Isaya 34 – NEN & NIRV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Isaya 34:1-17

Hukumu Dhidi Ya Mataifa

134:1 Isa 43:9; Kum 4:26; 32:1; Za 24:1; Isa 33:13Njooni karibu, enyi mataifa, nanyi msikilize;

sikilizeni kwa makini,

enyi kabila za watu!

Dunia na isikie, navyo vyote vilivyo ndani yake,

ulimwengu na vyote vitokavyo ndani yake!

234:2 Isa 13:5; Zek 5:3; Isa 10:25; 30:25Bwana ameyakasirikia mataifa yote;

ghadhabu yake ni juu ya majeshi yao yote.

Atawaangamiza kabisa,

atawatia mikononi mwa wachinjaji.

334:3 Yoe 2:20; Amo 4:10; Eze 38:22; Isa 5:25; Za 110:6; Eze 5:17; 14:19Waliouawa watatupwa nje,

maiti zao zitatoa uvundo,

milima itatota kwa damu zao.

434:4 2Pet 3:10; Yoe 2:31; Eze 32:7-8; Ay 9:7; Ufu 6:13; Isa 13:13; Mt 24:29; Ay 8:12; Mk 13:15; Isa 15:6; Ebr 1:12Nyota zote za mbinguni zitayeyuka

na anga litasokotwa kama kitabu,

jeshi lote la angani litaanguka

kama majani yaliyonyauka kutoka kwenye mzabibu,

kama tini iliyonyauka kutoka kwenye mtini.

534:5 Yer 49:7; 46:10; Zek 13:7; 2Sam 8:13-14; Yos 6:17; Kum 32:41-42; Amo 3:14-15; Yer 47:6; Eze 21:5; 2Nya 28:17; Amo 1:11-12; 6:11; Mal 1:4Upanga wangu umekunywa na kushiba huko mbinguni,

tazama, unashuka katika hukumu juu ya Edomu,

wale watu ambao nimeshawahukumu,

kuwaangamiza kabisa.

634:6 Kum 32:41; Law 3:9; Mwa 36:33; Isa 30:25; Yer 25:34; Ufu 19:17Upanga wa Bwana umeoga katika damu,

umefunikwa na mafuta ya nyama:

damu ya kondoo na mbuzi,

mafuta kutoka figo za kondoo dume.

Kwa maana Bwana ana dhabihu huko Bosra,

na machinjo makuu huko Edomu.

734:7 Hes 23:22; Za 68:30; 2Sam 1:22Nyati wataanguka pamoja nao,

ndama waume na mafahali wakubwa.

Nchi yao italowana kwa damu,

nayo mavumbi yataloa mafuta ya nyama.

834:8 Isa 2:12; 1:24; 59:18; Yoe 3:4; Eze 25:12-17; Amo 1:6-10Kwa sababu Bwana anayo siku ya kulipiza kisasi,

mwaka wa malipo,

siku ya kushindania shauri la Sayuni.

934:9 Mwa 19:24Vijito vya Edomu vitageuka kuwa lami,

mavumbi yake yatakuwa kiberiti kiunguzacho,

nchi yake itakuwa lami iwakayo!

1034:10 Ufu 14:10-11; 19:3; Yer 49:18; Mal 1:3; Isa 13:20; Eze 29:12; 35:3Haitazimishwa usiku wala mchana,

moshi wake utapaa juu milele.

Kutoka kizazi hadi kizazi itakuwa ukiwa,

hakuna mtu yeyote atakayepita huko tena.

1134:11 Law 11:16-18; Ufu 18:2; Mao 2:8; Amo 7:8; Kum 14:15-17; Yoe 3:19; 2Fal 21:13Bundi wa jangwani na bundi mwenye sauti nyembamba wataimiliki,

bundi wakubwa na kunguru wataweka viota humo.

Mungu atanyoosha juu ya Edomu

kamba ya kupimia ya machafuko matupu,

na timazi ya ukiwa.

1234:12 Isa 41:11-12; Za 107:10; Ay 12:21; Isa 40:23; Eze 24:5; Yer 39:6Watu wake wa kuheshimiwa hawatakuwa na chochote

kitakachoitwa ufalme huko,

nao wakuu wao wote watatoweka.

