Isaya 36 – NEN & NIV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Isaya 36:1-22

Senakeribu Atishia Yerusalemu

(2 Wafalme 18:13-27; 2 Nyakati 32:1-19)

136:1 2Nya 32:1; 2Fal 18:9; Za 109:11Katika mwaka wa kumi na nne wa utawala wa Mfalme Hezekia, Senakeribu mfalme wa Ashuru akaishambulia miji yote ya Yuda yenye ngome na kuiteka. 236:2 Isa 7:3; Yos 10:3Kisha mfalme wa Ashuru akamtuma jemadari wa jeshi pamoja na jeshi kubwa kutoka Lakishi hadi kwa Mfalme Hezekia huko Yerusalemu. Jemadari wa jeshi akasimama kwenye mfereji wa Bwawa la Juu, lililojengwa katika barabara iendayo kwenye Uwanja wa Dobi. 336:3 2Fal 18:18; Isa 37:2; 22:20-21; Mik 1:13; 2Sam 8:17; Mwa 41:40; 2Sam 8:16Eliakimu mwana wa Hilkia aliyekuwa msimamizi wa jumba la kifalme, Shebna aliyekuwa katibu, na Yoa mwana wa Asafu mwandishi wakamwendea.

4Jemadari wa jeshi akawaambia, “Mwambieni Hezekia,

“ ‘Hili ndilo asemalo mfalme mkuu, mfalme wa Ashuru: Ni wapi unapoweka hili tumaini lako? 536:5 2Fal 18:7Unasema mnayo mikakati na nguvu za kijeshi, lakini unasema maneno matupu tu. Je, wewe unamtegemea nani, hata ukaniasi mimi? 636:6 Isa 30:2-5; 58:5; Eze 29:6-7; 2Fal 17:4; Isa 8:12; Eze 17:17Tazama sasa, unaitegemea Misri, fimbo ile ya mwanzi uliopasuka, ambayo huuchoma na kuujeruhi mkono wa mtu akiiegemea! Hivyo ndivyo alivyo Farao mfalme wa Misri, kwa wote wanaomtegemea. 736:7 Kum 12:2-5; 2Fal 18:4; 2Nya 31:1; Za 22:8; Mt 27:43Nawe kama ukiniambia, “Tunamtumainia Bwana Mungu wetu”: je, siyo yeye ambaye Hezekia aliondoa mahali pake pa juu pa kuabudia miungu na madhabahu zake, akiwaambia Yuda na Yerusalemu, “Ni lazima mwabudu mbele ya madhabahu haya”?

836:8 Za 20:7; Isa 30:16“ ‘Njooni sasa, fanyeni mapatano na bwana wangu, mfalme wa Ashuru: Nitakupa farasi elfu mbili, kama unaweza kuwapandisha waendesha farasi juu yao! 936:9 Za 20:7; Isa 30:2-5; 31:3Utawezaje kumzuia hata afisa mmoja aliye mdogo kati ya maafisa wa bwana wangu, ijapo unategemea Misri kwa magari ya vita na wapanda farasi? 1036:10 1Fal 13:18; Isa 10:5-7Zaidi ya hayo, je, nimekuja kushambulia na kuangamiza nchi hii bila Bwana? Bwana mwenyewe ndiye aliniambia niishambulie nchi hii na kuiangamiza.’ ”

1136:11 Ezr 4:7Ndipo Eliakimu, Shebna na Yoa wakamwambia yule jemadari wa jeshi, “Tafadhali zungumza na watumishi wako kwa lugha ya Kiaramu, kwa kuwa tunaifahamu. Usiseme nasi kwa Kiebrania watu walioko juu ya ukuta wakiwa wanasikia.”

1236:12 2Fal 6:25; Eze 4:12Lakini yule jemadari wa jeshi akajibu, “Je, bwana wangu amenituma kutoa ujumbe huu kwa bwana wenu na kwenu tu? Je, hakunituma pia kwa watu walioketi ukutani, ambao, kama ninyi, itawabidi kula mavi yao na kunywa mikojo yao wenyewe?”

1336:13 2Nya 32:18; Isa 37:4Kisha yule jemadari wa jeshi akasimama na kuita kwa lugha ya Kiebrania, akasema: “Sikieni maneno ya mfalme mkuu, mfalme wa Ashuru! 1436:14 2Nya 32:15Hili ndilo asemalo mfalme: Msikubali Hezekia awadanganye. Hawezi kuwaokoa! 1536:15 Isa 37:10; Za 3:2-7Msikubali Hezekia awashawishi kumtumaini Bwana kwa kuwaambia, ‘Hakika Bwana atatuokoa. Mji huu hautaangukia mikononi mwa mfalme wa Ashuru.’

1636:16 1Fal 4:25; Zek 3:10; Mik 4:4; Mit 5:15“Msimsikilize Hezekia. Hili ndilo mfalme wa Ashuru asemalo: Fanyeni amani nami na mje kwangu. Kisha kila mmoja wenu atakula kutoka kwa mzabibu wake na mtini wake mwenyewe, na kunywa maji kutoka kisima chake mwenyewe, 1736:17 2Fal 15:29; Mwa 27:28; Kum 28:51mpaka nije nikawapeleke katika nchi iliyo kama nchi yenu wenyewe, nchi ya nafaka na divai mpya, nchi ya mkate na ya mashamba ya mizabibu.

