Kumbukumbu 14 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Kumbukumbu 14:1-29

Vyakula Vilivyo Najisi Na Vilivyo Safi

(Walawi 11:1-47)

114:1 Yn 1:12; Rum 8:14; 9:8; Yer 16:6; Mwa 6:2-4; Kut 4:22-23; Gal 3:26; 1The 4:13Ninyi ni watoto wa Bwana Mungu wenu. Msijichanje ama kujinyoa upara kwenye paji la uso kwa ajili ya aliyekufa, 214:2 Mwa 28:14; Kut 8:22; 22:31; Isa 6:13; Mt 2:15; Law 20:26; Rum 12:1; Kum 7:6; 26:18-1914:2 Kut 19:5; 2Sam 7:23, 24kwa maana ninyi ni taifa takatifu kwa Bwana Mungu wenu. Bwana amewachagua ninyi kuwa taifa la kipekee kutoka mataifa yote juu ya uso wa dunia, mwe tunu yake.

314:3 Eze 4:14; Isa 65:4; Mdo 10:13; Rum 14:14Msile kitu chochote ambacho ni machukizo. 414:4 Mdo 10:14; Law 7:23; 11:2-45Hawa ndio wanyama mtakaokula: ngʼombe, kondoo, mbuzi, 514:5 Kum 12:15; Ay 39:1; Za 104:18kulungu, paa, kongoni, paa mweupe, mbuzi-mwitu, pofu na kondoo wa mlimani. 6Mnaweza kumla mnyama yeyote mwenye kwato zilizogawanyika mara mbili, pia yule anayecheua. 7Hata hivyo, miongoni mwa wale wanaocheua au wale walio na kwato zilizogawanyika kamwe msile ngamia, sungura na pelele. Iwapo wanacheua, lakini hawana kwato zilizogawanyika; ni najisi kwenu kwa taratibu za kiibada. 814:8 Law 5:12; 11:26-27Nguruwe pia ni najisi; ingawa ana kwato zilizogawanyika, hacheui. Msile nyama yake wala kugusa mzoga wake.

9Katika viumbe hai vyote viishivyo kwenye maji, mnaweza kula yeyote aliye na mapezi na magamba. 10Lakini chochote kisicho na mapezi na magamba msile; kwenu ni najisi.

11Mnaweza kula ndege yeyote aliye safi. 1214:12 Law 11:13Lakini wafuatao msiwale: tai, furukombe, kipungu, 1314:13 Mwa 2:11; Isa 34:15kengewa mwekundu, kengewa mweusi, mwewe wa aina yoyote, 1414:14 Mwa 8:17kunguru wa aina yoyote, 15mbuni, kiruka-njia, dudumizi, kipanga wa aina yoyote, 16bundi, mumbi, bundi mkubwa, 1714:17 Za 102:6; Isa 13:21; 14:23; 34:11; Sef 2:14mwari, nderi, mnandi, 18korongo, koikoi wa aina yoyote, hudihudi na popo.

19Wadudu wote warukao kwa makundi ni najisi kwenu, msiwale. 2014:20 Law 20:25Lakini viumbe vyote vyenye mabawa vilivyo safi mwaweza kula.

2114:21 Law 11:39; 14:2; 17:15; Kut 23:19; 22:31; Law 22:8; Eze 44:31Msile kitu chochote mtakachokuta kimekufa. Mnaweza kumpa mgeni yeyote anayeishi katika mojawapo ya miji yenu, naye anaweza kula au mnaweza kumuuzia mtu wa nchi nyingine. Lakini ninyi ni watu watakatifu kwa Bwana Mungu wenu.

Msitokose mwana-mbuzi katika maziwa ya mama yake.

