Isaya 46 – NEN & KLB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Isaya 46:1-13

Miungu Ya Babeli

146:1 Yer 51:44; Isa 45:20; 21:9; Yer 50:2Beli anasujudu hadi nchi, Nebo anainama;

sanamu zao zabebwa na wanyama wa mizigo.

Vinyago hivi mnavyobeba kila mahali ni mzigo wa kulemea,

mzigo kwa waliochoka.

246:2 2Sam 5:21; Yer 51:47; Amu 18:17-18Vinyago pamoja na wale wanaovibeba wanainama chini;

hiyo miungu haiwezi kuwaokoa watu,

wote wanakwenda utumwani pamoja.

346:3 Isa 48:12; Kut 19:14; Isa 44:2; Kum 1:31; Za 28:9; 22:10“Nisikilizeni mimi, ee nyumba ya Yakobo,

ninyi nyote mliobaki wa nyumba ya Israeli,

ninyi ambao nimewategemeza tangu mlipotungwa mimba,

nami nimewabeba tangu kuzaliwa kwenu.

446:4 Mal 3:6; Za 71:18; Isa 43:13; Kum 32:39; Za 18:35; 119:117Hata mpaka wakati wa uzee wenu na mvi, Mimi ndiye,

Mimi ndiye nitakayewasaidia ninyi.

Nimewahuluku, nami nitawabeba,

nitawasaidia ninyi na kuwaokoa.

546:5 Kut 15:11; Ay 41:10; Isa 40:18, 25; Yer 49:19“Mtanilinganisha na nani, au mtanihesabu kuwa sawa na nani?

Ni nani mtakayenifananisha naye ili tuweze kulinganishwa?

646:6 Kut 20:5; Hos 13:2; Isa 40:19; 44:17Wengine humwaga dhahabu kutoka kwenye mifuko yao,

na kupima fedha kwenye mizani;

huajiri mfua dhahabu kutengeneza mungu,

kisha huisujudia na kuiabudu.

746:7 1Sam 5:3; Isa 41:7; 1Fal 16:26Huiinua mabegani na kuichukua;

huiweka mahali pake, papo hapo ndipo isimamapo.

Wala haiwezi kusogea kutoka mahali pale.

Ingawa mtu huililia, haimjibu;

haiwezi kumwokoa kwenye taabu zake.

846:8 Isa 44:21; 1:2“Kumbukeni hili, litieni akilini,

liwekeni moyoni, enyi waasi.

946:9 Kum 8:10; Kut 8:10; Mk 12:32; Isa 41:22; 45:21Kumbukeni mambo yaliyopita, yale ya zamani za kale;

mimi ndimi Mungu, wala hakuna mwingine;

mimi ndimi Mungu,

wala hakuna mwingine aliye kama mimi.

1046:10 Mit 19:21; Efe 1:11; Mdo 5:39; Isa 45:21; 41:22; 7:7-9; 44:26Ni mimi nitangazaye mwisho tangu mwanzo,

naam, tangu zamani za kale,

mambo ambayo hayajatendeka.

Ninasema: Kusudi langu ndilo litakalosimama,

nami nitatenda mapenzi yangu yote.

1146:11 Mwa 41:25; Yer 44:28; Amu 4:10; Ezr 1:2; Isa 8:5Kutoka mashariki ninaita ndege awindaye;

kutoka nchi ya mbali,

mtu atakayetimiza kusudi langu.

Lile ambalo nimelisema, ndilo nitakalolitimiza;

lile nililolipanga, ndilo nitakalolitenda.

1246:12 Yer 2:5; Za 119:150; Rum 10:3; Kut 32:9; Isa 9:9Nisikilizeni, ninyi wenye mioyo migumu,

ninyi mlio mbali na haki.

1346:13 Isa 24:23; Mdo 13:36; Rum 1:17; Isa 1:26; 45:8; Rum 3:21; Yoe 2:32Ninaleta haki yangu karibu,

haiko mbali;

wala wokovu wangu hautachelewa.

Nitawapa Sayuni wokovu,

Israeli utukufu wangu.

Korean Living Bible

이사야 46:1-13

바빌론의 우상과 살아 계신 하나님

1바빌론의 우상들이 쓰러졌다. 벨과 느보가 한때는 경배를 받았으 나 이제는 나귀 등에 실려 피곤한 짐승의 짐이 되고 말았구나.

2그 우상들은 구부러지고 엎드러졌으니 그들은 자신을 구하지 못하고 사로잡혀 끌려가고 말았다.

3여호와께서 말씀하신다. “야곱의 후손들아, 남아 있는 이스라엘 사람들아, 내 말을 들어라. 나는 너희를 창조하였고 너희가 태어날 때부터 너희를 보살펴 왔다.

4나는 너희가 늙어 백발이 될 때까지 너희 하나님이 되어 너희를 보살필 것이다. 내가 너희를 만들었으니 너희를 돌보고 보살필 것이며 너희를 도와주고 구해 주겠다.

5도대체 나와 같은 자가 어디 있느냐? 너희가 나를 누구와 비교할 수 있겠느냐?

6사람들이 주머니를 열어 금을 쏟아내고 은을 저울에 달며 금세공업자를 고용하여 그것으로 신을 만들어 절하고 섬긴다.

7그들이 그것을 어깨에 메어다가 일정한 곳에 두면 그것은 제자리에 서서 움직이지 못하며 사람이 기도하여도 응답해 주지 못하고 그를 환난에서 구해 주지 못한다.

8“너희 죄인들아, 이 일을 기억하고 마음에 새겨라.

9너희는 오래 전에 있었던 옛일을 기억하라. 나는 하나님이다. 나 외에는 다른 신이 없고 나와 같은 자도 없다.

10나는 처음부터 일의 결과를 말하였으며 오래 전에 벌써 앞으로 일어날 일을 예언하였고 내 계획이 실패하지 않을 것이며 내가 원하는 것을 모두 행할 것이라고 말하였다.

11내가 멀리 동방에서 내 뜻을 이룰 독수리 같은 자를 부를 것이다. 내가 말하고 계획한 것이니 분명히 이루고 말 것이다.

12의에서 멀리 떠난 악하고 고집스런 사람들아, 내 말을 들어라!

13나의 의로운 구원이 가까웠으니 머지않다. 내가 지체하지 않고 시온에 구원을 베풀어 이스라엘에 내 영광을 나타낼 것이다.”