Isaya 40 – NEN & NIRV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Isaya 40:1-31

Faraja Kwa Watu Wa Mungu

140:1 Zek 1:17; 2Kor 1:3; Sef 3:14-17; Yer 31:13; Isa 49:13; 57:18Wafarijini, wafarijini watu wangu,

asema Mungu wenu.

240:2 Mwa 34:3; Isa 41:11-13; 49:25; Zek 9:12; Ufu 18:6; Yer 16:18; Law 26:4Sema na Yerusalemu kwa upole,

umtangazie

kwamba kazi yake ngumu imekamilika,

kwamba dhambi yake imefanyiwa fidia,

kwamba amepokea kutoka mkononi mwa Bwana

maradufu kwa ajili ya dhambi zake zote.

340:3 Isa 11:16; Mt 3:3; Mal 3:1; Mk 1:3; Isa 43:19; Yn 1:23Sauti ya mtu aliaye:

“Itengenezeni jangwani njia ya Bwana,

nyoosheni njia kuu nyikani

kwa ajili ya Mungu wetu.

440:4 Za 26:12; Yer 31:9; Isa 2:14; 49:11; 26:7; 45:2Kila bonde litainuliwa,

kila mlima na kilima kitashushwa;

penye mabonde patanyooshwa,

napo palipoparuza patasawazishwa.

540:5 Kut 16:7; Isa 58:14; Lk 3:4-6; Eze 36:23; Hes 14:21; Isa 59:19; Lk 2:20Utukufu wa Bwana utafunuliwa,

nao wanadamu wote watauona pamoja.

Kwa maana kinywa cha Bwana kimenena.”

640:6 Ay 14:2; Mwa 6:3; Isa 29:5Sauti husema, “Piga kelele.”

Nami nikasema, “Nipige kelele gani?”

“Wanadamu wote ni kama majani,

nao utukufu wao wote

ni kama maua ya kondeni.

740:7 Kut 15:10; Ay 41:21; Yos 8:12; Isa 15:6; Za 103:6; Eze 22:21Majani hunyauka na maua huanguka,

kwa sababu pumzi ya Bwana huyapuliza.

Hakika wanadamu ni majani.

840:8 1Pet 1:25; Isa 59:21; Mt 5:18; Za 119:89; Isa 5:24; Yak 1:10; Mit 19:21Majani hunyauka na maua huanguka,

lakini neno la Mungu wetu ladumu milele.”

940:9 Nah 1:15; Isa 25:9; Rum 10:15; Isa 41:27; 52:7-10; 1Kor 15:1-4Wewe uletaye habari njema Sayuni,

panda juu ya mlima mrefu.

Wewe uletaye habari njema Yerusalemu,

inua sauti yako kwa kupiga kelele,

inua sauti, usiogope;

iambie miji ya Yuda,

“Yuko hapa Mungu wenu!”

1040:10 Ufu 22:7; Isa 35:4; Za 44:3; Isa 9:6-7; Ufu 22:12; Mt 21:5; Isa 28:2Tazameni, Bwana Mwenyezi anakuja na nguvu,

nao mkono wake ndio utawalao kwa ajili yake.

Tazameni, ujira wake u pamoja naye,

nayo malipo yake yanafuatana naye.

1140:11 Za 28:9; Yn 10:11; Ebr 13:20; Mwa 48:15; Mik 5:4; Hes 12:11; Kum 26:19Huchunga kundi lake kama mchungaji wa mifugo:

Hukusanya wana-kondoo katika mikono yake

na kuwachukua karibu na moyo wake,

huwaongoza taratibu wale wanyonyeshao.

1240:12 Mit 30:4; Ebr 1:10-12; Ay 38:10; 12:15; Mit 16:11Ni nani aliyepima maji ya bahari

kwenye konzi ya mkono wake,

au kuzipima mbingu kwa shibiri40:12 Shibiri ni sawa na sentimita 20 au inchi 8. yake?

Ni nani aliyeyashika mavumbi ya dunia katika kikapu,

au kupima milima kwenye kipimio

na vilima kwenye mizani?

1340:13 Ay 15:8; 1Kor 2:16; Rum 11:34Ni nani aliyeyafahamu mawazo ya Bwana,

au kumfundisha akiwa kama mshauri wake?

1440:14 Ay 21:22; Kol 2:3; Ay 12:13; 34:13; Isa 55:9Ni nani ambaye Bwana ametaka shauri kwake ili kumwelimisha,

naye ni nani aliyemfundisha njia iliyo sawa?

