Kumbukumbu 12 – NEN & NIRV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Kumbukumbu 12:1-32

Mahali Pekee Pa Kuabudia

112:1 Za 119:5; Kum 4:9-10; 6:15; 1Fal 8:40; Eze 20:19; Gal 6:9Hizi ndizo amri na sheria ambazo ni lazima mwe waangalifu kuzifuata katika nchi ambayo Bwana, Mungu wa baba zenu, amewapa kumiliki, kwa muda wote mtakaoishi katika nchi. 212:2 Hes 21:28; 1Fal 14:23; 2Fal 17:10; Isa 57:5; Yer 2:20; 3:6-13; Kut 34:33Haribuni kabisa kila mahali pao pa kuabudia kwenye milima mirefu, vilima na chini ya kila mti mkubwa ambamo mataifa haya mnayokwenda kuchukua ardhi yao huabudia miungu yao. 312:3 2Fal 11:8; Kut 32:20; 34:13; 1Fal 14:15; Hes 33:53; Kut 23:13; Amu 2:2; Za 16:4; Zek 13:2Bomoeni madhabahu zao, vunjeni yale mawe wanayoabudu, chomeni moto nguzo zao za Ashera; katilieni mbali sanamu za miungu yao na mfute majina yao mahali hapo.

412:4 2Fal 17:15; Yer 10:2Kamwe msimwabudu Bwana Mungu wenu kama wanavyoabudu wao. 512:5 Kut 20:24; 2Sam 7:13; Kum 14:23; 15:20; 16:2, 11; 18:6; 26:2; 1Sam 2:29; 1Fal 1:5; 5; 8:16; 9:3; 2Nya 2:4; 6:6; 7:12-16; Ezr 6:12; 7:15; Za 26:8; 78:68; Zek 2:12Bali mtatafuta mahali Bwana Mungu wenu atakapopachagua katika makabila yenu yote ili aliweke jina lake huko kuwa makao yake. Mahali hapo ndipo iwapasapo kwenda; 612:6 Law 27:30; Mwa 28:20; Yos 22:27; Isa 66:20; Kum 14:22hapo ndipo mtakapoleta sadaka zenu za kuteketezwa na dhabihu, zaka zenu na changizo zenu, kile ulichoweka nadhiri kutoa, sadaka zenu za hiari na malimbuko ya makundi yenu ya ngʼombe pamoja na mbuzi na kondoo. 712:7 Kut 18:12; Mhu 3:12-13; Law 23:40; Isa 62:9Hapo, katika uwepo wa Bwana Mungu wenu, ninyi pamoja na jamaa zenu, mtakula na kufurahia kila kitu ambacho mmegusa kwa mikono yenu, kwa sababu Bwana Mungu wenu amewabariki.

812:8 Amu 17:6; 21:25Msifanye kama tunavyofanya hapa leo, kila mtu anavyopenda mwenyewe, 912:9 Kut 33:14; Kum 3:20; Za 95:11; Mik 2:10; Kum 4:21kwa kuwa bado hamjafikia mahali pa mapumziko na urithi ambao Bwana Mungu wenu anawapa. 1012:10 Kum 11:31; Kut 33:14; Law 1:3; Yos 22:23Lakini mtavuka Yordani na kuishi katika nchi Bwana Mungu wenu anayowapa kama urithi, naye atawapa pumziko kutokana na adui zenu wote wanaowazunguka ili ninyi mpate kuishi kwa salama. 1112:11 Kum 14:23; 15:20; 16:2; Yos 18:1; 1Fal 8:29; Za 78:68; 87:2Kisha kuhusu mahali Bwana Mungu wenu atakapopachagua kuwa mahali pa makao ya Jina lake, hapo ndipo inapowapasa kuleta kila kitu ninachowaamuru: sadaka zenu za kuteketezwa na dhabihu, zaka zenu na changizo, pamoja na vitu vyote vyenye thamani ambavyo mmeweka nadhiri kumtolea Bwana. 1212:12 Kum 26:11-13; 18:20; 9:10; 10:9; 14:29Hapo furahini mbele za Bwana Mungu wenu, ninyi, wana wenu na binti zenu, watumishi wenu wa kiume na wa kike, pamoja na Walawi kutoka miji yenu ambao hawana mgawo wala urithi wao wenyewe. 1312:13 Law 17:4Kuweni waangalifu, msitoe dhabihu zenu za kuteketezwa mahali popote mnapopapenda. 14Mtazitoa tu mahali pale ambapo Bwana atachagua katika mojawapo ya makabila yenu, nanyi hapo zingatieni kila jambo ninalowaamuru.

