Isaya 7 – NEN & NIV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Isaya 7:1-25

Ishara Ya Imanueli

17:1 2Fal 16:5; 2Nya 28:5; 2Fal 15:25, 37; 1Nya 3:13; Isa 8:6; 7:5, 9Wakati Ahazi mwana wa Yothamu, mwana wa Uzia, alipokuwa mfalme wa Yuda, Mfalme Resini wa Aramu,7:1 Yaani Shamu. na Peka mwana wa Remalia mfalme wa Israeli walipanda kupigana dhidi ya Yerusalemu, lakini hawakuweza kuushinda.

27:2 2Sam 7:11; Amo 9:11; Hos 5:8; Isa 16:5; Yer 21:12; Isa 6:4; 22:22; 9:9; Dan 5:6; Hos 5:3Wakati huu nyumba ya Daudi iliambiwa, “Aramu wameungana na Efraimu.” Kwa hiyo mioyo ya Ahazi na watu wake ilitikiswa, kama miti ya msituni inavyotikiswa na upepo.

37:3 2Fal 18:17; Isa 36:2; 10:21-22Ndipo Bwana akamwambia Isaya, “Toka uende, wewe na mwanao Shear-Yashubu,7:3 Shear-Yashubu maana yake Mabaki Watarudi. mkutane na Ahazi huko mwisho wa mfereji wa Bwawa la Juu, kwenye barabara iendayo Shamba la Dobi. 47:4 Kum 3:2; 20:3; Mao 3:26; Zek 3:2; Mt 24:6; Isa 54:14; 30:15; 21:4; 8:12; 10:24; 51:13; Mwa 15:1Mwambie, ‘Uwe mwangalifu, utulie na usiogope. Usife moyo kwa ajili ya watu hawa wawili walio kama visiki vya kuni vifukavyo moshi, kwa ajili ya hasira kali ya Resini na Aramu na ya mwana wa Remalia. 57:5 Isa 6:1Aramu, Efraimu na mwana wa Remalia wamepanga shauri baya ili wakuangamize, wakisema, 67:6 Isa 24:3; 25:8; 28:10“Tuishambulie Yuda, naam, tuirarue vipande vipande na kuigawa miongoni mwetu, na kumtawaza mwana wa Tabeeli awe mfalme juu yake.” 77:7 Mdo 4:25; Isa 24:3; 25:8; 28:16; 8:10; 40:8; 46:10; 14:24; Za 2:1Lakini Bwana Mwenyezi asema hivi:

“ ‘Jambo hili halitatendeka,

halitatokea,

87:8 Mwa 3:15; 14:15; 2Sam 8:6; 2Fal 17:24; Isa 9:11; 17:1-3; 8:4; 17:1-3kwa kuwa kichwa cha Aramu ni Dameski,

na kichwa cha Dameski ni Resini peke yake.

Katika muda wa miaka sitini na mitano,

Efraimu atakuwa ameharibiwa

kiasi kwamba hataweza tena kuwa taifa.

97:9 2Nya 20:20; Isa 8:6-8; 30:12-14; 9:9; 9:1, 3; Za 20:8; 2Fal 15:29Kichwa cha Efraimu ni Samaria,

na kichwa cha Samaria

ni mwana wa Remalia peke yake.

Kama hamtasimama thabiti katika imani yenu,

hamtaimarika kamwe.’ ”

10Bwana akasema na Ahazi tena, 117:11 Kum 13:2; Za 139:8; Kut 7:9“Mwombe Bwana Mungu wako ishara, iwe kwenye vina virefu sana, au kwenye vimo virefu sana.”

127:12 Kum 4:34Lakini Ahazi akasema, “Sitaomba; sitamjaribu Bwana.”

137:13 Za 63:1; 118:28; Mwa 30:15; Isa 1:14; 49:4; 61:10Ndipo Isaya akasema, “Sikia sasa, ewe nyumba ya Daudi! Je, haitoshi kujaribu uvumilivu wa wanadamu? Je, mtaujaribu uvumilivu wa Mungu wangu pia? 147:14 Mwa 5:13; 21:22; 24:43; Kut 3:12; Lk 2:12; Mt 1:23; Mwa 3:15; 21:22; Lk 1:31Kwa hiyo Bwana mwenyewe atawapa ishara: Bikira atachukua mimba, naye atamzaa mwana, na ataitwa Imanueli.7:14 Imanueli maana yake Mungu yu pamoja nasi. 157:15 Mwa 18:8; Isa 8:4; Kum 1:39; 13:16Atakula jibini na asali atakapokuwa ameweza kukataa mabaya na kuchagua mema. 167:16 Isa 8:4; 17:3; Yer 13:5; 7:15; Kum 13:16; 1:39; Hos 5:9-13Lakini kabla mtoto hajajua kukataa mabaya na kuchagua mema, nchi ya wafalme hao wawili unaowaogopa itafanywa ukiwa. 177:17 2Nya 28:20; 1Fal 12:16; Neh 9:32; 2Nya 7:18; Isa 17:9; 34:13Bwana ataleta juu yako, juu ya watu wako, na juu ya nyumba ya baba yako wakati ambao haujawahi kuwako tangu Efraimu alipojitenga na Yuda: yeye atawaleteeni mfalme wa Ashuru.”