Ni nani aliyemfundisha maarifa

au kumwonyesha mapito ya ufahamu?

1540:15 Za 62:9; Isa 2:22; Kum 9:21Hakika mataifa ni kama tone ndani ya ndoo,

ni kama vumbi jembamba juu ya mizani,

huvipima visiwa kana kwamba vilikuwa vumbi laini.

1640:16 Mik 6:7; Ebr 10:5-9; Isa 37:24; Za 50:9-11Lebanoni hautoshi kwa moto wa madhabahuni,

wala wanyama wake hawatoshi kwa sadaka za kuteketezwa.

1740:17 Isa 30:28; Ay 12:19; Isa 29:7; Dan 4:35; Isa 37:19Mbele yake mataifa yote ni kama si kitu,

yanaonekana yasio na thamani

na zaidi ya bure kabisa.

1840:18 Mdo 17:29; Kut 8:10; Kum 4:15; 1Sam 2:2Basi, utamlinganisha Mungu na nani?

Utamlinganisha na kitu gani?

1940:19 Kut 20:4; Zek 10:2; Yer 10:3-4; Isa 31:7; 37:19; 42:17; Hab 2:18Kwa habari ya sanamu, fundi huisubu,

naye mfua dhahabu huifunika kwa dhahabu

na kuitengenezea mikufu ya fedha.

2040:20 Isa 44:19; 5:3Mtu aliye maskini sana asiyeweza kuleta sadaka kama hii

huuchagua mti usiooza.

Humtafuta fundi stadi

wa kusimamisha sanamu ambayo haitatikisika.

2140:21 Mdo 14:17; Rum 1:19; Isa 48:13; 51:13; 2Fal 19:25Je, hujui?

Je, hujasikia?

Je, hujaambiwa tangu mwanzo?

Je, hujafahamu tangu kuumbwa kwa dunia?

2240:22 Hes 13:33; Ay 22:14; 36:29; 2Nya 6:18; Isa 48:13; Ay 26:7Anakaa kwenye kiti cha enzi juu ya duara ya dunia,

nao watu wakaao ndani yake ni kama panzi.

Huzitandaza mbingu kama chandarua,

na kuzitandaza kama hema la kuishi.

2340:23 Ay 12:18; Isa 34:12; Za 107:40; Amo 2:3Huwafanya wakuu kuwa si kitu,

na kuwashusha watawala wa dunia hii kuwa kitu bure.

2440:24 2Sam 22:16; Isa 11:4; Ay 5:3; 8:12; 18:16; 24:24; Isa 41:2, 16Mara baada ya kupandwa,

mara baada ya kutiwa ardhini,

mara baada ya kutoa mizizi yao ardhini,

ndipo huwapulizia nao wakanyauka,

nao upepo wa kisulisuli

huwapeperusha kama makapi.

2540:25 Kum 4:15; Mdo 17:24-29; 1Nya 16:25; Isa 37:23“Utanilinganisha mimi na nani?

Au ni nani anayelingana nami?” asema yeye Aliye Mtakatifu.

2640:26 Za 89:11-13; 2Fal 17:16; Neh 9:6; Isa 34:16; 51:6; Ay 9:4; Efe 1:19Inueni macho yenu mtazame mbinguni:

Ni nani aliyeumba hivi vyote?

Ni yeye aletaye nje jeshi la nyota moja baada ya nyingine

na kuziita kila moja kwa jina lake.

Kwa sababu ya uweza wake mkuu na nguvu zake kuu,

hakuna hata mojawapo inayokosekana.

2740:27 Ay 6:29; Lk 18:7-8; Ay 27:2Kwa nini unasema, ee Yakobo,

nanyi ee Israeli, kulalamika,

“Njia yangu imefichwa Bwana asiione,

Mungu wangu hajali shauri langu?”

2840:28 Kum 33:27; Za 90:2; Rum 11:33; Isa 37:16; 44:12; Za 147:5Je wewe, hufahamu?

Je wewe, hujasikia?

Bwana ni Mungu wa milele,

Muumba wa miisho ya dunia.

Hatachoka wala kulegea,

wala hakuna hata mmoja

awezaye kuupima ufahamu wake.

2940:29 Isa 57:19; Yer 31:25; Mwa 18:14; Za 68:35; 119:28Huwapa nguvu waliolegea

na huongeza nguvu za wadhaifu.

3040:30 Isa 9:17; Yer 9:21; Isa 5:27Hata vijana huchoka na kulegea,

nao vijana wanaume hujikwaa na kuanguka,

3140:31 2Fal 6:33; Kut 19:4; Ebr 12:1-3; Mao 3:25; 2Kor 4:8-10, 16; Za 37:9; Isa 30:18bali wale wamtumainio Bwana

atafanya upya nguvu zao.

