Isaya 58 – NEN & CST

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Isaya 58:1-14

Mfungo Wa Kweli

158:1 Isa 24:20; 40:6; 48:8; Eze 3:17; Isa 57:12“Piga kelele, usizuie.

Paza sauti yako kama tarumbeta.

Watangazieni watu wangu uasi wao,

na kwa nyumba ya Yakobo dhambi zao.

258:2 Isa 29:13; Yak 4:8Kwa maana kila siku hunitafuta,

wanaonekana kutaka kujua njia zangu,

kana kwamba walikuwa taifa linalotenda lililo sawa,

na ambalo halijaziacha amri za Mungu wake.

Hutaka kwangu maamuzi ya haki,

nao hutamani Mungu awakaribie.

358:3 Law 16:29; Mal 3:14; Zek 7:5-6; Kut 10:3; 2Nya 6:37; Yer 44:10; Isa 22:13Wao husema, ‘Mbona tumefunga, nawe hujaona?

Mbona tumejinyenyekeza, nawe huangalii?’

“Lakini katika siku ya kufunga kwenu, mnafanya mnavyotaka

na kuwadhulumu wafanyakazi wenu wote.

458:4 Mal 2:16; Mao 3:44; Mik 3:4; 1Fal 21:9-13; Isa 59:6; Eze 7:11; 8:18; 1Sam 8:18Kufunga kwenu huishia kwenye magomvi na mapigano,

na kupigana ninyi kwa ninyi kwa ngumi za uovu.

Hamwezi kufunga kama mnavyofanya leo

na kutazamia sauti zenu kusikiwa huko juu.

558:5 Zek 7:5; 1Fal 21:27; Mt 6:16; Ay 2:8; Isa 36:6Je, hii ndiyo aina ya mfungo niliouchagua,

siku moja tu ya mtu kujinyenyekeza?

Je, ni kwa kuinamisha kichwa chini kama tete,

na kwa kujilaza juu ya nguo ya gunia na majivu?

Je, huo ndio mnaouita mfungo,

siku iliyokubalika kwa Bwana?

658:6 Neh 5:10-11; Kum 14:29; Lk 4:19; Yoe 2:12-13; Yer 34:9; Amo 4:1; Isa 9:4“Je, hii si ndiyo aina ya mfungo niliyoichagua:

kufungua minyororo ya udhalimu,

na kufungua kamba za nira,

kuwaweka huru walioonewa,

na kuvunja kila nira?

758:7 Ay 22:7; Dan 4:27; Ebr 13:12; Ay 31:19-20; Mwa 29:14; Mt 25:36; Eze 18:16Je, sio kushirikiana chakula chako na wenye njaa

na kuwapatia maskini wasiokuwa na makao hifadhi,

unapomwona aliye uchi, umvike,

wala si kumkimbia mtu wa nyama na damu yako mwenyewe?

858:8 Isa 9:2; 30:26; Kut 14:19; Ay 11:17; Isa 26:2Ndipo nuru yako itajitokeza kama mapambazuko

na uponyaji wako utatokea upesi;

ndipo haki yako itakapokutangulia mbele yako,

na utukufu wa Bwana utakuwa mlinzi nyuma yako.

958:9 Mit 6:13; Za 50:12; 12:2; Isa 59:13; Ay 8:6; Dan 9:20; Zek 10:6Ndipo utaita, naye Bwana atajibu,

utalia kuomba msaada,

naye atasema: Mimi hapa.

“Kama ukiiondoa nira ya udhalimu,

na kunyoosha kidole na kuzungumza maovu,

1058:10 Kum 15:7-8; Ay 11:17; Isa 42:16nanyi kama mkimkunjulia mtu mwenye njaa nafsi zenu

na kutosheleza mahitaji ya walioonewa,

ndipo nuru yenu itakapongʼaa gizani,

nao usiku wenu utakuwa kama adhuhuri.

1158:11 Za 104:28; Wim 4:15; Yn 4:14; Za 48:14; Isa 42:16; 48:7; Za 68:1; 72:6Bwana atakuongoza siku zote,

atayatosheleza mahitaji yako katika nchi kame,

naye ataitia nguvu mifupa yako.