187:18 Isa 5:26; 13:5; 7:25Katika siku ile Bwana atawapigia filimbi mainzi kutoka vijito vya mbali vya Misri, na nyuki kutoka nchi ya Ashuru. 197:19 Isa 2:19; 7:25; 17:9; 34:13; 55:13Wote watakuja na kukaa kwenye mabonde yenye miteremko, na kwenye nyufa za miamba, kwenye vichaka vyote vyenye miiba, na kwenye mashimo yote ya maji. 207:20 Isa 10:15; 29:16; 8:7; 11:15; 2Fal 18:16; Yer 27:6-7; 2:18; 2Sam 10:4; Kum 28:40Katika siku ile Bwana atatumia wembe ulioajiriwa kutoka ngʼambo ya Mto,7:20 Yaani Frati. yaani mfalme wa Ashuru, kunyoa nywele za kichwa chako na malaika ya miguu yako, na kuziondoa ndevu zako pia. 217:21 Isa 2:17; Yer 39:10Katika siku ile, mtu atahifadhi hai ndama mmoja na kondoo wawili. 227:22 Mwa 18:8; Isa 14:30Kwa ajili ya wingi wa maziwa watakayotoa, atapata jibini ya kula. Wote watakaobakia katika nchi watakula jibini na asali. 237:23 Isa 5:6; 8:11; 7:2; Hos 2:12Katika siku ile, kila mahali palipokuwa na mizabibu elfu moja yenye thamani ya shekeli 1,0007:23 Shekeli 1,000 ni kama kilo 11.5. za fedha, patakuwa na michongoma na miiba tu. 247:24 Isa 5:6Watu watakwenda huko wakiwa na upinde na mshale, kwa maana nchi itafunikwa na michongoma na miiba. 257:25 Isa 5:17; Hag 1:11Kuhusu vilima vyote vilivyokuwa vikilimwa kwa jembe, hamtakwenda huko tena kwa ajili ya hofu ya michongoma na miiba. Patakuwa mahali ambapo ngʼombe wataachiwa huru, na kondoo kukimbia kimbia.

New International Version

Isaiah 7:1-25

The Sign of Immanuel

1When Ahaz son of Jotham, the son of Uzziah, was king of Judah, King Rezin of Aram and Pekah son of Remaliah king of Israel marched up to fight against Jerusalem, but they could not overpower it.

2Now the house of David was told, “Aram has allied itself with7:2 Or has set up camp in Ephraim”; so the hearts of Ahaz and his people were shaken, as the trees of the forest are shaken by the wind.

3Then the Lord said to Isaiah, “Go out, you and your son Shear-Jashub,7:3 Shear-Jashub means a remnant will return. to meet Ahaz at the end of the aqueduct of the Upper Pool, on the road to the Launderer’s Field. 4Say to him, ‘Be careful, keep calm and don’t be afraid. Do not lose heart because of these two smoldering stubs of firewood—because of the fierce anger of Rezin and Aram and of the son of Remaliah. 5Aram, Ephraim and Remaliah’s son have plotted your ruin, saying, 6“Let us invade Judah; let us tear it apart and divide it among ourselves, and make the son of Tabeel king over it.” 7Yet this is what the Sovereign Lord says:

“ ‘It will not take place,

it will not happen,

8for the head of Aram is Damascus,

and the head of Damascus is only Rezin.

Within sixty-five years

Ephraim will be too shattered to be a people.

9The head of Ephraim is Samaria,

and the head of Samaria is only Remaliah’s son.

If you do not stand firm in your faith,

you will not stand at all.’ ”

10Again the Lord spoke to Ahaz, 11“Ask the Lord your God for a sign, whether in the deepest depths or in the highest heights.”

12But Ahaz said, “I will not ask; I will not put the Lord to the test.”

13Then Isaiah said, “Hear now, you house of David! Is it not enough to try the patience of humans? Will you try the patience of my God also? 14Therefore the Lord himself will give you7:14 The Hebrew is plural. a sign: The virgin7:14 Or young woman will conceive and give birth to a son, and7:14 Masoretic Text; Dead Sea Scrolls son, and he or son, and they will call him Immanuel.7:14 Immanuel means God with us. 15He will be eating curds and honey when he knows enough to reject the wrong and choose the right, 16for before the boy knows enough to reject the wrong and choose the right, the land of the two kings you dread will be laid waste. 17The Lord will bring on you and on your people and on the house of your father a time unlike any since Ephraim broke away from Judah—he will bring the king of Assyria.”

Assyria, the Lord’s Instrument

18In that day the Lord will whistle for flies from the Nile delta in Egypt and for bees from the land of Assyria. 19They will all come and settle in the steep ravines and in the crevices in the rocks, on all the thornbushes and at all the water holes. 20In that day the Lord will use a razor hired from beyond the Euphrates River—the king of Assyria—to shave your heads and private parts, and to cut off your beards also. 21In that day, a person will keep alive a young cow and two goats. 22And because of the abundance of the milk they give, there will be curds to eat. All who remain in the land will eat curds and honey. 23In that day, in every place where there were a thousand vines worth a thousand silver shekels,7:23 That is, about 25 pounds or about 12 kilograms there will be only briers and thorns. 24Hunters will go there with bow and arrow, for the land will be covered with briers and thorns. 25As for all the hills once cultivated by the hoe, you will no longer go there for fear of the briers and thorns; they will become places where cattle are turned loose and where sheep run.