Isaya 55 – NEN & CCB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Isaya 55:1-13

Mwaliko Kwa Wenye Kiu

155:1 Mao 5:4; Mit 9:5; Ufu 3:18; Yer 2:31; Isa 35:7; Mt 5:6; Lk 5:21; Yn 4:14; Zek 14:8; Hos 14:4; Eze 47:1, 12“Njooni, ninyi nyote wenye kiu,

njooni kwenye maji;

nanyi ambao hamna fedha,

njooni, nunueni na mle!

Njooni, nunueni divai na maziwa

bila fedha na bila gharama.

255:2 Yer 12:13; Hag 1:6; Za 22:26; Mhu 6:2; Isa 49:4; Hos 4:10; 8:7Kwa nini kutumia fedha kwa kitu ambacho si chakula,

na kutaabikia kitu kisichoshibisha?

Sikilizeni, nisikilizeni mimi na mle kilicho kizuri,

nazo nafsi zenu zitafurahia utajiri wa unono.

355:3 Law 18:5; Yn 6:27; Mwa 9:16; Ebr 13:20; Mdo 13:34; Rum 10:5; Isa 54:10Tegeni sikio mje kwangu,

nisikieni mimi, ili nafsi zenu zipate kuishi.

Nitafanya agano la milele nanyi,

pendo la uaminifu nililomwahidi Daudi.

455:4 1Tim 6:13; 1Sam 13:14; Eze 34:23-24; Ebr 2:10; 2Nya 7:18Tazama, nimemfanya kuwa shahidi wa mataifa,

kiongozi na jemadari wa mataifa.

5Hakika utaita mataifa usiyoyajua,

nayo mataifa yale yasiyokujua yataharakisha kukujia,

kwa sababu ya Bwana Mungu wako,

yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli,

kwa maana amekutukuza.”

655:6 Mdo 17:27; Za 32:6; Amo 5:14; Yer 33:3; Isa 9:13; Kum 4:29; 2Nya 15:2Mtafuteni Bwana maadamu anapatikana;

mwiteni maadamu yu karibu.

755:7 Yer 3:12; 26:3; Isa 32:7; Eze 18:32; 2Nya 6:21; 30:6; Eze 18:27-28Mtu mwovu na aiache njia yake,

na mtu mbaya na ayaache mawazo yake.

Yeye na amrudie Bwana, naye atamrehemu,

arudi kwa Mungu wetu, kwa kuwa atamsamehe bure kabisa.

855:8 Isa 53:6; Mik 4:12; Flp 2:5; 4:8“Kwa kuwa mawazo yangu si mawazo yenu,

wala njia zenu si njia zangu,”

asema Bwana.

955:9 Ay 11:8; Za 103:11; Hes 23:19; Isa 40:13-14“Kama vile mbingu zilivyo juu kuliko dunia,

ndivyo njia zangu zilivyo juu kuliko njia zenu

na mawazo yangu kuliko mawazo yenu.

1055:10 2Kor 9:10; Isa 30:23; Mwa 47:23; Za 67:6; Ay 14:9; Law 25:19Kama vile mvua na theluji

ishukavyo kutoka mbinguni,

nayo hairudi tena huko

bila kunywesha dunia

na kuichipusha na kuistawisha,

hivyo hutoa mbegu kwa mpanzi

na mkate kwa mlaji,

1155:11 Isa 54:10-13; 1Nya 16:33; Za 98:4; Isa 35:2; Za 65:12-13; 96:12-13; 98:8ndivyo lilivyo neno langu lile litokalo kinywani mwangu:

Halitanirudia tupu,

bali litatimiliza lile nililokusudia

na litafanikiwa katika kusudi lile nililolituma.

12Mtatoka nje kwa furaha

na kuongozwa kwa amani;

milima na vilima

vitapaza sauti kwa nyimbo mbele yenu,

nayo miti yote ya shambani

itapiga makofi.

1355:13 Hes 33:55; Za 102:12; Yer 32:20; Isa 5:6; 41:19; 63:12; Yer 33:9Badala ya kichaka cha miiba

itaota miti ya misunobari,

na badala ya michongoma

utaota mhadasi.55:13 Mhadasi ni aina ya mti ambao huota milimani karibu na Yerusalemu, hutoa harufu nzuri itumikayo kutengeneza manukato; kwa Kiebrania ni “hadas”, na ilikuwa inatumika kujenga vibanda wakati wa Sikukuu ya Vibanda (ona pia Neh 8:15).

Hili litakuwa jambo la kumpatia Bwana jina,

kwa ajili ya ishara ya milele,

ambayo haitaharibiwa.”

Chinese Contemporary Bible (Simplified)

以赛亚书 55:1-13

上帝施恩典

1耶和华说:“口渴的人啊,来喝水吧!

没有钱的人啊,

来买东西吃吧!

买酒买奶都不用付钱。

2你们为什么花钱买不能充饥的食物?

为什么拿辛苦赚来的钱买不能令人饱足的东西?

要留心听我的话,

就可以吃美物,

享受丰盛的佳肴。

3你们要到我这里来,

侧耳听我的话,就必得到生命。

我要跟你们立永久的约,

将应许给大卫的可靠恩福赐给你们。

4我使他统管万民,

向万民做见证。

5看啊,你必召集不认识的国民,

不认识你的国民必来投奔你,

因为以色列的圣者——你的上帝耶和华赐给你荣耀。”

6要趁着还可以找到耶和华的时候寻找祂,

趁祂还在附近的时候求告祂。

7愿邪恶的人停止作恶,

不义的人除掉恶念。

愿他们归向耶和华,

祂必怜悯他们;

愿他们归向我们的上帝,

祂必仁慈地赦免他们。

8耶和华说:“我的意念并非你们的意念,

我的道路并非你们的道路。

9正如天高过地,

我的道路也高过你们的道路,

我的意念也高过你们的意念。

10雨雪从天降下,并不返回,

而是要滋润大地,

使地上的植物发芽生长,

叫播种的有种子,

吃饭的有食粮。

11同样,我口中所出的话也不会徒然返回,

而是要成就我的旨意,

实现我的计划。

12你们必欢欢喜喜地出来,

平平安安地蒙引导,

大山小山都要在你们面前歌唱,

田野的树木也都拍掌。

13曾经的荆棘之地必长出松树,

曾经的蒺藜之地必长出番石榴。

这便是永远长存的记号,

以宣扬耶和华的名。”