Isaya 29 – NEN & NUB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Isaya 29:1-24

Ole Wa Mji Wa Daudi

129:1 Isa 22:12-13; 1:14; 2Sam 5:7; Isa 28:1Ole wako, wewe Arieli, Arieli,

mji alimokaa Daudi!

Ongezeni mwaka kwa mwaka,

na mzunguko wa sikukuu zenu uendelee.

229:2 Mao 2:5; Isa 3:26; Eze 43:15Hata hivyo nitauzunguka Arieli kwa jeshi,

utalia na kuomboleza,

utakuwa kwangu kama mahali

pa kuwashia moto madhabahuni.

329:3 Lk 19:43-44; 2Fal 25:1Nitapiga kambi pande zote dhidi yako,

nitakuzunguka kwa minara

na kupanga mazingirwa yangu dhidi yako.

429:4 Isa 8:19; 47:1; 52:2; 26:16; Law 19:31Utakaposhushwa, utanena kutoka ardhini,

utamumunya maneno yako kutoka mavumbini.

Sauti yako itatoka katika nchi kama vile ya mzimu,

utanongʼona maneno yako toka mavumbini.

529:5 Isa 17:13; 1The 5:3; Za 55:15; Kum 9:21; Za 78:39; Isa 51:12; Za 103:15Lakini adui zako wengi watakuwa kama vumbi laini,

kundi la wakatili watakuwa

kama makapi yapeperushwayo.

Naam, ghafula, mara moja,

629:6 Mk 13:8; Ufu 6:12; Isa 26:21; Zek 14:1-5; Kut 19:16; Mt 24:7; Za 83:13-15Bwana Mwenye Nguvu Zote atakuja

na ngurumo, tetemeko la ardhi, na kwa sauti kuu,

atakuja na dhoruba, tufani na miali ya moto iteketezayo.

729:7 Mik 4:11-12; Zek 12:9; Ay 20:8Kisha makundi ya mataifa yote yale yapiganayo dhidi ya Arieli,

yale yanayomshambulia yeye na ngome zake, na kumzunguka kwa jeshi,

watakuwa kama ilivyo ndoto,

kama maono wakati wa usiku:

829:8 Za 73:20; Yer 30:16; Isa 17:12-14; Zek 12:3; Isa 54:17kama vile mtu aliye na njaa aotavyo kuwa anakula,

lakini huamka, bado njaa yake ingalipo,

kama vile mtu mwenye kiu aotavyo kuwa anakunywa maji,

lakini huamka akiwa anazimia, akiwa bado angali ana kiu.

Hivyo ndivyo itakavyokuwa kwa makundi yote ya mataifa

yanayopigana dhidi ya Mlima Sayuni.

929:9 Yer 13:13; Isa 63:9; Law 10:9; Yer 4:9; Isa 6:10; 63:6; Za 60:3; Yer 13:13; Isa 51:22Duwaeni na kushangaa,

jifanyeni vipofu wenyewe na msione,

leweni, lakini si kwa mvinyo,

pepesukeni lakini si kwa kileo.

1029:10 2The 2:9-11; Za 69:23; Mik 3:6; Amu 4:21; Isa 44:18; 6:9-10; Rum 11:8Bwana amewaleteeni usingizi mzito:

Ameziba macho yenu (ninyi manabii);

amefunika vichwa vyenu (ninyi waonaji).

1129:11 Dan 8:26; Mt 13:11; Isa 28:7; Ufu 5:1-2; Isa 8:16; Dan 12:9Kwa maana kwenu ninyi, maono haya yote si kitu ila maneno yaliyotiwa lakiri katika kitabu. Kama mkimpa mtu yeyote awezaye kusoma kitabu hiki, nanyi mkamwambia, “Tafadhali kisome,” yeye atajibu, “Mimi siwezi, kwa kuwa kimetiwa lakiri.” 12Au kama mkimpa mtu yeyote kitabu hiki asiyeweza kusoma na kumwambia, “Tafadhali kisome,” atajibu, “Mimi sijui kusoma.”

