Kumbukumbu 23 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Kumbukumbu 23:1-25

Kutengwa Na Mkutano

123:1 Law 21:20Asiingie mtu yeyote aliyehasiwa kwa kupondwa makende au kwa kukatwa uume wake katika kusanyiko la Bwana.

2Mtu yeyote ambaye amezaliwa kwenye ndoa isiyo halali au wazao wake wasiingie kwenye kusanyiko la Bwana, hata mpaka kizazi cha kumi.

323:3 Mwa 19:38; Neh 13:2; Rut 4:5; Neh 4:3-7Hapatakuwa na Mwamoni au Mmoabu au yeyote wa wazao wao atakayeruhusiwa kuingia katika kusanyiko la Bwana, hata mpaka kizazi cha kumi. 423:4 Kum 2:28; Hes 23:7; 2Pet 2:15; Mwa 24:10; 14:18; Kum 2:29; 1Sam 25:11; 1Fal 18:4; Isa 63:9Kwa kuwa hawakuja kuwalaki wakiwa na mkate na maji mlipokuwa njiani mlipotoka Misri, tena walimwajiri Balaamu mwana wa Beori kutoka Pethori iliyoko Aramu-Naharaimu23:4 Yaani Mesopotamia ya Kaskazini-Magharibi. ili kuwalaani ninyi. 523:5 Hes 24:10; Yos 24:10; Mit 26:2; Kum 4:37Hata hivyo, Bwana Mungu wenu hakumsikiliza Balaamu bali aligeuza laana kuwa baraka kwenu kwa sababu Bwana Mungu wenu anawapenda. 623:6 Hes 24:17; Isa 15:1; 25:10; Yer 25:21; 27:3; 48:1; Eze 25:8; Sef 2:9; Ezr 9:12; Mt 5:43Msitafute mapatano ya urafiki nao maisha yenu yote.

723:7 Mwa 25:30; 25:26; Law 19:34; Kut 23:9; Oba 1:11-12; Law 15:1-33; Kum 10:19; Law 19:34Usimchukie Mwedomu, kwa kuwa yeye ni ndugu yako. Usimchukie Mmisri, kwa sababu uliishi kama mgeni katika nchi yake. 8Kizazi cha tatu cha watoto watakaozaliwa nao wanaweza kuingia katika kusanyiko la Bwana.

Unajisi Katika Kambi

9Unapokuwa umepiga kambi dhidi ya adui zako, jitenge na kitu chochote kisicho safi. 1023:10 Law 15:16Ikiwa mtu amechafuka kwa sababu ya kutokwa na shahawa usiku, inampasa atoke nje ya kambi na kukaa huko. 1123:11 Law 15:16; 1Sam 21:5Lakini jioni ikikaribia ataoga, na baada ya jua kuzama ataingia tena kambini.

12Tengeni mahali nje ya kambi ambapo mnaweza kwenda kujisaidia. 13Kama sehemu ya vifaa vyenu kuweni na kitu cha kulimia, nanyi mnapojisaidia, chimba shimo na kisha funika kile kikutokacho. 1423:14 Mwa 3:8; Kut 3:4-5; Law 26:12; Yer 32:40; 2Kor 6:16Kwa kuwa Bwana Mungu wenu hutembea katika kambi yenu ili kuwalinda na kuwaweka adui zenu mikononi mwenu. Kambi yenu ni lazima iwe takatifu, ili asione kitu chochote miongoni mwenu kilicho kichafu akageuka na kuwaacha.

Sheria Mbalimbali

1523:15 2Sam 22:3; Za 2:12; 71:1; 1Sam 30:15Ikiwa mtumwa amekimbilia kwako, usimrudishe kwa bwana wake. 1623:16 Kut 22:21; 23:6; Mt 22:22; Yer 7:6; Zek 7:10; Yak 2:6Mwache aishi miongoni mwenu mahali popote anapopapenda na katika mji wowote anaochagua. Usimwonee.

1723:17 1Fal 14:24; 15:12; 22:46; 2Fal 23:7; Ay 36:14; Mwa 38:21; Law 19:29; Mit 2:16; Mwa 19:5Asiwepo Mwisraeli mwanamke kahaba au mwanaume hanithi wa mahali pa kuabudia miungu. 1823:18 Mwa 19:5; Law 20:13; Ufu 22:15Kamwe usilete mapato ya ukahaba ikiwa ni ya mwanamke au ni ya mwanaume katika nyumba ya Bwana Mungu wako kwa ajili ya nadhiri yoyote, kwa sababu Bwana Mungu wako anachukizwa na yote mawili.

