Isaya 38 – NEN & JCB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Isaya 38:1-22

Kuugua Kwa Mfalme Hezekia

(2 Wafalme 20:1-11; 2 Nyakati 32:24-26)

138:1 Isa 37:2-3; 2Sam 17:23; 2Fal 8:10Katika siku hizo Hezekia akaugua, naye akawa karibu kufa. Nabii Isaya mwana wa Amozi akaenda kwake na kumwambia, “Hili ndilo asemalo Bwana: Tengeneza mambo ya nyumba yako, kwa sababu utakufa, hutapona.”

2Hezekia akaelekeza uso wake ukutani, akamwomba Bwana: 338:3 Neh 5:19; 13:14; Kum 6:18; Za 26:3; 1Fal 8:61; 2Nya 29:19; Za 6:8“Ee Bwana, kumbuka jinsi nilivyoenenda mbele zako kwa uaminifu na kujitoa kwa moyo wangu wote, na kufanya yaliyo mema machoni pako.” Naye Hezekia akalia kwa uchungu.

438:4 1Sam 13:13; Isa 39:5Ndipo neno la Bwana likamjia Isaya, kusema: 538:5 2Fal 18:2-3; Za 6:6“Nenda ukamwambie Hezekia, ‘Hili ndilo asemalo Bwana, Mungu wa baba yako Daudi: Nimeyasikia maombi yako na nimeona machozi yako. Nitakuongezea miaka kumi na mitano katika maisha yako. 638:6 Isa 31:5; 37:35Nami nitakuokoa wewe pamoja na mji huu mkononi mwa mfalme wa Ashuru. Nitaulinda mji huu.

738:7 Mwa 24:14; 2Fal 20:8; 2Nya 32:31; Isa 7:11, 14; 20:3“ ‘Hii ndiyo ishara ya Bwana kwako ya kwamba Bwana atafanya kile alichoahidi: 838:8 Yos 10:13Nitafanya kivuli cha jua kwenye ngazi iliyojengwa na Ahazi kirudi nyuma madaraja kumi.’ ” Hivyo jua likarudi nyuma madaraja kumi ambayo lilikuwa limeshuka.

9Maandiko ya Hezekia mfalme wa Yuda baada ya kuugua kwake na kupona:

1038:10 Ay 17:16; Za 102:24; 2Kor 1:9; Ay 17:11; Za 107:18Nilisema, “Katika ustawi wa maisha yangu,

je, ni lazima nipite katika malango ya mauti,38:10 Mauti hapa maana yake ni Kuzimu.

na kupokonywa miaka yangu iliyobaki?”

1138:11 Za 27:13; Ay 28:13; 35:14; Isa 12:2; Za 116:5Nilisema, “Sitamwona tena Bwana,

Bwana katika nchi ya walio hai,

wala sitamtazama tena mwanadamu,

wala kuwa na wale ambao sasa wanakaa katika ulimwengu huu.

1238:12 2Kor 5:4; Ay 4:21; Isa 33:20; Ebr 1:12; Hes 11:15; Za 32:4; 1Pet 1:13-14Kama hema la mchunga mifugo,

nyumba yangu imebomolewa na kutwaliwa kutoka kwangu.

Kama mfumaji nimevingirisha maisha yangu,

naye amenikatilia mbali kutoka kitanda cha mfumi.

Mchana na usiku uliyakomesha maisha yangu.

1338:13 Ay 9:17; Mao 3:4; Yer 34:17; Za 37:7; 51:8; Ay 10:16; Dan 6:24Nilingoja kwa uvumilivu hadi mapambazuko,

lakini alivunja mifupa yangu yote kama simba.

Mchana na usiku uliyakomesha maisha yangu.

1438:14 Isa 59:11; Mwa 50:24; Ay 17:3; Mwa 8:8; Za 6:7Nililia kama mbayuwayu au korongo,

niliomboleza kama hua aombolezaye.

Macho yangu yalififia nilipotazama mbinguni.

Ee Bwana, ninataabika, njoo unisaidie!”

1538:15 Ay 7:11; 1Fal 21:27; Za 39:9; 2Sam 7:20Lakini niseme nini?

Amesema nami, naye yeye mwenyewe amelitenda hili.

Nitatembea kwa unyenyekevu

katika miaka yangu yote

kwa sababu ya haya maumivu makali

ya nafsi yangu.

1638:16 Ebr 12:9; Za 119:25Bwana, kwa mambo kama haya watu huishi,

nayo roho yangu hupata uzima katika hayo pia.

Uliniponya

na kuniacha niishi.