1329:13 Yer 12:2; Kol 2:22; Eze 33:31; Mt 15:8-9; Mk 7:6-7; Isa 58:2; Za 119:70; Yer 14:11Bwana anasema:

“Watu hawa hunikaribia kwa vinywa vyao

na kuniheshimu kwa midomo yao,

lakini mioyo yao iko mbali nami.

Ibada yao kwangu inatokana na maagizo

waliyofundishwa na wanadamu.

1429:14 Yer 49:7; Ay 10:16; 5:13; Isa 6:9-10; 1Kor 1:19; Yer 8:9; Isa 6:9-10Kwa hiyo mara nyingine tena nitawashangaza watu hawa,

kwa ajabu juu ya ajabu.

Hekima ya wenye hekima itapotea,

nayo akili ya wenye akili itatoweka.”

1529:15 Ay 22:13-14; Eze 8:12; 2Fal 21:16; Ay 22:13; Isa 28:15; Ay 8:3; Za 10:11-13Ole kwa wale wanaokwenda kwenye vilindi virefu

kumficha Bwana mipango yao,

wafanyao kazi zao gizani na kufikiri,

“Ni nani anayetuona? Ni nani atakayejua?”

1629:16 Yer 18:6; Rum 9:20-21; Za 94:9; Ay 10:9; Isa 10:15; 45:9; Ay 9:12; Yer 18:6; Mwa 2:7Mnapindua mambo juu chini,

kana kwamba mfinyanzi aweza kufikiriwa kuwa kama udongo wa mfinyanzi!

Je, kile kilichofinyangwa chaweza kumwambia yule aliyekifinyanga,

“Wewe hukunifinyanga mimi?”

Je, chungu kinaweza kumwambia mfinyanzi,

“Wewe hujui chochote?”

1729:17 Za 84:6; Isa 32:15; 10:25; 2:13; Za 107:33Kwa muda mfupi sana, je, Lebanoni haitageuzwa kuwa shamba lenye rutuba,

na shamba lenye rutuba liwe kama msitu?

1829:18 Mk 7:37; Za 146:8; Mt 11:5; Lk 7:22; Isa 32:3; Za 107:14Katika siku ile viziwi watasikia maneno ya kitabu,

na katika utusitusi na giza

macho ya kipofu yataona.

1929:19 Za 72:4; 25:9; Isa 5:19; 12:6; 3:15; Yak 2:5; Mt 5:5; 11:29; Mwa 42:26Mara nyingine tena wanyenyekevu watafurahi katika Bwana,

wahitaji watafurahi katika yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli.

2029:20 2Nya 36:16; Isa 28:22; Eze 11:2; Isa 13:11; 59:4; Ay 15:35; Za 7:14Wakatili watatoweka na wenye kudhihaki watatokomea,

nao wote wenye jicho la uovu watakatiliwa mbali,

2129:21 Amo 5:10-15; Isa 5:23; Hab 1:4; Mit 21:28wale ambao kwa neno humfanya mtu kuwa mwenye hatia,

wamtegeao mtego mtetezi katika mahakama,

na kwa ushuhuda wa uongo humnyima haki

yeye asiye na hatia.

2229:22 Mwa 11:16; Yoe 2:26; Yos 24:3; Sef 3:11; Kut 6:6; Mwa 17:16; Isa 41:8; 51:2Kwa hiyo hili ndilo Bwana, aliyemkomboa Abrahamu, analosema kwa nyumba ya Yakobo:

“Yakobo hataaibishwa tena,

wala nyuso zao hazitabadilika sura tena.

2329:23 Isa 53:10; 54:1-4; 19:25; 49:20-26; 5:19; Mt 6:9Wakati watakapoona watoto wao miongoni mwao,

kazi ya mikono yangu,

watalitakasa Jina langu takatifu;

wataukubali utakatifu wa yeye Aliye Mtakatifu wa Yakobo,

nao watamcha Mungu wa Israeli.

2429:24 Mit 12:8; Ebr 5:2; Isa 60:16; 42:16; Za 95:10; Isa 28:7; 32:4Wale wanaopotoka rohoni watapata ufahamu,

nao wale wanaolalamika watayakubali mafundisho.”

