Isaya 30 – NEN & NIV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Isaya 30:1-33

Ole Wa Taifa Kaidi

130:1 Isa 29:15; 8:12; Kum 29:19; 21:18; 2Fal 17:4Bwana asema,

“Ole kwa watoto wakaidi,

kwa wale wanaotimiza mipango ambayo si yangu,

wakifanya makubaliano, lakini si kwa Roho wangu,

wakilundika dhambi juu ya dhambi,

230:2 Mwa 25:22; Hes 27:21; 2Fal 25:26; Isa 36:6; Yer 2:18, 36; 42:14; Eze 17:15; 29:16wale washukao kwenda Misri

bila kutaka shauri langu,

wanaotafuta msaada wa ulinzi wa Farao,

watafutao kivuli cha Misri kwa ajili ya kimbilio.

330:3 Yer 37:5-7; Isa 20:4-5; Amu 9:8-15; Za 44:13Lakini ulinzi wa Farao utakuwa kwa aibu yenu,

kivuli cha Misri kitawaletea fedheha.

430:4 Hes 13:22; Isa 19:11Ingawa wana maafisa katika Soani

na wajumbe wamewasili katika Hanesi,

530:5 Isa 20:5; 36:6; 2Fal 18:21; Za 108:12; Yer 37:3-5; Eze 17:15kila mmoja ataaibishwa

kwa sababu ya taifa lisilowafaa kitu,

ambalo haliwaletei msaada wala faida,

bali aibu tu na fedheha.”

630:6 Kut 1:3; Yer 11:4; Kum 8:15; Hos 8:9; Kut 5:10; Isa 13:1; 5:30; 5:29; Mwa 42:26Neno kuhusu wanyama wa Negebu:

Katika nchi ya taabu na shida,

ya simba za dume na jike,

ya nyoka mwenye sumu kali na nyoka warukao,

wajumbe huchukua utajiri wao juu ya migongo ya punda,

hazina zao juu ya nundu za ngamia,

kwa lile taifa lisilokuwa na faida,

730:7 Yer 2:36; Ay 9:13; 2Fal 18:2kuvipeleka Misri,

ambaye msaada wake haufai kabisa.

Kwa hiyo nimemwita “Rahabu Asiyefanya Chochote.”

830:8 Kut 17:14; Hab 2:2; Kum 27:8; Yer 25:13; Yos 24:26-27; Isa 8:1; Yer 30:2Nenda sasa, liandike neno hili juu ya kibao kwa ajili yao,

liandike kwenye kitabu,

ili liweze kuwa shahidi milele

kwa ajili ya siku zijazo.

930:9 Isa 28:15; Kum 32:20; Isa 59:3-4; Za 78:8; Eze 2:6Hawa ni watu waasi, watoto wadanganyifu,

watoto ambao hawataki kusikiliza mafundisho ya Bwana.

1030:10 Amo 7:13; Yer 11:21; 32:3; 1Sam 9:9; 1Fal 22:8; Yer 4:10; Eze 13:7; Rum 16:18; 2Tim 4:4Wanawaambia waonaji,

“Msione maono tena!”

Nako kwa manabii wanasema,

“Msiendelee kutupatia maono

ambayo ni ya kweli!

Tuambieni mambo ya kupendeza,

tabirini mambo ya uongo.

1130:11 Mdo 13:8; Ay 21:14; Isa 35:8-9; Mit 3:6; Isa 29:19; 48:17Acheni njia hii,

ondokeni katika mapito haya,

nanyi acheni kutukabili pamoja

na yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli!”

1230:12 Isa 5:19; 5:24; Za 10:7; 12:5; Isa 5:7, 24Kwa hiyo, hili ndilo asemalo yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli:

“Kwa sababu mmekataa ujumbe huu,

mkategemea uonevu na kutumainia udanganyifu,

1330:13 Neh 2:17; Za 80:12; 1Fal 20:30; Isa 17:14; Za 62:3dhambi hii itakuwa kwenu

kama ukuta mrefu,

wenye ufa na wenye kubetuka,

ambao unaanguka ghafula,

mara moja.

1430:14 Za 2:9; 2Pet 2:4-5Utavunjika vipande vipande kama chombo cha udongo

ukipasuka pasipo huruma

ambapo katika vipande vyake

hakuna kipande kitakachopatikana

kwa kuukulia makaa kutoka jikoni

au kuchotea maji kisimani.”

1530:15 Isa 32:17; 2Nya 20:12; Mt 23:37Hili ndilo Bwana Mwenyezi, yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli, asemalo:

“Katika kutubu na kupumzika ndio wokovu wenu,

katika kutulia na kutumaini ndizo nguvu zenu,

lakini hamkutaka.

1630:16 Yer 46:6; Kum 17:16; 1Fal 10:28-29Mlisema, ‘Hapana, tutakimbia kwa farasi.’

Kwa hiyo mtakimbia!

Mlisema, ‘Tutakimbia kwa farasi waendao kasi.’

Kwa hiyo wanaowafukuza watakwenda kasi!

