Isaya 8 – NEN & KJV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Isaya 8:1-22

Ashuru, Chombo Cha Bwana

18:1 Kum 27:8; Ay 19:23; Yer 20:3; 51:60; Isa 30:8; 8:3; Hos 1:4Bwana akaniambia, “Chukua gombo kubwa, uandike juu yake kwa kalamu ya kawaida jina: Maher-Shalal-Hash-Bazi.8:1 Maher-Shalal-Hash-Bazi maana yake ni Haraka kuteka nyara, Upesi kwenye hizo nyara. 28:2 2Fal 16:10; Yos 24:22; Rut 4:9; Yer 10:10-12; 32:10Nami nitawaita kuhani Uria, na Zekaria mwana wa Yeberekia kama mashahidi wangu waaminifu.”

38:3 Kut 15:20; Mwa 3:15Kisha nikaenda kwa nabii mke, naye akapata mimba, akazaa mwana. Kisha Bwana akaniambia, “Mwite huyo mtoto Maher-Shalal-Hash-Bazi. 48:4 Isa 7:8, 16; Mwa 14:15; Isa 7:8Kabla mtoto hajaweza kusema ‘Baba yangu’ au ‘Mama yangu,’ utajiri wa Dameski na nyara za Samaria zitachukuliwa na mfalme wa Ashuru.”

5Bwana akasema nami tena:

68:6 Neh 3:15; Isa 5:24; 7:1; Yn 9:7“Kwa sababu watu hawa wamekataa maji ya Shilo yatiririkayo taratibu

wakamfurahia Resini na mwana wa Remalia,

78:7 Isa 7:20; Dan 11:40; Nah 1:8; 2Nya 28:20; Isa 17:12-13; 30:28; Yos 3:15; Isa 10:16kwa hiyo Bwana yu karibu kuleta dhidi yao

mafuriko makubwa ya Mto:8:7 Yaani Frati.

yaani mfalme wa Ashuru na fahari yake yote.

Yatafurika juu ya mifereji yake yote,

yatamwagikia juu ya kingo zake zote,

88:8 Isa 7:14; 28:15; 18:6; 46:11; Yer 4:13; 48:40na kufika hadi Yuda, yakizunguka kwa kasi juu yake,

yakipita katikati na yakifika hadi shingoni.

Mabawa yake yaliyokunjuliwa

yatafunika upana wa nchi yako,

Ee Imanueli!”8:8 Imanueli maana yake Mungu yu pamoja nasi.

98:9 Isa 17:12-13; Eze 38:7; 38:3; Zek 14:2-3; Ay 34:24; Yer 46:3; 6:4; Zek 14:2; Yos 6:5Inueni kilio cha vita, enyi mataifa,

na mkavunjwevunjwe!

Sikilizeni, enyi nyote nchi za mbali.

Jiandaeni kwa vita, nanyi mkavunjwevunjwe!

Jiandaeni kwa vita, nanyi mkavunjwevunjwe!

108:10 Ay 5:12; Isa 7:7, 14; Rum 8:31; Mit 19:21; Mt 1:23Wekeni mikakati yenu, lakini itashindwa;

fanyeni mipango yenu, lakini haitafanikiwa,

kwa maana Mungu yu pamoja nasi.8:10 Kiebrania ni Imanueli.

Mwogope Mungu

118:11 Eze 3:14; 2:8; 1:3Bwana alisema nami mkono wake wenye nguvu ukiwa juu yangu, akinionya nisifuate njia za taifa hili. Akasema:

128:12 Isa 36:6; 7:2; 20:5; 1Pet 3:14; Mt 10:28“Usiite fitina kila kitu ambacho watu hawa hukiita fitina,

usiogope kile wanachokiogopa,

wala usikihofu.

138:13 Hes 20:12; Isa 29:23; Kut 20:20Bwana Mwenye Nguvu Zote ndiye peke yake

ikupasaye kumheshimu kuwa mtakatifu,

ndiye peke yake utakayemwogopa,

ndiye peke yake utakayemhofu,

148:14 Rum 9:33; Eze 11:16; Isa 24:17-18; Za 118:22; Yer 6:21; Lk 2:34; Isa 4:6; Lk 20:18; Eze 3:20naye atakuwa mahali patakatifu;

lakini kwa nyumba zote mbili za Israeli atakuwa

jiwe lile linalosababisha watu kujikwaa

na mwamba wa kuwaangusha.

Kwa watu wa Yerusalemu,

atakuwa mtego na tanzi.

158:15 Lk 20:18; Isa 28:13; 59:10; Rum 9:32; Mt 4:19; Lk 20:18; Isa 59:10Wengi wao watajikwaa;

wataanguka na kuvunjika,

watategwa na kunaswa.”

168:16 Dan 8:26; 12:4; Yer 32:14; Rut 4:7; Isa 29:11-12Funga ushuhuda na kutia muhuri sheria

miongoni mwa wanafunzi wangu.

