Isaya 41 – NEN & NIRV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Isaya 41:1-29

Msaidizi Wa Israeli

141:1 Za 37:7; Isa 48:16; 50:8; Hab 2:20; Zek 2:13; Isa 11:11; 1Sam 2:4“Nyamazeni kimya mbele zangu, enyi visiwa!

Mataifa na wafanye upya nguvu zao!

Wao na wajitokeze, kisha waseme,

tukutane pamoja mahali pa hukumu.

241:2 2Sam 22:43; Isa 40:24; Yer 51:11; Ezr 1:2; Isa 44:28; Yer 50:3; 25:9“Ni nani aliyemchochea mmoja kutoka mashariki,

akimwita katika haki kwa utumishi wake?

Huyatia mataifa mikononi mwake,

na kuwatiisha wafalme mbele zake.

Huwafanya kuwa mavumbi kwa upanga wake,

huwafanya makapi yapeperushwayo na upepo kwa upinde wake.

341:3 Dan 8:4Huwafuatia na kuendelea salama,

katika njia ambayo miguu yake haijawahi kupita.

441:4 Isa 48:12; Ufu 22:13; Mdo 15:18; Isa 43:7; Kum 32:29Ni nani aliyefanya jambo hili na kulitimiliza,

akiita vizazi tangu mwanzo?

Mimi, Bwana, ni wa kwanza

nami nitakuwa pamoja na wa mwisho:

mimi Bwana ndiye.”

541:5 Eze 26:17-18; Kum 30:4; Isa 11:11-12Visiwa vimeliona na kuogopa,

miisho ya dunia inatetemeka.

Wanakaribia na kuja mbele,

641:6 Isa 1:6kila mmoja humsaidia mwingine

na kusema kwa ndugu yake, “Uwe hodari!”

741:7 Isa 40:19; 44:13; Yer 30:3-5Fundi humtia moyo sonara,

yeye alainishaye kwa nyundo

humhimiza yeye agongeaye kwenye fuawe,

Humwambia yeye aunganishaye, “Ni kazi njema.”

Naye huikaza sanamu kwa misumari ili isitikisike.

841:8 Mwa 18:19; Isa 29:22; Neh 9:7; 2Nya 20:7; Yak 2:23; Isa 63:16; Za 136:22“Lakini wewe, ee Israeli, mtumishi wangu,

Yakobo, niliyemchagua,

ninyi wazao wa Abrahamu rafiki yangu,

941:9 Isa 37:16; Kum 7:6; Isa 20:3; 11:12nilikuchukua toka miisho ya dunia,

nilikuita kutoka pembe zake za mbali.

Nilisema, ‘Wewe ni mtumishi wangu’;

nimekuchagua, wala sikukukataa.

1041:10 Kum 3:22; Rum 8:3; Isa 49:8; Yer 30:10; 46:27-28; Ay 40:14; Za 18:35Hivyo usiogope, kwa maana niko pamoja nawe;

usifadhaike, kwa maana mimi ni Mungu wako.

Nitakutia nguvu na kukusaidia;

nitakutegemeza kwa mkono wa kuume wa haki yangu.

1141:11 Isa 17:12; 54:17; Kut 23:22; Isa 29:8; Zek 12:3; Yer 2:3; Isa 29:23“Wote walioona hasira dhidi yako

hakika wataaibika na kutahayarika,

wale wakupingao

watakuwa kama vile si kitu, na kuangamia.

1241:12 Za 37:35-36; Isa 34:12; Ay 7:8; Isa 29:20; 17:14Ingawa utawatafuta adui zako,

hutawaona.

Wale wanaopigana vita dhidi yako

watakuwa kama vile si kitu kabisa.

1341:13 Za 73:23; Isa 42:6; 45:1; 51:18Kwa maana Mimi ndimi Bwana, Mungu wako,

nikushikaye mkono wako wa kuume

na kukuambia, Usiwe na hofu,

nitakusaidia.

1441:14 Ay 4:19; Za 22:6; Kut 15:13; Ay 19:23; Isa 1:27Usiogope, ee Yakobo uliye mdudu,

ee Israeli uliye mdogo,

kwa kuwa Mimi mwenyewe nitakusaidia,” asema Bwana,

Mkombozi wako, yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli.

1541:15 Ay 41:30; Mik 4:13; Isa 21:10; Kut 19:18; Yer 9:10; Eze 33:28“Tazama, nitakufanya chombo cha kupuria,

kipya na chenye makali, chenye meno mengi.

