Isaya 29 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Isaya 29:1-24

Ole Wa Mji Wa Daudi

129:1 Isa 22:12-13; 1:14; 2Sam 5:7; Isa 28:1Ole wako, wewe Arieli, Arieli,

mji alimokaa Daudi!

Ongezeni mwaka kwa mwaka,

na mzunguko wa sikukuu zenu uendelee.

229:2 Mao 2:5; Isa 3:26; Eze 43:15Hata hivyo nitauzunguka Arieli kwa jeshi,

utalia na kuomboleza,

utakuwa kwangu kama mahali

pa kuwashia moto madhabahuni.

329:3 Lk 19:43-44; 2Fal 25:1Nitapiga kambi pande zote dhidi yako,

nitakuzunguka kwa minara

na kupanga mazingirwa yangu dhidi yako.

429:4 Isa 8:19; 47:1; 52:2; 26:16; Law 19:31Utakaposhushwa, utanena kutoka ardhini,

utamumunya maneno yako kutoka mavumbini.

Sauti yako itatoka katika nchi kama vile ya mzimu,

utanongʼona maneno yako toka mavumbini.

529:5 Isa 17:13; 1The 5:3; Za 55:15; Kum 9:21; Za 78:39; Isa 51:12; Za 103:15Lakini adui zako wengi watakuwa kama vumbi laini,

kundi la wakatili watakuwa

kama makapi yapeperushwayo.

Naam, ghafula, mara moja,

629:6 Mk 13:8; Ufu 6:12; Isa 26:21; Zek 14:1-5; Kut 19:16; Mt 24:7; Za 83:13-15Bwana Mwenye Nguvu Zote atakuja

na ngurumo, tetemeko la ardhi, na kwa sauti kuu,

atakuja na dhoruba, tufani na miali ya moto iteketezayo.

729:7 Mik 4:11-12; Zek 12:9; Ay 20:8Kisha makundi ya mataifa yote yale yapiganayo dhidi ya Arieli,

yale yanayomshambulia yeye na ngome zake, na kumzunguka kwa jeshi,

watakuwa kama ilivyo ndoto,

kama maono wakati wa usiku:

829:8 Za 73:20; Yer 30:16; Isa 17:12-14; Zek 12:3; Isa 54:17kama vile mtu aliye na njaa aotavyo kuwa anakula,

lakini huamka, bado njaa yake ingalipo,

kama vile mtu mwenye kiu aotavyo kuwa anakunywa maji,

lakini huamka akiwa anazimia, akiwa bado angali ana kiu.

Hivyo ndivyo itakavyokuwa kwa makundi yote ya mataifa

yanayopigana dhidi ya Mlima Sayuni.

929:9 Yer 13:13; Isa 63:9; Law 10:9; Yer 4:9; Isa 6:10; 63:6; Za 60:3; Yer 13:13; Isa 51:22Duwaeni na kushangaa,

jifanyeni vipofu wenyewe na msione,

leweni, lakini si kwa mvinyo,

pepesukeni lakini si kwa kileo.

1029:10 2The 2:9-11; Za 69:23; Mik 3:6; Amu 4:21; Isa 44:18; 6:9-10; Rum 11:8Bwana amewaleteeni usingizi mzito:

Ameziba macho yenu (ninyi manabii);

amefunika vichwa vyenu (ninyi waonaji).

1129:11 Dan 8:26; Mt 13:11; Isa 28:7; Ufu 5:1-2; Isa 8:16; Dan 12:9Kwa maana kwenu ninyi, maono haya yote si kitu ila maneno yaliyotiwa lakiri katika kitabu. Kama mkimpa mtu yeyote awezaye kusoma kitabu hiki, nanyi mkamwambia, “Tafadhali kisome,” yeye atajibu, “Mimi siwezi, kwa kuwa kimetiwa lakiri.” 12Au kama mkimpa mtu yeyote kitabu hiki asiyeweza kusoma na kumwambia, “Tafadhali kisome,” atajibu, “Mimi sijui kusoma.”

1329:13 Yer 12:2; Kol 2:22; Eze 33:31; Mt 15:8-9; Mk 7:6-7; Isa 58:2; Za 119:70; Yer 14:11Bwana anasema:

“Watu hawa hunikaribia kwa vinywa vyao

na kuniheshimu kwa midomo yao,

lakini mioyo yao iko mbali nami.

Ibada yao kwangu inatokana na maagizo

waliyofundishwa na wanadamu.

1429:14 Yer 49:7; Ay 10:16; 5:13; Isa 6:9-10; 1Kor 1:19; Yer 8:9; Isa 6:9-10Kwa hiyo mara nyingine tena nitawashangaza watu hawa,

kwa ajabu juu ya ajabu.

Hekima ya wenye hekima itapotea,

nayo akili ya wenye akili itatoweka.”

1529:15 Ay 22:13-14; Eze 8:12; 2Fal 21:16; Ay 22:13; Isa 28:15; Ay 8:3; Za 10:11-13Ole kwa wale wanaokwenda kwenye vilindi virefu

kumficha Bwana mipango yao,

wafanyao kazi zao gizani na kufikiri,

“Ni nani anayetuona? Ni nani atakayejua?”

1629:16 Yer 18:6; Rum 9:20-21; Za 94:9; Ay 10:9; Isa 10:15; 45:9; Ay 9:12; Yer 18:6; Mwa 2:7Mnapindua mambo juu chini,

kana kwamba mfinyanzi aweza kufikiriwa kuwa kama udongo wa mfinyanzi!

Je, kile kilichofinyangwa chaweza kumwambia yule aliyekifinyanga,

“Wewe hukunifinyanga mimi?”

