Kumbukumbu 23 – NEN & KJV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Kumbukumbu 23:1-25

Kutengwa Na Mkutano

123:1 Law 21:20Asiingie mtu yeyote aliyehasiwa kwa kupondwa makende au kwa kukatwa uume wake katika kusanyiko la Bwana.

2Mtu yeyote ambaye amezaliwa kwenye ndoa isiyo halali au wazao wake wasiingie kwenye kusanyiko la Bwana, hata mpaka kizazi cha kumi.

323:3 Mwa 19:38; Neh 13:2; Rut 4:5; Neh 4:3-7Hapatakuwa na Mwamoni au Mmoabu au yeyote wa wazao wao atakayeruhusiwa kuingia katika kusanyiko la Bwana, hata mpaka kizazi cha kumi. 423:4 Kum 2:28; Hes 23:7; 2Pet 2:15; Mwa 24:10; 14:18; Kum 2:29; 1Sam 25:11; 1Fal 18:4; Isa 63:9Kwa kuwa hawakuja kuwalaki wakiwa na mkate na maji mlipokuwa njiani mlipotoka Misri, tena walimwajiri Balaamu mwana wa Beori kutoka Pethori iliyoko Aramu-Naharaimu23:4 Yaani Mesopotamia ya Kaskazini-Magharibi. ili kuwalaani ninyi. 523:5 Hes 24:10; Yos 24:10; Mit 26:2; Kum 4:37Hata hivyo, Bwana Mungu wenu hakumsikiliza Balaamu bali aligeuza laana kuwa baraka kwenu kwa sababu Bwana Mungu wenu anawapenda. 623:6 Hes 24:17; Isa 15:1; 25:10; Yer 25:21; 27:3; 48:1; Eze 25:8; Sef 2:9; Ezr 9:12; Mt 5:43Msitafute mapatano ya urafiki nao maisha yenu yote.

723:7 Mwa 25:30; 25:26; Law 19:34; Kut 23:9; Oba 1:11-12; Law 15:1-33; Kum 10:19; Law 19:34Usimchukie Mwedomu, kwa kuwa yeye ni ndugu yako. Usimchukie Mmisri, kwa sababu uliishi kama mgeni katika nchi yake. 8Kizazi cha tatu cha watoto watakaozaliwa nao wanaweza kuingia katika kusanyiko la Bwana.

Unajisi Katika Kambi

9Unapokuwa umepiga kambi dhidi ya adui zako, jitenge na kitu chochote kisicho safi. 1023:10 Law 15:16Ikiwa mtu amechafuka kwa sababu ya kutokwa na shahawa usiku, inampasa atoke nje ya kambi na kukaa huko. 1123:11 Law 15:16; 1Sam 21:5Lakini jioni ikikaribia ataoga, na baada ya jua kuzama ataingia tena kambini.

12Tengeni mahali nje ya kambi ambapo mnaweza kwenda kujisaidia. 13Kama sehemu ya vifaa vyenu kuweni na kitu cha kulimia, nanyi mnapojisaidia, chimba shimo na kisha funika kile kikutokacho. 1423:14 Mwa 3:8; Kut 3:4-5; Law 26:12; Yer 32:40; 2Kor 6:16Kwa kuwa Bwana Mungu wenu hutembea katika kambi yenu ili kuwalinda na kuwaweka adui zenu mikononi mwenu. Kambi yenu ni lazima iwe takatifu, ili asione kitu chochote miongoni mwenu kilicho kichafu akageuka na kuwaacha.

Sheria Mbalimbali

1523:15 2Sam 22:3; Za 2:12; 71:1; 1Sam 30:15Ikiwa mtumwa amekimbilia kwako, usimrudishe kwa bwana wake. 1623:16 Kut 22:21; 23:6; Mt 22:22; Yer 7:6; Zek 7:10; Yak 2:6Mwache aishi miongoni mwenu mahali popote anapopapenda na katika mji wowote anaochagua. Usimwonee.

1723:17 1Fal 14:24; 15:12; 22:46; 2Fal 23:7; Ay 36:14; Mwa 38:21; Law 19:29; Mit 2:16; Mwa 19:5Asiwepo Mwisraeli mwanamke kahaba au mwanaume hanithi wa mahali pa kuabudia miungu. 1823:18 Mwa 19:5; Law 20:13; Ufu 22:15Kamwe usilete mapato ya ukahaba ikiwa ni ya mwanamke au ni ya mwanaume katika nyumba ya Bwana Mungu wako kwa ajili ya nadhiri yoyote, kwa sababu Bwana Mungu wako anachukizwa na yote mawili.

1923:19 Law 25:35-37; Neh 5:2-7; Kut 22:25; Za 15:5; Lk 6:34Usimtoze ndugu yako riba, iwe ni fedha ama chakula ama kitu kingine chochote ambacho waweza kupata riba juu yake. 2023:20 Hes 6:21; Amu 11:35; Za 15:4; Hes 30:1-2; Ay 22:27; Za 61:8; 65:1; 76:11; Mhu 5:4-5; Isa 19:21; Mt 5:33; Mdo 5:3; Kum 25:10; 28:12; Law 19:34Unaweza kumtoza mgeni riba, lakini siyo nduguyo Mwisraeli, ili kwamba Bwana Mungu wako akubariki katika kila kitu unachoweka mkono katika nchi unayoingia kuimiliki.