Zaka

2214:22 Mwa 14:20; Law 27:30; Hes 18:21; Neh 10:37; Kum 12:6, 17Hakikisheni mmetenga sehemu ya kumi ya mazao yote ya mashamba yenu kila mwaka. 2314:23 Kum 12:5, 17, 18; Za 4:7; 1Fal 3:2; Kum 4:10; Za 22:23; 33:8; Mal 2:5; Mit 3:13; Isa 8:13; Yer 32:38-41; Ebr 12:28Mtakula zaka za nafaka yenu, divai mpya, mafuta na wazaliwa wa kwanza wa makundi yenu ya ngʼombe na ya kondoo na mbuzi mbele za Bwana Mungu wenu pale mahali atakapopachagua kama maskani kwa ajili ya Jina lake, ili kwamba mpate kujifunza kumheshimu Bwana Mungu wenu daima. 2414:24 Kum 12:21Lakini ikiwa mahali pale ni mbali sana nanyi mmebarikiwa na Bwana Mungu wenu na hamwezi kubeba zaka yenu (kwa sababu mahali pale Bwana atakapopachagua kuliweka Jina lake ni mbali sana), 2514:25 Mt 21:12; Yn 2:14basi badilisheni zaka yenu kuwa fedha, mkaichukue hiyo fedha mwende nayo mahali Bwana Mungu wenu atakapopachagua. 2614:26 Law 10:9; 23:40; Mhu 10:16-17; Kum 12:7-8Tumieni hiyo fedha kununua chochote ukitakacho: ngʼombe, kondoo, divai au kinywaji chochote chenye chachu au chochote mnachotaka. Kisha ninyi na wa nyumbani mwenu mtaila mbele za Bwana Mungu wenu na kufurahi. 2714:27 Kum 12:19; Hes 18:20; 26:62; Kum 18:1-2; Rum 13:4; 15:27; 1Kor 9:1-14Msiache kuwajali Walawi waishio katika miji yenu, kwa kuwa hao hawana shamba wala urithi wao wenyewe.

2814:28 Law 27:30; Kum 26:12Mwishoni mwa kila mwaka wa tatu, leteni zaka zote za mazao ya miaka ile na uyahifadhi kwenye miji yenu, 2914:29 Mwa 47:22; Hes 26:62; Kum 16:11; 24:19-21; Za 94:6; Isa 1:17; 58:6; Kum 6:11; 15:10; Za 41:1; Mit 22:9; Mt 3:10; Kum 10:18; Eze 22:7, 29; Lk 14:12; Ebr 13:2; Mal 3:10; Lk 11:41; 2Kor 9:6-11ili Walawi (ambao hawana mashamba wala urithi wao wenyewe) na wageni, yatima na wajane wanaoishi kwenye miji yenu wapate kuja kula na kushiba, ili Bwana Mungu wenu apate kuwabariki ninyi katika kazi zote za mikono yenu.

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

申命記 14:1-29

做聖潔的子民

1「你們是你們上帝耶和華的兒女,不可為死人割傷自己或剃光前額。 2因為你們是屬於你們的上帝耶和華的聖潔子民,祂從天下萬族中揀選你們作祂寶貴的產業。

3「你們不可吃任何可憎之物。 4但你們可以吃牛、綿羊、山羊、 5鹿、瞪羚、野山羊、野綿羊和羚羊。 6凡蹄子分瓣且反芻的動物,你們都可以吃。 7在那些只是反芻或只是蹄子分瓣的動物中,你們不可吃駱駝、野兔和獾,因為牠們反芻但蹄子不分瓣,是不潔淨的。 8你們也不可吃豬,因為豬雖蹄子分瓣但不反芻,是不潔淨的。你們不可吃這些動物的肉,也不可摸牠們的屍體。

9「水族中,凡有鱗和鰭的,你們都可以吃。 10凡無鱗和鰭的都不潔淨,你們不可吃。

11「你們可以吃潔淨的鳥類。 12不可吃的鳥類有鵰、胡兀鷲、黑禿鷲、 13鳶、隼類、 14烏鴉類、 15駝鳥、夜鷹、海鷗、鷹類、 16小鴞、大鴞、倉鴞、 17鵜鶘、魚鷹、鸕鷀、 18鸛、鷺鳥類、戴鵀和蝙蝠。

19「凡有翅膀、會爬的昆蟲都不潔淨,你們不可吃。 20凡有翅膀的潔淨之物,你們都可以吃。

21「你們不可吃死掉的動物,但可以送給或賣給住在你們城裡的外族人吃。因為你們屬於你們的上帝耶和華,是聖潔的民族。你們不可用母山羊的奶煮牠的羊羔。

十一奉獻

22「你們每年要獻出收成的十分之一; 23要在你們的上帝耶和華選定的敬拜場所,在祂面前吃所獻的十分之一的穀物、新酒、油以及頭生的牛羊。這是為了讓你們學習一生敬畏你們的上帝耶和華。 24如果你們的上帝耶和華賜福你們,使你們豐收,而你們住的地方離祂選定的敬拜場所太遠,以致不能把收成的十分之一送去, 25就可以把那些收成換成銀錢帶去。 26在那裡,你們可以隨意買牛、羊、淡酒或烈酒,然後一家人在你們的上帝耶和華面前吃喝快樂。 27不可忘記住在你們城裡的利未人,因為利未人沒有分到土地作產業。

28「每逢第三年末,你們要把那年所有出產的十分之一拿出來,存放在你們的城裡, 29讓你們城中沒有土地的利未人、寄居者和孤兒寡婦都可以來吃飽。這樣,你們的上帝耶和華必使你們凡事蒙福。