Kumbukumbu 23 – NEN & CCB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Kumbukumbu 23:1-25

Kutengwa Na Mkutano

123:1 Law 21:20Asiingie mtu yeyote aliyehasiwa kwa kupondwa makende au kwa kukatwa uume wake katika kusanyiko la Bwana.

2Mtu yeyote ambaye amezaliwa kwenye ndoa isiyo halali au wazao wake wasiingie kwenye kusanyiko la Bwana, hata mpaka kizazi cha kumi.

323:3 Mwa 19:38; Neh 13:2; Rut 4:5; Neh 4:3-7Hapatakuwa na Mwamoni au Mmoabu au yeyote wa wazao wao atakayeruhusiwa kuingia katika kusanyiko la Bwana, hata mpaka kizazi cha kumi. 423:4 Kum 2:28; Hes 23:7; 2Pet 2:15; Mwa 24:10; 14:18; Kum 2:29; 1Sam 25:11; 1Fal 18:4; Isa 63:9Kwa kuwa hawakuja kuwalaki wakiwa na mkate na maji mlipokuwa njiani mlipotoka Misri, tena walimwajiri Balaamu mwana wa Beori kutoka Pethori iliyoko Aramu-Naharaimu23:4 Yaani Mesopotamia ya Kaskazini-Magharibi. ili kuwalaani ninyi. 523:5 Hes 24:10; Yos 24:10; Mit 26:2; Kum 4:37Hata hivyo, Bwana Mungu wenu hakumsikiliza Balaamu bali aligeuza laana kuwa baraka kwenu kwa sababu Bwana Mungu wenu anawapenda. 623:6 Hes 24:17; Isa 15:1; 25:10; Yer 25:21; 27:3; 48:1; Eze 25:8; Sef 2:9; Ezr 9:12; Mt 5:43Msitafute mapatano ya urafiki nao maisha yenu yote.

723:7 Mwa 25:30; 25:26; Law 19:34; Kut 23:9; Oba 1:11-12; Law 15:1-33; Kum 10:19; Law 19:34Usimchukie Mwedomu, kwa kuwa yeye ni ndugu yako. Usimchukie Mmisri, kwa sababu uliishi kama mgeni katika nchi yake. 8Kizazi cha tatu cha watoto watakaozaliwa nao wanaweza kuingia katika kusanyiko la Bwana.

Unajisi Katika Kambi

9Unapokuwa umepiga kambi dhidi ya adui zako, jitenge na kitu chochote kisicho safi. 1023:10 Law 15:16Ikiwa mtu amechafuka kwa sababu ya kutokwa na shahawa usiku, inampasa atoke nje ya kambi na kukaa huko. 1123:11 Law 15:16; 1Sam 21:5Lakini jioni ikikaribia ataoga, na baada ya jua kuzama ataingia tena kambini.

12Tengeni mahali nje ya kambi ambapo mnaweza kwenda kujisaidia. 13Kama sehemu ya vifaa vyenu kuweni na kitu cha kulimia, nanyi mnapojisaidia, chimba shimo na kisha funika kile kikutokacho. 1423:14 Mwa 3:8; Kut 3:4-5; Law 26:12; Yer 32:40; 2Kor 6:16Kwa kuwa Bwana Mungu wenu hutembea katika kambi yenu ili kuwalinda na kuwaweka adui zenu mikononi mwenu. Kambi yenu ni lazima iwe takatifu, ili asione kitu chochote miongoni mwenu kilicho kichafu akageuka na kuwaacha.

Sheria Mbalimbali

1523:15 2Sam 22:3; Za 2:12; 71:1; 1Sam 30:15Ikiwa mtumwa amekimbilia kwako, usimrudishe kwa bwana wake. 1623:16 Kut 22:21; 23:6; Mt 22:22; Yer 7:6; Zek 7:10; Yak 2:6Mwache aishi miongoni mwenu mahali popote anapopapenda na katika mji wowote anaochagua. Usimwonee.

1723:17 1Fal 14:24; 15:12; 22:46; 2Fal 23:7; Ay 36:14; Mwa 38:21; Law 19:29; Mit 2:16; Mwa 19:5Asiwepo Mwisraeli mwanamke kahaba au mwanaume hanithi wa mahali pa kuabudia miungu. 1823:18 Mwa 19:5; Law 20:13; Ufu 22:15Kamwe usilete mapato ya ukahaba ikiwa ni ya mwanamke au ni ya mwanaume katika nyumba ya Bwana Mungu wako kwa ajili ya nadhiri yoyote, kwa sababu Bwana Mungu wako anachukizwa na yote mawili.