Utakuwa kama bustani iliyonyweshwa vizuri,

kama chemchemi ambayo maji yake hayakauki kamwe.

12Watu wako watajenga tena magofu ya zamani

na kuinua misingi ya kale;

utaitwa Mwenye Kukarabati Kuta Zilizobomoka,

Mwenye Kurejeza Barabara za Makao.

1358:13 Law 19:20; Kut 20:8; Za 37:4; Isa 56:2“Kama ukitunza miguu yako isivunje Sabato,

na kutokufanya kama vile upendavyo katika siku yangu takatifu,

kama ukiita Sabato siku ya furaha

na siku takatifu ya Bwana ya kuheshimiwa,

kama utaiheshimu kwa kutoenenda

katika njia zako mwenyewe,

na kutokufanya yakupendezayo

au kusema maneno ya upuzi,

1458:14 Ay 22:26; Kum 32:13; Isa 1:20; Za 105:10-11ndipo utakapojipatia furaha yako katika Bwana,

nami nitakufanya upande juu ya miinuko ya nchi

na kusherehekea urithi wa Yakobo baba yako.”

Kinywa cha Bwana kimenena haya.

Nueva Versión Internacional (Castilian)

Isaías 58:1-14

El verdadero ayuno

1»¡Grita con toda tu fuerza, no te reprimas!

Alza tu voz como trompeta.

Denuncia a mi pueblo sus rebeldías;

sus pecados, a los descendientes de Jacob.

2Porque día tras día me buscan,

y desean conocer mis caminos,

como si fueran una nación

que practicara la justicia,

como si no hubieran abandonado

mis mandamientos.

Me piden decisiones justas,

y desean acercarse a mí,

3y hasta me reclaman:

“¿Para qué ayunamos, si no lo tienes en cuenta?

¿Para qué nos afligimos, si tú no lo notas?”

»Pero el día en que ayunáis,

hacéis negocios y explotáis a vuestros obreros.

4Vosotros solo ayunáis para pelear y reñir,

y daros puñetazos a mansalva.

Si queréis que el cielo atienda vuestros ruegos,

¡ayunad, pero no como ahora lo hacéis!

5¿Acaso el ayuno que he escogido

es solo un día para que el hombre se mortifique?

¿Y solo para que incline la cabeza como un junco,

haga duelo y se cubra de ceniza?

¿A eso llamáis vosotros día de ayuno

y día aceptable para el Señor?

6»El ayuno que he escogido,

¿no es más bien romper las cadenas de injusticia

y desatar las correas del yugo,

poner en libertad a los oprimidos

y romper toda atadura?

7¿No es acaso el ayuno compartir tu pan con el hambriento

y dar refugio a los pobres sin techo,

vestir al desnudo

y no dejar de lado a tus semejantes?

8Si así procedes,

tu luz despuntará como la aurora,

y al instante llegará tu sanidad;

tu justicia te abrirá el camino,

y la gloria del Señor te seguirá.

9Llamarás, y el Señor responderá;

pedirás ayuda, y él dirá: “¡Aquí estoy!”

»Si desechas el yugo de opresión,

el dedo acusador y la lengua maliciosa,

10si te dedicas a ayudar a los hambrientos

y a saciar la necesidad del desvalido,

entonces brillará tu luz en las tinieblas,

y como el mediodía será tu noche.

11El Señor te guiará siempre;

te saciará en tierras resecas,

y fortalecerá tus huesos.

Serás como jardín bien regado,

como manantial cuyas aguas no se agotan.

12Tu pueblo reconstruirá las ruinas antiguas

y levantará los cimientos de antaño;

serás llamado “reparador de muros derruidos”,

“restaurador de calles transitables”.

13»Si dejas de profanar el sábado,

y no haces negocios en mi día santo;

si llamas al sábado “delicia”,

y al día santo del Señor, “honorable”;

si te abstienes de profanarlo,

y lo honras no haciendo negocios

ni profiriendo palabras inútiles,

14entonces hallarás tu gozo en el Señor;

sobre las cumbres de la tierra te haré cabalgar,

y haré que te deleites

en la herencia de tu padre Jacob».

El Señor mismo lo ha dicho.