Isaya 43 – NEN & CCB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Isaya 43:1-28

Mwokozi Pekee Wa Israeli

143:1 Mwa 2:7; 32:28; Isa 45:3-4; Kut 6:6; Isa 42:6; 27:11; Ay 19:25Lakini sasa hili ndilo asemalo Bwana,

yeye aliyekuumba, ee Yakobo,

yeye aliyekuhuluku, ee Israeli:

“Usiogope kwa maana nimekukomboa,

nimekuita wewe kwa jina lako, wewe u wangu.

243:2 Mwa 26:3; Kum 31:6-8; Isa 30:27; 8:7; Dan 3:25-27; Kut 14:22; Isa 29:6Unapopita kwenye maji makuu,

nitakuwa pamoja nawe,

unapopita katika mito ya maji,

hayatakugharikisha.

Utakapopita katika moto,

hutaungua,

miali ya moto haitakuunguza.

343:3 Mit 21:18; Kut 30:2; Isa 20:3; Mwa 10:7; Eze 29:20; Za 68:31; Amu 2:18; Kut 14:30Kwa kuwa Mimi ndimi Bwana, Mungu wako,

yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli, Mwokozi wako.

Ninaitoa Misri kuwa fidia yako,

Kushi na Seba badala yako.

443:4 Isa 63:9; Ufu 3:9; Kut 19:5-6; Isa 49:5Kwa kuwa wewe ni wa thamani na wa kuheshimiwa machoni pangu,

nami kwa kuwa ninakupenda,

nitatoa watu badala yako

na mataifa badala ya maisha yako.

543:5 Isa 44:2; Mwa 21:22; Kut 14:22; Mdo 18:10; Yer 30:10-11; Mt 8:11; Zek 8:7; Isa 24:14Usiogope, kwa kuwa mimi nipo pamoja nawe,

nitawaleta watoto wako kutoka mashariki,

na kukukusanya kutoka magharibi.

643:6 Eze 16:61; 2Kor 6:18; Eze 36:24; Yer 23:8; Kum 30:4; Isa 60:4; 11:12Nitaiambia kaskazini, ‘Watoe!’

nayo kusini, ‘Usiwazuie.’

Walete wana wangu kutoka mbali,

na binti zangu kutoka miisho ya dunia:

743:7 Yak 2:7; Isa 29:23; Yer 15:16; Efe 2:10; Isa 56:5; 62:2; 63:19; Za 89:9kila mmoja ambaye ameitwa kwa Jina langu,

niliyemuumba kwa utukufu wangu,

niliyemhuluku na kumfanya.”

843:8 Isa 6:9-10; 42:20; Eze 12:2Uwaongoze wale wenye macho lakini hawaoni,

wenye masikio lakini hawasikii.

943:9 Isa 45:20; 48:14; 41:26Mataifa yote yanakutanika pamoja,

na makabila yanakusanyika.

Ni nani miongoni mwao aliyetangulia kutuambia haya,

na kututangazia mambo yaliyopita?

Walete mashahidi wao ili kuwathibitisha kuwa walikuwa sahihi,

ili wengine waweze kusikia, waseme, “Ni kweli.”

1043:10 Isa 41:8-9; 19:21; Za 86:10; Yer 14:22; Yos 24:22; Kum 4:35; Isa 45:5-6, 14“Ninyi ni mashahidi wangu,” asema Bwana,

“na mtumishi wangu niliyemchagua,

ili mpate kunijua na kuniamini,

na kutambua kwamba Mimi ndiye.

Kabla yangu hakuna mungu aliyefanyizwa,

wala hatakuwepo mwingine baada yangu.

1143:11 Isa 42:8; Za 18:31; Isa 25:9; 63:4; Kut 6:2Mimi, naam mimi, ndimi Bwana,

zaidi yangu hakuna mwokozi.

1243:12 Kum 32:16; Za 81:9; Isa 44:8Nimedhihirisha, kuokoa na kutangaza:

Mimi, wala si mungu mgeni katikati yenu.