1730:17 Kum 28:25; 2Fal 7:7; Law 26:8; Yos 23:10Watu 1,000 watakimbia

kwa ajili ya kitisho cha mtu mmoja,

kwa vitishio vya watu watano

wote mtakimbia,

hadi mtakapoachwa kama mlingoti wa bendera

juu ya kilele cha mlima,

kama bendera juu ya kilima.”

1830:18 Mwa 43:31; 2Pet 3:9, 15; Za 27:14; Mao 3:25; Isa 5:16; 42:14; 48:9; Yon 3:10Hata hivyo Bwana anatamani kutupatia neema,

anainuka ili kuwaonyesha huruma.

Kwa kuwa Bwana ni Mungu wa haki.

Wamebarikiwa wote wanaomngojea yeye!

1930:19 Isa 61:3; Ay 22:27; Mt 7:7-11; Isa 25:8; Ay 24:12; Zek 13:9; Za 86:7; Isa 41:17Enyi watu wa Sayuni, mnaoishi Yerusalemu, hamtalia tena. Tazameni jinsi atakavyokuwa na huruma mtakapolia kwa kumwomba msaada! Mara asikiapo, atawajibu. 2030:20 1Fal 22:27; Za 74:9; Isa 28:9; Amo 8:11Ingawa Bwana huwapa chakula cha shida na maji ya taabu, walimu wenu hawatafichwa tena, kwa macho yenu wenyewe mtawaona. 2130:21 Kum 5:32; Mit 4:27; Isa 29:24; Ay 33:11Mkigeuka kuume au kushoto, masikio yenu yatasikia sauti nyuma yenu ikisema, “Hii ndiyo njia, ifuateni.” 2230:22 Kut 32:4; Isa 2:20; Law 15:19-23; Eze 7:19-20Kisha mtanajisi sanamu zenu zilizofunikwa kwa fedha, na vinyago vyenu vilivyofunikwa kwa dhahabu. Mtazitupilia mbali kama vitambaa vya wakati wa hedhi na kuziambia, “Haya, tokeni hapa!”

2330:23 1Tim 4:8; Za 65:13; Kum 28:12; Isa 65:21-22; Yer 31:14; Ay 36:31Pia atawapa mvua kwa ajili ya mbegu mnazootesha ardhini, chakula kinachotoka ardhini kitakuwa kizuri sana, tena tele. Katika siku ile, ngʼombe wenu watalisha katika shamba pana la majani. 2430:24 Mt 3:12; Lk 3:17; Isa 32:14; Ay 6:5Maksai na punda walimao watakula majani makavu na vyakula vilivyotengenezwa, vinavyotandazwa kwa uma na sepeto. 2530:25 Isa 13:5; Kut 17:6; Isa 32:2; Yoe 3:18Katika siku ile ya mauaji makuu, wakati minara itakapoanguka, vijito vya maji vitatiririka juu ya kila mlima mrefu na kila kilima kilichoinuka sana. 2630:26 Zek 14:7-8; Ufu 21:23; 2Nya 7:14; Hos 14:4; Isa 60:19-20; Yer 3:22; 17:14Mwezi utaangaza kama jua, nao mwanga wa jua utangʼaa mara saba zaidi, kama nuru ya siku saba, wakati Bwana atakapoyafunga majeraha ya watu wake na kuwaponya vidonda alivyowatia.

2730:27 1Fal 18:24; Isa 26:20; 60:14; Eze 22:31; Ay 41:21Tazama, Jina la Bwana linakuja kutoka mbali,

likiwa na hasira kali inayowaka

pamoja na wingu zito la moshi,

midomo yake imejaa ghadhabu

na ulimi wake ni moto ulao.

2830:28 2The 2:8; Amo 9:9; 2Fal 19:28; Isa 37:29; 11:4; 28:15; Za 50:3Pumzi yake ni kama mkondo wa maji yaendayo kasi,

yakipanda hadi shingoni.

Hutikisa mataifa katika chekecheke ya uharibifu,

huweka lijamu katika mataya ya mataifa

ambayo huwaongoza upotevuni.

2930:29 Mt 26:30; Za 42:4; Isa 25:9; 1Sam 10:5; Mwa 49:24Nanyi mtaimba kama usiku ule mnaadhimisha

sikukuu takatifu.

Mioyo yenu itashangilia

kama vile watu wanapokwea na filimbi

kwenye mlima wa Bwana,

kwa Mwamba wa Israeli.

3030:30 Kut 19:18; Za 29:3; Kut 20:18; Isa 47:14; 9:12Bwana atawasababisha watu waisikie sauti yake ya utukufu,

naye atawafanya wauone mkono wake ukishuka

pamoja na hasira yake kali na moto ulao,

kukiwa na tufani ya mvua,

ngurumo za radi na mvua ya mawe.

3130:31 Isa 10:5, 12; 11:4Sauti ya Bwana itaivunjavunja Ashuru,

kwa fimbo yake ya utawala atawapiga.

3230:32 Isa 11:15; 10:26; Eze 32:10; Kut 15:20Kila pigo Bwana atakaloliweka juu yao

kwa fimbo yake ya kuadhibu,

litakuwa kwa wimbo wa matari na vinubi,

anapopigana nao katika vita

kwa mapigo ya mkono wake.

