Isaya 63 – NEN & KJV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Isaya 63:1-19

Siku Ya Mungu Ya Kisasi Na Ukombozi

163:1 Mwa 36:33; Amo 1:12; Yer 42:11; Sef 3:17; 2Nya 28:17; Isa 11:14; Ufu 19:13; Ay 9:4Ni nani huyu anayekuja kutoka Edomu,

kutoka Bosra, mwenye mavazi yaliyotiwa madoa mekundu?

Ni nani huyu, aliyevikwa joho la kifahari,

anayetembea kwa ukuu wa nguvu zake?

“Mimi ndimi, nisemaye katika haki,

mwenye nguvu wa kuokoa.”

263:2 Ufu 19:13; Mwa 49:11Kwa nini mavazi yako ni mekundu,

kama ya yule akanyagaye shinikizo la zabibu?

363:3 Amu 6:11; Ufu 19:15; Mao 1:15; Ufu 19:13; 14:19-20; Za 108:13“Nimekanyaga shinikizo la zabibu peke yangu;

kutoka mataifa hakuna mtu aliyekuwa pamoja nami.

Nimewaponda kwa miguu katika hasira yangu

na kuwakanyaga chini katika ghadhabu yangu;

damu yao ilitia matone kwenye mavazi yangu,

na kutia madoa nguo zangu zote.

463:4 Isa 1:24; Yer 50:15Kwa kuwa siku ya kisasi ilikuwa moyoni mwangu,

mwaka wa ukombozi wangu umefika.

563:5 2Fal 14:26; Isa 41:28; 59:16; Za 44:3; Yn 16:32; Isa 33:2Nilitazama, lakini hakuwepo yeyote wa kunisaidia,

nilishangaa kwa kuwa hakuwepo yeyote aliyetoa msaada;

hivyo mkono wangu wenyewe ndio ulionifanyia wokovu,

na ghadhabu yangu mwenyewe ndiyo iliyonitegemeza.

663:6 Isa 29:9; Mao 4:21; Isa 34:3; Ay 40:12Nilikanyaga mataifa kwa miguu katika hasira yangu,

katika ghadhabu yangu niliwalewesha,

na kumwaga damu yao juu ya ardhi.”

Kusifu Na Kuomba

763:7 Isa 54:8; Efe 2:4; Kut 18:9Nitasimulia juu ya wema wa Bwana,

kwa matendo ambayo apaswa kusifiwa,

sawasawa na yote ambayo Bwana

ametenda kwa ajili yetu:

naam, mambo mengi mema aliyoyatenda

kwa ajili ya nyumba ya Israeli,

sawasawa na huruma zake

na wema wake mwingi.

863:8 Mdo 9:4; Kut 14:19; 33:14; Kum 7:7-8; Ezr 9:9; Za 28:9; Ay 37:23Alisema, “Hakika wao ni watu wangu,

wana ambao hawatanidanganya”;

hivyo akawa Mwokozi wao.

963:9 Kut 14:19; 33:14; Kum 7:7-8; Ezr 9:9; Isa 48:20; Kum 1:31; 32:7; Za 28:9; Ay 37:23Katika taabu zao zote naye alitaabika,

na malaika wa uso wake akawaokoa.

Katika upendo wake na rehema zake aliwakomboa,

akawainua na kuwachukua siku zote zilizopita.

1063:10 Eze 20:8; Mdo 7:39-42; Efe 4:30; Za 106:40; 78:17; Isa 10:4; Yos 10:14Lakini waliasi,

na kumhuzunisha Roho Mtakatifu wake.

Hivyo aligeuka na kuwa adui yao,

na yeye mwenyewe akapigana dhidi yao.

1163:11 Kut 14:22, 30; Hes 11:17; Za 77:20Ndipo watu wake wakazikumbuka siku zilizopita,

siku za Mose na watu wake:

yuko wapi yeye aliyewaleta kupitia katikati ya bahari,

pamoja na wachungaji wa kundi lake?

Yuko wapi yule aliyeweka

Roho wake Mtakatifu katikati yao,

1263:12 Kut 14:21-22; Isa 11:15; Mwa 49:24aliyetuma mkono wake uliotukuka wenye nguvu

kuwa katika mkono wa kuume wa Mose,

aliyegawa maji ya bahari mbele yao,

ili kujipatia jina milele,

1363:13 Kum 32:12; Yer 31:9; Kut 14:24; Za 119:11aliyewaongoza kupitia kwenye vilindi?

Kama farasi katika nchi iliyo wazi,

wao hawakujikwaa,

1463:14 Kut 33:14; Kum 12:9kama ngʼombe washukao bondeni kwenye malisho,

walipewa pumziko na Roho wa Bwana.