1923:19 Law 25:35-37; Neh 5:2-7; Kut 22:25; Za 15:5; Lk 6:34Usimtoze ndugu yako riba, iwe ni fedha ama chakula ama kitu kingine chochote ambacho waweza kupata riba juu yake. 2023:20 Hes 6:21; Amu 11:35; Za 15:4; Hes 30:1-2; Ay 22:27; Za 61:8; 65:1; 76:11; Mhu 5:4-5; Isa 19:21; Mt 5:33; Mdo 5:3; Kum 25:10; 28:12; Law 19:34Unaweza kumtoza mgeni riba, lakini siyo nduguyo Mwisraeli, ili kwamba Bwana Mungu wako akubariki katika kila kitu unachoweka mkono katika nchi unayoingia kuimiliki.

2123:21 Ay 22:27; Za 61:8; Mhu 5:4-5Ukiweka nadhiri kwa Bwana Mungu wako, usichelewe kuitimiza, kwa kuwa Bwana Mungu wako atakudai, nawe utakuwa na hatia ya dhambi. 2223:22 Mdo 5:4Lakini ukijizuia kuweka nadhiri, hutakuwa na hatia. 2323:23 Za 66:13Chochote kitakachotamkwa kwa midomo yako ni lazima uhakikishe umekifanya, kwa sababu uliweka nadhiri yako kwa hiari mbele za Bwana Mungu wako kwa kinywa chako mwenyewe.

2423:24 Mt 12:1; Lk 12:15; 1Kor 6:10; Kol 3:5Kama ukiingia katika shamba la mizabibu la jirani yako, unaweza kula zabibu kadiri utakavyo, lakini usiweke chochote kwenye kikapu chako. 2523:25 Mt 12:1; Mk 2:23; Lk 6:1Kama ukiingia katika shamba la nafaka la jirani yako, unaweza kukwanyua kwa mikono yako, lakini usikate kwa mundu nafaka iliyosimama.

Chinese Contemporary Bible (Simplified)

申命记 23:1-25

会众的资格

1“凡睪丸受损或被阉割的,不可加入耶和华的会众。

2“私生子及其十代以内的子孙都不可加入耶和华的会众。

3亚扪人或摩押人及其十代以内的子孙都不可加入耶和华的会众。 4因为在你们离开埃及的途中,他们没有用水和食物款待你们,还雇用美索不达米亚毗夺人——比珥的儿子巴兰咒诅你们。 5但你们的上帝耶和华不听巴兰的话,反而把咒诅变为祝福,因为祂爱你们。 6你们一生一世永不可为他们谋求平安和好处。

7“不可憎恶以东人,因为他们是你们的弟兄;也不可憎恶埃及人,因为你们曾经在埃及寄居。 8他们的第三代子孙可以加入耶和华的会众。

保持军营圣洁的条例

9“你们出兵征战时,一定要远离恶事。 10如果有人因梦遗而不洁净,他就要离开营地住在营外。 11傍晚他要沐浴,日落才可以回营。 12要在营外指定一个地方作方便之处。 13你们每人都要有一把铲子,便溺时要挖个洞,事后要掩埋。 14因为你们的上帝耶和华常在营中巡视,要保护你们,击败你们的仇敌。军营必须保持圣洁,免得祂在你们中间看到任何污秽之事,便离开你们。

其他条例

15“如果有奴隶逃到你们那里避难,不可把逃亡的奴隶送交他们的主人。 16要让他们在你们当中选择他们喜欢的城邑与你们同住,不可压迫他们。

17“任何以色列人,不论男女,都不可做庙妓。 18不可把男女庙妓的收入带到你们上帝耶和华的殿还愿,因为你们的上帝耶和华憎恶他们。

19“你们借给同胞钱、粮食或其他任何东西,都不可收取利息。 20你们可以向外族人收取利息,但不可向同胞收取。这样,在你们将要占领的土地上,你们的上帝耶和华必使你们凡事蒙福。

21“如果你们向你们的上帝耶和华许愿,不可迟迟不还愿,因为你们的上帝耶和华必追讨许愿不还的罪。 22如果你们不许愿,反倒无罪; 23但如果你们亲口许了愿,一定要向你们的上帝耶和华信守诺言。

24“如果你们进了邻居的葡萄园,可以随意吃,但不可把葡萄放在篮子里带走。 25如果你们进了邻居的麦田,可以用手摘麦穗,但不可用镰刀割麦子。