Isaya 50 – NEN & CCB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Isaya 50:1-11

Dhambi Ya Israeli Na Utii Wa Mtumishi

150:1 Kum 24:1; Mk 10:4; Mt 18:25; Amu 3:8; Hos 2:2; Mt 19:7; Neh 5:5; Isa 1:25Hili ndilo asemalo Bwana:

“Iko wapi hati ya talaka ya mama yako

ambayo kwayo niliachana naye?

Au nimewauza ninyi kwa nani

miongoni mwa watu wanaonidai?

Kwa ajili ya dhambi zenu mliuzwa,

kwa sababu ya makosa, mama yenu aliachwa.

250:2 Mwa 18:14; Kut 14:22; Hes 11:23; 1Sam 8:19; Isa 41:28; Za 68:35; Yer 14:9Nilipokuja, kwa nini hakuwepo hata mmoja?

Nilipoita, kwa nini hakuwepo hata mmoja wa kujibu?

Je, mkono wangu ni mfupi mno hata nisiweze kuwakomboa?

Je, mimi sina nguvu za kukuokoa?

Kwa kukemea tu naikausha bahari,

naigeuza mito ya maji kuwa jangwa;

samaki wake wanaoza kwa kukosa maji

na kufa kwa ajili ya kiu.

350:3 Isa 5:30; Ufu 6:12; Kut 10:21Ninalivika anga weusi na kufanya nguo ya gunia

kuwa kifuniko chake.”

450:4 Kut 4:11-12; Za 88:13; Mt 7:29; Isa 40:29; Mt 11:28Bwana Mwenyezi amenipa ulimi uliofundishwa,

ili kujua neno limtegemezalo aliyechoka.

Huniamsha asubuhi kwa asubuhi,

huamsha sikio langu lisikie kama mtu afundishwaye.

550:5 Isa 35:5; Eze 2:8; Ebr 10:5; Isa 48:16; Eze 24:3; Mdo 26:19; Mt 26:39Bwana Mwenyezi amezibua masikio yangu,

nami sikuwa mwasi,

wala sikurudi nyuma.

650:6 Mt 27:30; Isa 53:5; Mao 3:30; Hes 12:14; Mt 26:67; Mk 14:65Niliwapa mgongo wangu wale wanipigao,

mashavu yangu wale wangʼoao ndevu zangu;

sikuuficha uso wangu kutokana na fedheha

na kutemewa mate.

750:7 Isa 41:10; Rum 8:31; Eze 3:8-9; Isa 48:16; 28:16; 29:22Kwa sababu Bwana Mwenyezi ananisaidia,

sitatahayarika.

Kwa hiyo nimekaza uso wangu kama jiwe la gumegume,

nami ninajua sitaaibika.

850:8 Ay 13:19; Rum 8:32-34; 1Kor 4:4; Isa 26:2; 49:4Yeye anipatiaye haki yangu yu karibu.

Ni nani basi atakayeleta mashtaka dhidi yangu?

Tukabiliane uso kwa uso!

Mshtaki wangu ni nani?

Ni nani aliye mshtaki wangu?

950:9 Ay 13:28; Isa 41:10; Ebr 1:11-12; Rum 8:1, 34; Isa 51:8Ni Bwana Mwenyezi anisaidiaye mimi.

Ni nani huyo atakayenihukumu?

Wote watachakaa kama vazi,

nondo watawala wawamalize.

1050:10 2Nya 20:20; Isa 49:3; 26:4; 1:19; Hag 1:12; Mdo 26:18; Isa 10:20Ni nani miongoni mwenu amchaye Bwana,

na kulitii neno la mtumishi wake?

Yeye atembeaye gizani,

yeye asiye na nuru,

na alitumainie jina la Bwana,

na amtegemee Mungu wake.

1150:11 Mit 26:18; Yak 3:6; Ay 15:20; Isa 65:13-15; Kum 21:22-23Lakini sasa, ninyi nyote mnaowasha mioto,

na kupeana mienge iwakayo ninyi kwa ninyi,

nendeni, tembeeni katika nuru ya moto wenu

na ya mienge mliyoiwasha.

Hili ndilo mtakalolipokea kutoka mkononi mwangu:

Mtalala chini kwa mateso makali.

Chinese Contemporary Bible (Simplified)

以赛亚书 50:1-11

以色列的罪恶

1耶和华说:

“我休你们母亲的休书在哪里呢?

我把你们卖给了我哪一个债主呢?

你们被卖是因为你们的罪恶,

你们母亲被休是因为你们的过犯。

2为什么我来的时候一个人也不在?

为什么我呼唤的时候没有人回答?

是我的臂膀太短不能救赎你们吗?

是我没有能力拯救你们吗?

看啊,我斥责一声,海就干了;

我使江河变为旷野,

鱼类因无水而干死,发出腥臭。

3我使黑暗遮蔽穹苍,

用麻布掩盖天空。”

主仆的顺服

4主耶和华赐我教导的能力,

使我知道用什么话帮助疲乏的人。

每天早晨,主唤醒我,

叫我像受教者那样侧耳聆听。

5主耶和华开了我的耳朵,

我没有悖逆,也没有退缩。

6人打我的背,我任他打;

人拔我的胡子,我任他拔;

人侮辱我,朝我吐唾沫,

我也不掩面。

7我并不觉得羞愧,

因为主耶和华帮助我。

我心如坚石,

知道自己必不会蒙羞。

8为我伸张正义的来了,

谁要控告我呢?

让我们来理论吧!

谁是我的控告者呢?

让他到我这里来吧!

9看啊,有主耶和华帮助我,

谁能定我有罪呢?

看啊,他们都要像衣服一样渐渐破旧,

被蛀虫吃掉。

信靠上帝

10你们中间谁敬畏耶和华,

听从祂仆人的话?

行在黑暗中、

没有光的人要信靠耶和华的名,

仰赖自己的上帝。

11然而,你们自己生火、自备火把的人啊,

靠自己点燃的火光行走吧!

你们必落入悲惨的境地,

这是耶和华亲手所定的。