Isaya 23 – NEN & NVI

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Isaya 23:1-18

Unabii Kuhusu Tiro

123:1 Zek 9:2-4; Amo 1:9-10; Eze 26:1-21; Mwa 10:4; 1Fal 10:22; Yos 19:29; Yer 47:4Neno kuhusu Tiro:

Ombolezeni, enyi meli za Tarshishi!

Kwa kuwa Tiro imeangamizwa,

imeachwa bila nyumba wala bandari.

Kuanzia nchi ya Kitimu23:1 Kitimu hapa ni Kipro, kisiwa katika Bahari ya Mediterania.

neno limewajia.

223:2 Ay 2:13; Eze 27:1-24; Amu 1:31Nyamazeni kimya, enyi watu wa kisiwani,

pia ninyi wafanyabiashara wa Sidoni,

ambao mabaharia wamewatajirisha.

323:3 Isa 19:7; Za 83:7; Eze 27:3; Mwa 41:5Kwenye maji makuu

nafaka za Shihori zilikuja;

mavuno ya Naili yalikuwa mapato ya Tiro,

naye akawa soko la mataifa.

423:4 Mwa 10:15, 19Uaibishwe ee Sidoni, nawe ee ngome la bahari,

kwa kuwa bahari imesema:

“Sijapata kuwa na uchungu wa kuzaa wala sijapata kuzaa,

wala sijapata kulea wana wala kutunza mabinti.”

523:5 Eze 30:9; 26:17-18Habari ifikapo Misri,

watakuwa katika maumivu makuu kwa ajili ya taarifa kutoka Tiro.

623:6 Mwa 10:4Vukeni mpaka Tarshishi,

ombolezeni, enyi watu wa kisiwani.

723:7 Isa 5:14; 32:13; 22:2; Eze 26:13; Isa 23:12Je, huu ndio mji wenu uliojaa sherehe,

mji wa zamani, zamani kabisa

ambao miguu yake imeuchukua

kufanya makao nchi za mbali sana?

823:8 Isa 2:12; Eze 28:2; 1Tim 3:4; Nah 3:16; Eze 28:5; Ufu 18:23Ni nani amepanga hili dhidi ya Tiro,

mji utoao mataji,

ambao wafanyabiashara wake ni wana wa mfalme

na wachuuzi wake ni watu mashuhuri wa dunia?

923:9 Ay 40:11; Isa 13:11; 5:13; Eze 27:3; Isa 14:24; 9:15Bwana Mwenye Nguvu Zote ndiye alipanga jambo hili,

ili kukishusha kiburi cha utukufu wote

na kuwanyenyekesha wale wote

ambao ni mashuhuri duniani.

10Ee Binti Tarshishi,

pita katika nchi yako kama vile Mto Naili

kwa kuwa huna tena bandari.

1123:11 Kut 14:21; Eze 26:4; Zek 9:3-4; Za 46:6Bwana amenyoosha mkono wake juu ya bahari

na kuzifanya falme zake zitetemeke.

Ametoa amri kuhusu Kanaani

kwamba ngome zake ziangamizwe.

1223:12 Ufu 18:22; Sef 3:14; Zek 2:10; Isa 37:22; Yer 14:17; Mao 2:13; Mwa 10:4Alisema, “Usizidi kufurahi,

ee Bikira Binti Sidoni, sasa umepondwa!

“Simama, vuka uende Kitimu;

hata huko hutapata pumziko.”

1323:13 Isa 43:14; Yer 51:12; Za 74:14; Isa 18:6Tazama katika nchi ya Wakaldayo,

watu hawa ambao sasa hawaonekani kama wapo!

Waashuru wameifanya nchi hiyo

kuwa mahali pa viumbe wa jangwani.

Wamesimamisha minara yao ya vita kuuzunguka,

wameziteka ngome zake na kuziacha tupu

na kuufanya kuwa magofu.

1423:14 Mwa 10:4; Isa 2:16; Eze 27:25; 1Fal 10:22Ombolezeni, enyi meli za Tarshishi;

ngome yenu imeangamizwa!

