Isaya 40 – NEN & NIVUK

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Isaya 40:1-31

Faraja Kwa Watu Wa Mungu

140:1 Zek 1:17; 2Kor 1:3; Sef 3:14-17; Yer 31:13; Isa 49:13; 57:18Wafarijini, wafarijini watu wangu,

asema Mungu wenu.

240:2 Mwa 34:3; Isa 41:11-13; 49:25; Zek 9:12; Ufu 18:6; Yer 16:18; Law 26:4Sema na Yerusalemu kwa upole,

umtangazie

kwamba kazi yake ngumu imekamilika,

kwamba dhambi yake imefanyiwa fidia,

kwamba amepokea kutoka mkononi mwa Bwana

maradufu kwa ajili ya dhambi zake zote.

340:3 Isa 11:16; Mt 3:3; Mal 3:1; Mk 1:3; Isa 43:19; Yn 1:23Sauti ya mtu aliaye:

“Itengenezeni jangwani njia ya Bwana,

nyoosheni njia kuu nyikani

kwa ajili ya Mungu wetu.

440:4 Za 26:12; Yer 31:9; Isa 2:14; 49:11; 26:7; 45:2Kila bonde litainuliwa,

kila mlima na kilima kitashushwa;

penye mabonde patanyooshwa,

napo palipoparuza patasawazishwa.

540:5 Kut 16:7; Isa 58:14; Lk 3:4-6; Eze 36:23; Hes 14:21; Isa 59:19; Lk 2:20Utukufu wa Bwana utafunuliwa,

nao wanadamu wote watauona pamoja.

Kwa maana kinywa cha Bwana kimenena.”

640:6 Ay 14:2; Mwa 6:3; Isa 29:5Sauti husema, “Piga kelele.”

Nami nikasema, “Nipige kelele gani?”

“Wanadamu wote ni kama majani,

nao utukufu wao wote

ni kama maua ya kondeni.

740:7 Kut 15:10; Ay 41:21; Yos 8:12; Isa 15:6; Za 103:6; Eze 22:21Majani hunyauka na maua huanguka,

kwa sababu pumzi ya Bwana huyapuliza.

Hakika wanadamu ni majani.

840:8 1Pet 1:25; Isa 59:21; Mt 5:18; Za 119:89; Isa 5:24; Yak 1:10; Mit 19:21Majani hunyauka na maua huanguka,

lakini neno la Mungu wetu ladumu milele.”

940:9 Nah 1:15; Isa 25:9; Rum 10:15; Isa 41:27; 52:7-10; 1Kor 15:1-4Wewe uletaye habari njema Sayuni,

panda juu ya mlima mrefu.

Wewe uletaye habari njema Yerusalemu,

inua sauti yako kwa kupiga kelele,

inua sauti, usiogope;

iambie miji ya Yuda,

“Yuko hapa Mungu wenu!”

1040:10 Ufu 22:7; Isa 35:4; Za 44:3; Isa 9:6-7; Ufu 22:12; Mt 21:5; Isa 28:2Tazameni, Bwana Mwenyezi anakuja na nguvu,

nao mkono wake ndio utawalao kwa ajili yake.

Tazameni, ujira wake u pamoja naye,

nayo malipo yake yanafuatana naye.

1140:11 Za 28:9; Yn 10:11; Ebr 13:20; Mwa 48:15; Mik 5:4; Hes 12:11; Kum 26:19Huchunga kundi lake kama mchungaji wa mifugo:

Hukusanya wana-kondoo katika mikono yake

na kuwachukua karibu na moyo wake,

huwaongoza taratibu wale wanyonyeshao.

1240:12 Mit 30:4; Ebr 1:10-12; Ay 38:10; 12:15; Mit 16:11Ni nani aliyepima maji ya bahari

kwenye konzi ya mkono wake,

au kuzipima mbingu kwa shibiri40:12 Shibiri ni sawa na sentimita 20 au inchi 8. yake?

Ni nani aliyeyashika mavumbi ya dunia katika kikapu,

au kupima milima kwenye kipimio

na vilima kwenye mizani?

1340:13 Ay 15:8; 1Kor 2:16; Rum 11:34Ni nani aliyeyafahamu mawazo ya Bwana,

au kumfundisha akiwa kama mshauri wake?

1440:14 Ay 21:22; Kol 2:3; Ay 12:13; 34:13; Isa 55:9Ni nani ambaye Bwana ametaka shauri kwake ili kumwelimisha,

naye ni nani aliyemfundisha njia iliyo sawa?

