Isaya 5 – NEN & CARSA

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Isaya 5:1-30

Wimbo Wa Shamba La Mizabibu

15:1 Za 80:8-9; Yn 15:1; Isa 27:2Nitaimba wimbo kwa ajili ya mmoja nimpendaye,

kuhusu shamba lake la mizabibu:

Mpendwa wangu alikuwa na shamba la mizabibu

kwenye kilima chenye rutuba.

25:2 Kum 32:6; Kut 15:17; Yer 2:21; Mt 21:19; Mk 11:13; Isa 16:8; 27:3; 1Sam 2:9; Ay 24:11; Mt 21:33; Lk 13:6Alililima na kuondoa mawe

na akaliotesha mizabibu bora sana.

Akajenga mnara wa ulinzi ndani yake,

na kutengeneza shinikizo la kukamulia divai pia.

Kisha akatazamia kupata mazao ya zabibu nzuri,

lakini lilizaa matunda mabaya tu.

35:3 Mt 21:40“Basi enyi wakazi wa Yerusalemu na watu wa Yuda,

hukumuni kati yangu na shamba langu la mizabibu.

45:4 2Nya 36:15; Mt 23:37; Yer 2:5-7; 2:21; Mk 6:3-4; Yer 24:2; 29:17Ni nini zaidi ambacho kingeweza kufanyika kwa shamba langu la mizabibu

kuliko yale niliyofanya?

Nilipotazamia kupata zabibu nzuri,

kwa nini lilizaa zabibu mbaya tu?

55:5 Za 80:12; Lk 21:24; Yer 12:10; Isa 6:12; 27:10; 22:5; 10:6; 2Nya 36:21Sasa nitawaambia lile nitakalolitendea

shamba langu la mizabibu:

Nitaondoa uzio wake,

nalo litaharibiwa,

nitabomoa ukuta wake,

nalo litakanyagwa.

65:6 Hos 2:12; Ebr 6:8; Mwa 6:13; Isa 6:13; 49:17; 2Sam 23:6; Isa 7:23-24; Law 26:32; Eze 28:24; 2Sam 1:21; Amo 4:7Nitalifanya nchi ya ukiwa isiyokaliwa na watu,

halitakatiwa matawi wala kulimwa,

nayo michongoma na miiba itamea huko,

nitaamuru mawingu yasinyeshe mvua juu yake.”

75:7 Isa 37:30; Eze 9:9; 22:29; Za 80:8; Isa 17:10; 10:2; 29:21; 61:8; Za 12:5Shamba la mzabibu la Bwana Mwenye Nguvu Zote

ni nyumba ya Israeli,

na watu wa Yuda

ni bustani yake ya kumpendeza.

Alitazamia haki, lakini akaona umwagaji damu,

alitazamia uadilifu, lakini akasikia vilio vya taabu.

Ole Na Hukumu

85:8 Yer 22:13; Isa 24:16; 6:5; 10:1; Hab 2:9-12; Ay 20:19; Mik 2:2Ole wenu mnaoongeza nyumba baada ya nyumba

na kuunganisha mashamba baada ya mashamba

hadi hakuna nafasi iliyobaki,

nanyi mnaishi peke yenu katika nchi.

95:9 Isa 6:11-12; Mt 23:38; Yer 44:11; Isa 22:14; Mt 23:38Bwana Mwenye Nguvu Zote amesema nikisikia:

“Hakika nyumba kubwa zitakuwa ukiwa,

nayo majumba ya fahari yatabaki bila kukaliwa.

105:10 Law 27:16; Kum 28:38; Zek 8:10; Law 26:26; 27:16Shamba la mizabibu la eka kumi

litatoa bathi5:10 Bathi moja ni sawa na lita 22. moja ya divai,

na homeri5:10 Homeri moja ni sawa na lita 220. ya mbegu zilizopandwa

itatoa efa5:10 Efa moja ni sawa na lita 22. moja tu ya nafaka.”