Utaipura milima na kuiponda

na kuvifanya vilima kuwa kama makapi.

1641:16 Yer 51:2; Isa 45:25; 60:19; Dan 2:35; Yer 15:7; Isa 25:9; Mk 1:24Utaipepeta, nao upepo utaichukua,

dhoruba itaipeperushia mbali.

Bali wewe utajifurahisha katika Bwana

na katika utukufu wa yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli.

1741:17 Isa 43:20; 35:7; 30:19“Maskini na wahitaji wanatafuta maji,

lakini hayapo,

ndimi zao zimekauka kwa kiu.

Lakini Mimi Bwana nitawajibu,

Mimi, Mungu wa Israeli, sitawaacha.

1841:18 Isa 30:25; 43:19; Ay 38:26; Isa 35:7; 2Fal 3:17Nitaifanya mito itiririke juu ya vilima vilivyo kame,

nazo chemchemi ndani ya mabonde.

Nitaligeuza jangwa liwe mabwawa ya maji,

nayo ardhi iliyokauka kuwa chemchemi za maji.

1941:19 Isa 60:13; Kut 25:10-13; Isa 37:24; 44:14Katika jangwa nitaotesha

mwerezi, mshita, mhadasi na mzeituni.

Nitaweka misunobari, mivinje na misanduku

pamoja huko nyikani,

2041:20 Ay 12:9; Isa 4:5ili kwamba watu wapate kuona na kujua,

wapate kufikiri na kuelewa,

kwamba mkono wa Bwana umetenda hili,

kwamba yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli ndiye alilifanya.”

2141:21 Isa 43:14; 44:6Bwana asema, “Leta shauri lako.

Toa hoja yako,” asema Mfalme wa Yakobo.

2241:22 Isa 48:14; 65:17; Yn 13:19; Isa 43:9; 45:21“Leteni sanamu zenu zituambie

ni nini kitakachotokea.

Tuambieni mambo ya zamani yalikuwa nini,

ili tupate kuyatafakari

na kujua matokeo yake ya mwisho.

Au tutangazieni mambo yatakayokuja,

2341:23 Kum 18:22; Isa 44:7-8; Yer 10:5; Isa 43:5; 2Fal 19:26tuambieni ni nini kitakachotokea baadaye,

ili tupate kujua kuwa ninyi ni miungu.

Fanyeni jambo lolote zuri au baya,

ili tupate kutishika na kujazwa na hofu.

2441:24 Isa 37:19; 1Kor 8:4; Za 115:8; 1Sam 12:21; Isa 48:8Lakini ninyi ni zaidi ya bure kabisa,

na kazi zenu hazifai kitu kabisa;

yeye awachaguaye ni chukizo sana.

2541:25 Yer 51:48; Nah 3:14; 2Sam 22:43; Yer 50:9“Nimemchochea mtu mmoja kutoka kaskazini,

naye yuaja, mmoja toka mawio ya jua aliitaye Jina langu.

Huwakanyaga watawala kana kwamba ni matope,

kama mfinyanzi akanyagavyo udongo wa kufinyangia.

2641:26 Hab 2:18-19; 1Fal 18:26; Isa 52:6Ni nani aliyenena hili tokea mwanzoni, ili tupate kujua,

au kabla, ili tuweze kusema, ‘Alikuwa sawa’?

Hakuna aliyenena hili,

hakuna aliyetangulia kusema hili,

hakuna yeyote aliyesikia maneno kutoka kwenu.

2741:27 Isa 48:3, 16; 40:9Nilikuwa wa kwanza kumwambia Sayuni,

‘Tazama, wako hapa!’

Nilimpa Yerusalemu mjumbe wa habari njema.

2841:28 Eze 22:30; Za 22:11; Isa 40:13-14; 50:2; 59:16; 64:7; Yer 25:4Ninatazama, lakini hakuna yeyote:

hakuna yeyote miongoni mwao awezaye kutoa shauri,

hakuna yeyote wa kutoa jibu wakati ninapowauliza.

2941:29 Yer 5:13; 1Sam 12:21; Isa 37:19Tazama, wote ni ubatili!

Matendo yao ni bure;

vinyago vyao ni upepo mtupu na machafuko.

New International Reader’s Version

Isaiah 41:1-29

The Lord Helps Israel

1The Lord says, “People who live on the islands,

come and stand quietly in front of me.