3330:33 2Fal 23:10; Yer 7:31; Mwa 19:24; Ufu 9:17; 2Sam 22:16Tofethi imeandaliwa toka zamani,

imewekwa tayari kwa ajili ya mfalme.

Shimo lake la moto limetengenezwa kwa kina kirefu

na kwa upana mkubwa,

likiwa na moto na kuni tele;

pumzi ya Bwana,

kama kijito cha kiberiti,

huuwasha moto.

New International Version

Isaiah 30:1-33

Woe to the Obstinate Nation

1“Woe to the obstinate children,”

declares the Lord,

“to those who carry out plans that are not mine,

forming an alliance, but not by my Spirit,

heaping sin upon sin;

2who go down to Egypt

without consulting me;

who look for help to Pharaoh’s protection,

to Egypt’s shade for refuge.

3But Pharaoh’s protection will be to your shame,

Egypt’s shade will bring you disgrace.

4Though they have officials in Zoan

and their envoys have arrived in Hanes,

5everyone will be put to shame

because of a people useless to them,

who bring neither help nor advantage,

but only shame and disgrace.”

6A prophecy concerning the animals of the Negev:

Through a land of hardship and distress,

of lions and lionesses,

of adders and darting snakes,

the envoys carry their riches on donkeys’ backs,

their treasures on the humps of camels,

to that unprofitable nation,

7to Egypt, whose help is utterly useless.

Therefore I call her

Rahab the Do-Nothing.

8Go now, write it on a tablet for them,

inscribe it on a scroll,

that for the days to come

it may be an everlasting witness.

9For these are rebellious people, deceitful children,

children unwilling to listen to the Lord’s instruction.

10They say to the seers,

“See no more visions!”

and to the prophets,

“Give us no more visions of what is right!

Tell us pleasant things,

prophesy illusions.

11Leave this way,

get off this path,

and stop confronting us

with the Holy One of Israel!”

12Therefore this is what the Holy One of Israel says:

“Because you have rejected this message,

relied on oppression

and depended on deceit,

13this sin will become for you

like a high wall, cracked and bulging,

that collapses suddenly, in an instant.

14It will break in pieces like pottery,

shattered so mercilessly

that among its pieces not a fragment will be found

for taking coals from a hearth

or scooping water out of a cistern.”

15This is what the Sovereign Lord, the Holy One of Israel, says:

“In repentance and rest is your salvation,

in quietness and trust is your strength,

but you would have none of it.

16You said, ‘No, we will flee on horses.’

Therefore you will flee!

You said, ‘We will ride off on swift horses.’

Therefore your pursuers will be swift!

17A thousand will flee

at the threat of one;

at the threat of five

you will all flee away,

till you are left

like a flagstaff on a mountaintop,

like a banner on a hill.”

18Yet the Lord longs to be gracious to you;

therefore he will rise up to show you compassion.

For the Lord is a God of justice.

Blessed are all who wait for him!

19People of Zion, who live in Jerusalem, you will weep no more. How gracious he will be when you cry for help! As soon as he hears, he will answer you. 20Although the Lord gives you the bread of adversity and the water of affliction, your teachers will be hidden no more; with your own eyes you will see them. 21Whether you turn to the right or to the left, your ears will hear a voice behind you, saying, “This is the way; walk in it.” 22Then you will desecrate your idols overlaid with silver and your images covered with gold; you will throw them away like a menstrual cloth and say to them, “Away with you!”

23He will also send you rain for the seed you sow in the ground, and the food that comes from the land will be rich and plentiful. In that day your cattle will graze in broad meadows. 24The oxen and donkeys that work the soil will eat fodder and mash, spread out with fork and shovel. 25In the day of great slaughter, when the towers fall, streams of water will flow on every high mountain and every lofty hill. 26The moon will shine like the sun, and the sunlight will be seven times brighter, like the light of seven full days, when the Lord binds up the bruises of his people and heals the wounds he inflicted.

27See, the Name of the Lord comes from afar,

with burning anger and dense clouds of smoke;

his lips are full of wrath,

and his tongue is a consuming fire.

28His breath is like a rushing torrent,

rising up to the neck.

He shakes the nations in the sieve of destruction;

he places in the jaws of the peoples

a bit that leads them astray.

29And you will sing

as on the night you celebrate a holy festival;

your hearts will rejoice

as when people playing pipes go up

to the mountain of the Lord,

to the Rock of Israel.

30The Lord will cause people to hear his majestic voice

and will make them see his arm coming down

with raging anger and consuming fire,

with cloudburst, thunderstorm and hail.

31The voice of the Lord will shatter Assyria;

with his rod he will strike them down.

32Every stroke the Lord lays on them

with his punishing club

will be to the music of timbrels and harps,

as he fights them in battle with the blows of his arm.

33Topheth has long been prepared;

it has been made ready for the king.

Its fire pit has been made deep and wide,

with an abundance of fire and wood;

the breath of the Lord,

like a stream of burning sulfur,

sets it ablaze.