Isaya 39 – NEN & CARST

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Isaya 39:1-8

Wajumbe Kutoka Babeli

(2 Wafalme 20:12-19)

139:1 2Fal 20:12; 2Nya 32:31Wakati huo Merodaki-Baladani, mwana wa Baladani mfalme wa Babeli, akamtumia Hezekia barua na zawadi, kwa sababu alikuwa amesikia habari za kuugua na kupona kwake. 239:2 2Nya 32:31; 2Fal 18:15; 2Nya 32:27-29Hezekia akawapokea wale wajumbe kwa furaha na kuwaonyesha vitu vile vilivyokuwa katika ghala zake: yaani fedha, dhahabu, vikolezo na mafuta safi, ghala la silaha lote, na kila kitu kilichokuwa katika hazina zake. Hapakuwa na kitu chochote katika jumba lake la kifalme au katika ufalme wake wote ambacho Hezekia hakuwaonyesha.

339:3 Kum 28:49Ndipo nabii Isaya akaenda kwa Mfalme Hezekia na kumuuliza, “Watu hao walisema nini, na wametoka wapi?”

Hezekia akamjibu, “Wametoka nchi ya mbali. Walikuja kwangu kutoka Babeli.”

4Nabii akauliza, “Waliona nini katika jumba lako la kifalme?”

Hezekia akajibu, “Waliona kila kitu katika jumba langu la kifalme. Hakuna kitu chochote katika hazina yangu ambacho sikuwaonyesha.”

539:5 Isa 38:4Ndipo Isaya akamwambia Hezekia, “Sikia neno la Bwana Mwenye Nguvu Zote: 639:6 Law 26:33; Amu 6:4; Yer 20:5; Amo 5:27; 2Fal 24:13Hakika wakati unakuja ambapo vitu vyote katika jumba lako la kifalme, na vyote ambavyo baba zako waliweka akiba mpaka siku hii, vitachukuliwa kwenda Babeli. Hakuna chochote kitakachosalia, asema Bwana. 739:7 2Fal 24:15; Dan 1:1-7Nao baadhi ya wazao wako, nyama yako na damu yako mwenyewe watakaozaliwa kwako, watachukuliwa mbali, nao watakuwa matowashi katika jumba la mfalme wa Babeli.”

839:8 1Sam 3:18; 2Nya 32:26; Amu 10:15; Ay 1:21; Za 39:9Hezekia akamjibu Isaya, “Neno la Bwana ulilosema ni jema.” Kwa kuwa alifikiri, “Patakuwepo amani na usalama wakati wa uhai wangu.”

Священное Писание (Восточный перевод), версия для Таджикистана

Исаия 39:1-8

Немудрый поступок Езекии

(4 Цар. 20:12-19)

1В то время вавилонский царь Меродах-Баладан, сын Баладана, отправил Езекии письма и подарок, потому что услышал о его болезни и выздоровлении. 2Езекия радушно принял послов и показал им то, что было у него в хранилищах, – серебро, золото, пряности и драгоценные масла, – и всю оружейную палату, и всё, что хранилось в его сокровищницах. Ни во дворце, ни во всём его царстве не осталось ничего такого, чего бы он им не показал.

3Пророк Исаия пришёл к царю и спросил:

– Что говорили эти люди, и откуда они к тебе приходили?

– Из далёкой страны, – ответил Езекия. – Они приходили ко мне из Вавилона.

4Пророк спросил:

– Что они видели у тебя во дворце?

– У меня во дворце они видели всё, – ответил Езекия. – В моих сокровищницах нет ничего, чего бы я им не показал.

5Тогда Исаия сказал Езекии:

– Слушай слово Вечного, Повелителя Сил: 6«Непременно наступит время, когда всё, что у тебя во дворце, и всё, что накопили до сегодняшнего дня твои отцы, будет унесено в Вавилон. Не останется ничего, – говорит Вечный. – 7А некоторые из твоих потомков, которые родятся у тебя, твоя плоть и кровь, будут уведены и станут евнухами во дворце царя Вавилона».

8– Хорошую весть передал ты мне от Вечного, – ответил Езекия, потому что думал: «Ведь в мои-то дни будет мир и безопасность».