1738:17 Yer 31:34; Mik 7:19; Ay 17:16; Za 103:3, 12; Rum 8:28; Ebr 12:11; Isa 43:25Hakika ilikuwa ya faida yangu

ndiyo maana nikapata maumivu makali.

Katika upendo wako ukaniokoa

kutoka shimo la uharibifu;

umeziweka dhambi zangu zote

nyuma yako.

1838:18 Mhu 9:10; Hes 16:30; Za 6:5; 30:9; 88:10-11; 115:17Kwa maana kaburi38:18 Kaburini hapa maana yake ni Kuzimu, kwa Kiebrania ni Sheol. haliwezi kukusifu,

mauti haiwezi kuimba sifa zako;

wale washukao chini shimoni

hawawezi kuutarajia uaminifu wako.

1938:19 Kum 6:7; 11:19; Za 78:3; 118:7; 119:175Walio hai, walio hai: hao wanakusifu,

kama ninavyofanya leo.

Baba huwaambia watoto wao

habari za uaminifu wako.

2038:20 Za 68:25; 9:13; 45:8; 116:17-19; 63:4; 23:6Bwana ataniokoa,

nasi tutaimba kwa vyombo vya nyuzi

siku zote za maisha yetu

katika Hekalu la Bwana.

21Isaya alikuwa amesema, “Tengenezeni dawa ya kubandika ya tini, mweke juu ya jipu, naye atapona.”

22Hezekia alikuwa ameuliza, “Kutakuwa na ishara gani kwamba nitapanda kwenda Hekalu la Bwana?”

Japanese Contemporary Bible

イザヤ書 38:1-22

38

ヒゼキヤの病といやし

1この出来事の少し前、ヒゼキヤは死の病に取りつかれました。そこへアモツの子である預言者イザヤが来て、主のことばを伝えました。「あなたはもう長くない。身の回りを整理しておきなさい。治る見込みはない。」 2ヒゼキヤはこれを聞いて顔を壁に向け、必死に祈りました。 3「ああ神よ、お忘れになったのですか。あんなに真実を尽くし、いつも言いつけに従おうと努力してきましたのに。」王は肩を震わせ、大声で泣きました。

4それを見て、主はイザヤに告げました。 5「さあ行って、ヒゼキヤに言ってやりなさい。『あなたの父祖ダビデの神である主は、確かにあなたの祈りを聞いた。あなたの涙を見て、あと十五年いのちを延ばすことにした。 6あなたとこの都をアッシリヤ王の手から救い出し、あなたを守る、と主は言われる。 7-8その保証として、アハズの日時計の目盛りを十度あとに戻す。』」

すると、日時計に落ちる日の影は十度あと戻りしました。

9ヒゼキヤは元気になると、この経験を詩にまとめました。

10「まだ働き盛りだというのに、

いっさいをあきらめなければならないのか。

これからの歳月は奪い取られ、

よみの門に入ろうとしている。

11もう二度と、

生きている人の国で主を見ることはないだろう。

この世で友人の顔を見ることもない。

12私のいのちは、羊飼いの天幕のように

風で吹き飛ばされ、機を織る人が中途で

手を止めるように中断された。

私のいのちは、たった一日で消えていく。

13私は夜通しうめいた。

まるでライオンに引き裂かれるような苦しみだ。

14私は錯乱状態になり、

雀のようにさえずり、鳩のようにうめいた。

助けを求めて上を見続けていたので、

目はすっかりかすんでしまった。

私は叫んだ。『ああ神様、助けてください。

苦しくてたまりません。』

15しかし、私に何を言うことができよう。

私を病気にしたのは主なのだから。

苦しさのあまり眠ることもできない。

16『主よ、あなたの懲らしめは益となり、

いのちと健康に導きます。

どうか病気を治し、私を生かしてください。

17今やっとわかりました。

この苦しい経験は、みな私のためだったのです。

神が愛をもって私を死から救い出し、

いっさいの罪を赦してくださったからです。

18死人はあなたを賛美できません。

そこには希望も喜びもありません。

19生きていてこそ、今日の私のように、

あなたを賛美できるのです。

あなたの真実は父から子へ代々語り継がれます。』

20ああ、主は病気を治してくださった。

これからは毎日、いのちある限り、

神殿で主への賛美を奏でよう。」

21イザヤは王の召使に、「いちじくで塗り薬をつくり、はれものに塗りなさい。そうすれば、王様は元どおり元気になられます」と言いました。 22するとヒゼキヤは、「病気が必ず治る保証として、主はどんなしるしを与えてくださいますか」と尋ねてきました。