Isaya 36 – NEN & CCB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Isaya 36:1-22

Senakeribu Atishia Yerusalemu

(2 Wafalme 18:13-27; 2 Nyakati 32:1-19)

136:1 2Nya 32:1; 2Fal 18:9; Za 109:11Katika mwaka wa kumi na nne wa utawala wa Mfalme Hezekia, Senakeribu mfalme wa Ashuru akaishambulia miji yote ya Yuda yenye ngome na kuiteka. 236:2 Isa 7:3; Yos 10:3Kisha mfalme wa Ashuru akamtuma jemadari wa jeshi pamoja na jeshi kubwa kutoka Lakishi hadi kwa Mfalme Hezekia huko Yerusalemu. Jemadari wa jeshi akasimama kwenye mfereji wa Bwawa la Juu, lililojengwa katika barabara iendayo kwenye Uwanja wa Dobi. 336:3 2Fal 18:18; Isa 37:2; 22:20-21; Mik 1:13; 2Sam 8:17; Mwa 41:40; 2Sam 8:16Eliakimu mwana wa Hilkia aliyekuwa msimamizi wa jumba la kifalme, Shebna aliyekuwa katibu, na Yoa mwana wa Asafu mwandishi wakamwendea.

4Jemadari wa jeshi akawaambia, “Mwambieni Hezekia,

“ ‘Hili ndilo asemalo mfalme mkuu, mfalme wa Ashuru: Ni wapi unapoweka hili tumaini lako? 536:5 2Fal 18:7Unasema mnayo mikakati na nguvu za kijeshi, lakini unasema maneno matupu tu. Je, wewe unamtegemea nani, hata ukaniasi mimi? 636:6 Isa 30:2-5; 58:5; Eze 29:6-7; 2Fal 17:4; Isa 8:12; Eze 17:17Tazama sasa, unaitegemea Misri, fimbo ile ya mwanzi uliopasuka, ambayo huuchoma na kuujeruhi mkono wa mtu akiiegemea! Hivyo ndivyo alivyo Farao mfalme wa Misri, kwa wote wanaomtegemea. 736:7 Kum 12:2-5; 2Fal 18:4; 2Nya 31:1; Za 22:8; Mt 27:43Nawe kama ukiniambia, “Tunamtumainia Bwana Mungu wetu”: je, siyo yeye ambaye Hezekia aliondoa mahali pake pa juu pa kuabudia miungu na madhabahu zake, akiwaambia Yuda na Yerusalemu, “Ni lazima mwabudu mbele ya madhabahu haya”?

836:8 Za 20:7; Isa 30:16“ ‘Njooni sasa, fanyeni mapatano na bwana wangu, mfalme wa Ashuru: Nitakupa farasi elfu mbili, kama unaweza kuwapandisha waendesha farasi juu yao! 936:9 Za 20:7; Isa 30:2-5; 31:3Utawezaje kumzuia hata afisa mmoja aliye mdogo kati ya maafisa wa bwana wangu, ijapo unategemea Misri kwa magari ya vita na wapanda farasi? 1036:10 1Fal 13:18; Isa 10:5-7Zaidi ya hayo, je, nimekuja kushambulia na kuangamiza nchi hii bila Bwana? Bwana mwenyewe ndiye aliniambia niishambulie nchi hii na kuiangamiza.’ ”

1136:11 Ezr 4:7Ndipo Eliakimu, Shebna na Yoa wakamwambia yule jemadari wa jeshi, “Tafadhali zungumza na watumishi wako kwa lugha ya Kiaramu, kwa kuwa tunaifahamu. Usiseme nasi kwa Kiebrania watu walioko juu ya ukuta wakiwa wanasikia.”

1236:12 2Fal 6:25; Eze 4:12Lakini yule jemadari wa jeshi akajibu, “Je, bwana wangu amenituma kutoa ujumbe huu kwa bwana wenu na kwenu tu? Je, hakunituma pia kwa watu walioketi ukutani, ambao, kama ninyi, itawabidi kula mavi yao na kunywa mikojo yao wenyewe?”

1336:13 2Nya 32:18; Isa 37:4Kisha yule jemadari wa jeshi akasimama na kuita kwa lugha ya Kiebrania, akasema: “Sikieni maneno ya mfalme mkuu, mfalme wa Ashuru! 1436:14 2Nya 32:15Hili ndilo asemalo mfalme: Msikubali Hezekia awadanganye. Hawezi kuwaokoa! 1536:15 Isa 37:10; Za 3:2-7Msikubali Hezekia awashawishi kumtumaini Bwana kwa kuwaambia, ‘Hakika Bwana atatuokoa. Mji huu hautaangukia mikononi mwa mfalme wa Ashuru.’