Swedish Contemporary Bible

Jesaja 29:1-24

Profetia över Ariel (Jerusalem)

1Ve över Ariel, Ariel,

staden där David slog sig ner.

Lägg år till år,

låt högtidscykeln fullbordas.

2Jag ska anfalla Ariel,

och då blir det sorg och klagan.

Ariel blir då min altarhärd29:2 På hebreiska Ariel. Ariel kan också översättas Guds lejon, eller: altarhärd; se Hes 43:15..

3Jag ska slå läger

och omringa dig med belägringstorn

och bygga upp vallar mot dig.

4Du ska förnedras

och få tala krälande i gruset,

mumlande ur stoftet.

Som en spöklik röst från jorden

ska du stöna fram dina ord.

5Men dina många fiender ska då bli som damm,

de våldsammas hop som agnar för vinden.

Oväntat och plötsligt ska det ske.

6Härskarornas Herre ska själv gripa in,

med åska och dån och larm,

med storm och jordbävning

och flammor av förtärande eld.

7Som en dröm, som en nattlig syn,

blir då hopen av alla folk

som stred mot Ariel,

anföll det, dess befästning

och belägrade det.

8Som när en hungrig drömmer om att han äter

men fortfarande är hungrig när han vaknar,

och som när en törstig drömmer om att han dricker

men ändå försmäktar av törst när han slår upp ögonen,

så blir det med hela den hop av folk och länder

som dragit ut i strid mot berget Sion.

9Häpna och förundras!

Stirra er blinda, så att ni inget ser!

Var berusade, men inte av vin,

ragla, fast inte av öl!

10Herren har låtit en sömnens ande drabba er.

Han har tillslutit era ögon

– profeternas –

och han har täckt över era huvuden

– siarnas.

11För hela denna syn har för er blivit som en förseglad bokrulle. När man räcker den till någon läskunnig och ber honom läsa, svarar han: ”Jag kan inte. Den är förseglad.” 12Om man räcker den till någon som inte kan läsa och ber honom läsa, så svarar denne: ”Jag kan inte läsa.”

13Herren säger:

”Det här folket nalkas mig med sina ord

och ärar mig med sin mun,

men deras hjärtan är långt ifrån mig,

och deras gudsfruktan är bara inlärda människobud.

14Därför ska jag än en gång

göra stora under bland detta folk,

förunderliga ting.

De visas vishet ska förgå

och de förståndigas förstånd komma bort.”

15Ve dem som i djupen

försöker dölja sina planer för Herren

och utför sina gärningar i mörkret

och säger:

”Vem skulle kunna se oss

eller veta något om oss?”

16Ni vänder ju allting upp och ner!29:16 Grundtextens innebörd är osäker.

Kan leran likställas med krukmakaren?

Kan det som är gjort säga till den som gjorde det:

”Han har inte gjort mig?”

Kan det som är format säga till den som formade det:

”Han kan ingenting!”

17Snart, efter en liten tid,

ska Libanon förvandlas till bördig åkermark

och åkermark räknas som skog.

18På den dagen ska de döva kunna höra

orden ur en bok,

och ur dunkel och mörker

ska de blinda kunna se.

19De ödmjuka ska än en gång glädjas i Herren,

och de fattiga ska fröjdas i Israels Helige.

20De grymma ska försvinna,

bespottarna förgås,

alla ontsinta utplånas,

21de som anklagade den oskyldige i rätten,

låg på lur för domare i porten

och med falskt vittnesbörd

berövade den rättfärdige sin rätt.

22Därför säger Herren till Jakobs släkt, han som befriade Abraham:

”Jakob ska inte längre behöva blygas

och inte mer blekna.

23För när han ser sina barn,

mina händers verk i sin mitt,

ska de hålla mitt namn heligt.

Jakobs Helige ska de hålla helig,

bäva för Israels Gud.

24De som i sin ande farit vilse ska få insikt,

och de missnöjda ska låta sig undervisas.”