Je, chungu kinaweza kumwambia mfinyanzi,

“Wewe hujui chochote?”

1729:17 Za 84:6; Isa 32:15; 10:25; 2:13; Za 107:33Kwa muda mfupi sana, je, Lebanoni haitageuzwa kuwa shamba lenye rutuba,

na shamba lenye rutuba liwe kama msitu?

1829:18 Mk 7:37; Za 146:8; Mt 11:5; Lk 7:22; Isa 32:3; Za 107:14Katika siku ile viziwi watasikia maneno ya kitabu,

na katika utusitusi na giza

macho ya kipofu yataona.

1929:19 Za 72:4; 25:9; Isa 5:19; 12:6; 3:15; Yak 2:5; Mt 5:5; 11:29; Mwa 42:26Mara nyingine tena wanyenyekevu watafurahi katika Bwana,

wahitaji watafurahi katika yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli.

2029:20 2Nya 36:16; Isa 28:22; Eze 11:2; Isa 13:11; 59:4; Ay 15:35; Za 7:14Wakatili watatoweka na wenye kudhihaki watatokomea,

nao wote wenye jicho la uovu watakatiliwa mbali,

2129:21 Amo 5:10-15; Isa 5:23; Hab 1:4; Mit 21:28wale ambao kwa neno humfanya mtu kuwa mwenye hatia,

wamtegeao mtego mtetezi katika mahakama,

na kwa ushuhuda wa uongo humnyima haki

yeye asiye na hatia.

2229:22 Mwa 11:16; Yoe 2:26; Yos 24:3; Sef 3:11; Kut 6:6; Mwa 17:16; Isa 41:8; 51:2Kwa hiyo hili ndilo Bwana, aliyemkomboa Abrahamu, analosema kwa nyumba ya Yakobo:

“Yakobo hataaibishwa tena,

wala nyuso zao hazitabadilika sura tena.

2329:23 Isa 53:10; 54:1-4; 19:25; 49:20-26; 5:19; Mt 6:9Wakati watakapoona watoto wao miongoni mwao,

kazi ya mikono yangu,

watalitakasa Jina langu takatifu;

wataukubali utakatifu wa yeye Aliye Mtakatifu wa Yakobo,

nao watamcha Mungu wa Israeli.

2429:24 Mit 12:8; Ebr 5:2; Isa 60:16; 42:16; Za 95:10; Isa 28:7; 32:4Wale wanaopotoka rohoni watapata ufahamu,

nao wale wanaolalamika watayakubali mafundisho.”

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

以賽亞書 29:1-24

耶路撒冷被圍

1耶和華說:「亞利伊勒29·1 亞利伊勒」在此處用來指錫安/耶路撒冷,2節、7節同。亞利伊勒

大衛安營的城啊!

你有禍了!

儘管你年復一年地守節期,

2我還是要叫你受苦。

你必悲傷哀號,

在我面前成為一座祭壇。

3我必把你團團圍住,

屯兵圍困你,

修築高臺攻打你。

4你必一敗塗地,

躺在塵土中說話,

你細微的聲音從土中傳來,

好像地下幽靈的聲音。

你耳語般的低聲從土中傳來。

5但你的眾仇敵必像纖細的塵埃一樣消散,

眾多的殘暴之徒必如被風颳去的糠秕。

突然,刹那之間,

6萬軍之耶和華必帶著雷轟、地震、巨響、旋風、暴風和烈火來臨。

7攻打、圍困耶路撒冷及其堡壘的各國軍隊必如夢幻,

如夜間的異象一樣消失。

8他們好像饑餓的人夢中吃飯,

醒來仍然饑餓;

像口渴的人夢中喝水,

醒來仍然渴得發昏。

攻打錫安山的各國軍隊結局都必如此。」

9你們駐足驚奇吧!

你們自我蒙蔽,繼續瞎眼吧!

你們醉了,但不是因為酒;

你們東倒西歪,但不是因為烈酒。

10因為耶和華把沉睡的靈傾倒在你們身上,

祂封住你們的眼睛,

蓋住你們的頭。

你們的眼睛就是先知,

你們的頭就是先見。

11對你們而言,所有的啟示都好像封了印的書卷。你們把書卷交給識字的人讀,他會說:「我不能讀,這書卷是封著的。」 12你們把書卷交給不識字的人讀,他會說:「我不識字。」

13主說:「這些人嘴上親近我,

尊崇我,心卻遠離我。

他們敬拜我不過是遵行人定的規條。

14所以,我要再次行奇妙無比的事,使他們震驚。

他們智者的智慧必泯滅,

明哲的聰明必消失。」

15那些向耶和華深藏計謀的人有禍了!

他們暗中行事,

自以為無人看見也無人知道。

16他們太愚蠢了!

窯匠怎能跟泥土相提並論?

被造的怎能對造它的說:

「你沒有造我」?

陶器怎能對陶匠說:

「你什麼也不懂」?

17再過不久,黎巴嫩將變成沃野,

沃野上莊稼茂密如林。

18那時,聾子必聽見那書卷上的話,

黑暗中的瞎子必能看見。

19卑微的人必因耶和華而歡喜,

貧窮的人必因以色列的聖者而快樂。

20殘暴之徒必消失,

嘲諷者必絕跡,

所有心懷不軌者必被剷除。

21他們誣陷人,

暗算審判官,

冤枉無辜。

22因此,關於雅各家,

救贖亞伯拉罕的耶和華說:

雅各的子孫必不再羞愧,

臉上再無懼色。

23因為他們看見我賜給他們的子孫時,

必尊我的名為聖,

必尊雅各的聖者為聖,

必敬畏以色列的上帝。

24心裡迷惘的必明白真理,

發怨言的必欣然受教。」