Isaya 47 – NEN & KLB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Isaya 47:1-15

Anguko La Babeli

147:1 Mao 2:10; Isa 21:9; 23:12; Yer 51:33; Zek 2:7; Ay 2:13; Isa 29:4“Shuka uketi mavumbini,

ee Bikira Binti Babeli;

keti chini pasipo na kiti cha enzi,

ee binti wa Wakaldayo.

Hutaitwa tena mwororo wala wa kupendeza.

247:2 Mt 24:41; Kut 11:5; Amu 16:21; Mwa 24:65; Isa 32:11Chukua mawe ya kusagia, usage unga,

vua shela yako.

Pandisha mavazi yako, ondoa viatu vyako,

vuka vijito kwa shida.

347:3 Mwa 2:25; Rum 12:19; Neh 3:5; Isa 13:18-19; 20:4; 34:8; Eze 16:37Uchi wako utafunuliwa

na aibu yako itaonekana.

Nitalipa kisasi;

sitamhurumia hata mmoja.”

447:4 Yer 50:34; Amo 4:13; Isa 48:2, 17; Ay 19:25Mkombozi wetu: Bwana Mwenye Nguvu Zote ndilo jina lake;

ndiye yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli.

547:5 Dan 2:37; Isa 13:10, 19; 9:2; 21:9; Ufu 17:18; Ay 2:13; Ufu 18:7“Keti kimya, ingia gizani,

Binti wa Wakaldayo,

hutaitwa tena malkia wa falme.

647:6 2Nya 28:9; Isa 10:13; Zek 1:15; Kum 13:15; Yer 50:11; Isa 14:6; 42:24Niliwakasirikia watu wangu

na kuaibisha urithi wangu;

niliwatia mikononi mwako,

nawe hukuwaonea huruma.

Hata juu ya wazee

uliweka nira nzito sana.

747:7 Ufu 18:7; Kum 32:29; Isa 10:13; Dan 4:30; Isa 42:23-25Ukasema, ‘Nitaendelea

kuwa malkia milele!’

Lakini hukutafakari mambo haya

wala hukuwaza juu ya kile kingeweza kutokea.

847:8 Isa 32:9; 45:6; 49:21; 54:4; Sef 2:15; Ufu 18:7“Sasa basi, sikiliza, ewe kiumbe mpenda anasa,

ukaaye mahali pako pa salama,

na kujiambia mwenyewe,

‘Mimi ndiye, wala hakuna mwingine zaidi yangu.

Kamwe sitakuwa mjane,

wala sitafiwa na watoto.’

947:9 1The 5:3; Isa 13:8; Nah 3:4; Za 55:15; Mal 3:5; Kum 18:10-11; Ufu 9:21; 18:8-10Haya mawili yatakupata, kufumba na kufumbua,

katika siku moja:

kufiwa na watoto, na ujane.

Yote yatakupata kwa kipimo kikamilifu,

ijapokuwa uchawi wako ni mwingi,

na uaguzi wako ni mwingi.

1047:10 Ay 15:31; 2Fal 21:16; Isa 5:21; 29:15; Za 52:7; 62:10Umeutegemea uovu wako,

nawe umesema, ‘Hakuna yeyote anionaye.’

Hekima yako na maarifa yako vinakupoteza

unapojiambia mwenyewe,

‘Mimi ndiye, wala hakuna mwingine zaidi yangu.’

1147:11 Dan 5:30; Za 55:15; 1The 5:3; Isa 10:3; 14:15; 21:9; Lk 17:27; Isa 17:14Maafa yatakujia,

nawe hutaweza kuyaondoa kwa uaguzi.

Janga litakuangukia,

wala hutaweza kulikinga kwa fidia;

msiba mkuu usioweza kuutabiri

utakujia ghafula.

1247:12 Kut 7:11“Endelea basi na uaguzi wako,

na wingi wa uchawi wako,

ambao umeutumikia tangu utoto wako.

Labda utafanikiwa,

labda unaweza ukasababisha hofu kuu.

1347:13 Yer 51:58; Hab 2:13; Isa 19:3; 5:29; 43:13; 57:10; 46:7; Dan 2:2Ushauri wote uliopokea umekuchosha bure!

