Kumbukumbu 21 – NEN & KLB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Kumbukumbu 21:1-23

Upatanisho Kuhusu Mauaji

121:1 Hes 25:17; Za 9:12; Mit 28:17Kama mtu akikutwa ameuawa, naye amelala kwenye shamba katika nchi ambayo Bwana Mungu wenu anawapa kuimiliki, wala haijulikani ni nani aliyemuua, 2wazee wenu na waamuzi watatoka na kupima umbali kutoka maiti alipolala mpaka kwenye miji ya jirani. 321:3 Hes 19:2Kisha wazee wa ule mji ulio karibu zaidi na yule maiti watamchukua mtamba ambaye hajapata kufanyishwa kazi na ambaye hajafungwa nira, 4na kumpeleka kwenye bonde ambalo halijapata kulimwa au kupandwa mazao na ambapo kuna chemchemi itiririkayo. Huko kwenye hilo bonde, wazee watamvunja yule mtamba shingo. 521:5 Mwa 48:20; Kut 39:43; Kum 17:8-11Makuhani, hao wana wa Lawi, watasogea mbele, kwa kuwa Bwana Mungu wenu, amewachagua kuhudumu na kutoa baraka katika jina la Bwana, na kuamua mashauri yote ya mabishano na mashambulio. 621:6 Mt 27:24; 1Nya 23:1321:6 Ay 9:30; Za 19:12; Yer 2:22; Mt 27:14; Ebr 9:10Ndipo wazee wote wa mji ulio karibu zaidi na huyo maiti watanawa mikono yao juu ya huyo mtamba ambaye shingo yake imevunjwa huko kwenye bonde, 721:7 2Sam 3:28nao watatangaza: “Mikono yetu haikumwaga damu hii, wala macho yetu hayakuona likifanyika. 821:8 Hes 35:33-34; Yer 26:15; Eze 22:3; Yn 1:14Ee Bwana, ukubali upatanisho kwa watu wako Israeli, ambao umewakomboa, wala usiwahesabie watu wako hatia ya damu ya mtu asiyekuwa na hatia.” Nayo damu iliyomwagika itakuwa imefanyiwa upatanisho. 921:9 Kum 19:13Hivyo mtakuwa mmejitakasa wenyewe kutoka hatia ya kumwaga damu isiyokuwa na hatia, kwa kuwa mmefanya lile lililo sawa mbele za macho ya Bwana.

Kuoa Mwanamke Mateka

1021:10 Yos 21:44; 1Fal 8:46; 1Nya 9:1; Ezr 5:12; Yer 40:1; Eze 1:1; 17:12; Dan 2:25; Mik 4:10; 2Nya 32:8Mkienda vitani kupigana na adui zenu naye Bwana Mungu wenu akawatia adui mikononi mwenu, nanyi mkachukua mateka, 1121:11 Mwa 6:2; 34:8kama ukiona miongoni mwa mateka mwanamke mzuri wa sura nawe wavutwa naye, waweza kumwoa akawa mke wako. 1221:12 Law 14:9; Hes 8:7; 1Kor 11:5; Hes 6:9Mlete nyumbani mwako, anyoe nywele na kukata kucha zake, 1321:13 Za 45:10avue nguo alizokuwa amevaa alipotekwa. Baada ya kuishi nyumbani mwako na kumwombolezea baba yake na mama yake kwa mwezi mzima, ndipo utakapoweza kumwendea na kuwa mume wake naye atakuwa mke wako. 1421:14 Mwa 34:2; Amu 19:24Lakini kama hutaendelea kupendezwa naye, mwache aende popote anapotaka. Kamwe huwezi kumuuza au kumtendea kama mtumwa, kwa sababu utakuwa umemvunjia heshima.

Haki Ya Mzaliwa Wa Kwanza

1521:15 Mwa 4:19; 29:33Kama mwanaume ana wake wawili, naye anampenda mmoja na mwingine hampendi na wote wawili wamemzalia wana wa kiume, lakini mwana mzaliwa wa kwanza ni wa yule mke asiyempenda, 1621:16 1Nya 26:10; Rum 8:29wakati anapotoa wosia wa mali yake kwa wanawe, kamwe asitoe haki za mzaliwa wa kwanza kwa mwana wa mke ampendaye kwa upendeleo, badala ya mzaliwa hasa wa kwanza, ambaye ni mwana wa mke ambaye hampendi. 1721:17 2Fal 2:9; Isa 40:2; 61:7; Zek 9:12; Mwa 49:3; 25:31; Lk 15:12; 1Nya 5:1Ni lazima amkubali mwana wa mke asiyempenda kama mzaliwa wa kwanza kwa kumpa sehemu ya vile vyote alivyo navyo maradufu. Mwana huyo ni ishara ya kwanza ya nguvu za baba yake. Haki ya mzaliwa wa kwanza ni yake yeye.

Mwana Mwasi

1821:18 Za 78:8; Yer 5:23; Sef 3:1; Mit 30:17; Mwa 31:35; Mit 1:8; Isa 30:1; Efe 6:1-3; Kut 20:12; 21:15, 17; Law 19:3; 21:9Kama mtu ana mwana mkaidi na mwasi ambaye hamtii baba yake na mama yake, na hasikii wazazi wanapomrudi, 19baba yake na mama yake watamleta kwa wazee kwenye lango la mji wake. 20Watawaambia wazee, “Huyu mwanetu ni mkaidi na mwasi. Hatutii sisi, yeye ni mpotovu na mlevi.” 2121:21 Law 20:9; Kum 19:19; 1Kor 5:13; Kum 13:11; 1Sam 26:16Kisha wanaume wote wa mjini mwake watampiga kwa mawe mpaka afe. Ndivyo imewapasa kuondoa maovu kati yenu. Israeli yote itasikia hili na kuogopa.

