Kumbukumbu 17 – NEN & HOF

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Kumbukumbu 17:1-20

117:1 Kut 12:5; Law 22:20; Kum 7:25; 15:21; Mal 1:8, 13Msimtolee Bwana Mungu wenu dhabihu ya maksai au kondoo ambaye ana dosari yoyote au hitilafu ndani yake, kwa kuwa hilo litakuwa chukizo kwake.

217:2 Kum 13:6-11Ikiwa mwanaume au mwanamke anayeishi kati ya mojawapo ya miji akupayo Bwana, anakutwa anafanya uovu mbele za Bwana Mungu wenu, kwa kuvunja Agano lake, 317:3 Yer 7:31; Kut 22:20; Mwa 1:16; 2:1; 37:9; Ay 31:26naye amekwenda kinyume na agizo langu kuabudu miungu mingine na kuisujudia, kama vile jua, mwezi au nyota za angani, 417:4 Kum 22:20; 13:12-14hili likiwa limeletwa mbele yenu, ni lazima kulichunguza kikamilifu. Ikiwa ni kweli na kuwa limehakikishwa kwamba hili ni chukizo lililofanyika katika Israeli, 517:5 Law 24:14mchukueni huyo mwanaume au mwanamke ambaye amelifanya tendo hili ovu kwenye lango la mji wenu na kumpiga mawe mtu huyo mpaka afe. 617:6 Hes 35:30; Kum 19:15; Mt 18:16; Yos 7:25; Yn 8:1717:6 Hes 35:30; Mt 18:16; Yn 8:17; 2Kor 13:1; 1Tim 5:19; Ebr 10:28Kwa ushuhuda wa mashahidi wawili au watatu mtu huyo atauawa, bali hakuna mtu atakayeuawa kwa ushuhuda wa shahidi mmoja tu. 717:7 Yn 8:7; Law 24:14; Mdo 7:58; Kum 13:5, 9; 1Kor 15:13Ni lazima kwanza mikono ya mashahidi itangulie kumuua huyo mtu, kisha mikono ya watu wote. Ni lazima mwondoe uovu miongoni mwenu.

Mahakama Za Sheria

817:8 Kut 21:6, 13; 2Nya 19:10; Kum 12:5; Za 122:3-5; Hag 2:11; Mal 2:7; Hes 35:11; Kum 19:17Kama mashauri yanaletwa katika mahakama zenu ambayo ni magumu zaidi kwenu kuyaamua, ikiwa ni umwagaji wa damu, madai au mashambulio, yapelekeni mahali ambapo Bwana Mungu wenu atapachagua. 917:9 Kum 24:8; 27:9; Kut 21:6; Mwa 25:22; Kum 19:17; Eze 44:24; Hag 2:11; Amu 4:5; 1Fal 3:16Nendeni kwa makuhani, ambao ni Walawi, na kwa mwamuzi ambaye atakuwa kazini wakati huo. Ulizeni kwao nao watawapa maamuzi. 10Ni lazima mtende sawasawa na maamuzi watakayowapa mahali Bwana atakapopachagua. Kuweni waangalifu kufanya kila kitu watakachowaongoza kufanya. 1117:11 Law 10:11; Kum 5:32; 25:1Fanyeni sawasawa na sheria wanayowafundisha na maamuzi wanayowapa. Msigeuke mkono wa kuume au kushoto kuacha kufanya yale wanayowaambia. 1217:12 Hes 15:30; 16:9-13; Mwa 17:14; Kum 13:11; 18:20; 19:20; 1Fal 18:40; Yer 14:14; Hos 4:4; Zek 13:3; Kum 13:5Mwanaume atakayeonyesha dharau kwa mwamuzi au kwa kuhani ambaye amewekwa kumtumikia Bwana Mungu wenu lazima auawe. Lazima mwondoe uovu katika Israeli. 1317:13 Kum 13:11Watu wote watasikia na kuogopa, nao hawatakuwa wenye kudharau tena.

Mfalme

1417:14 Hes 33:53; Yos 21:43; 1Sam 8:5-9; 19:20; 10:19Wakati utakapoingia katika nchi anayowapa Bwana Mungu wenu kuimiliki na kukaa humo, nanyi mkasema, “Na tumweke mfalme juu yetu kama mataifa yanayotuzunguka,” 1517:15 1Sam 16:3; 2Sam 5:3; Yer 30:21kuweni na uhakika wa kumweka mfalme juu yenu ambaye Bwana Mungu wenu atamchagua. Ni lazima atoke miongoni mwa ndugu zenu wenyewe. Msimweke mgeni juu yenu ambaye si ndugu wa Kiisraeli. 1617:16 Isa 2:7; 30:16; 1Sam 8:11; 1Fal 4:26; 9:19; 10:26; 2Nya 1:14; Za 20:7; Isa 31:1; Yer 42:14; 1Fal 10:28-29; Eze 17:15; Kut 13:17Hata hivyo, kamwe mfalme asijipatie hesabu kubwa ya farasi kwa ajili yake mwenyewe, au kuwafanya watu warudi Misri ili kupata farasi zaidi, kwa maana Bwana amekuambia, “Hamtairudia njia ile tena.” 1717:17 Kut 34:16; 2Sam 5:13; 12:11; 1Fal 11:3; 2Nya 11:21; Za 31:3Kamwe asioe wake wengi, la sivyo moyo wake utapotoka. Kamwe asijilimbikizie kiasi kikubwa cha fedha na dhahabu.