Wanajimu wako na waje mbele,

wale watazama nyota watabiriao mwezi baada ya mwezi,

wao na wawaokoe na lile linalokuja juu yenu.

1447:14 Isa 5:24; Nah 1:10; Yer 50:30-32; Isa 30:30; 10:17Hakika wako kama mabua makavu;

moto utawateketeza.

Hawawezi hata kujiokoa wao wenyewe

kutokana na nguvu za mwali wa moto.

Hapa hakuna makaa ya kumtia mtu yeyote joto;

hapa hakuna moto wa kuota.

1547:15 Ufu 18:11; Isa 44:17Hayo ndiyo yote wanayoweza kuwatendea ninyi,

hawa ambao umetaabika nao

na kufanya nao biashara tangu utoto.

Kila mmoja atatoroka;

hakuna yeyote awezaye kukuokoa.

Korean Living Bible

이사야 47:1-15

바빌론에 대한 심판

1여호와께서 말씀하신다. “처녀처럼 한 번도 정복당해 보지 않은 바 빌론아, 네 보좌에서 내려와 땅에 앉아라. 이제는 너의 화려하던 시절이 끝났다. 네가 다시는 곱고 아름답다는 말을 듣지 못할 것이다.

2맷돌을 돌려 곡식을 갈아라. 너는 베일을 벗고 치마를 걷어 다리를 드러내고 강을 건너라.

3네 살이 드러나고 너의 부끄러운 곳이 보일 것이다. 내가 복수할 것이니 한 사람도 아끼지 않을 것이다.”

4이스라엘의 거룩하신 하나님은 우리의 구원자가 되시니 그의 이름은 전능하신 여호와이시다.

5여호와께서 말씀하신다. “47:5 또는 ‘딸 갈대아여’바빌론아, 말없이 앉아 있어라. 흑암으로 들어가거라. 다시는 너를 세계의 여왕이라고 부를 사람이 없을 것이다.

6내가 내 백성에게 분노하여 그들을 욕되게 하고 네 손에 맡겼으나 네가 그들에게 자비를 베풀지 않고 늙은 노인들까지 가혹하게 다루었다.

7너는 항상 여왕이라는 생각만 했지 내 백성을 학대하는 일과 그 일의 결과에 대해서는 조금도 생각하지 않았다.

8편안히 살면서 쾌락을 사랑하는 자여, 들어라. 너는 너와 같은 신이 없다고 생각하며 과부가 되거나 자녀를 잃는 일이 없을 것이라고 말하고 있다.

9그러나 네가 과부가 되고 자녀를 잃는 이 두 가지 일이 단 하루 만에 갑자기 일어날 것이다. 네가 아무리 마술을 행하고 주문을 외워도 반드시 그런 일을 당하고 말 것이다.

10너는 악을 행하고도 안전하리라고 생각하며 너를 보는 자가 아무도 없다고 말한다. 네가 ‘나는 신이며 나 외에는 아무도 없다’ 고 말하니 네 지혜와 지식이 너를 잘못된 길로 인도하였구나.

11그러므로 너에게 재앙이 닥칠 것이다. 네가 아무리 주문을 외워도 그것을 쫓아 버릴 방도를 알지 못할 것이다. 네가 예상하지 못한 파멸이 갑자기 너를 덮칠 것이니 네가 그것을 피할 방법이 없을 것이다.

12“네가 어렸을 때부터 사용해 온 마술과 주문으로 버텨 보아라. 어쩌면 그것이 도움이 되어 네 원수들에게 공포를 일으킬지도 모른다.

13너는 수많은 조언으로 지쳐 있다. 점성가들과 달과 별을 보고 예언하는 자들이 네가 당할 재앙에서 너를 구하게 하라.

14보라! 그들은 다 지푸라기 같아서 불에 타고 말 것이다. 그들이 그 불의 세력에서 자신을 구원할 수 없을 것이다. 이 불은 곁에 앉아서 몸을 따뜻하게 할 숯불이 아니다.

15네가 어렸을 때부터 너와 함께 수고하고 무역하던 자들도 너에게 도움이 되지 않을 것이다. 그들이 다 너를 버리고 자기 길로 갈 것이니 너를 구해 줄 자가 없을 것이다.”