115:11 1Sam 25:36; Mit 23:29-30Ole wao wale waamkao asubuhi na mapema

wakikimbilia kunywa vileo,

wale wakawiao sana mpaka usiku,

mpaka wamewaka kwa mvinyo.

125:12 1Sam 12:24; Ay 34:27; Eze 26:13; Amo 6:5-6; Isa 24:8; Ay 21:12; Za 28:5; 68:25Wana vinubi na zeze kwenye karamu zao,

matari, filimbi na mvinyo,

lakini hawayajali matendo ya Bwana,

wala hawana heshima kwa ajili ya kazi ya mikono yake.

135:13 Isa 49:21; 1:3; 3:3; Mit 10:21; Hos 4:6; Rum 1:28; Ay 22:8Kwa hiyo watu wangu watakwenda uhamishoni

kwa sababu ya kukosa ufahamu,

watu wao wenye vyeo watakufa kwa njaa

na watu wao wengi watakauka kwa kiu.

145:14 Mit 30:16; Hes 16:30; Isa 22:13; 23:7; 24:8Kwa hiyo kaburi5:14 Kaburi hapa maana yake ni Kuzimu, kwa Kiebrania ni Sheol. limeongeza hamu yake

na kupanua mdomo wake bila kikomo,

ndani mwake watashuka wakuu wao na wingi wa watu,

pamoja na wagomvi wao, na wafanyao sherehe wote.

155:15 Isa 2:9-11; 10:33Hivyo mwanadamu atashushwa,

na binadamu kunyenyekezwa,

macho ya wenye majivuno yatanyenyekezwa.

165:16 Isa 61:8; Law 10:3; Eze 36:23; Za 97:6; Isa 33:10; 28:17; 30:18; 29:23Lakini Bwana Mwenye Nguvu Zote atatukuzwa

kwa ajili ya haki yake,

naye Mungu Mtakatifu atajionyesha mwenyewe

kuwa mtakatifu kwa haki yake.

175:17 Sef 2:6, 14; Isa 32:14; 7:25; 17:2Kondoo watajilisha kwenye malisho yao wenyewe,

wana-kondoo watajilisha katika magofu ya matajiri.

185:18 Isa 59:4-8; 5:8; Amo 5:8; Yer 17:5; 23:14; Hos 11:4Ole wao wanaovuta dhambi kwa kamba za udanganyifu

na uovu kama kwa kamba za mkokoteni,

195:19 2Pet 3:3-4; Eze 12:22; Yer 17:15; Isa 30:11-12; 29:23; 1:4; 60:22kwa wale wanaosema, “Mungu na afanye haraka,

aharakishe kazi yake ili tupate kuiona.

Huo mpango wa Aliye Mtakatifu wa Israeli na ukamilike,

tena udhihirike ili tupate kuujua.”

205:20 Ay 24:13; Amo 5:7; Mwa 18:25; 1Fal 22:8; Za 94:21; Isa 5:8; Mt 6:22-23; Lk 11:22, 34-35Ole wao wanaoita ubaya ni wema,

na wema ni ubaya,

wawekao giza badala ya nuru,

na nuru badala ya giza,

wawekao uchungu badala ya utamu,

na utamu badala ya uchungu.

215:21 Mit 3:7; Rum 12:16; Isa 47:10; 1Kor 3:18-20Ole wao walio na hekima machoni pao wenyewe,

na kujiona wenye akili machoni pao wenyewe.

225:22 1Sam 25:36; Mit 23:20; Isa 22:13; Mit 31:4; Yer 7:18Ole wao walio mashujaa kwa kunywa mvinyo,

nao walio hodari katika kuchanganya vileo,

235:23 Kut 23:8; Amo 5:12; Yak 5:6; Eze 22:12; Isa 1:17; 29:21; 59:13-15; Za 94:21wale wanaoachilia wenye hatia kwa kupokea hongo,

lakini huwanyima haki wasio na hatia.

