Isaya 50 – NEN & KLB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Isaya 50:1-11

Dhambi Ya Israeli Na Utii Wa Mtumishi

150:1 Kum 24:1; Mk 10:4; Mt 18:25; Amu 3:8; Hos 2:2; Mt 19:7; Neh 5:5; Isa 1:25Hili ndilo asemalo Bwana:

“Iko wapi hati ya talaka ya mama yako

ambayo kwayo niliachana naye?

Au nimewauza ninyi kwa nani

miongoni mwa watu wanaonidai?

Kwa ajili ya dhambi zenu mliuzwa,

kwa sababu ya makosa, mama yenu aliachwa.

250:2 Mwa 18:14; Kut 14:22; Hes 11:23; 1Sam 8:19; Isa 41:28; Za 68:35; Yer 14:9Nilipokuja, kwa nini hakuwepo hata mmoja?

Nilipoita, kwa nini hakuwepo hata mmoja wa kujibu?

Je, mkono wangu ni mfupi mno hata nisiweze kuwakomboa?

Je, mimi sina nguvu za kukuokoa?

Kwa kukemea tu naikausha bahari,

naigeuza mito ya maji kuwa jangwa;

samaki wake wanaoza kwa kukosa maji

na kufa kwa ajili ya kiu.

350:3 Isa 5:30; Ufu 6:12; Kut 10:21Ninalivika anga weusi na kufanya nguo ya gunia

kuwa kifuniko chake.”

450:4 Kut 4:11-12; Za 88:13; Mt 7:29; Isa 40:29; Mt 11:28Bwana Mwenyezi amenipa ulimi uliofundishwa,

ili kujua neno limtegemezalo aliyechoka.

Huniamsha asubuhi kwa asubuhi,

huamsha sikio langu lisikie kama mtu afundishwaye.

550:5 Isa 35:5; Eze 2:8; Ebr 10:5; Isa 48:16; Eze 24:3; Mdo 26:19; Mt 26:39Bwana Mwenyezi amezibua masikio yangu,

nami sikuwa mwasi,

wala sikurudi nyuma.

650:6 Mt 27:30; Isa 53:5; Mao 3:30; Hes 12:14; Mt 26:67; Mk 14:65Niliwapa mgongo wangu wale wanipigao,

mashavu yangu wale wangʼoao ndevu zangu;

sikuuficha uso wangu kutokana na fedheha

na kutemewa mate.

750:7 Isa 41:10; Rum 8:31; Eze 3:8-9; Isa 48:16; 28:16; 29:22Kwa sababu Bwana Mwenyezi ananisaidia,

sitatahayarika.

Kwa hiyo nimekaza uso wangu kama jiwe la gumegume,

nami ninajua sitaaibika.

850:8 Ay 13:19; Rum 8:32-34; 1Kor 4:4; Isa 26:2; 49:4Yeye anipatiaye haki yangu yu karibu.

Ni nani basi atakayeleta mashtaka dhidi yangu?

Tukabiliane uso kwa uso!

Mshtaki wangu ni nani?

Ni nani aliye mshtaki wangu?

950:9 Ay 13:28; Isa 41:10; Ebr 1:11-12; Rum 8:1, 34; Isa 51:8Ni Bwana Mwenyezi anisaidiaye mimi.

Ni nani huyo atakayenihukumu?

Wote watachakaa kama vazi,

nondo watawala wawamalize.

1050:10 2Nya 20:20; Isa 49:3; 26:4; 1:19; Hag 1:12; Mdo 26:18; Isa 10:20Ni nani miongoni mwenu amchaye Bwana,

na kulitii neno la mtumishi wake?

Yeye atembeaye gizani,

yeye asiye na nuru,

na alitumainie jina la Bwana,

na amtegemee Mungu wake.

1150:11 Mit 26:18; Yak 3:6; Ay 15:20; Isa 65:13-15; Kum 21:22-23Lakini sasa, ninyi nyote mnaowasha mioto,

na kupeana mienge iwakayo ninyi kwa ninyi,

nendeni, tembeeni katika nuru ya moto wenu

na ya mienge mliyoiwasha.

Hili ndilo mtakalolipokea kutoka mkononi mwangu:

Mtalala chini kwa mateso makali.

Korean Living Bible

이사야 50:1-11

이스라엘의 죄와 순종하는 여호와의 종

1여호와께서 말씀하신다. “남자가 자기 아내를 내쫓듯이 내가 너희를 쫓아내었느냐? 그렇다면 그 이혼 증서는 어디 있느냐? 너희는 사람이 자기 자녀를 종으로 팔듯이 내가 너희를 팔았다고 생각하느냐? 아니다. 너희는 너희 죄와 허물 때문에 팔려 포로로 잡혀갔다.

2“내가 내 백성을 구원하려고 찾아왔어도 반응을 보이는 자가 아무도 없었다. 내가 불러도 어째서 그들은 대답하지 않는가? 내가 50:2 또는 ‘손이 짧아’힘이 부족하고 능력이 없어서 그들을 구원하지 못하겠느냐? 내 명령 한마디면 바다가 마르고 강이 사막이 되어 물이 없으므로 고기들이 죽어 악취가 난다.

3그리고 나는 하늘을 온통 흑암으로 덮어 버릴 수도 있다.”

4주 여호와께서 나에게 할 말을 가르치셔서 피곤한 자를 격려하고 도와줄 수 있게 하시며 아침마다 나를 깨우치셔서 그의 가르치심을 알아듣게 하시는구나.

5여호와께서 나에게 깨닫는 마음을 주셨으므로 나는 거역하거나 뒤로 물러가지 않았으며

6나를 때리는 자들에게 내 등을 맡기고 내 수염을 뽑는 자들에게 내 뺨을 맡기며 그들이 침을 뱉고 모욕할 때에도 내가 얼굴을 가리지 않았다.

7주 여호와께서 나를 도우시므로 내가 당황하지 않을 것이며 내가 얼굴을 부싯돌처럼 굳게 하였으니 수치를 당하지 않을 줄로 안다.

8나를 변호하시는 분이 가까이 계시는데 누가 감히 나와 다툴 수 있겠는가? 내 고소자가 누구냐? 함께 법정으로 가서 맞서 보자.

9주 여호와께서 나를 도우시는데 나를 죄인으로 단정할 자가 누구냐? 나의 모든 원수들은 좀먹은 옷처럼 해어져 없어질 것이다.

10너희 중에 여호와를 두려운 마음으로 섬기며 그 종의 말에 순종하는 자가 누구냐? 빛 없이 흑암 가운데 사는 자들도 여호와를 신뢰하며 자기 하나님을 의지하게 하라.

11다른 사람을 해치려고 하는 자들아, 너희는 너희 꾀에 스스로 망할 것이니 너희가 여호와의 형벌을 받아 고통을 당할 것이다.