Hivi ndivyo ulivyowaongoza watu wako

ili kujipatia mwenyewe jina tukufu.

1563:15 Za 80:14; Mao 3:50; 1Fal 22:19; 2:26; Hos 11:8; Kum 26:15; Isa 64:12Tazama chini kutoka mbinguni ukaone

kutoka kiti chako cha enzi

kilichoinuliwa juu, kitakatifu na kitukufu.

Uko wapi wivu wako na uweza wako?

Umetuzuilia wema wako na huruma zako.

1663:16 Ay 14:21; Gal 3:28; Isa 44:6; Kut 4:22; Yer 3:4; Yn 8:41; Isa 59:20Lakini wewe ni Baba yetu,

ingawa Abrahamu hatufahamu sisi

wala Israeli hatutambui;

wewe, Ee Bwana, ndiwe Baba yetu,

Mkombozi wetu tangu zamani za kale ndilo jina lako.

1763:17 Isa 6:10; 29:13; Hes 10:36; Mt 13:15; Mwa 20:13; Mao 3:9; Kut 4:21; 34:9Ee Bwana, kwa nini unatuacha twende mbali na njia zako,

na kuifanya mioyo yetu migumu hata hatukukuheshimu?

Rudi kwa ajili ya watumishi wako,

yale makabila ambayo ni urithi wako.

1863:18 Law 26:31; Dan 8:24; Za 74:3-8; Kum 4:26; Isa 28:18; Lk 21:24; Dan 8:13Kwa maana kwa muda mfupi watu wako walimiliki mahali pako patakatifu,

lakini sasa adui zetu wamepakanyaga mahali patakatifu pako.

1963:19 Isa 43:7; Yer 14:9Sisi tumekuwa kama wale ambao hujawatawala kamwe,

kama wale ambao hawajaitwa kwa jina lako.

King James Version

Isaiah 63:1-19

1Who is this that cometh from Edom, with dyed garments from Bozrah? this that is glorious in his apparel, travelling in the greatness of his strength? I that speak in righteousness, mighty to save.63.1 glorious: Heb. decked 2Wherefore art thou red in thine apparel, and thy garments like him that treadeth in the winefat? 3I have trodden the winepress alone; and of the people there was none with me: for I will tread them in mine anger, and trample them in my fury; and their blood shall be sprinkled upon my garments, and I will stain all my raiment. 4For the day of vengeance is in mine heart, and the year of my redeemed is come. 5And I looked, and there was none to help; and I wondered that there was none to uphold: therefore mine own arm brought salvation unto me; and my fury, it upheld me. 6And I will tread down the people in mine anger, and make them drunk in my fury, and I will bring down their strength to the earth.

7¶ I will mention the lovingkindnesses of the LORD, and the praises of the LORD, according to all that the LORD hath bestowed on us, and the great goodness toward the house of Israel, which he hath bestowed on them according to his mercies, and according to the multitude of his lovingkindnesses. 8For he said, Surely they are my people, children that will not lie: so he was their Saviour. 9In all their affliction he was afflicted, and the angel of his presence saved them: in his love and in his pity he redeemed them; and he bare them, and carried them all the days of old.

10¶ But they rebelled, and vexed his holy Spirit: therefore he was turned to be their enemy, and he fought against them. 11Then he remembered the days of old, Moses, and his people, saying, Where is he that brought them up out of the sea with the shepherd of his flock? where is he that put his holy Spirit within him?63.11 shepherd: or, shepherds 12That led them by the right hand of Moses with his glorious arm, dividing the water before them, to make himself an everlasting name? 13That led them through the deep, as an horse in the wilderness, that they should not stumble? 14As a beast goeth down into the valley, the Spirit of the LORD caused him to rest: so didst thou lead thy people, to make thyself a glorious name.

15¶ Look down from heaven, and behold from the habitation of thy holiness and of thy glory: where is thy zeal and thy strength, the sounding of thy bowels and of thy mercies toward me? are they restrained?63.15 the sounding: or, the multitude 16Doubtless thou art our father, though Abraham be ignorant of us, and Israel acknowledge us not: thou, O LORD, art our father, our redeemer; thy name is from everlasting.63.16 our redeemer…: or, our redeemer from everlasting is thy name

17¶ O LORD, why hast thou made us to err from thy ways, and hardened our heart from thy fear? Return for thy servants’ sake, the tribes of thine inheritance. 18The people of thy holiness have possessed it but a little while: our adversaries have trodden down thy sanctuary. 19We are thine: thou never barest rule over them; they were not called by thy name.63.19 they…: Heb. thy name was not called upon them