1512:15 Kum 14:5; 15:22; Mwa 9:3Hata hivyo, mnaweza kuwachinja wanyama wenu katika miji yenu yoyote ile na kula nyama nyingi mpendavyo kama vile mmemchinja paa au kulungu, kulingana na baraka mtakazojaliwa na Bwana Mungu wenu. Watu walio najisi au walio safi wanaweza kula. 1612:16 Mwa 9:4; Mdo 15:20; Mwa 35:14; 1Nya 11:18; Yer 7:18; Law 17:13; Kum 15:23; Yn 19:34; Law 7:26Lakini kamwe usinywe damu; imwage juu ya ardhi kama maji. 1712:17 Law 27:30; Hes 18:12-19; Kum 14:23; 15:20Hamruhusiwi kula katika miji yenu zaka yenu ya nafaka, ya divai mpya na ya mafuta, au mzaliwa wa kwanza wa makundi yenu ya ngʼombe na makundi yenu ya mbuzi na kondoo, wala chochote ambacho mmeweka nadhiri kukitoa, au sadaka zako za hiari, wala matoleo maalum. 1812:18 Kum 14:23; 15:20; 14:26; Neh 8:10; Mhu 3:12-13; 5:18-20Badala yake, mtakula vitu hivyo katika uwepo wa Bwana Mungu wenu mahali ambapo Bwana Mungu wenu atapachagua: wewe, wana wako na binti zako, watumishi wako wa kiume na wa kike, na Walawi kutoka miji yenu. Mnatakiwa mfurahi mbele za Bwana Mungu wenu kwa kula kitu mtakachoweka mikono yenu. 1912:19 Kum 14:27; Neh 13:10; Mal 3:8Mwe waangalifu msiwapuuze Walawi kwa muda wote mnaoishi katika nchi yenu.

2012:20 Kut 34:24; Mwa 15:8, 18; Kum 11:24; Kut 16:3Bwana Mungu wenu atakapokuwa ameongeza nchi yenu kama alivyowaahidi, nanyi mkitamani nyama na mkisema, “Ningependa nyama,” hapo unaweza kula nyingi upendavyo. 2112:21 Kum 14:24; Law 17:4Kama mahali ambapo Bwana Mungu wenu atapachagua kuweka Jina lake ni mbali sana kutoka kwenu, unaweza kuchinja wanyama kutoka makundi yenu ya ngʼombe, ya mbuzi na ya kondoo ambayo Bwana amewapa, kama nilivyokuamuru, na mkiwa katika miji yenu wenyewe mnaweza kula nyingi mtakavyo. 22Mle kama vile mngekula paa na kulungu. Wote walio najisi kiibada na walio safi mwaweza kula. 2312:23 Law 7:26; Eze 33:25; Mwa 9:4; Law 17:11, 14Lakini hakikisheni kwamba hamkunywa damu, kwa sababu damu ni uhai, kamwe msile uhai pamoja na nyama. 24Hamruhusiwi kamwe kunywa damu; imwageni juu ya ardhi kama maji. 2512:25 Kum 4:40; Kut 15:26; Kum 13:18; 1Fal 11:38; 2Fal 12:2; Isa 3:10Msinywe damu, ili mweze kufanikiwa ninyi pamoja na watoto wenu baada yenu, kwa sababu mtakuwa mkifanya lililo haki machoni pa Bwana.

2612:26 Hes 5:9-10; 18:19Lakini vichukueni vitu vyenu vilivyowekwa wakfu pamoja na vile mlivyoweka nadhiri, mwende mahali pale Bwana atakapopachagua. 2712:27 Law 1:13; 3:1-17Leteni sadaka zenu za kuteketezwa juu ya madhabahu ya Bwana Mungu wenu, vyote nyama na damu. Damu ya dhabihu zenu lazima imiminwe kando ya madhabahu ya Bwana Mungu wenu, lakini nyama mnaweza kula. 2812:28 Kum 4:40; Mhu 8:12; Za 25:12, 13; Mit 1:33; 3:1-4Mwe waangalifu kutii masharti haya yote ninayowapa, ili kwamba siku zote mweze kufanikiwa, ninyi pamoja na watoto wenu baada yenu, kwa sababu mtakuwa mkifanya lililo jema na sahihi mbele za macho ya Bwana Mungu wenu.

2912:29 Yos 23:4; Kum 6:10; Kut 23:23; Yos 23:4; Za 78:55Bwana Mungu wenu atayakatilia mbali mbele yenu mataifa ambayo punde kidogo mtayavamia na kuyaondoa. Lakini mtakapokuwa mmeyafukuza na kuishi katika nchi yao, 3012:30 Kut 10:7na baada ya kuangamizwa mbele yenu, mwe waangalifu msijiingize katika tanzi kwa kuuliza habari za miungu yao, mkisema, “Je, mataifa haya hutumikiaje miungu yao? Nasi tutafanya vivyo hivyo.” 3112:31 Law 18:25; 2Fal 3:27; Kum 9:5; Yer 32:35; 2Fal 17:15; 2Nya 33:2; 36:14Kamwe msimwabudu Bwana Mungu wenu kwa njia wanayoabudu miungu yao, kwa sababu katika kuabudu miungu yao, wanafanya aina zote za machukizo anayoyachukia Bwana. Hata huwateketeza wana wao na binti zao kwa moto kama kafara kwa miungu yao.