18“Msikubali Hezekia awapotoshe asemapo, ‘Bwana atatuokoa.’ Je, yuko mungu wa taifa lolote aliyewahi kuokoa nchi yake kutoka mkononi mwa mfalme wa Ashuru? 1936:19 Hes 34:8; Yos 13:5; 2Fal 18:34; 17:24; 15:29Iko wapi miungu ya Hamathi na ya Arpadi? Iko wapi miungu ya Sefarvaimu? Je, imeokoa Samaria kutoka mkononi mwangu? 2036:20 1Fal 20:23; Dan 3:15; 2Nya 32:15; 25:15; Kut 5:2; Isa 10:8-11Ni yupi miongoni mwa miungu yote ya nchi hizi ameweza kuokoa nchi yake mkononi mwangu? Inawezekanaje basi Bwana aiokoe Yerusalemu mkononi mwangu?”

2136:21 Amo 5:13; Mit 9:7-8; 26:4Lakini wale watu wakakaa kimya, wala hawakujibu lolote, kwa kuwa mfalme alikuwa amewaamuru, “Msimjibu lolote.”

2236:22 Mwa 37:29; 1Sam 4:12; Ay 1:20; 2Fal 18:18; 2Sam 8:16; 2Nya 34:19Kisha Eliakimu mwana wa Hilkia msimamizi wa jumba la kifalme, Shebna katibu, na Yoa mwana wa Asafu, mwandishi wakamwendea Hezekia, nguo zao zikiwa zimeraruliwa, na kumwambia yale jemadari wa jeshi aliyoyasema.

New International Version

Isaiah 36:1-22

Sennacherib Threatens Jerusalem

1In the fourteenth year of King Hezekiah’s reign, Sennacherib king of Assyria attacked all the fortified cities of Judah and captured them. 2Then the king of Assyria sent his field commander with a large army from Lachish to King Hezekiah at Jerusalem. When the commander stopped at the aqueduct of the Upper Pool, on the road to the Launderer’s Field, 3Eliakim son of Hilkiah the palace administrator, Shebna the secretary, and Joah son of Asaph the recorder went out to him.

4The field commander said to them, “Tell Hezekiah:

“ ‘This is what the great king, the king of Assyria, says: On what are you basing this confidence of yours? 5You say you have counsel and might for war—but you speak only empty words. On whom are you depending, that you rebel against me? 6Look, I know you are depending on Egypt, that splintered reed of a staff, which pierces the hand of anyone who leans on it! Such is Pharaoh king of Egypt to all who depend on him. 7But if you say to me, “We are depending on the Lord our God”—isn’t he the one whose high places and altars Hezekiah removed, saying to Judah and Jerusalem, “You must worship before this altar”?

8“ ‘Come now, make a bargain with my master, the king of Assyria: I will give you two thousand horses—if you can put riders on them! 9How then can you repulse one officer of the least of my master’s officials, even though you are depending on Egypt for chariots and horsemen36:9 Or charioteers? 10Furthermore, have I come to attack and destroy this land without the Lord? The Lord himself told me to march against this country and destroy it.’ ”

11Then Eliakim, Shebna and Joah said to the field commander, “Please speak to your servants in Aramaic, since we understand it. Don’t speak to us in Hebrew in the hearing of the people on the wall.”

12But the commander replied, “Was it only to your master and you that my master sent me to say these things, and not to the people sitting on the wall—who, like you, will have to eat their own excrement and drink their own urine?”

13Then the commander stood and called out in Hebrew, “Hear the words of the great king, the king of Assyria! 14This is what the king says: Do not let Hezekiah deceive you. He cannot deliver you! 15Do not let Hezekiah persuade you to trust in the Lord when he says, ‘The Lord will surely deliver us; this city will not be given into the hand of the king of Assyria.’

16“Do not listen to Hezekiah. This is what the king of Assyria says: Make peace with me and come out to me. Then each of you will eat fruit from your own vine and fig tree and drink water from your own cistern, 17until I come and take you to a land like your own—a land of grain and new wine, a land of bread and vineyards.

18“Do not let Hezekiah mislead you when he says, ‘The Lord will deliver us.’ Have the gods of any nations ever delivered their lands from the hand of the king of Assyria? 19Where are the gods of Hamath and Arpad? Where are the gods of Sepharvaim? Have they rescued Samaria from my hand? 20Who of all the gods of these countries have been able to save their lands from me? How then can the Lord deliver Jerusalem from my hand?”

21But the people remained silent and said nothing in reply, because the king had commanded, “Do not answer him.”

22Then Eliakim son of Hilkiah the palace administrator, Shebna the secretary and Joah son of Asaph the recorder went to Hezekiah, with their clothes torn, and told him what the field commander had said.