2123:21 Ay 22:27; Za 61:8; Mhu 5:4-5Ukiweka nadhiri kwa Bwana Mungu wako, usichelewe kuitimiza, kwa kuwa Bwana Mungu wako atakudai, nawe utakuwa na hatia ya dhambi. 2223:22 Mdo 5:4Lakini ukijizuia kuweka nadhiri, hutakuwa na hatia. 2323:23 Za 66:13Chochote kitakachotamkwa kwa midomo yako ni lazima uhakikishe umekifanya, kwa sababu uliweka nadhiri yako kwa hiari mbele za Bwana Mungu wako kwa kinywa chako mwenyewe.

2423:24 Mt 12:1; Lk 12:15; 1Kor 6:10; Kol 3:5Kama ukiingia katika shamba la mizabibu la jirani yako, unaweza kula zabibu kadiri utakavyo, lakini usiweke chochote kwenye kikapu chako. 2523:25 Mt 12:1; Mk 2:23; Lk 6:1Kama ukiingia katika shamba la nafaka la jirani yako, unaweza kukwanyua kwa mikono yako, lakini usikate kwa mundu nafaka iliyosimama.

King James Version

Deuteronomy 23:1-25

1He that is wounded in the stones, or hath his privy member cut off, shall not enter into the congregation of the LORD. 2A bastard shall not enter into the congregation of the LORD; even to his tenth generation shall he not enter into the congregation of the LORD. 3An Ammonite or Moabite shall not enter into the congregation of the LORD; even to their tenth generation shall they not enter into the congregation of the LORD for ever: 4Because they met you not with bread and with water in the way, when ye came forth out of Egypt; and because they hired against thee Balaam the son of Beor of Pethor of Mesopotamia, to curse thee. 5Nevertheless the LORD thy God would not hearken unto Balaam; but the LORD thy God turned the curse into a blessing unto thee, because the LORD thy God loved thee. 6Thou shalt not seek their peace nor their prosperity all thy days for ever.23.6 prosperity: Heb. good

7¶ Thou shalt not abhor an Edomite; for he is thy brother: thou shalt not abhor an Egyptian; because thou wast a stranger in his land. 8The children that are begotten of them shall enter into the congregation of the LORD in their third generation.

9¶ When the host goeth forth against thine enemies, then keep thee from every wicked thing.

10¶ If there be among you any man, that is not clean by reason of uncleanness that chanceth him by night, then shall he go abroad out of the camp, he shall not come within the camp: 11But it shall be, when evening cometh on, he shall wash himself with water: and when the sun is down, he shall come into the camp again.23.11 cometh…: Heb. turneth toward

12¶ Thou shalt have a place also without the camp, whither thou shalt go forth abroad: 13And thou shalt have a paddle upon thy weapon; and it shall be, when thou wilt ease thyself abroad, thou shalt dig therewith, and shalt turn back and cover that which cometh from thee:23.13 wilt…: Heb. sittest down 14For the LORD thy God walketh in the midst of thy camp, to deliver thee, and to give up thine enemies before thee; therefore shall thy camp be holy: that he see no unclean thing in thee, and turn away from thee.23.14 unclean…: Heb. nakedness of any thing

15¶ Thou shalt not deliver unto his master the servant which is escaped from his master unto thee: 16He shall dwell with thee, even among you, in that place which he shall choose in one of thy gates, where it liketh him best: thou shalt not oppress him.23.16 liketh…: Heb. is good for him

17¶ There shall be no whore of the daughters of Israel, nor a sodomite of the sons of Israel.23.17 whore: or, sodomitess 18Thou shalt not bring the hire of a whore, or the price of a dog, into the house of the LORD thy God for any vow: for even both these are abomination unto the LORD thy God.

19¶ Thou shalt not lend upon usury to thy brother; usury of money, usury of victuals, usury of any thing that is lent upon usury: 20Unto a stranger thou mayest lend upon usury; but unto thy brother thou shalt not lend upon usury: that the LORD thy God may bless thee in all that thou settest thine hand to in the land whither thou goest to possess it.

21¶ When thou shalt vow a vow unto the LORD thy God, thou shalt not slack to pay it: for the LORD thy God will surely require it of thee; and it would be sin in thee. 22But if thou shalt forbear to vow, it shall be no sin in thee. 23That which is gone out of thy lips thou shalt keep and perform; even a freewill offering, according as thou hast vowed unto the LORD thy God, which thou hast promised with thy mouth.

24¶ When thou comest into thy neighbour’s vineyard, then thou mayest eat grapes thy fill at thine own pleasure; but thou shalt not put any in thy vessel. 25When thou comest into the standing corn of thy neighbour, then thou mayest pluck the ears with thine hand; but thou shalt not move a sickle unto thy neighbour’s standing corn.