Isaya 48 – NEN & CST

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Isaya 48:1-22

Israeli Mkaidi

148:1 Kum 6:13; Kut 23:13; Dan 8:12; Zek 8:3; Mwa 17:5; 29:35; Isa 19:18“Sikilizeni hili, ee nyumba ya Yakobo,

ninyi mnaoitwa kwa jina la Israeli,

na mnaotoka katika ukoo wa Yuda,

ninyi mnaoapa kwa jina la Bwana,

mnaomwomba Mungu wa Israeli,

lakini si katika kweli au kwa haki;

248:2 Neh 11:1; Rum 2:17; Mik 3:11; Isa 1:26; Mt 4:5; Isa 10:20; 47:4ninyi mnaojiita raiya wa mji mtakatifu,

na kumtegemea Mungu wa Israeli,

Bwana Mwenye Nguvu Zote ndilo jina lake:

348:3 Isa 40:21; 45:21; Yos 21:45; Isa 41:22; 17:14; 30:13Nilitoa unabii mambo ya kwanza tangu zamani,

kinywa changu kiliyatangaza na kuyafanya yajulikane;

kisha ghafula nikayatenda, nayo yakatokea.

448:4 Kum 9:27; 31:27; Mdo 5:21; Isa 9:9; Kut 32:9; Eze 3:9; Mdo 7:51Kwa kuwa nalijua jinsi ulivyokuwa mkaidi;

mishipa ya shingo yako ilikuwa chuma,

kipaji chako cha uso kilikuwa shaba.

548:5 Yer 44:15-18; Isa 42:9; 40:21Kwa hiyo nilikuambia mambo haya tangu zamani,

kabla hayajatokea nilikutangazia

ili usije ukasema,

‘Sanamu zangu zilifanya hayo;

kinyago changu cha mti na mungu wangu wa chuma aliyaamuru.’

648:6 Isa 41:22; Rum 16:25Umesikia mambo haya; yaangalie hayo yote.

Je, hutayakubali?

“Kuanzia sasa na kuendelea nitakueleza mambo mapya,

juu ya mambo yaliyofichika usiyoyajua.

748:7 Isa 65:18; 45:21; Kut 6:7Yameumbwa sasa, wala si tangu zamani;

hukupata kuyasikia kabla ya siku ya leo.

Hivyo huwezi kusema,

‘Naam, niliyajua hayo.’

848:8 Za 58:3; Kum 9:24; Isa 41:24; Mal 2:11-14; Isa 43:27Hujayasikia wala kuyaelewa,

tangu zamani sikio lako halikufunguka.

Ninafahamu vyema jinsi ulivyo mdanganyifu,

uliitwa mwasi tangu kuzaliwa kwako.

948:9 Yos 7:9; Ay 9:13; Za 78:38; 1Sam 12:22; Isa 37:35; 30:18Kwa ajili ya Jina langu mwenyewe

ninaichelewesha ghadhabu yangu,

kwa ajili ya sifa zangu nimeizuia isikupate,

ili nisije nikakukatilia mbali.

1048:10 Za 66:10Tazama, nimekusafisha, ingawa si kama fedha,

nimekujaribu katika tanuru ya mateso.

1148:11 1Sam 12:22; Law 18:21; Isa 42:8; Kum 32:26-27; Eze 20:9; Yer 14:7, 21Kwa ajili yangu mwenyewe,

kwa ajili yangu mwenyewe, nafanya hili.

Jinsi gani niliache Jina langu lichafuliwe?

Sitautoa utukufu wangu kwa mwingine.

Israeli Anawekwa Huru

1248:12 Isa 46:3; 41:4; Ufu 22:13; Isa 43:13; 42:6“Ee Yakobo, nisikilize mimi,

Israeli, ambaye nimekuita:

Mimi ndiye;

mimi ndimi mwanzo na mwisho.

1348:13 Ebr 1:10-12; Ay 9:8; Isa 34:16; 40:26; Kut 20:11; Isa 45:18Mkono wangu mwenyewe uliweka misingi ya dunia,

nao mkono wangu wa kuume umezitanda mbingu;

niziitapo, zote husimama pamoja.

1448:14 Isa 43:9; 46:10-11; 41:2, 22; Yer 50:45; Isa 21:9“Kusanyikeni, ninyi nyote, msikilize:

Ni ipi miongoni mwa hizo sanamu

ambayo imetabiri vitu hivi?

Watu wa Bwana waliochaguliwa na kuungana

watatimiza kusudi lake dhidi ya Babeli;

mkono wa Mungu utakuwa dhidi ya Wakaldayo.

1548:15 Amu 4:10; Isa 45:1Mimi, naam, Mimi, nimenena;

naam, nimemwita yeye.

Nitamleta,

naye atafanikiwa katika lile nililomtuma.

1648:16 Isa 45:19; Zek 2:8-11; Isa 33:13; 50:5-9; 11:2“Nikaribieni na msikilize hili:

“Tangu tangazo la kwanza sikusema kwa siri;

wakati litokeapo, nitakuwako hapo.”

Sasa Bwana Mwenyezi amenituma,

kwa Roho wake.

1748:17 Ay 19:25; Za 32:4; Isa 54:8; 47:4; 28:9; Yer 7:13; Isa 49:10Hili ndilo asemalo Bwana,

Mkombozi wako, yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli:

“Mimi ni Bwana, Mungu wako,

nikufundishaye ili upate faida,

nikuongozaye katika njia ikupasayo kuiendea.