1334:13 Hos 9:6; Isa 32:13; 13:22; Yer 9:11; Isa 7:19; Za 44:19Miiba itaenea katika ngome za ndani,

viwawi na michongoma itaota

kwenye ngome zake.

Itakuwa maskani ya mbweha,

makao ya bundi.

1434:14 Za 74:14; Isa 13:22; Ufu 18:2Viumbe vya jangwani vitakutana na fisi,

nao mbuzi-mwitu watalia wakiitana;

huko viumbe vya usiku vitastarehe pia

na kujitafutia mahali pa kupumzika.

1534:15 Za 17:8; Kum 14:13Bundi wataweka viota huko na kutaga mayai,

atayaangua na kutunza makinda yake

chini ya uvuli wa mabawa yake;

pia huko vipanga watakusanyika,

kila mmoja na mwenzi wake.

1634:16 Isa 30:8; Dan 7:10; Isa 1:20; 58:14; 48:13Angalieni katika gombo la Bwana na msome:

Hakuna hata mmoja katika hawa atakayekosekana,

hakuna hata mmoja atakayemkosa mwenzi wake.

Kwa kuwa ni kinywa chake Mungu kimeagiza,

na Roho wake atawakusanya pamoja.

1734:17 Za 78:55; Isa 17:14; Yer 13:25Huwagawia sehemu zao,

mkono wake huwagawanyia kwa kipimo.

Wataimiliki hata milele

na kuishi humo kutoka kizazi hadi kizazi.

New International Reader’s Version

Isaiah 34:1-17

The Lord Will Judge the Nations

1Nations, come near and listen to me!

Pay attention to what I’m about to say.

Let the earth and everything in it listen.

Let the world and everything that comes out of it pay attention.

2The Lord is angry with all the nations.

His anger is against all their armies.

He will totally destroy them.

He will have them killed.

3Those who are killed won’t be buried.

Their dead bodies will be thrown on the ground.

They will stink.

Their blood will cover the mountains.

4All the stars in the sky will vanish.

The heavens will be rolled up like a scroll.

All the stars in the sky will fall like dried-up leaves from a vine.

They will drop like wrinkled figs from a fig tree.

5The sword of the Lord will finish its deadly work in the sky.

Then it will come down to strike Edom.

He will totally destroy that nation.

6His sword will be red with blood.

It will be covered with fat.

The blood will flow like the blood

of lambs and goats being sacrificed.

The fat will be like the fat

taken from the kidneys of rams.

That’s because the Lord will offer a sacrifice

in the city of Bozrah.

He will kill many people in the land of Edom.

7The people and their leaders will be killed

like wild oxen and young bulls.

Their land will be wet with their blood.

The dust will be covered with their fat.

8That’s because the Lord has set aside a day to pay Edom back.

He has set aside a year to pay them back. He will pay them back for what they did to Zion.

9The streams of Edom will be turned into tar.

Its dust will be turned into blazing sulfur.

Its land will become burning tar.

10The fire will keep burning night and day.

It can’t be put out.

Its smoke will go up forever.

Edom will lie empty for all time to come.

No one will ever travel through it again.

11The desert owl and screech owl will make it their home.

The great owl and the raven will build their nests there.

God will use his measuring line

to show how completely Edom will be destroyed.

He will use his plumb line

to show how empty Edom will become.

12Edom’s nobles won’t have anything left there

that can be called a kingdom.

All its princes will vanish.

13Thorns will cover its forts.

Bushes and weeds will cover its safest places.

It will become a home for wild dogs.

It will become a place where owls live.

14Desert creatures will meet with hyenas.

Wild goats will call out to each other.

Night creatures will also lie down there.

They will find places where they can rest.

15Owls will make their nests and lay their eggs there.

And they will hatch them.

They will take care of their little ones

under the shadow of their wings.

Male and female falcons will also gather there.

16Look in the book of the Lord. Here is what you will read there.

None of those animals will be missing.

Male and female alike will be there.

The Lord himself has commanded it.

And his Spirit will gather them together.

17The Lord will decide what part of the land goes to each animal.

Then he will give each one its share.

It will belong to them forever.

And they will live there for all time to come.