Watapaa juu kwa mbawa kama tai;

watapiga mbio wala hawatachoka,

watatembea kwa miguu wala hawatazimia.

New International Reader’s Version

Isaiah 40:1-31

God Comforts His People

1“Comfort my people,” says your God.

“Comfort them.

2Speak tenderly to the people of Jerusalem.

Announce to them

that their hard labor has been completed.

Tell them that their sin has been paid for.

Tell them the Lord has punished them enough

for all their sins.”

3A messenger is calling out,

“In the desert prepare

the way for the Lord.

Make a straight road through it

for our God.

4Every valley will be filled in.

Every mountain and hill will be made level.

The rough ground will be smoothed out.

The rocky places will be made flat.

5Then the glory of the Lord will appear.

And everyone will see it together.

The Lord has spoken.”

6Another messenger says, “Cry out.”

And I said, “What should I cry?”

“Cry out, ‘All people are like grass.

They don’t stay faithful to me any longer than wildflowers last.

7The grass dries up. The flowers fall to the ground.

That happens when the Lord makes his wind blow on them.

So people are just like grass.

8The grass dries up. The flowers fall to the ground.

But what our God says will stand forever.’ ”

9Zion, you are bringing good news to your people.

Go up on a high mountain and announce it.

Jerusalem, you are bringing good news to them.

Shout the message loudly.

Shout it out loud. Don’t be afraid.

Say to the towns of Judah,

“Your God is coming!”

10The Lord and King is coming with power.

He rules with a powerful arm.

He has set his people free.

He is bringing them back as his reward.

He has won the battle over their enemies.

11He takes care of his flock like a shepherd.

He gathers the lambs in his arms.

He carries them close to his heart.

He gently leads those that have little ones.

12Who has measured the oceans by using the palm of his hand?

Who has used the width of his hand to mark off the sky?

Who has measured out the dust of the earth in a basket?

Who has weighed the mountains on scales?

Who has weighed the hills in a balance?

13Who can ever understand the Spirit of the Lord?

Who can ever give him advice?

14Did the Lord have to ask anyone to help him understand?

Did he have to ask someone to teach him the right way?

Who taught him what he knows?

Who showed him how to understand?

15The nations are only a drop in a bucket to him.

He considers them as nothing but dust on the scales.

He weighs the islands as if they were only fine dust.

16Lebanon doesn’t have enough trees to keep his altar fires burning.

It doesn’t have enough animals to sacrifice as burnt offerings to him.

17To him, all the nations don’t amount to anything.

He considers them to be worthless.

In fact, they are less than nothing in his sight.

18So who will you compare God with?

Is there any other god like him?

19Will you compare him with a statue of a god?

Anyone who works with metal can make a statue.

Then another worker covers it with gold

and makes silver chains for it.

20But someone who is too poor to bring that kind of offering

will choose some wood that won’t rot.

Then they look for a skilled worker.

They pay the worker to make a statue of a god that won’t fall over.

21Don’t you know who made everything?

Haven’t you heard about him?

Hasn’t it been told to you from the beginning?

Haven’t you understood it ever since the earth was made?

22God sits on his throne high above the earth.

Its people look like grasshoppers to him.

He spreads out the heavens like a cover.

He sets it up like a tent to live in.

23He takes the power of princes away from them.

He reduces the rulers of this world to nothing.

24They are planted.

They are scattered like seeds.

They put down roots in the ground.

But as soon as that happens, God blows on them and they dry up.

Then a windstorm sweeps them away like straw.

25“So who will you compare me with?

Who is equal to me?” says the Holy One.

26Look up toward the sky.

Who created everything you see?

The Lord causes the stars to come out at night one by one.

He calls out each one of them by name.

His power and strength are great.

So none of the stars is missing.

27Family of Jacob, why do you complain,

“The Lord doesn’t notice our condition”?

People of Israel, why do you say,

“Our God doesn’t pay any attention to our rightful claims”?

28Don’t you know who made everything?

Haven’t you heard about him?

The Lord is the God who lives forever.

He created everything on earth.

He won’t become worn out or get tired.

No one will ever know how great his understanding is.

29He gives strength to those who are tired.

He gives power to those who are weak.

30Even young people become worn out and get tired.

Even the best of them trip and fall.

31But those who trust in the Lord

will receive new strength.

They will fly as high as eagles.

They will run and not get tired.

They will walk and not grow weak.