1923:19 Law 25:35-37; Neh 5:2-7; Kut 22:25; Za 15:5; Lk 6:34Usimtoze ndugu yako riba, iwe ni fedha ama chakula ama kitu kingine chochote ambacho waweza kupata riba juu yake. 2023:20 Hes 6:21; Amu 11:35; Za 15:4; Hes 30:1-2; Ay 22:27; Za 61:8; 65:1; 76:11; Mhu 5:4-5; Isa 19:21; Mt 5:33; Mdo 5:3; Kum 25:10; 28:12; Law 19:34Unaweza kumtoza mgeni riba, lakini siyo nduguyo Mwisraeli, ili kwamba Bwana Mungu wako akubariki katika kila kitu unachoweka mkono katika nchi unayoingia kuimiliki.

2123:21 Ay 22:27; Za 61:8; Mhu 5:4-5Ukiweka nadhiri kwa Bwana Mungu wako, usichelewe kuitimiza, kwa kuwa Bwana Mungu wako atakudai, nawe utakuwa na hatia ya dhambi. 2223:22 Mdo 5:4Lakini ukijizuia kuweka nadhiri, hutakuwa na hatia. 2323:23 Za 66:13Chochote kitakachotamkwa kwa midomo yako ni lazima uhakikishe umekifanya, kwa sababu uliweka nadhiri yako kwa hiari mbele za Bwana Mungu wako kwa kinywa chako mwenyewe.

2423:24 Mt 12:1; Lk 12:15; 1Kor 6:10; Kol 3:5Kama ukiingia katika shamba la mizabibu la jirani yako, unaweza kula zabibu kadiri utakavyo, lakini usiweke chochote kwenye kikapu chako. 2523:25 Mt 12:1; Mk 2:23; Lk 6:1Kama ukiingia katika shamba la nafaka la jirani yako, unaweza kukwanyua kwa mikono yako, lakini usikate kwa mundu nafaka iliyosimama.

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

申命記 23:1-25

會眾的資格

1「凡睪丸受損或被閹割的,不可加入耶和華的會眾。

2「私生子及其十代以內的子孫都不可加入耶和華的會眾。

3亞捫人或摩押人及其十代以內的子孫都不可加入耶和華的會眾。 4因為在你們離開埃及的途中,他們沒有用水和食物款待你們,還雇用美索不達米亞毗奪人——比珥的兒子巴蘭咒詛你們。 5但你們的上帝耶和華不聽巴蘭的話,反而把咒詛變為祝福,因為祂愛你們。 6你們一生一世永不可為他們謀求平安和好處。

7「不可憎惡以東人,因為他們是你們的弟兄;也不可憎惡埃及人,因為你們曾經在埃及寄居。 8他們的第三代子孫可以加入耶和華的會眾。

保持軍營聖潔的條例

9「你們出兵征戰時,一定要遠離惡事。 10如果有人因夢遺而不潔淨,他就要離開營地住在營外。 11傍晚他要沐浴,日落才可以回營。 12要在營外指定一個地方作方便之處。 13你們每人都要有一把鏟子,便溺時要挖個洞,事後要掩埋。 14因為你們的上帝耶和華常在營中巡視,要保護你們,擊敗你們的仇敵。軍營必須保持聖潔,免得祂在你們中間看到任何污穢之事,便離開你們。

其他條例

15「如果有奴隸逃到你們那裡避難,不可把逃亡的奴隸送交他們的主人。 16要讓他們在你們當中選擇他們喜歡的城邑與你們同住,不可壓迫他們。

17「任何以色列人,不論男女,都不可做廟妓。 18不可把男女廟妓的收入帶到你們上帝耶和華的殿還願,因為你們的上帝耶和華憎惡他們。

19「你們借給同胞錢、糧食或其他任何東西,都不可收取利息。 20你們可以向外族人收取利息,但不可向同胞收取。這樣,在你們將要佔領的土地上,你們的上帝耶和華必使你們凡事蒙福。

21「如果你們向你們的上帝耶和華許願,不可遲遲不還願,因為你們的上帝耶和華必追討許願不還的罪。 22如果你們不許願,反倒無罪; 23但如果你們親口許了願,一定要向你們的上帝耶和華信守諾言。

24「如果你們進了鄰居的葡萄園,可以隨意吃,但不可把葡萄放在籃子裡帶走。 25如果你們進了鄰居的麥田,可以用手摘麥穗,但不可用鐮刀割麥子。