Ninyi ni mashahidi wangu,” asema Bwana,

“kwamba Mimi ndimi Mungu.

1343:13 Hes 23:8; Ay 9:12; Za 90:2; Mit 8:23; Kum 32:39; Isa 48:12Naam, tangu siku za kale, Mimi ndiye.

Hakuna hata mmoja awezaye kuokoa

kutoka mkononi wangu.

Mimi ninapotenda,

ni nani awezaye kutangua?”

Huruma Za Mungu, Na Kukosa Uaminifu Kwa Israeli

1443:14 Isa 13:14-15; 23:13; Kut 15:13; Ay 19:25; Isa 41:20Hili ndilo Bwana asemalo,

Mkombozi wako, yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli:

“Kwa ajili yenu nitatumana Babeli

na kuwaleta Wakaldayo wote kama wakimbizi,

katika meli walizozionea fahari.

1543:15 Isa 42:8; 27:11; 45:11; 41:21Mimi ndimi Bwana, yeye Aliye Mtakatifu wako,

Muumba wa Israeli, Mfalme wako.”

1643:16 Kut 14:29; Za 77:19; Kut 15:8; Isa 11:15Hili ndilo asemalo Bwana,

yeye aliyefanya njia baharini,

mahali pa kupita kwenye maji mengi,

1743:17 Za 118:12; Kut 14:4-9, 22; Za 76:5-6; Ay 13:25; Yer 51:21; Eze 38:4aliyeyakokota magari ya vita na farasi,

jeshi pamoja na askari wa msaada,

nao wakalala huko, wala hawatainuka tena kamwe,

wakakomeshwa, na wakazimika kama utambi:

1843:18 Isa 41:22“Msiyakumbuke mambo yaliyopita,

wala msiyatafakari mambo ya zamani.

1943:19 Hes 20:11; Yer 23:8-9; Ufu 21:5; Isa 40:3; 41:22; Yer 16:14-15; 2Kor 5:17; Isa 35:7Tazama, nitafanya jambo jipya!

Sasa litachipuka, je, hamtalitambua?

Nitafanya njia jangwani

na vijito vya maji katika nchi kame.

2043:20 Hes 20:8; Isa 48:21; 41:17; Za 148:10; Isa 13:22Wanyama wa mwituni wataniheshimu,

mbweha na bundi,

kwa sababu ninawapatia maji jangwani,

na vijito katika nchi kame,

ili kuwapa watu wangu maji, wale niliowachagua,

2143:21 Za 66:2; 1Pet 2:9; Mwa 2:7; Mal 3:17; Za 102:18watu wale niliowaumba kwa ajili yangu,

ili wapate kutangaza sifa zangu.

22“Hata hivyo hukuniita mimi, ee Yakobo,

hujajitaabisha kwa ajili yangu, ee Israeli.

2343:23 Zek 7:5-6; Kut 30:35; Yer 7:22; Amo 5:25; Kut 29:41; Mik 6:3; Mal 1:12-13Hujaniletea kondoo kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa,

wala kuniheshimu kwa dhabihu zako.

Sikukulemea kwa sadaka za nafaka

wala kukuchosha kwa kuhitaji uvumba.

2443:24 Kut 30:23; Mal 2:17; Isa 7:13; Yer 8:21; Law 3:9; Yer 44:22Hukuninunulia uvumba wowote wenye manukato,

wala hukunipa kwa ukarimu

mafuta ya wanyama wa dhabihu zako.

Lakini umenilemea kwa dhambi zako,

na kunitaabisha kwa makosa yako.

2543:25 2Sam 12:13; Lk 5:21; Eze 20:44; Yer 31:34; Ay 7:21; 2Nya 6:21; Isa 64:9“Mimi, naam mimi, ndimi nizifutaye dhambi zako,

kwa ajili yangu mwenyewe,

wala sizikumbuki dhambi zako tena.

2643:26 Isa 1:18; 41:1; 49:25; 50:8Tafakari mambo yaliyopita,

njoo na tuhojiane,

leta shauri lako uweze kupewa haki yako.