245:24 2Fal 19:20; Za 107:11; Ay 18:16; Isa 47:14; Ay 24:24; 40:8; 6:10; Isa 1:31; Nah 1:10; 2Fal 19:30Kwa hiyo, kama ndimi za moto zirambavyo nyasi,

na kama vile majani makavu yazamavyo katika miali ya moto,

ndivyo mizizi yao itakavyooza

na maua yao yatakavyopeperushwa kama mavumbi;

kwa kuwa wameikataa sheria ya Bwana Mwenye Nguvu Zote

na kulisukumia mbali neno la Aliye Mtakatifu wa Israeli.

255:25 2Fal 22:13; Yer 6:12; 2Fal 9:37; Dan 9:16; Ay 40:11; Kut 19:18; Isa 26:11; 10:17; Ay 40:11; Yer 6:12Kwa hiyo hasira ya Bwana inawaka dhidi ya watu wake,

mkono wake umeinuliwa na anawapiga.

Milima inatetemeka,

maiti ni kama takataka kwenye barabara.

Hata kwa haya yote, hasira yake haijageukia mbali,

mkono wake bado umeinuliwa juu.

265:26 Za 20:5; Isa 7:18; Zek 10:8; Kum 28:4-9; Isa 13:5; 18:2Yeye anainua bendera kwa ajili ya mataifa yaliyo mbali,

anapiga filimbi kwa ajili ya wale walio kwenye miisho ya dunia.

Tazama wamekuja,

kwa kasi na kwa haraka!

275:27 Yoe 2:7-8; Eze 23:15; Isa 22:21; 40:29-31; 14:31; Ay 12:18Hakuna hata mmoja wao anayechoka wala kujikwaa,

hakuna hata mmoja anayesinzia wala kulala,

hakuna mkanda uliolegezwa kiunoni,

hakuna gidamu ya kiatu iliyokatika.

285:28 Ay 39:23; Za 45:6; 7:12; Eze 26:11; Ay 1:19; Za 25:5; 2Fal 2:1Mishale yao ni mikali,

pinde zao zote zimevutwa,

kwato za farasi wao ziko kama jiwe la gumegume,

magurudumu ya magari yao ya vita ni kama upepo wa kisulisuli.

295:29 Isa 42:22; 49:24-25; 2Fal 17:25; Mik 5:8; Yer 51:38; Zek 11:3; Sef 3:3; Isa 10:6Ngurumo yao ni kama ile ya simba,

wananguruma kama wana simba,

wanakoroma wanapokamata mawindo yao,

na kuondoka nayo pasipo yeyote wa kuokoa.

305:30 Yer 4:23-28; Za 93:3; Yoe 2:10; Isa 2:1; 2:11; 50:3; Yer 50:42; Ay 21:30; Lk 21:25; 1Sam 2:9; Za 18:28Katika siku ile watanguruma juu yake

kama ngurumo za bahari.

Kama mtu akiitazama nchi,

ataona giza na dhiki;

hata nuru itatiwa giza kwa mawingu.

Священное Писание (Восточный перевод), версия с «Аллахом»

Исаия 5:1-30

Песнь о винограднике

1Я спою моему Другу

песню о Его винограднике:

Виноградник был у Друга моего

на плодородном холме.

2Он окопал его, от камней очистил

и засадил отборною лозою.

Он построил в нём сторожевую башню

и вытесал давильный пресс.

Он ждал от него плодов хороших –

а тот принёс дикие.

3– Теперь вы, жители Иерусалима и народ Иудеи,

рассудите Меня с Моим виноградником.

4Что ещё можно было сделать для него,

чего Я ещё не сделал?

Когда Я ждал плодов хороших,

почему он принёс дикие?

5Теперь Я скажу вам,

что Я сделаю с Моим виноградником:

отниму у него ограду,

и он будет опустошён;

разрушу его стену,

и он будет вытоптан.

6Я сделаю его пустошью,

не будут его ни подрезать, ни вскапывать;

зарастёт он терновником и колючками.