Sheria Mbalimbali

2221:22 Kum 22:26; Mt 26:66; Mk 14:64; Mdo 23:29Kama mtu ana hatia ya kosa linalompasa kuuawa naye akauawa, mwili wake utaangikwa mtini, 2321:23 Yos 8:29; 10:27; Yn 19:31; Eze 39:12; Ezr 6:11; Es 2:23; 7:9; 8:7; 9:13, 25; Isa 50:11; Gal 3:13; Law 18:25kamwe msiuache mwili wake mtini usiku kucha. Hakikisheni mnauzika mwili wake siku ile ile, kwa sababu kila mtu anayeangikwa mtini yupo chini ya laana ya Mungu. Msiinajisi nchi ambayo Bwana Mungu wenu anawapa kama urithi wenu.

Korean Living Bible

신명기 21:1-23

범인을 알 수 없는 살인 사건에 관한 규정

1“여러분의 하나님 여호와께서 주시는 땅에서 피살된 시체가 들에 있는 것이 발견되었는데도 살인자가 누군지 알지 못하면

2여러분의 지도자들과 재판관들이 나가서 피살체가 발견된 곳에서부터 그 주변 성에까지 거리를 재도록 하십시오.

3그런 다음에 그 피살체에서 가장 가까이 있는 성의 지도자들은 아직 한 번도 부리지 않고 멍에도 메어 보지 않은 암송아지 한 마리를 택하여

4항상 물이 흐르고 갈거나 무엇을 심어 보지도 않은 골짜기로 끌고 가 거기서 그 송아지의 목을 꺾어야 합니다.

5그리고 레위 자손의 제사장들도 그리로 가야 합니다. 그것은 여러분의 하나님 여호와께서 자기를 섬기게 하시고 또 여호와의 이름으로 축복하게 하시며 모든 소송과 분쟁을 판결하도록 그들을 택하셨기 때문입니다.

6그런 다음 피살체에서 가장 가까운 성의 모든 지도자들이 목을 부러뜨린 그 송아지 위에서 손을 씻으며

7이렇게 말하도록 하십시오. ‘우리 손은 이 피를 흘리지 않았고 우리 눈도 이것을 보지 못했습니다.

8여호와여, 주께서 구원하신 주의 백성 이스라엘을 용서하시고 죄 없는 사람을 죽인 살인죄에 대한 책임을 우리에게 돌리지 마소서.’ 그러면 그 살인죄가 용서될 것입니다.

9이와 같이 여러분은 여호와께서 요구하시는 것을 행함으로 죄 없는 사람의 피를 흘린 죄를 여러분 가운데서 제거할 수 있을 것입니다.”

전쟁터에서 사로잡힌 여자에 관하여

10“여러분이 원수들과 싸우는 전쟁에서 여호와 하나님이 여러분에게 승리를 주어 여러분이 그들을 생포하게 될 때

11만일 여러분이 그 포로 중에 아름다운 여자를 보고 좋아하여 그녀와 결혼하고 싶으면

12그 여자를 여러분의 집으로 데리고 가십시오. 그리고 그 여자는 자기 머리를 밀고 손톱을 깎고

13옷을 갈아 입은 다음 여러분의 집에서 한 달 동안 자기 부모를 위해 애도해야 합니다. 그래야만 여러분이 그 여자와 결혼할 수 있습니다.

14그러나 후에 여러분이 그 여자를 좋아하지 않으면 그녀를 마음대로 가게 하십시오. 여러분은 이미 그 여자를 욕되게 하였으므로 그녀를 종으로 취급하여 돈을 받고 팔아서는 안 됩니다.”

장자 상속권

15“어떤 사람에게 두 아내가 있는데 하나는 사랑을 받고 하나는 미움을 받다가 그들이 모두 아들을 낳았을 경우에 만일 미움을 받는 여자의 아들이 장남이라면

16재산을 분배할 때 장자권을 무시하고 사랑하는 여자의 아들이라고 해서 미워하는 여자의 아들보다 그에게 더 많은 재산을 주어서는 안 됩니다.

17여러분은 미워하는 여자의 아들이라도 먼저 난 자를 장남으로 인정하여 두 몫을 그에게 주도록 하십시오. 그는 자기 아버지의 정력의 첫열매이며 장자권을 가진 자입니다.”

거역하고 불순종하는 아들의 처리 문제

18“만일 어떤 사람에게 고집 세고 막돼먹은 아들이 있는데 부모에게 순종하지 않고 벌을 받아도 듣지 않으면

19부모가 그 성의 지도자들에게 그를 끌고 가서

20‘이놈은 고집 세고 막돼먹어 우리에게 순종하지 않는 방탕한 술주정꾼입니다’ 하고 말하도록 하십시오.

21그러면 그 성의 주민들이 그를 돌로 쳐죽여야 합니다. 여러분은 이렇게 하여 여러분 가운데서 이런 악을 제거하십시오. 이스라엘에 있는 모든 사람들이 그 일을 듣고 두려워할 것입니다.”

여러 가지 법

22“만일 어떤 사람이 죽을 죄를 지어 여러분이 그를 처형한 후 그 시체를 나무에 매달 경우

23그 시체를 밤새도록 그대로 두지 말고 그 날에 그를 매장하십시오. 나무에 달린 사람은 하나님께 저주받은 자입니다. 그러므로 여러분은 시체를 그대로 두어 여러분의 하나님 여호와께서 주신 땅을 더럽혀서는 안 됩니다.”