Ni nani aliyemfundisha maarifa

au kumwonyesha mapito ya ufahamu?

1540:15 Za 62:9; Isa 2:22; Kum 9:21Hakika mataifa ni kama tone ndani ya ndoo,

ni kama vumbi jembamba juu ya mizani,

huvipima visiwa kana kwamba vilikuwa vumbi laini.

1640:16 Mik 6:7; Ebr 10:5-9; Isa 37:24; Za 50:9-11Lebanoni hautoshi kwa moto wa madhabahuni,

wala wanyama wake hawatoshi kwa sadaka za kuteketezwa.

1740:17 Isa 30:28; Ay 12:19; Isa 29:7; Dan 4:35; Isa 37:19Mbele yake mataifa yote ni kama si kitu,

yanaonekana yasio na thamani

na zaidi ya bure kabisa.

1840:18 Mdo 17:29; Kut 8:10; Kum 4:15; 1Sam 2:2Basi, utamlinganisha Mungu na nani?

Utamlinganisha na kitu gani?

1940:19 Kut 20:4; Zek 10:2; Yer 10:3-4; Isa 31:7; 37:19; 42:17; Hab 2:18Kwa habari ya sanamu, fundi huisubu,

naye mfua dhahabu huifunika kwa dhahabu

na kuitengenezea mikufu ya fedha.

2040:20 Isa 44:19; 5:3Mtu aliye maskini sana asiyeweza kuleta sadaka kama hii

huuchagua mti usiooza.

Humtafuta fundi stadi

wa kusimamisha sanamu ambayo haitatikisika.

2140:21 Mdo 14:17; Rum 1:19; Isa 48:13; 51:13; 2Fal 19:25Je, hujui?

Je, hujasikia?

Je, hujaambiwa tangu mwanzo?

Je, hujafahamu tangu kuumbwa kwa dunia?

2240:22 Hes 13:33; Ay 22:14; 36:29; 2Nya 6:18; Isa 48:13; Ay 26:7Anakaa kwenye kiti cha enzi juu ya duara ya dunia,

nao watu wakaao ndani yake ni kama panzi.

Huzitandaza mbingu kama chandarua,

na kuzitandaza kama hema la kuishi.

2340:23 Ay 12:18; Isa 34:12; Za 107:40; Amo 2:3Huwafanya wakuu kuwa si kitu,

na kuwashusha watawala wa dunia hii kuwa kitu bure.

2440:24 2Sam 22:16; Isa 11:4; Ay 5:3; 8:12; 18:16; 24:24; Isa 41:2, 16Mara baada ya kupandwa,

mara baada ya kutiwa ardhini,

mara baada ya kutoa mizizi yao ardhini,

ndipo huwapulizia nao wakanyauka,

nao upepo wa kisulisuli

huwapeperusha kama makapi.

2540:25 Kum 4:15; Mdo 17:24-29; 1Nya 16:25; Isa 37:23“Utanilinganisha mimi na nani?

Au ni nani anayelingana nami?” asema yeye Aliye Mtakatifu.

2640:26 Za 89:11-13; 2Fal 17:16; Neh 9:6; Isa 34:16; 51:6; Ay 9:4; Efe 1:19Inueni macho yenu mtazame mbinguni:

Ni nani aliyeumba hivi vyote?

Ni yeye aletaye nje jeshi la nyota moja baada ya nyingine

na kuziita kila moja kwa jina lake.

Kwa sababu ya uweza wake mkuu na nguvu zake kuu,

hakuna hata mojawapo inayokosekana.

2740:27 Ay 6:29; Lk 18:7-8; Ay 27:2Kwa nini unasema, ee Yakobo,

nanyi ee Israeli, kulalamika,

“Njia yangu imefichwa Bwana asiione,

Mungu wangu hajali shauri langu?”

2840:28 Kum 33:27; Za 90:2; Rum 11:33; Isa 37:16; 44:12; Za 147:5Je wewe, hufahamu?

Je wewe, hujasikia?

Bwana ni Mungu wa milele,

Muumba wa miisho ya dunia.

Hatachoka wala kulegea,

wala hakuna hata mmoja

awezaye kuupima ufahamu wake.

2940:29 Isa 57:19; Yer 31:25; Mwa 18:14; Za 68:35; 119:28Huwapa nguvu waliolegea

na huongeza nguvu za wadhaifu.

