Isaya 41 – NEN & KJV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Isaya 41:1-29

Msaidizi Wa Israeli

141:1 Za 37:7; Isa 48:16; 50:8; Hab 2:20; Zek 2:13; Isa 11:11; 1Sam 2:4“Nyamazeni kimya mbele zangu, enyi visiwa!

Mataifa na wafanye upya nguvu zao!

Wao na wajitokeze, kisha waseme,

tukutane pamoja mahali pa hukumu.

241:2 2Sam 22:43; Isa 40:24; Yer 51:11; Ezr 1:2; Isa 44:28; Yer 50:3; 25:9“Ni nani aliyemchochea mmoja kutoka mashariki,

akimwita katika haki kwa utumishi wake?

Huyatia mataifa mikononi mwake,

na kuwatiisha wafalme mbele zake.

Huwafanya kuwa mavumbi kwa upanga wake,

huwafanya makapi yapeperushwayo na upepo kwa upinde wake.

341:3 Dan 8:4Huwafuatia na kuendelea salama,

katika njia ambayo miguu yake haijawahi kupita.

441:4 Isa 48:12; Ufu 22:13; Mdo 15:18; Isa 43:7; Kum 32:29Ni nani aliyefanya jambo hili na kulitimiliza,

akiita vizazi tangu mwanzo?

Mimi, Bwana, ni wa kwanza

nami nitakuwa pamoja na wa mwisho:

mimi Bwana ndiye.”

541:5 Eze 26:17-18; Kum 30:4; Isa 11:11-12Visiwa vimeliona na kuogopa,

miisho ya dunia inatetemeka.

Wanakaribia na kuja mbele,

641:6 Isa 1:6kila mmoja humsaidia mwingine

na kusema kwa ndugu yake, “Uwe hodari!”

741:7 Isa 40:19; 44:13; Yer 30:3-5Fundi humtia moyo sonara,

yeye alainishaye kwa nyundo

humhimiza yeye agongeaye kwenye fuawe,

Humwambia yeye aunganishaye, “Ni kazi njema.”

Naye huikaza sanamu kwa misumari ili isitikisike.

841:8 Mwa 18:19; Isa 29:22; Neh 9:7; 2Nya 20:7; Yak 2:23; Isa 63:16; Za 136:22“Lakini wewe, ee Israeli, mtumishi wangu,

Yakobo, niliyemchagua,

ninyi wazao wa Abrahamu rafiki yangu,

941:9 Isa 37:16; Kum 7:6; Isa 20:3; 11:12nilikuchukua toka miisho ya dunia,

nilikuita kutoka pembe zake za mbali.

Nilisema, ‘Wewe ni mtumishi wangu’;

nimekuchagua, wala sikukukataa.

1041:10 Kum 3:22; Rum 8:3; Isa 49:8; Yer 30:10; 46:27-28; Ay 40:14; Za 18:35Hivyo usiogope, kwa maana niko pamoja nawe;

usifadhaike, kwa maana mimi ni Mungu wako.

Nitakutia nguvu na kukusaidia;

nitakutegemeza kwa mkono wa kuume wa haki yangu.

1141:11 Isa 17:12; 54:17; Kut 23:22; Isa 29:8; Zek 12:3; Yer 2:3; Isa 29:23“Wote walioona hasira dhidi yako

hakika wataaibika na kutahayarika,

wale wakupingao

watakuwa kama vile si kitu, na kuangamia.

1241:12 Za 37:35-36; Isa 34:12; Ay 7:8; Isa 29:20; 17:14Ingawa utawatafuta adui zako,

hutawaona.

Wale wanaopigana vita dhidi yako

watakuwa kama vile si kitu kabisa.

1341:13 Za 73:23; Isa 42:6; 45:1; 51:18Kwa maana Mimi ndimi Bwana, Mungu wako,

nikushikaye mkono wako wa kuume

na kukuambia, Usiwe na hofu,

nitakusaidia.

1441:14 Ay 4:19; Za 22:6; Kut 15:13; Ay 19:23; Isa 1:27Usiogope, ee Yakobo uliye mdudu,

ee Israeli uliye mdogo,

kwa kuwa Mimi mwenyewe nitakusaidia,” asema Bwana,

Mkombozi wako, yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli.

