Isaya 53 – NEN & KLB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Isaya 53:1-12

153:1 Isa 28:9; Yn 12:38; Rum 10:16; Za 98:1; Isa 30:30Ni nani aliyeamini ujumbe wetu,

na mkono wa Bwana umefunuliwa kwa nani?

253:2 Mk 9:12; Isa 52:14; 2Fal 19:26; Ay 14:7; Isa 4:2; 11:10Alikua mbele yake kama mche mwororo

na kama mzizi katika nchi kavu.

Hakuwa na uzuri wala utukufu wa kutuvutia kwake,

hakuwa na chochote katika sura yake cha kutufanya tumtamani.

353:3 Ebr 4:15; Mt 16:21; 27:29; 1Sam 2:30; Za 69:29; Kut 1:10; Lk 18:31-33Alidharauliwa na kukataliwa na wanadamu,

mtu wa huzuni nyingi, ajuaye mateso.

Kama mtu ambaye watu humficha nyuso zao,

alidharauliwa, wala hatukumhesabu kuwa kitu.

453:4 Mt 8:17; Zek 13:7; Yn 19:7; Kum 5:24; Ay 4:5; Yer 23:5-6; Eze 34:23-24; Mik 5:2Hakika alichukua udhaifu wetu

na akajitwika huzuni zetu,

hata hivyo tulidhania kuwa amepigwa na Mungu,

akapigwa sana naye, na kuteswa.

553:5 Kum 32:39; Yn 3:17; 1Pet 2:24-25; 2Nya 7:14; Rum 4:25; 1Kor 15:3; Ebr 9:8; Kut 28:38Lakini alitobolewa kwa ajili ya makosa yetu,

alichubuliwa kwa ajili ya maovu yetu;

adhabu iliyotuletea sisi amani ilikuwa juu yake,

na kwa majeraha yake sisi tumepona.

653:6 Za 119:176; 1Pet 2:25Sisi sote, kama kondoo, tumepotea,

kila mmoja wetu amegeukia njia yake mwenyewe,

naye Bwana aliweka juu yake

maovu yetu sisi sote.

753:7 Mdo 8:32; Mk 14:61; 1Pet 2:23; Isa 49:26; Mt 27:31; Yn 1:29; Za 44:22Alionewa na kuteswa,

hata hivyo hakufungua kinywa chake;

aliongozwa kama mwana-kondoo

apelekwaye machinjoni,

kama vile kondoo anyamazavyo mbele ya wao wamkataye manyoya,

hivyo hakufungua kinywa chake.

853:8 Za 88:5; Dan 9:26; Mdo 8:32-33; Za 39:8; Mk 14:49Kwa kuonewa na kuhukumiwa aliondolewa.

Nani awezaye kueleza kuhusu kizazi chake?

Kwa maana alikatiliwa mbali na nchi ya walio hai,

alipigwa kwa ajili ya makosa ya watu wangu.

953:9 Mk 15:43-46; Lk 23:50-53; Isa 42:1-3; Ay 16:17; Ufu 14:5; Yn 19:19, 38-41Wakamfanyia kaburi pamoja na waovu,

pamoja na matajiri katika kifo chake,

ingawa hakutenda jeuri,

wala hapakuwa na hila kinywani mwake.

1053:10 2Kor 5:21; Mwa 12:17; Za 22:30; Mdo 2:23; Isa 46:10; Law 5:15; Yn 3:17Lakini yalikuwa ni mapenzi ya Bwana

kumchubua na kumsababisha ateseke.

Ingawa Bwana amefanya maisha yake

kuwa sadaka ya hatia,

ataona uzao wake na kuishi siku nyingi,

nayo mapenzi ya Bwana yatafanikiwa mkononi mwake.

1153:11 Yn 10:14-18; Rum 5:18-19; Ay 33:30; Isa 20:3; Mdo 7:52; Yn 1:29; Rum 4:24; Mdo 10:43Baada ya maumivu ya nafsi yake,

ataona nuru ya uzima na kuridhika;

kwa maarifa yake, mtumishi wangu mwenye haki

atawafanya wengi kuwa wenye haki,

naye atayachukua maovu yao.

1253:12 Flp 2:9; Mt 26:28, 38; 27:38; Lk 23:34; Kut 15:9; Za 119:162; Ebr 9:28; Isa 59:19; Rum 8:34; Mk 15:27; Lk 22:37Kwa hiyo nitamgawia sehemu miongoni mwa wakuu,

naye atagawana nyara pamoja na wenye nguvu,

kwa sababu aliyamimina maisha yake hadi mauti,

naye alihesabiwa pamoja na wakosaji.

Kwa kuwa alichukua dhambi za wengi,

na kuwaombea wakosaji.

Korean Living Bible

이사야 53:1-12

1우리가 전한 것을 누가 믿었으며 53:1 원문에는 ‘여호와의 팔이’여호와의 능력이 누구에게 나타났는 가?

2그는 연한 순처럼, 마른 땅에서 나온 줄기처럼 주 앞에서 자랐으니 그에게는 풍채나 위엄이 없고 우리의 시선을 끌 만한 매력이나 아름다움도 없다.

3그는 사람들에게 멸시와 천대를 받고 슬픔과 고통을 당하는 사람이 되었으니 사람들이 그를 외면하고 우리도 그를 귀하게 여기지 않았다.

4그는 우리의 질병을 지고 우리를 대신하여 슬픔을 당하였으나 우리는 그가 하나님의 형벌을 받아 고난을 당하는 것으로 생각하였다.

5그가 우리의 죄 때문에 찔림을 당하고 상처를 입었으니 그가 징계를 받음으로 우리가 평화를 누리게 되었고 그가 채찍에 맞음으로 우리가 고침을 받았다.

6우리는 다 길 잃은 양처럼 제각기 잘못된 길로 갔으나 여호와께서는 우리 모든 사람의 죄를 그에게 담당시키셨다.

7그가 곤욕을 당하면서도 침묵을 지켰으니 도살장으로 끌려가는 어린 양과 털 깎는 사람 앞에서 잠잠한 양처럼 그의 입을 열지 않았다.

8그가 체포되어 심문을 당하고 끌려갔으나 그 세대 사람들 중에 그가 죽음을 당하게 된 것이 자기들의 죄 때문이라고 누가 생각했겠는가?

9그는 범죄하거나 거짓말을 한 적이 없었으나 악인들처럼 죽음을 당하여 53:9 또는 ‘그 묘실이 부자와 함께 되었도다’부자의 묘실에 묻혔다.

10여호와께서 말씀하신다. “그가 상처를 입고 고통을 당한 것은 내 뜻이었다. 그가 죄를 속하는 희생제물이 되면 그는 자손을 보게 될 것이며 그의 날이 장구할 것이니 그를 통해 내 뜻이 성취될 것이다.

11그는 자기 영혼이 고통을 당해 얻어진 결과를 보고 만족스럽게 여길 것이다. 나의 의로운 종은 자기 지식으로 많은 사람을 의롭게 하며 그들의 죄를 담당할 것이다.

12그러므로 내가 강하고 위대한 자들의 영예를 그에게 주겠다. 그는 기꺼이 자기 생명을 바쳐 범죄자처럼 되었으며 많은 사람들의 죄를 짊어지고 그들이 용서받도록 기도하였다.”