Isaya 6 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Isaya 6:1-13

Agizo Kwa Isaya

16:1 2Nya 26:22-23; Hes 12:8; Ufu 4:2; 1:13; 2Fal 15:7; Kut 24:10; Ufu 4:2; Yn 12:41; 1Fal 22:19Katika mwaka ule Mfalme Uzia alikufa, nilimwona Bwana ameketi katika kiti cha enzi, kilicho juu na kilichotukuzwa sana, nalo pindo la joho lake likajaza Hekalu. 26:2 Eze 1:5; 10:15; 1:11; Ufu 4:8Juu yake walikuwepo maserafi, kila mmoja alikuwa na mabawa sita: Kwa mabawa mawili walifunika nyuso zao, kwa mengine mawili walifunika miguu yao, na kwa mawili walikuwa wakiruka. 36:3 Ufu 4:8; Kut 16:7; 15:11; Hes 14:21; Isa 54:5; 11:9; Za 89:9; 72:19; 89:8; Mal 1:11Nao walikuwa wakiitana kila mmoja na mwenzake:

“Mtakatifu, Mtakatifu, Mtakatifu

ni Bwana Mwenye Nguvu Zote;

dunia yote imejaa utukufu wake.”

46:4 Kut 19:18; Eze 43:5; 44:4; Ufu 15:8Kwa sauti zao, miimo ya milango na vizingiti vilitikisika, nalo Hekalu likajaa moshi.

56:5 Isa 59:3; Yer 9:3-8; 51:57; Hes 17:12; Kum 5:26; Kut 6:12; 24:10; Isa 24:23; 5:8; Lk 5:8; Yer 5:3; 51:57; Ay 42:5Ndipo nikalia, “Ole wangu! Nimeangamia! Kwa kuwa mimi ni mtu mwenye midomo michafu, nami ninaishi katikati ya watu wenye midomo michafu, nayo macho yangu yamemwona Mfalme, Bwana Mwenye Nguvu Zote.”

66:6 Law 10:1; Eze 10:2Ndipo mmoja wa wale maserafi akaruka kunijia akiwa na kaa la moto linalowaka mkononi mwake, ambalo alikuwa amelichukua kwa koleo kutoka madhabahuni. 76:7 Dan 10:16; 12:3; 1Yn 1:7; Isa 45:25; Yer 1:9; Law 26:41Akanigusa nalo kinywa changu na kusema, “Tazama, hili limegusa midomo yako, uovu wako umeondolewa, nayo dhambi yako imesamehewa.”

86:8 Mdo 9:4; Ay 40:9; Yer 26:12-15; Mwa 1:26; 22:1; Kut 3:4Kisha nikasikia sauti ya Bwana ikisema, “Nimtume nani? Ni nani atakayekwenda kwa ajili yetu?”

Nami nikasema, “Mimi hapa. Nitume mimi!”

96:9 Mt 13:15; Lk 8:10; Mt 28:196:9 Amo 7:15; Yer 5:21; Eze 3:11; Mt 13:15; Lk 8:10Akasema, “Nenda ukawaambie watu hawa:

“ ‘Mtaendelea daima kusikiliza,

lakini kamwe hamtaelewa;

mtaendelea daima kutazama,

lakini kamwe hamtatambua.’

106:10 Kut 4:21; Kum 32:39; 29:4; Eze 12:2; Isa 44:18; Yn 12:40; Mk 4:12; 8:18Fanya mioyo ya watu hawa kuwa migumu,

fanya masikio yao yasisikie,

na upofushe macho yao.

Wasije wakaona kwa macho yao,

na wakasikiliza kwa masikio yao,

wakaelewa kwa mioyo yao,

nao wakageuka, nikawaponywa.”

116:11 Yer 4:13; Za 79:5; 79:1; Isa 24:10; Yer 35:17; Za 119:11; Law 26:31, 43Ndipo nikasema, “Hadi lini, Ee Bwana?”

Naye akanijibu:

“Hadi miji iwe imeachwa magofu

na bila wakazi,

hadi nyumba zitakapobaki bila watu,

na mashamba yatakapoharibiwa na kuangamizwa,

126:12 Kum 28:64; Yer 30:17; 4:29; Isa 5:5-9; 60:15; 62:4; 62:4hadi Bwana atakapokuwa amekwisha kumpeleka kila mmoja mbali sana,

na nchi itakapokuwa imeachwa kabisa.

136:13 Rum 11:5; Ay 14:7; 14:8; Isa 10:22; Kum 14:2; Law 27:30; Isa 5:6; 1:9Hata kama sehemu ya kumi ya watu watabaki katika nchi,

itaharibiwa tena.

Lakini kama vile mvinje na mwaloni

ibakizavyo visiki inapokatwa,

ndivyo mbegu takatifu

itakavyokuwa kisiki katika nchi.”

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

以賽亞書 6:1-13

上帝呼召以賽亞

1烏西雅王駕崩那年,我看見主坐在高高的寶座上,衣袍下垂,覆蓋了聖殿。 2在祂上方侍立著撒拉弗天使,他們各有三對翅膀:一對遮臉,一對遮腳,一對飛翔。 3他們彼此呼喊:

「聖哉,聖哉,聖哉,

萬軍之耶和華!

祂的榮耀充滿大地。」

4他們的聲音震動聖殿的根基,聖殿裡煙雲彌漫。 5那時我說:「我有禍了!我要滅亡了!因為我口出不潔之言,又住在口出不潔之言的人群中,並且親眼看見了大君王——萬軍之耶和華。」 6有個撒拉弗天使用火鉗從祭壇上取了一塊燃燒的炭,飛到我面前, 7用炭碰我的嘴唇,說:「看啊,這炭碰了你的嘴唇,你的過犯已被除掉,你的罪惡已被赦免。」 8然後,我聽見主說:「我可以差遣誰呢?誰肯為我們去呢?」我說:「我在這裡,請差遣我!」 9祂說:「你去告訴以色列人,

『你們聽了又聽,卻不明白;

看了又看,卻不領悟。』

10要讓這些人心靈麻木,

耳朵發背,

眼睛昏花,

免得他們眼睛看見,

耳朵聽見,

心裡明白,

回心轉意,就得到醫治。」

11我說:「主啊,這要到什麼時候呢?」祂說:

「直到城邑荒涼,無人居住,房屋空置,

土地荒廢的時候。

12那時,我必把他們趕到遠方,

他們的土地必荒蕪。

13即使境內只剩下十分之一的人,

也必被消滅。

然而,就像砍掉松樹和橡樹後必留下樹墩,

這地方必有聖潔的苗裔存留下來。」