Kumbukumbu 19 – NEN & NIRV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Kumbukumbu 19:1-21

Miji Ya Makimbilio

(Hesabu 35:9-34; Yoshua 20:1-9)

119:1 Kum 6:10-11; 12:29Wakati Bwana Mungu wenu atakapokuwa amewaangamiza mataifa ambayo nchi yao anawapa ninyi, wakati mtakapokuwa mmewafukuza na kuishi katika miji yao na nyumba zao, 219:2 Yos 20:2ndipo mtenge miji mitatu iliyopo katikati ya nchi kwa ajili yenu, katika nchi ambayo Bwana Mungu wenu anawapa kuimiliki. 3Jengeni barabara katika miji hiyo na kuigawa mara tatu, nchi anayowapa Bwana Mungu wenu kama urithi, ili kwamba yeyote amuuaye mtu aweze kukimbilia humo.

4Hii ndiyo kanuni kuhusu mtu amuuaye mwingine na kukimbilia humo kuokoa maisha yake, yaani, yeye amuuaye jirani yake bila kukusudia, wala hakumchukia kabla ya hapo. 5Kwa mfano, mtu aweza kwenda msituni na jirani yake kukata miti, naye anapozungusha shoka kuangusha mti, shoka linaweza kuchomoka kutoka kwenye mpini na kumpiga jirani yake na kumuua. Yule mtu anaweza kukimbilia katika mmojawapo ya miji hii na kuokoa maisha yake. 619:6 Hes 35:12Kama sivyo, mlipiza kisasi cha damu anaweza kumfuatilia kwa hasira kali, naye akamkamata na kumuua kama umbali ni mrefu sana hata ingawa hastahili kifo, kwa sababu amemuua jirani yake bila kukusudia. 7Hii ndiyo sababu nimewaagiza ninyi kutenga miji mitatu ya makimbilio kwa ajili yenu.

819:8 Kut 34:24; Mwa 15:18; Kum 11:24Kama Bwana Mungu wenu akipanua nchi yenu, kama alivyoahidi kwa kiapo kwa baba zenu na kuwapa nchi yote aliyowaahidi, 919:9 Kum 6:5; Yos 20:7-8kwa sababu mmefuata kwa uangalifu sheria zote ninazowaamuru leo, kumpenda Bwana Mungu wenu na kuenenda siku zote katika njia zake, ndipo mtenge miji mingine, mitatu zaidi. 1019:10 Mit 6:17; Yer 7:6; 26:15; Kum 21:1-9; Hes 35:33Fanyeni hivi ili damu isiyo na hatia isimwagwe katika nchi yenu, ambayo Bwana Mungu wenu anawapa kama urithi wenu, ili kwamba msije mkawa na hatia ya kumwaga damu.

1119:11 Kut 21:12; Hes 35:16; 1Yn 3:15; Mit 28:17; 29:10Lakini kama mtu anamchukia ndugu yake, akamvizia, akamshambulia na kumuua, kisha akakimbilia katika mmojawapo ya miji hii, 12wazee wa mji wake watatuma ujumbe kwake, kumleta kutoka mji ule na kumkabidhi mlipiza kisasi cha damu kumuua. 1319:13 Kum 7:2; 21:9; 1Fal 2:31Msimwonee huruma. Lazima mwondoe katika Israeli hatia ya umwagaji damu isiyo na hatia ili kwamba mpate kufanikiwa.

1419:14 Kum 27:17; Ay 24:2; Za 16:6; Mit 15:25; 22:28; 23:10; Isa 1:23; Hos 5:10Usisogeze jiwe la mpaka wa jirani yako ambao uliwekwa na wale waliokutangulia katika urithi upokeao katika nchi Bwana Mungu wako anayowapa kuimiliki.

Mashahidi

1519:15 Kum 17:6; Mt 18:16; 26:60; 2Kor 3:1; Yn 8:17; 1Tim 5:19; Ebr 10:28Shahidi mmoja hatoshi kumtia hatiani mtu kwa uhalifu au kosa lolote ambalo anaweza kuwa amelitenda. Lazima shauri lolote lithibitishwe kwa ushuhuda wa mashahidi wawili au watatu.