2743:27 Rum 5:12; Isa 28:7; Yer 5:31; Mwa 12:18; Isa 9:15; 24:20Baba yako wa kwanza alitenda dhambi,

wasemaji wako wameasi dhidi yangu.

2843:28 Eze 5:15; Za 39:8; Hes 5:27; Kum 13:15; Isa 42:24; Zek 5:3; Yer 24:9Kwa hiyo nitawaaibisha wakuu wa Hekalu lako,

nami nitamtoa Yakobo aangamizwe,

na Israeli adhihakiwe.

Chinese Contemporary Bible (Simplified)

以赛亚书 43:1-28

以色列的唯一救主

1雅各啊,以色列啊,创造你、使你成形的耶和华说:

“不要害怕,我已经救赎了你;

我点名呼召了你,你属于我。

2你穿越洪涛,我必与你同在;

你渡过江河,必不会被水淹没;

你在火中走过,必不会被烧伤,

火焰不会烧到你身上。

3因为我是你的上帝耶和华,

以色列的圣者,是你的救主。

我用埃及作你的赎价,

使古实西巴代替你。

4我珍视你,看重你,深爱你,

所以我用他人代替你,

用列邦交换你的生命。

5不要害怕,因为我与你同在,

我必从东方、从西方召集你和你的儿女。

6我要对北方说,‘交出来!’

对南方说,‘不要扣留!’

要从远方把我的儿子们带来,

从地极把我的女儿们领回。

7所有属于我的人都要回来,

他们是我为自己的荣耀而创造的。

8“要把那些有眼看不见、

有耳听不见的人带出来。

9让万国聚集,列邦会合。

他们的神明中谁曾启示这事?

谁曾预言所发生的事?

他们可以找证人来证实,

好叫听见的人都说这是真的。

10耶和华说:

以色列人啊,你们是我的证人,

我拣选你们做我的仆人,

要叫你们认识我,相信我,

明白我是耶和华,

在我以前没有上帝,

在我以后也没有。

11唯有我是耶和华,

除我以外没有别的救主。

12我曾启示,我曾拯救,

我曾宣告。

你们中间没有别的神明。

我是上帝,你们是我的证人。’

这是耶和华说的。

13‘我从太初就是上帝。

无人能逃脱我的手。

谁能阻挠我行事呢?’”

14你们的救赎主耶和华——以色列的圣者说:

“为了你们的缘故,

我必派大军进攻巴比伦

使迦勒底人坐着他们引以为荣的船逃亡。

15我是你们的圣者耶和华,

以色列的创造主,

是你们的君王。”

16耶和华曾在汹涌的大海中开辟道路。

17祂使埃及的战车、马匹、军兵、

勇士倾巢而出,

一同倒下,不再起来,

像熄灭的灯火一样灭没。

18耶和华说:

“不要想念过去,

不要留恋往事。

19看啊,我要行一件新事,

这事现在就要发生,

难道你们没有察觉吗?

我要在旷野辟道路,

在沙漠开江河。

20旷野的走兽必尊崇我,

其中有豺狼和鸵鸟,

因为我使旷野有甘泉,

使沙漠有江河,

供我拣选的子民饮用。

21他们是我为自己所造的子民,

他们要颂扬我。

22雅各啊,你却没有求告我;

以色列啊,你竟然厌烦我。

23你没有带来作燔祭的羊,

也没有用祭物来尊崇我。

我没有让你因祭物而受累,

也没有让你因香料而烦扰。

24你并没有花钱买菖蒲献给我,

也没有用祭物的脂肪满足我,

反而使我因你的罪恶而受累,

因你的过犯而烦扰。

25“我,是我为自己的缘故,

除去你的过犯,忘掉你的罪恶。

26你可以提醒我,你我可以理论,

你可以提出理由证明自己的清白。

27你的始祖犯了罪,

你的首领也背叛了我。

28所以我要使你圣殿的祭司受辱,

使雅各遭毁灭,

使以色列被辱骂。