Kumbukumbu 14 – NEN & KJV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Kumbukumbu 14:1-29

Vyakula Vilivyo Najisi Na Vilivyo Safi

(Walawi 11:1-47)

114:1 Yn 1:12; Rum 8:14; 9:8; Yer 16:6; Mwa 6:2-4; Kut 4:22-23; Gal 3:26; 1The 4:13Ninyi ni watoto wa Bwana Mungu wenu. Msijichanje ama kujinyoa upara kwenye paji la uso kwa ajili ya aliyekufa, 214:2 Mwa 28:14; Kut 8:22; 22:31; Isa 6:13; Mt 2:15; Law 20:26; Rum 12:1; Kum 7:6; 26:18-1914:2 Kut 19:5; 2Sam 7:23, 24kwa maana ninyi ni taifa takatifu kwa Bwana Mungu wenu. Bwana amewachagua ninyi kuwa taifa la kipekee kutoka mataifa yote juu ya uso wa dunia, mwe tunu yake.

314:3 Eze 4:14; Isa 65:4; Mdo 10:13; Rum 14:14Msile kitu chochote ambacho ni machukizo. 414:4 Mdo 10:14; Law 7:23; 11:2-45Hawa ndio wanyama mtakaokula: ngʼombe, kondoo, mbuzi, 514:5 Kum 12:15; Ay 39:1; Za 104:18kulungu, paa, kongoni, paa mweupe, mbuzi-mwitu, pofu na kondoo wa mlimani. 6Mnaweza kumla mnyama yeyote mwenye kwato zilizogawanyika mara mbili, pia yule anayecheua. 7Hata hivyo, miongoni mwa wale wanaocheua au wale walio na kwato zilizogawanyika kamwe msile ngamia, sungura na pelele. Iwapo wanacheua, lakini hawana kwato zilizogawanyika; ni najisi kwenu kwa taratibu za kiibada. 814:8 Law 5:12; 11:26-27Nguruwe pia ni najisi; ingawa ana kwato zilizogawanyika, hacheui. Msile nyama yake wala kugusa mzoga wake.

9Katika viumbe hai vyote viishivyo kwenye maji, mnaweza kula yeyote aliye na mapezi na magamba. 10Lakini chochote kisicho na mapezi na magamba msile; kwenu ni najisi.

11Mnaweza kula ndege yeyote aliye safi. 1214:12 Law 11:13Lakini wafuatao msiwale: tai, furukombe, kipungu, 1314:13 Mwa 2:11; Isa 34:15kengewa mwekundu, kengewa mweusi, mwewe wa aina yoyote, 1414:14 Mwa 8:17kunguru wa aina yoyote, 15mbuni, kiruka-njia, dudumizi, kipanga wa aina yoyote, 16bundi, mumbi, bundi mkubwa, 1714:17 Za 102:6; Isa 13:21; 14:23; 34:11; Sef 2:14mwari, nderi, mnandi, 18korongo, koikoi wa aina yoyote, hudihudi na popo.

19Wadudu wote warukao kwa makundi ni najisi kwenu, msiwale. 2014:20 Law 20:25Lakini viumbe vyote vyenye mabawa vilivyo safi mwaweza kula.

2114:21 Law 11:39; 14:2; 17:15; Kut 23:19; 22:31; Law 22:8; Eze 44:31Msile kitu chochote mtakachokuta kimekufa. Mnaweza kumpa mgeni yeyote anayeishi katika mojawapo ya miji yenu, naye anaweza kula au mnaweza kumuuzia mtu wa nchi nyingine. Lakini ninyi ni watu watakatifu kwa Bwana Mungu wenu.

Msitokose mwana-mbuzi katika maziwa ya mama yake.

Zaka

2214:22 Mwa 14:20; Law 27:30; Hes 18:21; Neh 10:37; Kum 12:6, 17Hakikisheni mmetenga sehemu ya kumi ya mazao yote ya mashamba yenu kila mwaka. 2314:23 Kum 12:5, 17, 18; Za 4:7; 1Fal 3:2; Kum 4:10; Za 22:23; 33:8; Mal 2:5; Mit 3:13; Isa 8:13; Yer 32:38-41; Ebr 12:28Mtakula zaka za nafaka yenu, divai mpya, mafuta na wazaliwa wa kwanza wa makundi yenu ya ngʼombe na ya kondoo na mbuzi mbele za Bwana Mungu wenu pale mahali atakapopachagua kama maskani kwa ajili ya Jina lake, ili kwamba mpate kujifunza kumheshimu Bwana Mungu wenu daima. 2414:24 Kum 12:21Lakini ikiwa mahali pale ni mbali sana nanyi mmebarikiwa na Bwana Mungu wenu na hamwezi kubeba zaka yenu (kwa sababu mahali pale Bwana atakapopachagua kuliweka Jina lake ni mbali sana), 2514:25 Mt 21:12; Yn 2:14basi badilisheni zaka yenu kuwa fedha, mkaichukue hiyo fedha mwende nayo mahali Bwana Mungu wenu atakapopachagua. 2614:26 Law 10:9; 23:40; Mhu 10:16-17; Kum 12:7-8Tumieni hiyo fedha kununua chochote ukitakacho: ngʼombe, kondoo, divai au kinywaji chochote chenye chachu au chochote mnachotaka. Kisha ninyi na wa nyumbani mwenu mtaila mbele za Bwana Mungu wenu na kufurahi. 2714:27 Kum 12:19; Hes 18:20; 26:62; Kum 18:1-2; Rum 13:4; 15:27; 1Kor 9:1-14Msiache kuwajali Walawi waishio katika miji yenu, kwa kuwa hao hawana shamba wala urithi wao wenyewe.