1541:15 Ay 41:30; Mik 4:13; Isa 21:10; Kut 19:18; Yer 9:10; Eze 33:28“Tazama, nitakufanya chombo cha kupuria,

kipya na chenye makali, chenye meno mengi.

Utaipura milima na kuiponda

na kuvifanya vilima kuwa kama makapi.

1641:16 Yer 51:2; Isa 45:25; 60:19; Dan 2:35; Yer 15:7; Isa 25:9; Mk 1:24Utaipepeta, nao upepo utaichukua,

dhoruba itaipeperushia mbali.

Bali wewe utajifurahisha katika Bwana

na katika utukufu wa yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli.

1741:17 Isa 43:20; 35:7; 30:19“Maskini na wahitaji wanatafuta maji,

lakini hayapo,

ndimi zao zimekauka kwa kiu.

Lakini Mimi Bwana nitawajibu,

Mimi, Mungu wa Israeli, sitawaacha.

1841:18 Isa 30:25; 43:19; Ay 38:26; Isa 35:7; 2Fal 3:17Nitaifanya mito itiririke juu ya vilima vilivyo kame,

nazo chemchemi ndani ya mabonde.

Nitaligeuza jangwa liwe mabwawa ya maji,

nayo ardhi iliyokauka kuwa chemchemi za maji.

1941:19 Isa 60:13; Kut 25:10-13; Isa 37:24; 44:14Katika jangwa nitaotesha

mwerezi, mshita, mhadasi na mzeituni.

Nitaweka misunobari, mivinje na misanduku

pamoja huko nyikani,

2041:20 Ay 12:9; Isa 4:5ili kwamba watu wapate kuona na kujua,

wapate kufikiri na kuelewa,

kwamba mkono wa Bwana umetenda hili,

kwamba yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli ndiye alilifanya.”

2141:21 Isa 43:14; 44:6Bwana asema, “Leta shauri lako.

Toa hoja yako,” asema Mfalme wa Yakobo.

2241:22 Isa 48:14; 65:17; Yn 13:19; Isa 43:9; 45:21“Leteni sanamu zenu zituambie

ni nini kitakachotokea.

Tuambieni mambo ya zamani yalikuwa nini,

ili tupate kuyatafakari

na kujua matokeo yake ya mwisho.

Au tutangazieni mambo yatakayokuja,

2341:23 Kum 18:22; Isa 44:7-8; Yer 10:5; Isa 43:5; 2Fal 19:26tuambieni ni nini kitakachotokea baadaye,

ili tupate kujua kuwa ninyi ni miungu.

Fanyeni jambo lolote zuri au baya,

ili tupate kutishika na kujazwa na hofu.

2441:24 Isa 37:19; 1Kor 8:4; Za 115:8; 1Sam 12:21; Isa 48:8Lakini ninyi ni zaidi ya bure kabisa,

na kazi zenu hazifai kitu kabisa;

yeye awachaguaye ni chukizo sana.

2541:25 Yer 51:48; Nah 3:14; 2Sam 22:43; Yer 50:9“Nimemchochea mtu mmoja kutoka kaskazini,

naye yuaja, mmoja toka mawio ya jua aliitaye Jina langu.

Huwakanyaga watawala kana kwamba ni matope,

kama mfinyanzi akanyagavyo udongo wa kufinyangia.

2641:26 Hab 2:18-19; 1Fal 18:26; Isa 52:6Ni nani aliyenena hili tokea mwanzoni, ili tupate kujua,

au kabla, ili tuweze kusema, ‘Alikuwa sawa’?

Hakuna aliyenena hili,

hakuna aliyetangulia kusema hili,

hakuna yeyote aliyesikia maneno kutoka kwenu.

2741:27 Isa 48:3, 16; 40:9Nilikuwa wa kwanza kumwambia Sayuni,

‘Tazama, wako hapa!’

Nilimpa Yerusalemu mjumbe wa habari njema.

2841:28 Eze 22:30; Za 22:11; Isa 40:13-14; 50:2; 59:16; 64:7; Yer 25:4Ninatazama, lakini hakuna yeyote:

hakuna yeyote miongoni mwao awezaye kutoa shauri,

hakuna yeyote wa kutoa jibu wakati ninapowauliza.

2941:29 Yer 5:13; 1Sam 12:21; Isa 37:19Tazama, wote ni ubatili!

Matendo yao ni bure;

vinyago vyao ni upepo mtupu na machafuko.