178:17 Kum 31:17; Za 27:14; 22:5; Ebr 2:13Nitamngojea Bwana,

ambaye ameificha nyumba ya Yakobo uso wake.

Nitaliweka tumaini langu kwake.

188:18 Mwa 33:5; Ebr 2:13; Kut 3:12; Lk 2:34; Eze 12:6; 24:24; 4:3; Kum 28:46; Eze 12:11; Za 9:11Niko hapa, pamoja na watoto ambao Bwana amenipa. Sisi ni ishara na mfano wake katika Israeli, kutoka kwa Bwana Mwenye Nguvu Zote, anayeishi juu ya Mlima Sayuni.

198:19 1Sam 28:8; Isa 29:4; Hes 27:21; Law 19:31Wakati watu wanapowaambia ninyi kutafuta ushauri kwa waaguzi na wenye kuongea na mizimu, ambao hunongʼona na kunungʼunika, je, watu wasingeuliza kwa Mungu wao? Kwa nini watake shauri kwa wafu kwa ajili ya walio hai? 208:20 Mik 3:6; Isa 60:2; 1:10; Rut 4:7; Lk 16:29; Isa 9:2; 59:9; 9:2Kwa sheria na kwa ushuhuda! Kama hawatasema sawasawa na neno hili, hawana mwanga wa mapambazuko. 218:21 Ay 18:12; Kut 22:28; Ay 30:3; Ufu 16:11Watazunguka katika nchi yote, wakiwa na dhiki na njaa. Watakapotaabika kwa njaa, watapatwa na hasira kali, nao, wakiwa wanatazama juu, watamlaani mfalme wao na Mungu wao. 228:22 Ay 15:24; 3:13; Isa 5:30; Ufu 16:10; Mt 25:30Kisha wataangalia duniani na kuona tu dhiki na giza, hofu na huzuni tupu, nao watasukumiwa kwenye giza nene kabisa.

King James Version

Isaiah 8:1-22

1Moreover the LORD said unto me, Take thee a great roll, and write in it with a man’s pen concerning Maher-shalal-hash-baz.8.1 Maher-shalal-hash-baz: Heb. In making speed to the spoil he hasteneth the prey, or, Make speed, etc 2And I took unto me faithful witnesses to record, Uriah the priest, and Zechariah the son of Jeberechiah. 3And I went unto the prophetess; and she conceived, and bare a son. Then said the LORD to me, Call his name Maher-shalal-hash-baz.8.3 went: Heb. approached 4For before the child shall have knowledge to cry, My father, and my mother, the riches of Damascus and the spoil of Samaria shall be taken away before the king of Assyria.8.4 the riches…: or, he that is before the king of Assyria shall take away the riches, etc

5¶ The LORD spake also unto me again, saying, 6Forasmuch as this people refuseth the waters of Shiloah that go softly, and rejoice in Rezin and Remaliah’s son; 7Now therefore, behold, the Lord bringeth up upon them the waters of the river, strong and many, even the king of Assyria, and all his glory: and he shall come up over all his channels, and go over all his banks: 8And he shall pass through Judah; he shall overflow and go over, he shall reach even to the neck; and the stretching out of his wings shall fill the breadth of thy land, O Immanuel.8.8 stretching…: Heb. fulness of the breadth of thy land shall be the stretchings out of his wings

9¶ Associate yourselves, O ye people, and ye shall be broken in pieces; and give ear, all ye of far countries: gird yourselves, and ye shall be broken in pieces; gird yourselves, and ye shall be broken in pieces.8.9 people, and: or, people, yet 10Take counsel together, and it shall come to nought; speak the word, and it shall not stand: for God is with us.

11¶ For the LORD spake thus to me with a strong hand, and instructed me that I should not walk in the way of this people, saying,8.11 with…: Heb. in strength of hand 12Say ye not, A confederacy, to all them to whom this people shall say, A confederacy; neither fear ye their fear, nor be afraid. 13Sanctify the LORD of hosts himself; and let him be your fear, and let him be your dread. 14And he shall be for a sanctuary; but for a stone of stumbling and for a rock of offence to both the houses of Israel, for a gin and for a snare to the inhabitants of Jerusalem. 15And many among them shall stumble, and fall, and be broken, and be snared, and be taken.

16Bind up the testimony, seal the law among my disciples. 17And I will wait upon the LORD, that hideth his face from the house of Jacob, and I will look for him. 18Behold, I and the children whom the LORD hath given me are for signs and for wonders in Israel from the LORD of hosts, which dwelleth in mount Zion.

19¶ And when they shall say unto you, Seek unto them that have familiar spirits, and unto wizards that peep, and that mutter: should not a people seek unto their God? for the living to the dead? 20To the law and to the testimony: if they speak not according to this word, it is because there is no light in them.8.20 no…: Heb. no morning 21And they shall pass through it, hardly bestead and hungry: and it shall come to pass, that when they shall be hungry, they shall fret themselves, and curse their king and their God, and look upward. 22And they shall look unto the earth; and behold trouble and darkness, dimness of anguish; and they shall be driven to darkness.