1636:16 1Fal 4:25; Zek 3:10; Mik 4:4; Mit 5:15“Msimsikilize Hezekia. Hili ndilo mfalme wa Ashuru asemalo: Fanyeni amani nami na mje kwangu. Kisha kila mmoja wenu atakula kutoka kwa mzabibu wake na mtini wake mwenyewe, na kunywa maji kutoka kisima chake mwenyewe, 1736:17 2Fal 15:29; Mwa 27:28; Kum 28:51mpaka nije nikawapeleke katika nchi iliyo kama nchi yenu wenyewe, nchi ya nafaka na divai mpya, nchi ya mkate na ya mashamba ya mizabibu.

18“Msikubali Hezekia awapotoshe asemapo, ‘Bwana atatuokoa.’ Je, yuko mungu wa taifa lolote aliyewahi kuokoa nchi yake kutoka mkononi mwa mfalme wa Ashuru? 1936:19 Hes 34:8; Yos 13:5; 2Fal 18:34; 17:24; 15:29Iko wapi miungu ya Hamathi na ya Arpadi? Iko wapi miungu ya Sefarvaimu? Je, imeokoa Samaria kutoka mkononi mwangu? 2036:20 1Fal 20:23; Dan 3:15; 2Nya 32:15; 25:15; Kut 5:2; Isa 10:8-11Ni yupi miongoni mwa miungu yote ya nchi hizi ameweza kuokoa nchi yake mkononi mwangu? Inawezekanaje basi Bwana aiokoe Yerusalemu mkononi mwangu?”

2136:21 Amo 5:13; Mit 9:7-8; 26:4Lakini wale watu wakakaa kimya, wala hawakujibu lolote, kwa kuwa mfalme alikuwa amewaamuru, “Msimjibu lolote.”

2236:22 Mwa 37:29; 1Sam 4:12; Ay 1:20; 2Fal 18:18; 2Sam 8:16; 2Nya 34:19Kisha Eliakimu mwana wa Hilkia msimamizi wa jumba la kifalme, Shebna katibu, na Yoa mwana wa Asafu, mwandishi wakamwendea Hezekia, nguo zao zikiwa zimeraruliwa, na kumwambia yale jemadari wa jeshi aliyoyasema.

Chinese Contemporary Bible (Simplified)

以赛亚书 36:1-22

亚述王入侵犹大

1希西迦王十四年,亚述西拿基立率兵攻打犹大,攻陷所有的坚城。 2然后,亚述王从拉吉差遣将军率领大军去耶路撒冷希西迦王。大军停在上池的水沟旁、通往漂布场的路上。 3希勒迦的儿子宫廷总管以利亚敬、书记舍伯那亚萨的儿子史官约亚出来见亚述的将军。

4亚述的将军对他们说:“你们去告诉希西迦,伟大的亚述王说,‘你凭什么这样自信呢? 5你所谓的战略和军力不过是空话。你究竟倚靠谁,竟敢背叛我? 6看啊,你所倚靠的埃及不过是一根破裂的芦苇,倚靠它的必被刺破手。倚靠埃及王法老的下场都是这样。’ 7也许你说,‘我们倚靠我们的上帝耶和华。’希西迦不是拆毁了祂的庙宇和祭坛,又吩咐犹大耶路撒冷的人只能在这座祭坛前敬拜吗? 8来,跟我主人亚述王打个赌,你若能找到两千骑士,我就给你两千匹马! 9你们即使依靠埃及的战车和骑兵,又怎能打败我主人的一个最小的将领呢? 10更何况我来攻打、毁灭这地方不正是耶和华的意思吗?耶和华吩咐我攻打、毁灭这地方。”

11以利亚敬舍伯那约亚亚述的将军说:“求你用亚兰语跟仆人们说话,我们都听得懂。求你不要用希伯来语跟我们说话,免得城墙上的人听见。” 12亚述的将军却说:“难道我主派我来只对希西迦和你们说这些话吗?不也是对城墙上的人说吗?他们和你们一样都要吃自己的粪,喝自己的尿。”

13于是,他站着用希伯来语大喊:“你们要听伟大的亚述王的话, 14王说,‘你们不要被希西迦欺骗,他不能救你们。 15不要听希西迦的话去倚靠耶和华,说什么耶和华必拯救你们,这城必不会落在亚述王手中。’ 16不要听希西迦的话。亚述王说,‘你们要跟我讲和,出来归顺我。这样,你们就可以吃自己葡萄树和无花果树的果子,喝自己井里的水。 17以后我会来领你们到一个地方,那里和这里一样有五谷和新酒、饼和葡萄园。 18不要让希西迦欺骗你们,以为耶和华必拯救你们。列国的神明中有哪个曾经从亚述王手中救他的国家呢? 19哈马亚珥拔的神明在哪里呢?西法瓦音的神明在哪里呢?他们从我手中救撒玛利亚了吗? 20这些国家的神明中有哪个曾从我手中救自己的国家呢?难道耶和华能从我手中救耶路撒冷吗?’” 21民众默不作声,一言不发,因为希西迦曾吩咐他们不要答话。 22于是,宫廷总管以利亚敬、书记舍伯那和史官约亚都撕裂衣服,去向希西迦禀告亚述的将军说的话。