King James Version

Isaiah 41:1-29

1Keep silence before me, O islands; and let the people renew their strength: let them come near; then let them speak: let us come near together to judgment. 2Who raised up the righteous man from the east, called him to his foot, gave the nations before him, and made him rule over kings? he gave them as the dust to his sword, and as driven stubble to his bow.41.2 the righteous…: Heb. righteousness 3He pursued them, and passed safely; even by the way that he had not gone with his feet.41.3 safely: Heb. in peace 4Who hath wrought and done it, calling the generations from the beginning? I the LORD, the first, and with the last; I am he. 5The isles saw it, and feared; the ends of the earth were afraid, drew near, and came. 6They helped every one his neighbour; and every one said to his brother, Be of good courage.41.6 Be…: Heb. Be strong 7So the carpenter encouraged the goldsmith, and he that smootheth with the hammer him that smote the anvil, saying, It is ready for the sodering: and he fastened it with nails, that it should not be moved.41.7 goldsmith: or, founder41.7 him…: or, the smiting41.7 saying…: or, saying of the soder, It is good 8But thou, Israel, art my servant, Jacob whom I have chosen, the seed of Abraham my friend. 9Thou whom I have taken from the ends of the earth, and called thee from the chief men thereof, and said unto thee, Thou art my servant; I have chosen thee, and not cast thee away.

10¶ Fear thou not; for I am with thee: be not dismayed; for I am thy God: I will strengthen thee; yea, I will help thee; yea, I will uphold thee with the right hand of my righteousness. 11Behold, all they that were incensed against thee shall be ashamed and confounded: they shall be as nothing; and they that strive with thee shall perish.41.11 they that strive…: Heb. the men of thy strife 12Thou shalt seek them, and shalt not find them, even them that contended with thee: they that war against thee shall be as nothing, and as a thing of nought.41.12 them that…: Heb. the men of thy contention41.12 they…: Heb. the men of thy war 13For I the LORD thy God will hold thy right hand, saying unto thee, Fear not; I will help thee. 14Fear not, thou worm Jacob, and ye men of Israel; I will help thee, saith the LORD, and thy redeemer, the Holy One of Israel.41.14 men: or, few men 15Behold, I will make thee a new sharp threshing instrument having teeth: thou shalt thresh the mountains, and beat them small, and shalt make the hills as chaff.41.15 teeth: Heb. mouths 16Thou shalt fan them, and the wind shall carry them away, and the whirlwind shall scatter them: and thou shalt rejoice in the LORD, and shalt glory in the Holy One of Israel. 17When the poor and needy seek water, and there is none, and their tongue faileth for thirst, I the LORD will hear them, I the God of Israel will not forsake them. 18I will open rivers in high places, and fountains in the midst of the valleys: I will make the wilderness a pool of water, and the dry land springs of water. 19I will plant in the wilderness the cedar, the shittah tree, and the myrtle, and the oil tree; I will set in the desert the fir tree, and the pine, and the box tree together: 20That they may see, and know, and consider, and understand together, that the hand of the LORD hath done this, and the Holy One of Israel hath created it.

21Produce your cause, saith the LORD; bring forth your strong reasons, saith the King of Jacob.41.21 Produce: Heb. Cause to come near 22Let them bring them forth, and shew us what shall happen: let them shew the former things, what they be, that we may consider them, and know the latter end of them; or declare us things for to come.41.22 consider…: Heb. set our heart upon them 23Shew the things that are to come hereafter, that we may know that ye are gods: yea, do good, or do evil, that we may be dismayed, and behold it together. 24Behold, ye are of nothing, and your work of nought: an abomination is he that chooseth you.41.24 of nothing: or, worse than nothing41.24 of nought: or, worse than of a viper 25I have raised up one from the north, and he shall come: from the rising of the sun shall he call upon my name: and he shall come upon princes as upon morter, and as the potter treadeth clay. 26Who hath declared from the beginning, that we may know? and beforetime, that we may say, He is righteous? yea, there is none that sheweth, yea, there is none that declareth, yea, there is none that heareth your words. 27The first shall say to Zion, Behold, behold them: and I will give to Jerusalem one that bringeth good tidings. 28For I beheld, and there was no man; even among them, and there was no counsellor, that, when I asked of them, could answer a word.41.28 answer: Heb. return 29Behold, they are all vanity; their works are nothing: their molten images are wind and confusion.