1817:18 2Fal 11:12; Kum 31:9; 2Fal 22:8Atakapokuwa amekalia kiti cha ufalme wake, ajiandikie kwenye kitabu nakala ya sheria kwa ajili yake mwenyewe kutoka zile sheria za makuhani ambao ni Walawi. 1917:19 Yos 8; Za 119:97Atakuwa na nakala hiyo, naye ataisoma siku zote za maisha yake ili kwamba ajifunze kumheshimu Bwana Mungu wake na kufuata kwa uangalifu maneno yote ya sheria hii na amri hizi, 2017:20 Kum 5:32naye asijifikirie kuwa ni bora kuliko ndugu zake na kuipotosha sheria. Ndipo yeye na wazao wake watatawala katika ufalme wake kwa muda mrefu katika Israeli.

Hoffnung für Alle

5. Mose 17:1-20

1Er verabscheut es auch, wenn ihr ihm kranke oder minderwertige Rinder, Schafe oder Ziegen opfert.

2-3Es kann geschehen, dass in einer der Städte, die der Herr, euer Gott, euch gibt, ein Mann oder eine Frau andere Götter verehren. Sie beten die Sonne, den Mond oder die Sterne an und widersetzen sich damit meinen Weisungen. Sie handeln gegen den Willen des Herrn und verletzen den Bund, den er mit uns geschlossen hat. 4Wenn ihr davon hört, dann forscht genau nach, ob es wahr ist. Stellt sich heraus, dass tatsächlich etwas so Abscheuliches in Israel geschehen ist, 5dann sollt ihr den Mann oder die Frau außerhalb der Stadt steinigen. 6Für ein Todesurteil sind jedoch mindestens zwei oder drei Zeugen nötig. Eine einzelne Aussage genügt nicht. 7Die Zeugen sollen die ersten Steine werfen, um den Verurteilten zu töten, danach sollen alle anderen ihn steinigen. Ihr müsst das Böse aus eurem Volk beseitigen!

Das oberste Gericht beim Heiligtum

8Wenn den Richtern in eurer Stadt ein Fall zu schwierig ist, dann kommt zum Heiligtum – ganz gleich ob es dabei um Tötung, Körperverletzung oder etwas anderes geht. 9Wendet euch dort an die Priester vom Stamm Levi und an den Richter, der gerade im Amt ist, und legt ihnen den Fall vor. Sie werden ein Urteil sprechen. 10Daran müsst ihr euch halten. Was sie dort entscheiden, wo der Herr wohnt, das gilt. 11Befolgt ihre Anweisungen und Vorschriften genau! Weicht in keiner Hinsicht davon ab!

12Wenn jemand so vermessen ist, dass er nicht auf den Richter oder den Priester hört, der im Auftrag des Herrn, eures Gottes, sein Amt ausübt, dann soll er getötet werden. Ihr müsst das Böse aus Israel beseitigen! 13Alle sollen davon hören, damit sie gewarnt sind und sich niemand mehr so etwas anmaßt.

Weisungen für den König

14Bald werdet ihr das Land in Besitz nehmen, das der Herr, euer Gott, euch geben will. Vielleicht werdet ihr dort eines Tages sagen: »Wir wollen einen König haben, so wie alle anderen Völker ringsum!« 15Dann ernennt aber nur den zum König, den der Herr, euer Gott, erwählt! Er soll aus eurem Volk stammen. Ihr dürft keinen Ausländer einsetzen, sondern nur einen Israeliten! 16Wenn er König geworden ist, soll er kein großes Reiterheer aufbauen. Er darf auch niemanden von euch nach Ägypten schicken, um von dort noch mehr Pferde zu bekommen. Denn der Herr hat euch verboten, nach Ägypten zurückzukehren. 17Euer König soll auch nicht viele Frauen haben, denn sie könnten ihn dazu verleiten, dem Herrn untreu zu werden. Er darf auch kein Gold und Silber anhäufen.

18Wenn er den Thron seines Reiches besteigt, soll er sich eine Abschrift von diesem Gesetz geben lassen,17,18 Oder: soll er sich eine Abschrift von diesem Gesetz machen. das bei den Priestern aus dem Stamm Levi aufbewahrt wird. 19Er muss sie immer bei sich haben und täglich darin lesen, solange er lebt. So soll er lernen, Ehrfurcht vor dem Herrn, seinem Gott, zu haben und alle Ordnungen dieses Gesetzes genau zu befolgen. 20Das wird ihn davor bewahren, sich für wichtiger zu halten als die anderen Menschen aus seinem Volk. Wenn er in keiner Hinsicht von diesen Geboten abweicht, werden er und seine Nachkommen lange Zeit in Israel Könige sein.