1523:15 Yer 25:22; Za 90:10Wakati huo Tiro utasahauliwa kwa miaka sabini, muda wa maisha ya mfalme. Lakini mwisho wa miaka hiyo sabini, itakuwa kwa Tiro kama ilivyo katika wimbo wa kahaba:

1623:16 Mit 7:10“Twaa kinubi, tembea mjini kote,

ewe kahaba uliyesahauliwa;

piga kinubi vizuri, imba nyimbo nyingi,

ili upate kukumbukwa.”

1723:17 Kum 23:17-18; Mwa 10:15-19; Ufu 17:1; 18:3-9; Eze 16:26; Yer 25:26; Nah 3:4Mwishoni mwa miaka sabini, Bwana atashughulika na Tiro. Naye atarudia ajira yake ya ukahaba, na atafanya biashara yake na falme zote juu ya uso wa dunia. 1823:18 Yos 6:17-19; Za 72:10; Zek 14:20-21; Isa 61:6; Mik 4:13; Kut 28:36; Isa 18:7; 60:5-9; Amo 1:9-10Lakini faida na mapato yake yatawekwa wakfu kwa Bwana; hayatahifadhiwa wala kufichwa. Faida zake zitakwenda kwa wale wakaao mbele za Bwana kwa ajili ya chakula tele na mavazi mazuri.

Nueva Versión Internacional

Isaías 23:1-18

Profecía contra Tiro

1Profecía contra Tiro:

¡Giman, barcos de Tarsis!,

porque fueron destruidas su casa y su puerto.

Desde la tierra de Chipre

les ha llegado la noticia.

2¡Callen, habitantes de la costa,

comerciantes de Sidón,

ciudad que han enriquecido los marinos!

3Sobre las grandes aguas

llegó el grano de Sijor;

Tiro se volvió el centro comercial de las naciones;

la cosecha del Nilo le aportaba ganancias.

4Avergüénzate, Sidón, fortaleza del mar,

porque el mar ha dicho:

«No he estado con dolores de parto ni he dado a luz;

no he criado hijos ni educado hijas».

5Cuando la noticia llegue a Egipto,

lo que se diga de Tiro los angustiará.

6Pasen a Tarsis;

giman, habitantes de la costa.

7¿Es esta su ciudad alegre,

la ciudad tan antigua,

cuyos pies la han llevado

a establecerse en tierras lejanas?

8¿Quién planeó esto contra Tiro,

la ciudad que confiere coronas,

cuyos comerciantes son príncipes,

y sus negociantes reconocidos en la tierra?

9Lo planeó el Señor de los Ejércitos

para abatir la altivez de toda gloria

y humillar a toda la gente importante de la tierra.

10Hija de Tarsis,

cultiva23:10 cultiva (Qumrán y LXX); atraviesa (TM). tu tierra como en el Nilo,

porque tu puerto ya no existe.

11El Señor ha extendido su mano sobre el mar

y ha puesto a temblar a los reinos;

ha ordenado destruir las fortalezas de Canaán.

12Él dijo:

«¡Virgen oprimida, hija de Sidón:

no volverás a alegrarte!

»Levántate y cruza hasta Chipre;

¡ni siquiera allí encontrarás descanso!».

13¡Mira la tierra de los babilonios!23:13 Lit. caldeos.

¡Ese pueblo ya no existe!

Asiria la ha convertido

en refugio de las fieras del desierto;

levantaron torres de asedio,

demolieron sus fortalezas

y las convirtieron en ruinas.

14¡Giman, barcos de Tarsis,

porque destruida está su fortaleza!

15En aquel tiempo Tiro será olvidada durante setenta años, que es lo que vive un rey. Pero al cabo de esos setenta años sucederá a Tiro lo que dice la canción de la prostituta:

16«Tú, prostituta olvidada,

toma un arpa y recorre la ciudad;

toca lo mejor que puedas y canta muchas canciones,

para que te recuerden».

17Al cabo de setenta años, el Señor se ocupará de Tiro, la cual volverá a venderse y prostituirse con todos los reinos de la tierra. 18Pero sus ingresos y ganancias se consagrarán al Señor; no serán almacenados ni atesorados. Sus ganancias serán para los que habitan en presencia del Señor, para que se alimenten en abundancia y se vistan con ropas finas.