁判官も、行政官もみな、主の前に立っています。 11妻子も、在留外国人も、たきぎを割り、水をくむ下働きの者までも含め全員です。 12今日ここに立っているのは、主と契約を結ぶためです。 13先祖のアブラハム、イサク、ヤコブに約束されたとおり、今日、主はあなたを神の民とし、またご自分があなたの神となられるためです。 14-15この契約は、今、主の前に立っている者とだけでなく、イスラエルの子孫全員と結ばれます。

16エジプトでどんなみじめな生活をしたか、そこを出てからは、敵の領地を通りながら、いかに安全に過ごしてきたか、今さら言うまでもないでしょう。 17木、石、銀、金でできた異教の偶像も、いやと言うほど見ました。 18あなたがたの中に、個人だろうが家族だろうが部族だろうが、主に背を向け、外国の神々を拝みたいと言いだす者が出たら気をつけなさい。それは、渋くて毒のある実しか結ばない根を植えるのと同じです。

19こののろいのことばを聞きながら、『何と言われたって、やりたいようにやるだけだ。大丈夫、絶対にうまくいく』などとうそぶいているなら、 20主は決してお赦しになりません。そのような者は激しいねたみと怒りを買うだけです。この書に書かれたすべてののろいが降りかかり、地上から永遠に消し去られてしまうでしょう。 21主はその者をイスラエルの全部族から除外し、契約の違反者に下ることになっている、すべてののろいを下されるのです。 22その結果、子孫たちや遠くから来た外国人が、ひどい災害や疫病のつめ跡をまざまざと見ることになるでしょう。 23全土が塩分を含んだアルカリ性の荒れ地となり、種もまけず収穫もなく、一本の草木も生えません。まるで、主の怒りによって滅ぼされたソドム、ゴモラ、アデマ、ツェボイムのようになってしまいます。

24『こんなひどいことをするとは、いったいどういうわけか。それも特別に目をかけていた国に、なぜ主はこれほどまでに怒りを燃やすのか』と、国々の民は不思議がるでしょう。 25答えはこうです。『彼らの先祖の神が昔、彼らをエジプトから助け出し、特別な契約を結ばれたのに、彼らのほうからその契約を破った。 26はっきり禁止されていたのに、ほかの神々を拝んだからである。 27それで主は激しく怒り、前もって警告してあったすべてののろいを下された。 28彼らを一人残らずこの国から追い出し、情け容赦なく外国へ追いやったのである。彼らは今もまだ故国に帰れず、そこに住んでいる。』

29主はすべてのことをお示しになったわけではありません。確かに、主だけがご存じの秘密もあります。しかし、はっきり示されたことには、私たちも子孫も永遠に従わなければならないのです。