2814:28 Law 27:30; Kum 26:12Mwishoni mwa kila mwaka wa tatu, leteni zaka zote za mazao ya miaka ile na uyahifadhi kwenye miji yenu, 2914:29 Mwa 47:22; Hes 26:62; Kum 16:11; 24:19-21; Za 94:6; Isa 1:17; 58:6; Kum 6:11; 15:10; Za 41:1; Mit 22:9; Mt 3:10; Kum 10:18; Eze 22:7, 29; Lk 14:12; Ebr 13:2; Mal 3:10; Lk 11:41; 2Kor 9:6-11ili Walawi (ambao hawana mashamba wala urithi wao wenyewe) na wageni, yatima na wajane wanaoishi kwenye miji yenu wapate kuja kula na kushiba, ili Bwana Mungu wenu apate kuwabariki ninyi katika kazi zote za mikono yenu.

King James Version

Deuteronomy 14:1-29

1Ye are the children of the LORD your God: ye shall not cut yourselves, nor make any baldness between your eyes for the dead. 2For thou art an holy people unto the LORD thy God, and the LORD hath chosen thee to be a peculiar people unto himself, above all the nations that are upon the earth.

3¶ Thou shalt not eat any abominable thing. 4These are the beasts which ye shall eat: the ox, the sheep, and the goat, 5The hart, and the roebuck, and the fallow deer, and the wild goat, and the pygarg, and the wild ox, and the chamois.14.5 pygarg: or bison: Heb. dishon 6And every beast that parteth the hoof, and cleaveth the cleft into two claws, and cheweth the cud among the beasts, that ye shall eat. 7Nevertheless these ye shall not eat of them that chew the cud, or of them that divide the cloven hoof; as the camel, and the hare, and the coney: for they chew the cud, but divide not the hoof; therefore they are unclean unto you. 8And the swine, because it divideth the hoof, yet cheweth not the cud, it is unclean unto you: ye shall not eat of their flesh, nor touch their dead carcase.

9¶ These ye shall eat of all that are in the waters: all that have fins and scales shall ye eat: 10And whatsoever hath not fins and scales ye may not eat; it is unclean unto you.

11Of all clean birds ye shall eat. 12But these are they of which ye shall not eat: the eagle, and the ossifrage, and the ospray, 13And the glede, and the kite, and the vulture after his kind, 14And every raven after his kind, 15And the owl, and the night hawk, and the cuckow, and the hawk after his kind, 16The little owl, and the great owl, and the swan, 17And the pelican, and the gier eagle, and the cormorant, 18And the stork, and the heron after her kind, and the lapwing, and the bat. 19And every creeping thing that flieth is unclean unto you: they shall not be eaten. 20But of all clean fowls ye may eat.

21¶ Ye shall not eat of any thing that dieth of itself: thou shalt give it unto the stranger that is in thy gates, that he may eat it; or thou mayest sell it unto an alien: for thou art an holy people unto the LORD thy God. Thou shalt not seethe a kid in his mother’s milk.

22Thou shalt truly tithe all the increase of thy seed, that the field bringeth forth year by year. 23And thou shalt eat before the LORD thy God, in the place which he shall choose to place his name there, the tithe of thy corn, of thy wine, and of thine oil, and the firstlings of thy herds and of thy flocks; that thou mayest learn to fear the LORD thy God always. 24And if the way be too long for thee, so that thou art not able to carry it; or if the place be too far from thee, which the LORD thy God shall choose to set his name there, when the LORD thy God hath blessed thee: 25Then shalt thou turn it into money, and bind up the money in thine hand, and shalt go unto the place which the LORD thy God shall choose: 26And thou shalt bestow that money for whatsoever thy soul lusteth after, for oxen, or for sheep, or for wine, or for strong drink, or for whatsoever thy soul desireth: and thou shalt eat there before the LORD thy God, and thou shalt rejoice, thou, and thine household,14.26 desireth: Heb. asketh of thee 27And the Levite that is within thy gates; thou shalt not forsake him; for he hath no part nor inheritance with thee.

28¶ At the end of three years thou shalt bring forth all the tithe of thine increase the same year, and shalt lay it up within thy gates: 29And the Levite, (because he hath no part nor inheritance with thee,) and the stranger, and the fatherless, and the widow, which are within thy gates, shall come, and shall eat and be satisfied; that the LORD thy God may bless thee in all the work of thine hand which thou doest.