Let the nations gain new strength

in order to state their case.

Let them come forward and speak.

Let us go to court and find out who is right.

2“Who has stirred up a king from the east?

Who has helped him win his battles?

I hand nations over to him.

I bring kings under his control.

He turns them into dust with his sword.

With his bow he turns them into straw blowing in the wind.

3He hunts them down. Then he moves on unharmed.

He travels so fast that his feet

don’t seem to touch the ground.

4Who has made that happen? Who has carried it out?

Who has created all the people who have ever lived?

I, the Lord, have done it.

I was with the first of them.

And I will be with the last of them.”

5The people on the islands have seen that king coming.

And it has made them afraid.

People tremble with fear from one end of the earth to the other.

They come and gather together.

6They help one another.

They say to one another, “Be strong!”

7One skilled worker makes a statue of a god.

Another covers it with gold.

The first worker says to the second,

“You have done a good job.”

Another worker smooths out the metal with a hammer.

Still another gives the statue its final shape.

The one who hammers says to the one who shapes,

“You have done a good job.”

Then they nail the statue down so it won’t fall over.

8The Lord says, “People of Israel, you are my servants.

Family of Jacob, I have chosen you.

You are the children of my friend Abraham.

9I gathered you from one end of the earth to the other.

From the farthest places on earth I brought you together.

I said, ‘You are my servants.’

I have chosen you.

I have not turned my back on you.

10So do not be afraid. I am with you.

Do not be terrified. I am your God.

I will make you strong and help you.

I will hold you safe in my hands.

I always do what is right.

11“All those who are angry with you will be put to shame.

And they will be dishonored.

Those who oppose you will be destroyed.

And they will vanish.

12You might search for your enemies.

But you will not find them.

Those who go to war against you

will completely disappear.

13I am the Lord your God.

I take hold of your right hand.

I say to you, ‘Do not be afraid.

I will help you.’

14Family of Jacob, you are as weak as a worm.

But do not be afraid.

People of Israel, there are only a few of you.

But do not be afraid.

I myself will help you,” announces the Lord.

He is the one who sets his people free.

He is the Holy One of Israel.

15He says, “I will make you into a threshing sled.

It will be new and sharp.

It will have many teeth.

You will grind the mountains down and crush them.

You will turn the hills into nothing but straw.

16You will toss them in the air.

A strong wind will catch them and blow them away.

You will be glad because I will make that happen.

You will praise me.

I am the Holy One of Israel.

17“Those who are poor and needy search for water.

But there isn’t any.

Their tongues are dry because they are thirsty.

But I will help them. I am the Lord.

I will not desert them.

I am Israel’s God.

18I will make streams flow on the bare hilltops.

I will make springs come up in the valleys.

I will turn the desert into pools of water.

I will turn the dry and cracked ground into flowing springs.

19I will make trees grow in the desert.

I will plant cedar and acacia trees there.

I will plant myrtle and olive trees there.

I will make juniper trees grow in the dry and empty desert.

I will plant fir and cypress trees there.

20Then people will see and know

that my powerful hand has done it.

They will consider and understand

that I have created it.

I am the Holy One of Israel.”

21The Lord says to the nations and their gods,

“State your case.”

Jacob’s King says to them,

“Prove your case to me.

22Tell us, you false gods,

what is going to happen.

Tell us what happened in the past.

Then we can check it out

and see if it is really true.

Or announce to us the things that will take place.

23Tell us what will happen in the days ahead.

Then we will know that you are gods.

Do something. It does not matter whether it is good or bad.

Then we will be terrified and filled with fear.

24But you false gods are less than nothing.

Your actions are completely worthless.

I hate it when people worship you.

25“I have stirred up a king

who will come from the north.

He lives in the east.

He will bring honor to me.

He walks all over rulers as if they were mud.

He steps on them just as a potter stomps on clay.

26Which one of you false gods said those things

would happen before they did?

Who told us about them

so we could know them?

Who told us ahead of time?

Who told us so we could say,

‘You are right’?

None of you false gods told us about them.

None of you told us ahead of time.

In fact, no one heard you say anything at all.

27I was the first to tell Zion.

I said, ‘Look! The people of Israel are coming back!’

I sent a messenger to Jerusalem with the good news.

28I look, but there is no one

among the gods that can give me advice.

None of them can answer

when I ask them the simplest question.

29So they are not really gods at all.

What they do does not amount to anything.

They are as useless as wind.