Isaya 6 – NEN & NIV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Isaya 6:1-13

Agizo Kwa Isaya

16:1 2Nya 26:22-23; Hes 12:8; Ufu 4:2; 1:13; 2Fal 15:7; Kut 24:10; Ufu 4:2; Yn 12:41; 1Fal 22:19Katika mwaka ule Mfalme Uzia alikufa, nilimwona Bwana ameketi katika kiti cha enzi, kilicho juu na kilichotukuzwa sana, nalo pindo la joho lake likajaza Hekalu. 26:2 Eze 1:5; 10:15; 1:11; Ufu 4:8Juu yake walikuwepo maserafi, kila mmoja alikuwa na mabawa sita: Kwa mabawa mawili walifunika nyuso zao, kwa mengine mawili walifunika miguu yao, na kwa mawili walikuwa wakiruka. 36:3 Ufu 4:8; Kut 16:7; 15:11; Hes 14:21; Isa 54:5; 11:9; Za 89:9; 72:19; 89:8; Mal 1:11Nao walikuwa wakiitana kila mmoja na mwenzake:

“Mtakatifu, Mtakatifu, Mtakatifu

ni Bwana Mwenye Nguvu Zote;

dunia yote imejaa utukufu wake.”

46:4 Kut 19:18; Eze 43:5; 44:4; Ufu 15:8Kwa sauti zao, miimo ya milango na vizingiti vilitikisika, nalo Hekalu likajaa moshi.

56:5 Isa 59:3; Yer 9:3-8; 51:57; Hes 17:12; Kum 5:26; Kut 6:12; 24:10; Isa 24:23; 5:8; Lk 5:8; Yer 5:3; 51:57; Ay 42:5Ndipo nikalia, “Ole wangu! Nimeangamia! Kwa kuwa mimi ni mtu mwenye midomo michafu, nami ninaishi katikati ya watu wenye midomo michafu, nayo macho yangu yamemwona Mfalme, Bwana Mwenye Nguvu Zote.”

66:6 Law 10:1; Eze 10:2Ndipo mmoja wa wale maserafi akaruka kunijia akiwa na kaa la moto linalowaka mkononi mwake, ambalo alikuwa amelichukua kwa koleo kutoka madhabahuni. 76:7 Dan 10:16; 12:3; 1Yn 1:7; Isa 45:25; Yer 1:9; Law 26:41Akanigusa nalo kinywa changu na kusema, “Tazama, hili limegusa midomo yako, uovu wako umeondolewa, nayo dhambi yako imesamehewa.”

86:8 Mdo 9:4; Ay 40:9; Yer 26:12-15; Mwa 1:26; 22:1; Kut 3:4Kisha nikasikia sauti ya Bwana ikisema, “Nimtume nani? Ni nani atakayekwenda kwa ajili yetu?”

Nami nikasema, “Mimi hapa. Nitume mimi!”

96:9 Mt 13:15; Lk 8:10; Mt 28:196:9 Amo 7:15; Yer 5:21; Eze 3:11; Mt 13:15; Lk 8:10Akasema, “Nenda ukawaambie watu hawa:

“ ‘Mtaendelea daima kusikiliza,

lakini kamwe hamtaelewa;

mtaendelea daima kutazama,

lakini kamwe hamtatambua.’

106:10 Kut 4:21; Kum 32:39; 29:4; Eze 12:2; Isa 44:18; Yn 12:40; Mk 4:12; 8:18Fanya mioyo ya watu hawa kuwa migumu,

fanya masikio yao yasisikie,

na upofushe macho yao.

Wasije wakaona kwa macho yao,

na wakasikiliza kwa masikio yao,

wakaelewa kwa mioyo yao,

nao wakageuka, nikawaponywa.”

116:11 Yer 4:13; Za 79:5; 79:1; Isa 24:10; Yer 35:17; Za 119:11; Law 26:31, 43Ndipo nikasema, “Hadi lini, Ee Bwana?”

Naye akanijibu:

“Hadi miji iwe imeachwa magofu

na bila wakazi,

hadi nyumba zitakapobaki bila watu,

na mashamba yatakapoharibiwa na kuangamizwa,

126:12 Kum 28:64; Yer 30:17; 4:29; Isa 5:5-9; 60:15; 62:4; 62:4hadi Bwana atakapokuwa amekwisha kumpeleka kila mmoja mbali sana,

na nchi itakapokuwa imeachwa kabisa.

136:13 Rum 11:5; Ay 14:7; 14:8; Isa 10:22; Kum 14:2; Law 27:30; Isa 5:6; 1:9Hata kama sehemu ya kumi ya watu watabaki katika nchi,

itaharibiwa tena.

Lakini kama vile mvinje na mwaloni

ibakizavyo visiki inapokatwa,

ndivyo mbegu takatifu

itakavyokuwa kisiki katika nchi.”

New International Version

Isaiah 6:1-13

Isaiah’s Commission

1In the year that King Uzziah died, I saw the Lord, high and exalted, seated on a throne; and the train of his robe filled the temple. 2Above him were seraphim, each with six wings: With two wings they covered their faces, with two they covered their feet, and with two they were flying. 3And they were calling to one another:

“Holy, holy, holy is the Lord Almighty;

the whole earth is full of his glory.”

4At the sound of their voices the doorposts and thresholds shook and the temple was filled with smoke.

5“Woe to me!” I cried. “I am ruined! For I am a man of unclean lips, and I live among a people of unclean lips, and my eyes have seen the King, the Lord Almighty.”

6Then one of the seraphim flew to me with a live coal in his hand, which he had taken with tongs from the altar. 7With it he touched my mouth and said, “See, this has touched your lips; your guilt is taken away and your sin atoned for.”

8Then I heard the voice of the Lord saying, “Whom shall I send? And who will go for us?”

And I said, “Here am I. Send me!”

9He said, “Go and tell this people:

“ ‘Be ever hearing, but never understanding;

be ever seeing, but never perceiving.’

10Make the heart of this people calloused;

make their ears dull

and close their eyes.6:9,10 Hebrew; Septuagint ‘You will be ever hearing, but never understanding; / you will be ever seeing, but never perceiving.’ / 10 This people’s heart has become calloused; / they hardly hear with their ears, / and they have closed their eyes

Otherwise they might see with their eyes,

hear with their ears,

understand with their hearts,

and turn and be healed.”

11Then I said, “For how long, Lord?”

And he answered:

“Until the cities lie ruined

and without inhabitant,

until the houses are left deserted

and the fields ruined and ravaged,

12until the Lord has sent everyone far away

and the land is utterly forsaken.

13And though a tenth remains in the land,

it will again be laid waste.

But as the terebinth and oak

leave stumps when they are cut down,

so the holy seed will be the stump in the land.”