1848:18 Kum 5:29; Isa 42:23; Za 147:14; 45:8; Isa 54:13; 33:21; 45:5Laiti ungesikiliza kwa makini maagizo yangu,

amani yako ingekuwa kama mto,

haki yako kama mawimbi ya bahari.

1948:19 Mwa 22:17; Ay 5:25; Yer 35:19; Isa 43:5; 61:9; Mwa 12:2; Isa 56:5Wazao wako wangekuwa kama mchanga,

watoto wako kama chembe zake zisizohesabika;

kamwe jina lao lisingefutiliwa mbali,

wala kuangamizwa kutoka mbele zangu.”

2048:20 Zek 2:6-7; Ufu 18:4; Isa 12:6; Mik 4:10; Isa 52:11; Yer 48:6; 50:8Tokeni huko Babeli,

kimbieni kutoka kwa Wakaldayo!

Tangazeni hili kwa kelele za shangwe

na kulihubiri.

Lipelekeni mpaka miisho ya dunia;

semeni, “Bwana amemkomboa

mtumishi wake Yakobo.”

2148:21 Isa 41:17; 33:16; 30:25; Kut 17:6; Za 105:41; Hes 20:11Hawakuona kiu alipowaongoza kupita jangwani;

alifanya maji yatiririke kutoka kwenye mwamba kwa ajili yao;

akapasua mwamba

na maji yakatoka kwa nguvu.

2248:22 Isa 3:11; 57:21; Ay 3:26“Hakuna amani kwa waovu,” asema Bwana.

Nueva Versión Internacional (Castilian)

Isaías 48:1-22

El Israel obstinado

1»Escuchad esto vosotros,

los de la familia de Jacob,

descendientes de Judá,

que llevan el nombre de Israel;

que juran en el nombre del Señor,

e invocan al Dios de Israel,

pero no con sinceridad ni justicia.

2Vosotros que os llamáis ciudadanos de la ciudad santa

y confiáis en el Dios de Israel,

cuyo nombre es el Señor Todopoderoso:

3Desde hace mucho tiempo

anuncié las cosas pasadas.

Yo las profeticé;

yo mismo las di a conocer.

Actué de repente,

y se hicieron realidad.

4Porque yo sabía que eres muy obstinado;

que tu cuello es un tendón de hierro,

y que tu frente es de bronce.

5Por eso te declaré esas cosas desde hace tiempo;

te las di a conocer antes que sucedieran,

para que no dijeras:

“¡Fue mi ídolo quien las hizo!

¡Mi imagen tallada o fundida las dispuso!”

6De todo esto has tenido noticia,

¿y no vas a proclamarlo?

»Desde ahora te haré conocer cosas nuevas;

cosas que te son ocultas y desconocidas.

7Son cosas creadas ahora, y no hace tiempo;

hasta hoy no habías oído hablar de ellas,

para que no dijeras:

“¡Sí, ya las sabía!”

8Nunca habías oído ni entendido;

nunca antes se te había abierto el oído.

Yo sé bien que eres muy traicionero,

y que desde tu nacimiento te llaman rebelde.

9Por amor a mi nombre contengo mi ira;

por causa de mi alabanza me refreno,

para no aniquilarte.

10¡Mira! Te he refinado, pero no como a la plata;

te he probado en el horno de la aflicción.

11Y lo he hecho por mí, por mí mismo.

¿Cómo puedo permitir que se me profane?

¡No cederé mi gloria a ningún otro!

Liberación de Israel

12»Escúchame, Jacob,

Israel, a quien he llamado:

Yo soy Dios;

yo soy el primero, y yo soy el último.

13Con la mano izquierda afirmé la tierra,

y con la derecha desplegué los cielos.

Yo pronuncié su nombre,

y todos ellos aparecieron.

14»Reuníos, todos vosotros, y escuchad:

¿Quién de ellos ha profetizado estas cosas?

El amado del Señor

ejecutará su propósito contra Babilonia;

su brazo estará contra los caldeos.

15Solo yo he hablado;

solo yo lo he llamado.

Lo haré venir,

y triunfará en su misión.

16»Acercaos a mí, escuchad esto:

»Desde el principio, jamás hablé en secreto;

cuando las cosas suceden, allí estoy yo».

Y ahora el Señor omnipotente

me ha enviado con su Espíritu.

17Esto es lo que dice el Señor,

tu Redentor, el Santo de Israel:

«Yo soy el Señor tu Dios,

que te enseña lo que te conviene,

que te guía por el camino en que debes andar.

18Si hubieras prestado atención a mis mandamientos,

tu paz habría sido como un río;

tu justicia, como las olas del mar.

19Como la arena serían tus descendientes;

como los granos de arena, tus hijos;

su nombre nunca habría sido eliminado

ni borrado de mi presencia».

20¡Salid de Babilonia!

¡Huid de los caldeos!

Anunciad esto con gritos de alegría

y hacedlo saber.

Publicadlo hasta en los confines de la tierra;

decid: «El Señor ha redimido a su siervo Jacob».

21Cuando los guio a través de los desiertos,

no tuvieron sed;

hizo que de la roca brotara agua para ellos;

partió la roca, y manaron las aguas.

22«No hay paz para el malvado»,

dice el Señor.