Kumbukumbu 19 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Kumbukumbu 19:1-21

Miji Ya Makimbilio

(Hesabu 35:9-34; Yoshua 20:1-9)

119:1 Kum 6:10-11; 12:29Wakati Bwana Mungu wenu atakapokuwa amewaangamiza mataifa ambayo nchi yao anawapa ninyi, wakati mtakapokuwa mmewafukuza na kuishi katika miji yao na nyumba zao, 219:2 Yos 20:2ndipo mtenge miji mitatu iliyopo katikati ya nchi kwa ajili yenu, katika nchi ambayo Bwana Mungu wenu anawapa kuimiliki. 3Jengeni barabara katika miji hiyo na kuigawa mara tatu, nchi anayowapa Bwana Mungu wenu kama urithi, ili kwamba yeyote amuuaye mtu aweze kukimbilia humo.

4Hii ndiyo kanuni kuhusu mtu amuuaye mwingine na kukimbilia humo kuokoa maisha yake, yaani, yeye amuuaye jirani yake bila kukusudia, wala hakumchukia kabla ya hapo. 5Kwa mfano, mtu aweza kwenda msituni na jirani yake kukata miti, naye anapozungusha shoka kuangusha mti, shoka linaweza kuchomoka kutoka kwenye mpini na kumpiga jirani yake na kumuua. Yule mtu anaweza kukimbilia katika mmojawapo ya miji hii na kuokoa maisha yake. 619:6 Hes 35:12Kama sivyo, mlipiza kisasi cha damu anaweza kumfuatilia kwa hasira kali, naye akamkamata na kumuua kama umbali ni mrefu sana hata ingawa hastahili kifo, kwa sababu amemuua jirani yake bila kukusudia. 7Hii ndiyo sababu nimewaagiza ninyi kutenga miji mitatu ya makimbilio kwa ajili yenu.

819:8 Kut 34:24; Mwa 15:18; Kum 11:24Kama Bwana Mungu wenu akipanua nchi yenu, kama alivyoahidi kwa kiapo kwa baba zenu na kuwapa nchi yote aliyowaahidi, 919:9 Kum 6:5; Yos 20:7-8kwa sababu mmefuata kwa uangalifu sheria zote ninazowaamuru leo, kumpenda Bwana Mungu wenu na kuenenda siku zote katika njia zake, ndipo mtenge miji mingine, mitatu zaidi. 1019:10 Mit 6:17; Yer 7:6; 26:15; Kum 21:1-9; Hes 35:33Fanyeni hivi ili damu isiyo na hatia isimwagwe katika nchi yenu, ambayo Bwana Mungu wenu anawapa kama urithi wenu, ili kwamba msije mkawa na hatia ya kumwaga damu.

1119:11 Kut 21:12; Hes 35:16; 1Yn 3:15; Mit 28:17; 29:10Lakini kama mtu anamchukia ndugu yake, akamvizia, akamshambulia na kumuua, kisha akakimbilia katika mmojawapo ya miji hii, 12wazee wa mji wake watatuma ujumbe kwake, kumleta kutoka mji ule na kumkabidhi mlipiza kisasi cha damu kumuua. 1319:13 Kum 7:2; 21:9; 1Fal 2:31Msimwonee huruma. Lazima mwondoe katika Israeli hatia ya umwagaji damu isiyo na hatia ili kwamba mpate kufanikiwa.

1419:14 Kum 27:17; Ay 24:2; Za 16:6; Mit 15:25; 22:28; 23:10; Isa 1:23; Hos 5:10Usisogeze jiwe la mpaka wa jirani yako ambao uliwekwa na wale waliokutangulia katika urithi upokeao katika nchi Bwana Mungu wako anayowapa kuimiliki.

Mashahidi

1519:15 Kum 17:6; Mt 18:16; 26:60; 2Kor 3:1; Yn 8:17; 1Tim 5:19; Ebr 10:28Shahidi mmoja hatoshi kumtia hatiani mtu kwa uhalifu au kosa lolote ambalo anaweza kuwa amelitenda. Lazima shauri lolote lithibitishwe kwa ushuhuda wa mashahidi wawili au watatu.

1619:16 Kut 23:1; Mit 6:19; Za 27:12; 1Fal 21:13Kama shahidi mwenye nia ya kumdhuru mwingine akisimama kumshtaki mtu kwa uhalifu, 1719:17 Kut 21:6; Kum 17:6watu wawili wanaohusika katika mabishano lazima wasimame mbele za Bwana na mbele ya makuhani na waamuzi ambao wako kazini wakati huo. 1819:18 Kut 23:7Waamuzi lazima wafanye uchunguzi kwa makini na shahidi akionekana kuwa ni mwongo, akitoa ushuhuda wa uongo dhidi ya ndugu yake, 1919:19 Mit 19:5-10; 1Kor 5:13; Dan 6:24basi mtende kama alivyotaka kumtendea ndugu yake. Ni lazima mwondoe uovu miongoni mwenu. 2019:20 Kum 13:11; 17:13; 13:13; 21:21Watu watakaosalia watasikia hili na kuogopa, uovu kama huo kamwe hautatendeka tena miongoni mwenu. 2119:21 Kut 21:24; Mt 5:38Msionyeshe huruma, uhai kwa uhai, jicho kwa jicho, jino kwa jino, mkono kwa mkono, mguu kwa mguu.

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

申命記 19:1-21

設立避難城

1「你們的上帝耶和華毀滅那些民族,把他們的土地賜給你們,使你們趕走他們,住進他們的城邑和房屋後, 2-3你們要把土地劃分為三個地區,在每個地區設立一座避難城,修好通往這三座城的道路,以便誤殺人者可以逃往最近的避難城。

4「如果有人無意間殺了素無冤仇的同伴,他可以逃往避難城,以保住性命。 5例如,有人和朋友去森林砍樹,斧頭脫柄,誤殺了朋友,他就可以逃往避難城,以保住性命。 6否則,如果避難城離誤殺人者太遠,怒火中燒的報仇者就會追上去殺死他。其實他是不該死的,因為他與被誤殺的人素無冤仇。 7因此,我吩咐你們要設立三座避難城。

8-9「如果你們謹遵我今天吩咐你們的這一切誡命,愛你們的上帝耶和華,一生遵行祂的旨意,祂就會按照祂對你們祖先所起的誓,擴張你們的疆域,把應許給你們祖先的土地賜給你們。那時,你們要再設三座避難城, 10免得無辜人的血流在你們的上帝耶和華賜給你們作產業之地,以致你們擔當枉殺無辜的罪。

11「如果有人因憎恨鄰居而暗中埋伏,殺了鄰居,然後逃到避難城, 12他本城的長老要派人去把他帶回來,交給復仇的人,將他處死。 13不可憐憫他,要從以色列除掉這種濫殺無辜的罪,這樣你們才會順利。

14「在你們的上帝耶和華將要賜給你們作產業之地,你們不可挪動鄰居的界石,因為那是先人立的。

15「如果人犯了什麼罪或有什麼過失,不可憑一個證人作證就定罪,要有兩三個證人才可以定案。 16如果有人作偽證誣陷別人, 17訴訟雙方要站在耶和華面前,讓當值的祭司和審判官定奪。 18審判官要仔細審查案件,如果發現那人作偽證, 19就要按照他企圖加給被誣告者的傷害處罰他。這樣,就從你們當中除掉了罪惡。 20其他人聽說後,都會害怕,不敢再做這種惡事。 21你們對惡人不可心軟,要以命償命,以眼還眼,以牙還牙,以手還手,以腳還腳。