Isaya 61 – NEN & NUB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Isaya 61:1-11

Mwaka Wa Upendeleo Wa Bwana

161:1 Isa 11:2; Mdo 4:26; Lk 4:18-19; Zek 9:12; 2Kor 3:17; Isa 50:4; Dan 9:24-26; Ay 5:16Roho wa Bwana Mwenyezi yu juu yangu,

kwa sababu Bwana amenitia mafuta

kuwahubiria maskini habari njema.

Amenituma kuwaganga waliovunjika moyo,

kuwatangazia mateka uhuru wao,

na hao waliofungwa

habari za kufunguliwa kwao;

261:2 Isa 49:8; Mal 4:1-3; Mt 5:4; Isa 1:24; Lk 4:18-19; Ay 5:1; Lk 6:21kutangaza mwaka wa Bwana uliokubaliwa,

na siku ya kisasi ya Mungu wetu,

kuwafariji wote waombolezao,

361:3 Isa 60:20-21; 3:23; Ay 2:8; Rut 3:3; Ebr 1:9; Yer 31:13; Za 92:12-13; Mt 15:13na kuwapa mahitaji

wale wanaohuzunika katika Sayuni,

ili kuwapa taji ya uzuri badala ya majivu,

mafuta ya furaha badala ya maombolezo,

vazi la sifa badala ya roho ya kukata tamaa.

Nao wataitwa mialoni ya haki,

pando la Bwana,

ili kuonyesha utukufu wake.

461:4 Amo 9:14; Yn 15:8; Zek 1:16-17; Isa 44:26; Eze 36:33Watajenga upya magofu ya zamani

na kupatengeneza mahali palipoachwa ukiwa zamani;

watafanya upya miji iliyoharibiwa,

iliyoachwa ukiwa kwa vizazi vingi.

561:5 Isa 14:1-2; Eze 36:33; Isa 56:6Wageni watayachunga makundi yenu,

wageni watafanya kazi katika mashamba yenu,

na kutunza mashamba yenu ya mizabibu.

661:6 Kut 19:6; Kum 33:19; 1Pet 2:5; Isa 60:1Nanyi mtaitwa makuhani wa Bwana,

mtaitwa watumishi wa Mungu wetu.

Mtakula utajiri wa mataifa,

nanyi katika utajiri wao mtajisifu.

761:7 Kum 21:17; Zek 9:12; Isa 29:22; 41:11; 60:21; Za 126:5; Isa 25:9Badala ya aibu yao

watu wangu watapokea sehemu maradufu,

na badala ya fedheha

watafurahia katika urithi wao;

hivyo watarithi sehemu maradufu katika nchi yao,

nayo furaha ya milele itakuwa yao.

861:8 Mwa 9:16; Isa 1:17; 55:3; 5:16; Za 11:7; Ebr 13:20; Isa 42:6“Kwa maana Mimi, Bwana, napenda haki,

na ninachukia unyangʼanyi na uovu.

Katika uaminifu wangu nitawapa malipo yao

na kufanya agano la milele nao.

961:9 Isa 43:5; 48:19; Mwa 12:2; Kum 28:3-12Wazao wao watajulikana miongoni mwa mataifa,

na uzao wao miongoni mwa kabila za watu.

Wale wote watakaowaona watatambua

kuwa ni taifa ambalo Bwana amelibariki.”

1061:10 Hab 3:18; Ay 27:6; Isa 49:18; Ufu 21:2; Za 2:11; Isa 7:13; Lk 1:47; Ufu 19:8Ninafurahia sana katika Bwana,

nafsi yangu inashangilia katika Mungu wangu.

Kwa maana amenivika mavazi ya wokovu,

na kunipamba kwa joho la haki,

kama vile bwana arusi apambavyo

kichwa chake kama kuhani,

na kama bibi arusi ajipambavyo

kwa vito vyake vya thamani.

1161:11 Za 85:11; Isa 45:8; Mwa 47:23; Isa 58:11Kwa maana kama vile ardhi ifanyavyo chipukizi kuota,

na bustani isababishavyo mbegu kuota,

ndivyo Bwana Mwenyezi atafanya haki na sifa

zichipuke mbele ya mataifa yote.

Swedish Contemporary Bible

Jesaja 61:1-11

Nådens år

1Herrens, Herrens Ande är över mig,

för Herren har smort mig

till att förkunna goda nyheter till de förtryckta.

Han har sänt mig till att ge de förkrossade bot,

att förkunna frihet för de fångna

och befrielse för de bundna,

2att ropa ut ett nådens år från Herren,

en hämndens dag från vår Gud,

att trösta alla som sörjer

3och ge de sörjande i Sion

en huvudprydnad i stället för aska,

glädjens olja i stället för sorgdräkt,

lovsång i stället för modlöshet.

De ska kallas ’rättfärdighetens ekar’,

som Herren har planterat till sin ära.

4De ska bygga upp de gamla ruinerna

och resa upp det som länge legat öde.

De ska återuppbygga förstörda städer

som legat öde i generationer.

5Främlingar ska valla era hjordar,

utlänningar bruka era åkrar och vingårdar.

6Ni ska kallas Herrens präster,

benämnas som vår Guds tjänare.

Ni ska få njuta av folkens välfärd

och berömma er av deras rikedomar.

7De har fått dubbelt upp av skam,

hån och förakt har de fått sig till dels.

Så ska de också få dubbel del i sitt land

och evig glädje.

8För jag är Herren som älskar rättvisa.

Jag hatar plundring och brott.

Jag ska troget belöna dem

och ingå ett evigt förbund med dem.

9Deras ättlingar ska bli kända bland folken,

deras efterkommande bland folkslagen.

Alla som ser dem ska inse

att de är ett släkte som Herren har välsignat.”

10Jag gläder mig i Herren

och jublar över min Gud,

för han har klätt mig i frälsningens dräkt

och svept mig i rättfärdighetens klädnad,

som när en brudgum sätter på sig sin högtidsturban

och brud pryder sig med sina smycken.

11Liksom jorden får sin gröda att spira

och trädgården sin sådd att växa fram,

så låter Herren, Herren rättfärdigheten

och lovsången växa fram inför alla folk.