1619:16 Kut 23:1; Mit 6:19; Za 27:12; 1Fal 21:13Kama shahidi mwenye nia ya kumdhuru mwingine akisimama kumshtaki mtu kwa uhalifu, 1719:17 Kut 21:6; Kum 17:6watu wawili wanaohusika katika mabishano lazima wasimame mbele za Bwana na mbele ya makuhani na waamuzi ambao wako kazini wakati huo. 1819:18 Kut 23:7Waamuzi lazima wafanye uchunguzi kwa makini na shahidi akionekana kuwa ni mwongo, akitoa ushuhuda wa uongo dhidi ya ndugu yake, 1919:19 Mit 19:5-10; 1Kor 5:13; Dan 6:24basi mtende kama alivyotaka kumtendea ndugu yake. Ni lazima mwondoe uovu miongoni mwenu. 2019:20 Kum 13:11; 17:13; 13:13; 21:21Watu watakaosalia watasikia hili na kuogopa, uovu kama huo kamwe hautatendeka tena miongoni mwenu. 2119:21 Kut 21:24; Mt 5:38Msionyeshe huruma, uhai kwa uhai, jicho kwa jicho, jino kwa jino, mkono kwa mkono, mguu kwa mguu.

New International Reader’s Version

Deuteronomy 19:1-21

Cities to Run to for Safety

1The Lord your God will destroy the nations whose land he is giving you. You will drive them out. And you will make your homes in their towns and their houses. 2When you do, set apart for yourselves three cities in the land. It’s the land the Lord your God is giving you to take as your own. 3Figure out the distances and then separate the land into three parts. Then anyone who kills another person can run to one of these cities for safety. They are in the land the Lord your God is giving you as your own.

4Here is the rule about a person who kills someone. That person can run to one of those cities for safety. The rule applies to anyone who kills a neighbor they didn’t hate and didn’t mean to kill. 5For example, suppose a man goes into a forest with his neighbor to cut wood. When he swings his ax to chop down a tree, the head of the ax flies off. And it hits his neighbor and kills him. Then that man can run to one of those cities and save his life. 6If he doesn’t go to one of those cities, the dead man’s nearest male relative might become very angry. He might chase the man. If the city is too far away, he might catch him and kill him. But the man running to the city isn’t worthy of death, because he didn’t hate his neighbor. 7That’s why I command you to set apart for yourselves three cities.

8The Lord your God will increase the size of your territory. He promised your people of long ago that he would do it. He will give you the whole land he promised them. 9But he’ll do it only if you are careful to obey all the laws I’m commanding you today. I command you to love the Lord your God. You must always live as he wants you to live. Suppose you are careful to obey, and the Lord your God gives you more land. Then you must set apart three more cities. 10Do it to protect those not guilty of murder. Then you won’t spill their blood in your land. It’s the land the Lord your God is giving you as your own.

11But suppose a man hates his neighbor. So he hides and waits for him. Then he attacks him and kills him. And he runs to one of those cities for safety. 12If he does, the elders of his own town must send for him. He must be brought back from the city. He must be handed over to the dead man’s nearest male relative. Then the relative will kill him. 13Don’t feel sorry for him. He has killed someone who hadn’t done anything wrong. Crimes like that must be punished in Israel. Then things will go well with you.

14Don’t move your neighbor’s boundary stone. It was set up by people who lived there before you. It marks the border of a field in the land you will receive as your own. The Lord your God is giving you that land. You will take it over.

Witnesses

15Suppose someone is charged with committing a crime of any kind. Then one witness won’t be enough to prove that person is guilty. Every matter must be proved by the words of two or three witnesses.

16Suppose a witness who tells lies goes to court and brings charges against someone. The witness says someone committed a crime. 17Then the two people in the case must stand in front of the Lord. They must stand in front of the priests and the judges who are in office at that time. 18The judges must check out the matter carefully. And suppose the witness is proved to be lying. Then he has said something false in court against another Israelite. 19So do to the lying witness what he tried to do to the other person. Get rid of that evil witness. 20The rest of the people will hear about it. And they will be afraid. They won’t allow such an evil thing to be done among them again. 21Don’t feel sorry for that evil person. A life must be taken for a life. An eye must be put out for an eye. A tooth must be knocked out for a tooth. A hand must be cut off for a hand and a foot for a foot.