Mwaka Wa Upendeleo Wa Bwana
161:1 Isa 11:2; Mdo 4:26; Lk 4:18-19; Zek 9:12; 2Kor 3:17; Isa 50:4; Dan 9:24-26; Ay 5:16Roho wa Bwana Mwenyezi yu juu yangu,
kwa sababu Bwana amenitia mafuta
kuwahubiria maskini habari njema.
Amenituma kuwaganga waliovunjika moyo,
kuwatangazia mateka uhuru wao,
na hao waliofungwa
habari za kufunguliwa kwao;
261:2 Isa 49:8; Mal 4:1-3; Mt 5:4; Isa 1:24; Lk 4:18-19; Ay 5:1; Lk 6:21kutangaza mwaka wa Bwana uliokubaliwa,
na siku ya kisasi ya Mungu wetu,
kuwafariji wote waombolezao,
361:3 Isa 60:20-21; 3:23; Ay 2:8; Rut 3:3; Ebr 1:9; Yer 31:13; Za 92:12-13; Mt 15:13na kuwapa mahitaji
wale wanaohuzunika katika Sayuni,
ili kuwapa taji ya uzuri badala ya majivu,
mafuta ya furaha badala ya maombolezo,
vazi la sifa badala ya roho ya kukata tamaa.
Nao wataitwa mialoni ya haki,
pando la Bwana,
ili kuonyesha utukufu wake.
461:4 Amo 9:14; Yn 15:8; Zek 1:16-17; Isa 44:26; Eze 36:33Watajenga upya magofu ya zamani
na kupatengeneza mahali palipoachwa ukiwa zamani;
watafanya upya miji iliyoharibiwa,
iliyoachwa ukiwa kwa vizazi vingi.
561:5 Isa 14:1-2; Eze 36:33; Isa 56:6Wageni watayachunga makundi yenu,
wageni watafanya kazi katika mashamba yenu,
na kutunza mashamba yenu ya mizabibu.
661:6 Kut 19:6; Kum 33:19; 1Pet 2:5; Isa 60:1Nanyi mtaitwa makuhani wa Bwana,
mtaitwa watumishi wa Mungu wetu.
Mtakula utajiri wa mataifa,
nanyi katika utajiri wao mtajisifu.
761:7 Kum 21:17; Zek 9:12; Isa 29:22; 41:11; 60:21; Za 126:5; Isa 25:9Badala ya aibu yao
watu wangu watapokea sehemu maradufu,
na badala ya fedheha
watafurahia katika urithi wao;
hivyo watarithi sehemu maradufu katika nchi yao,
nayo furaha ya milele itakuwa yao.
861:8 Mwa 9:16; Isa 1:17; 55:3; 5:16; Za 11:7; Ebr 13:20; Isa 42:6“Kwa maana Mimi, Bwana, napenda haki,
na ninachukia unyangʼanyi na uovu.
Katika uaminifu wangu nitawapa malipo yao
na kufanya agano la milele nao.
961:9 Isa 43:5; 48:19; Mwa 12:2; Kum 28:3-12Wazao wao watajulikana miongoni mwa mataifa,
na uzao wao miongoni mwa kabila za watu.
Wale wote watakaowaona watatambua
kuwa ni taifa ambalo Bwana amelibariki.”
1061:10 Hab 3:18; Ay 27:6; Isa 49:18; Ufu 21:2; Za 2:11; Isa 7:13; Lk 1:47; Ufu 19:8Ninafurahia sana katika Bwana,
nafsi yangu inashangilia katika Mungu wangu.
Kwa maana amenivika mavazi ya wokovu,
na kunipamba kwa joho la haki,
kama vile bwana arusi apambavyo
kichwa chake kama kuhani,
na kama bibi arusi ajipambavyo
kwa vito vyake vya thamani.
1161:11 Za 85:11; Isa 45:8; Mwa 47:23; Isa 58:11Kwa maana kama vile ardhi ifanyavyo chipukizi kuota,
na bustani isababishavyo mbegu kuota,
ndivyo Bwana Mwenyezi atafanya haki na sifa
zichipuke mbele ya mataifa yote.
Nådens år
1Herrens, Herrens Ande är över mig,
för Herren har smort mig
till att förkunna goda nyheter till de förtryckta.
Han har sänt mig till att ge de förkrossade bot,
att förkunna frihet för de fångna
och befrielse för de bundna,
2att ropa ut ett nådens år från Herren,
en hämndens dag från vår Gud,
att trösta alla som sörjer
3och ge de sörjande i Sion
en huvudprydnad i stället för aska,
glädjens olja i stället för sorgdräkt,
lovsång i stället för modlöshet.
De ska kallas ’rättfärdighetens ekar’,
som Herren har planterat till sin ära.
4De ska bygga upp de gamla ruinerna
och resa upp det som länge legat öde.
De ska återuppbygga förstörda städer
som legat öde i generationer.
5Främlingar ska valla era hjordar,
utlänningar bruka era åkrar och vingårdar.
6Ni ska kallas Herrens präster,
benämnas som vår Guds tjänare.
Ni ska få njuta av folkens välfärd
och berömma er av deras rikedomar.
7De har fått dubbelt upp av skam,
hån och förakt har de fått sig till dels.
Så ska de också få dubbel del i sitt land
och evig glädje.
8För jag är Herren som älskar rättvisa.
Jag hatar plundring och brott.
Jag ska troget belöna dem
och ingå ett evigt förbund med dem.
9Deras ättlingar ska bli kända bland folken,
deras efterkommande bland folkslagen.
Alla som ser dem ska inse
att de är ett släkte som Herren har välsignat.”
10Jag gläder mig i Herren
och jublar över min Gud,
för han har klätt mig i frälsningens dräkt
och svept mig i rättfärdighetens klädnad,
som när en brudgum sätter på sig sin högtidsturban
och brud pryder sig med sina smycken.
11Liksom jorden får sin gröda att spira
och trädgården sin sådd att växa fram,
så låter Herren, Herren rättfärdigheten
och lovsången växa fram inför alla folk.