3212:32 Kum 4:2; Ufu 22:18-19; Yos 1:7; Mit 30:6Angalieni kwamba mnafanya yote niliyowaamuru; msiongeze kitu wala msipunguze kitu.

New International Reader’s Version

Deuteronomy 12:1-32

Worship Only Where the Lord Wants You To

1Here are the rules and laws you must obey. Be careful to obey them in the land the Lord has given you to take as your own. He’s the God of your people who lived long ago. Obey these rules and laws as long as you live in the land. 2You will soon drive the nations out of it. Completely destroy all the places where they worship their gods. Destroy them on the high mountains, on the hills and under every green tree. 3Break down their altars. Smash their sacred stones. Burn up the poles they use to worship the female god named Asherah. Cut down the statues of their gods. Wipe out the names of their gods from those places.

4You must not worship the Lord your God the way those nations worship their gods. 5Instead, go to the special place he will choose from among all your tribes. He will put his Name there. That’s where you must go. 6Take your burnt offerings and sacrifices to that place. Bring your special gifts and a tenth of everything you produce. Take with you what you have promised to give. Bring any other offerings you choose to give. And bring the male animals among your livestock that were born first to their mothers. 7You and your families will eat at the place the Lord your God will choose. He will be with you there. You will find joy in everything you have done. That’s because he has blessed you.

8You must not do as we’re doing here today. All of us are doing only what we think is right. 9That’s because you haven’t yet reached the place the Lord is giving you. Your God will give you peace and rest there. 10But first you will go across the Jordan River. You will settle in the land he’s giving you. It will belong to you as your share. He will give you peace and rest from all your enemies around you. You will live in safety. 11The Lord your God will choose a special place. He will put his Name there. That’s where you must bring everything I command you to bring. That includes your burnt offerings and sacrifices. It includes your special gifts and a tenth of everything you produce. It also includes all the things of value that you promised to give to the Lord. 12Be filled with joy there in the sight of the Lord your God. Your children should also be joyful. So should your male and female servants. And so should the Levites from your towns. The Levites won’t receive any part of the land as their share. 13Be careful not to sacrifice your burnt offerings anywhere you want to. 14Offer them only at the place the Lord will choose in one of your tribes. There you must obey everything I command you.

15But you can kill your animals in any of your towns. You can eat as much of the meat as you want to. You can eat it as if it were antelope or deer meat. That is part of the blessing the Lord your God is giving you. Those who are “clean” and those who are not can eat it. 16But you must not eat meat that still has blood in it. Pour the blood out on the ground like water. 17Here are the things you must not eat in your own towns. You must not eat the tenth part of your grain, olive oil and fresh wine. It belongs to the Lord. You must not eat the male animals among your livestock that were born first to their mothers. Don’t eat anything you have promised to give. Don’t eat any offerings you have chosen to give. And you must not eat any of your special gifts. 18Instead, you must eat all those things in the sight of the Lord your God. Do it at the place he will choose. You, your children, your male and female servants and the Levites from your towns can eat them. Be filled with joy in the sight of the Lord your God. Be joyful in everything you do. 19Don’t forget to take care of the Levites as long as you live in your land.

20The Lord your God will increase your territory, just as he has promised you. When he does, you might get hungry for meat. You might say, “I’d really like some meat.” Then you can eat as much of it as you want to. 21The Lord your God will choose a special place. He will put his Name there. But suppose that place is too far away from you. Then you can kill animals from the herds and flocks the Lord has given you. Do it just as I have commanded you. In your own towns you can eat as much of the meat as you want to. 22Eat it as you would eat antelope or deer meat. Those who are “clean” and those who are not can eat it. 23But be sure you don’t eat meat that still has blood in it. The blood is the animal’s life. So you must not eat the life along with the meat. 24You must not eat the blood. Pour it out on the ground like water. 25Don’t eat it. Then things will go well with you and your children after you. You will be doing what is right in the eyes of the Lord.

26But go to the place the Lord will choose. Take with you the things you have set apart for him. Bring what you have promised to give him. 27Sacrifice your burnt offerings on the altar of the Lord your God. Offer the meat and the blood there. The blood of your sacrifices must be poured out beside his altar. But you can eat the meat. 28Make sure you obey all the rules I’m giving you. Then things will always go well with you and your children after you. That’s because you will be doing what is good and right in the eyes of the Lord your God.

29You are about to attack the land and take it over as your own. When you do, the Lord your God will destroy the nations who live there. He will do it to make room for you. You will drive them out. You will settle in their land. 30They will be destroyed to make room for you. But when they are destroyed, be careful. Don’t be trapped. Don’t ask questions about their gods. Don’t say, “How do these nations serve their gods? We’ll do it in the same way.” 31You must not worship the Lord your God the way they worship their gods. When they worship, they do all kinds of evil things the Lord hates. They even burn up their children in the fire as sacrifices to their gods.

32Be sure you do everything I am commanding you to do. Do not add anything to my commands. And do not take anything away from them.