3040:30 Isa 9:17; Yer 9:21; Isa 5:27Hata vijana huchoka na kulegea,

nao vijana wanaume hujikwaa na kuanguka,

3140:31 2Fal 6:33; Kut 19:4; Ebr 12:1-3; Mao 3:25; 2Kor 4:8-10, 16; Za 37:9; Isa 30:18bali wale wamtumainio Bwana

atafanya upya nguvu zao.

Watapaa juu kwa mbawa kama tai;

watapiga mbio wala hawatachoka,

watatembea kwa miguu wala hawatazimia.

New International Version – UK

Isaiah 40:1-31

Comfort for God’s people

1Comfort, comfort my people,

says your God.

2Speak tenderly to Jerusalem,

and proclaim to her

that her hard service has been completed,

that her sin has been paid for,

that she has received from the Lord’s hand

double for all her sins.

3A voice of one calling:

‘In the wilderness prepare

the way for the Lord40:3 Or A voice of one calling in the wilderness: / ‘Prepare the way for the Lord;

make straight in the desert

a highway for our God.40:3 Hebrew; Septuagint make straight the paths of our God

4Every valley shall be raised up,

every mountain and hill made low;

the rough ground shall become level,

the rugged places a plain.

5And the glory of the Lord will be revealed,

and all people will see it together.

For the mouth of the Lord has spoken.’

6A voice says, ‘Cry out.’

And I said, ‘What shall I cry?’

‘All people are like grass,

and all their faithfulness is like the flowers of the field.

7The grass withers and the flowers fall,

because the breath of the Lord blows on them.

Surely the people are grass.

8The grass withers and the flowers fall,

but the word of our God endures for ever.’

9You who bring good news to Zion,

go up on a high mountain.

You who bring good news to Jerusalem,40:9 Or Zion, bringer of good news, / go up on a high mountain. / Jerusalem, bringer of good news

lift up your voice with a shout,

lift it up, do not be afraid;

say to the towns of Judah,

‘Here is your God!’

10See, the Sovereign Lord comes with power,

and he rules with a mighty arm.

See, his reward is with him,

and his recompense accompanies him.

11He tends his flock like a shepherd:

he gathers the lambs in his arms

and carries them close to his heart;

he gently leads those that have young.

12Who has measured the waters in the hollow of his hand,

or with the breadth of his hand marked off the heavens?

Who has held the dust of the earth in a basket,

or weighed the mountains on the scales

and the hills in a balance?

13Who can fathom the Spirit40:13 Or mind of the Lord,

or instruct the Lord as his counsellor?

14Whom did the Lord consult to enlighten him,

and who taught him the right way?

Who was it that taught him knowledge,

or showed him the path of understanding?

15Surely the nations are like a drop in a bucket;

they are regarded as dust on the scales;

he weighs the islands as though they were fine dust.

16Lebanon is not sufficient for altar fires,

nor its animals enough for burnt offerings.

17Before him all the nations are as nothing;

they are regarded by him as worthless

and less than nothing.

18With whom, then, will you compare God?

To what image will you liken him?

19As for an idol, a metalworker casts it,

and a goldsmith overlays it with gold

and fashions silver chains for it.

20A person too poor to present such an offering

selects wood that will not rot;

they look for a skilled worker

to set up an idol that will not topple.

21Do you not know?

Have you not heard?

Has it not been told you from the beginning?

Have you not understood since the earth was founded?

22He sits enthroned above the circle of the earth,

and its people are like grasshoppers.

He stretches out the heavens like a canopy,

and spreads them out like a tent to live in.

23He brings princes to naught

and reduces the rulers of this world to nothing.

24No sooner are they planted,

no sooner are they sown,

no sooner do they take root in the ground,

than he blows on them and they wither,

and a whirlwind sweeps them away like chaff.

25‘To whom will you compare me?

Or who is my equal?’ says the Holy One.

26Lift up your eyes and look to the heavens:

who created all these?

He who brings out the starry host one by one

and calls forth each of them by name.

Because of his great power and mighty strength,

not one of them is missing.

27Why do you complain, Jacob?

Why do you say, Israel,

‘My way is hidden from the Lord;

my cause is disregarded by my God’?

28Do you not know?

Have you not heard?

The Lord is the everlasting God,

the Creator of the ends of the earth.

He will not grow tired or weary,

and his understanding no-one can fathom.

29He gives strength to the weary

and increases the power of the weak.

30Even youths grow tired and weary,

and young men stumble and fall;

31but those who hope in the Lord

will renew their strength.

They will soar on wings like eagles;

they will run and not grow weary,

they will walk and not be faint.