Isaya 31 – NEN & HTB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Isaya 31:1-9

Ole Wa Wale Wanaotegemea Misri

131:1 Eze 17:15; Kum 17:16; 20:1; Yer 37:5; Dan 9:13; Hos 11:8; Isa 30:2-5; Ay 6:10Ole wao wale washukao Misri kwa ajili ya msaada,

wale wategemeao farasi,

wanaoweka tumaini katika wingi wa magari yao ya vita,

na katika nguvu nyingi za wapanda farasi,

lakini hawamwangalii yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli,

wala hawatafuti msaada kwa Bwana.

231:2 Za 92:5; Rum 16:27; Hes 23:19; Mit 19:21; Isa 29:15; Amo 3:6; Isa 29:19; 32:6Hata hivyo yeye pia ana hekima na anaweza kuleta maafa,

wala hayatangui maneno yake.

Yeye atainuka dhidi ya nyumba ya mwovu,

dhidi ya wale ambao huwasaidia watenda mabaya.

331:3 Eze 28:9; Isa 20:5; Za 9:20; 2The 2:4; Ay 30:21; Yer 51:25; Isa 30:5-7; Neh 1:10Lakini Wamisri ni wanadamu, wala si Mungu,

farasi wao ni nyama, wala si roho.

Wakati Bwana atakaponyoosha Mkono wake,

yeye anayesaidia atajikwaa,

naye anayesaidiwa ataanguka,

wote wawili wataangamia pamoja.

431:4 Nah 3:18; Ay 30:21; Isa 30:5-7; Hes 24:9; 1Sam 17:34; Eze 34:23; Isa 42:13; Hos 11:10Hili ndilo Bwana analoniambia:

“Kama vile simba angurumavyo,

simba mkubwa juu ya mawindo yake:

hata ingawa kundi lote la wachunga mifugo

huitwa pamoja dhidi yake,

hatiwi hofu na kelele zao

wala kusumbuliwa na ghasia zao;

ndivyo Bwana Mwenye Nguvu Zote atakavyoshuka

kufanya vita juu ya Mlima Sayuni

na juu ya vilele vyake.

531:5 Za 91:4; Kum 32:11; Zek 9:15; Za 34:7; Mt 23:37; Kut 12:23Kama ndege warukao,

Bwana Mwenye Nguvu Zote ataukinga Yerusalemu;

ataukinga na kuuokoa,

atapita juu yake na kuufanya salama.”

631:6 Ay 22:23; Isa 1:5, 27Mrudieni yeye ambaye nyumba ya Israeli imemwasi sana. 731:7 Isa 2:20; 30:22; 1Fal 12:30; Za 135:5Kwa kuwa katika siku ile kila mmoja wenu atazikataa sanamu za fedha na za dhahabu zilizotengenezwa kwa mikono yenu yenye dhambi.

831:8 Isa 10:12; Kut 12:12; Hab 2:8; Mwa 49:15; Isa 14:25; Yer 25:12; Kum 20:11“Ashuru itaanguka kwa upanga ambao si wa mwanadamu;

upanga usio wa kibinadamu utawaangamiza.

Watakimbia mbele ya upanga

na vijana wao wa kiume watafanyizwa kazi kwa lazima.

931:9 Kum 32:31-37; Isa 10:17; Law 6:13; Isa 18:3; Yer 4:6; 51:9; Za 21:9Ngome zao zitaanguka kwa sababu ya hofu;

kwa kuona bendera ya vita,

majemadari wao watashikwa na hofu ya ghafula,”

asema Bwana,

ambaye moto wake uko Sayuni,

nayo tanuru yake iko Yerusalemu.

Het Boek

Jesaja 31:1-9

Het ‘zwaard van God’ zal toeslaan

1Wee hen die naar Egypte gaan om hulp, die vertrouwen op paarden, strijdwagens en machtige ruiters in plaats van op de Heilige van Israël en Hem niet om raad vragen. 2In zijn wijsheid brengt Hij een groot kwaad over zijn volk en Hij verandert niet van gedachten. Hij keert Zich tegen zijn volk om hun slechtheid en tegen ieder die hun helpt.

3Want deze Egyptenaren zijn slechts mensen, geen God! Hun paarden zijn van vlees, geen machtige geesten! Als de Here zijn vuist tegen hen balt, zullen zij struikelen en vallen, samen met degenen die zij wilden helpen. Zij zullen allen te gronde worden gericht.

4-5 Maar de Here heeft mij dit gezegd: als een leeuw, zelfs al is hij nog maar jong, een schaap doodt, schenkt hij geen aandacht aan het geschreeuw en lawaai van de herder. Hij gaat zijn gang en eet van zijn prooi. Zo zal de Here ook doen als Hij komt om op de berg Sion te strijden. Niemand zal Hem kunnen afschrikken! Hij, de Here van de hemelse legers, zal over Jeruzalem waken als vogels die rond hun nest wieken. Hij zal de stad verdedigen en haar verlossen.

6Daarom, mijn volk, keer terug naar Hem van wie u zo ver bent afgedwaald. 7Ik weet dat de dag zal komen dat ieder van u zijn gouden en zilveren afgodsbeelden zal weggooien die u in uw zondigheid hebt gemaakt. 8Dan zullen de Assyriërs worden vernietigd, maar niet door zwaarden van mensen. Het ‘zwaard van God’ zal hen verslaan. Zij zullen in paniek op de vlucht slaan. De sterke, jonge Assyriërs zullen worden weggeleid als slaven. 9Zelfs hun aanvoerders zullen beven van schrik en op de vlucht slaan wanneer zij de oorlogsvaandels van Israël zien, zegt de Here. Want de vlam van God brandt helder in Jeruzalem.