Я повелю облакам

не проливаться на него дождём.

7Виноградник Вечного, Повелителя Сил,

есть народ Исраила,

и народ Иудеи –

Его любимый сад.

Он ждал правосудия, но увидел кровопролитие,

ждал праведности, но услышал горестный крик.

Шестикратное горе

8Горе вам, прибавляющие дом к дому

и поле к полю,

так что другим не остаётся места,

словно вы одни на земле живёте!

9Я слышал, как Вечный, Повелитель Сил, сказал мне:

– Большие дома будут опустошены,

прекрасные особняки останутся без жителей.

10Виноградник в десять гектаров5:10 Букв.: «десятиупряжечный». Виноградник площадью равной полю, для вспашки которого десяти парам волов понадобился бы целый день. принесёт лишь немного5:10 Букв.: «один бат», т. е. 22 л. вина,

двести килограммов5:10 Букв.: «один хомер». семян – лишь полмешка5:10 Букв.: «одну ефу», т. е. 22 л (около 20 кг зерна). зерна.

11Горе тем, кто встаёт с утра пораньше,

чтобы пойти за пивом,

кто до самого вечера

разгорячается вином!

12У них на пирах арфы и лиры,

бубны, свирели, вино,

но о делах Вечного они не думают,

не вникают в деяния Его рук.

13Поэтому мой народ пойдёт в плен

из-за недостатка ведения;

его знать умрёт от голода,

его чернь будет томиться жаждой.

14Расширится мир мёртвых

и без меры разверзнет пасть;

сойдёт туда и знать, и чернь,

все крикуны и бражники.

15Унижены будут люди,

смирится всякий,

и глаза надменных потупятся.

16Но Вечный, Повелитель Сил, возвысится Своим правосудием,

святой Бог Своей праведностью явит Свою святость.

17И овцы будут пастись, как на своих пастбищах,

ягнята будут кормиться5:17 Или: «чужеземцы будут есть». среди разорённых домов богачей.

18Горе тем, кто обольщён грехом

и, словно впрягшись в повозку,

тянет за собой беззаконие.

19Они говорят: «Пусть Аллах поспешит,

пусть действует поскорее,

а мы на это посмотрим.

Пусть приблизится,

пусть исполнится замысел святого Бога Исраила,

и тогда мы будем знать».

20Горе тем, кто зло называет добром,

а добро – злом,

тьму считает светом,

а свет – тьмой,

горькое считает сладким,

а сладкое – горьким!

21Горе тем, кто мудр в своих глазах

и разумен сам пред собой!

22Горе тем, кто доблестен пить вино

и силён смешивать крепкие напитки,

23кто оправдывает виновного за взятку,

но лишает правосудия невиновного!

24За это, как языки огня съедают солому

и пламя пожирает сено,

сгниют их корни,

и цветы их разлетятся, как прах;

ведь они отвергли Закон Вечного, Повелителя Сил,

и презрели слово святого Бога Исраила.

25За это вспыхнет гнев Вечного на Его народ;

Он поднимет руку Свою на них и поразит их.

Вздрогнут горы,

и будут их трупы точно отбросы на улицах.

Но и тогда гнев Его не отвратится,

и рука Его ещё будет занесена.

26Он поднимает боевое знамя, призывая дальние народы,

свистом созывает тех, кто на краях земли.

И вот они идут

быстро и стремительно.

27Никто из них не устанет и не споткнётся,

никто не задремлет и не заснёт;

ни пояс у них на бёдрах не развяжется,

ни ремешок на сандалиях не лопнет.

28Остры у них стрелы,

все луки у них туги.

Кремню подобны копыта их коней,

урагану подобны колёса их колесниц.

29Их рык точно львиный,

они ревут, как молодые львы;

рычат, хватая добычу,

уносят её, и никто не отнимет.

30В тот день они взревут над добычей,

словно рёвом моря.

И если кто посмотрит на землю,

то увидит тьму и горе;

и облака застят свет.