Isaya 23 – NEN & JCB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Isaya 23:1-18

Unabii Kuhusu Tiro

123:1 Zek 9:2-4; Amo 1:9-10; Eze 26:1-21; Mwa 10:4; 1Fal 10:22; Yos 19:29; Yer 47:4Neno kuhusu Tiro:

Ombolezeni, enyi meli za Tarshishi!

Kwa kuwa Tiro imeangamizwa,

imeachwa bila nyumba wala bandari.

Kuanzia nchi ya Kitimu23:1 Kitimu hapa ni Kipro, kisiwa katika Bahari ya Mediterania.

neno limewajia.

223:2 Ay 2:13; Eze 27:1-24; Amu 1:31Nyamazeni kimya, enyi watu wa kisiwani,

pia ninyi wafanyabiashara wa Sidoni,

ambao mabaharia wamewatajirisha.

323:3 Isa 19:7; Za 83:7; Eze 27:3; Mwa 41:5Kwenye maji makuu

nafaka za Shihori zilikuja;

mavuno ya Naili yalikuwa mapato ya Tiro,

naye akawa soko la mataifa.

423:4 Mwa 10:15, 19Uaibishwe ee Sidoni, nawe ee ngome la bahari,

kwa kuwa bahari imesema:

“Sijapata kuwa na uchungu wa kuzaa wala sijapata kuzaa,

wala sijapata kulea wana wala kutunza mabinti.”

523:5 Eze 30:9; 26:17-18Habari ifikapo Misri,

watakuwa katika maumivu makuu kwa ajili ya taarifa kutoka Tiro.

623:6 Mwa 10:4Vukeni mpaka Tarshishi,

ombolezeni, enyi watu wa kisiwani.

723:7 Isa 5:14; 32:13; 22:2; Eze 26:13; Isa 23:12Je, huu ndio mji wenu uliojaa sherehe,

mji wa zamani, zamani kabisa

ambao miguu yake imeuchukua

kufanya makao nchi za mbali sana?

823:8 Isa 2:12; Eze 28:2; 1Tim 3:4; Nah 3:16; Eze 28:5; Ufu 18:23Ni nani amepanga hili dhidi ya Tiro,

mji utoao mataji,

ambao wafanyabiashara wake ni wana wa mfalme

na wachuuzi wake ni watu mashuhuri wa dunia?

923:9 Ay 40:11; Isa 13:11; 5:13; Eze 27:3; Isa 14:24; 9:15Bwana Mwenye Nguvu Zote ndiye alipanga jambo hili,

ili kukishusha kiburi cha utukufu wote

na kuwanyenyekesha wale wote

ambao ni mashuhuri duniani.

10Ee Binti Tarshishi,

pita katika nchi yako kama vile Mto Naili

kwa kuwa huna tena bandari.

1123:11 Kut 14:21; Eze 26:4; Zek 9:3-4; Za 46:6Bwana amenyoosha mkono wake juu ya bahari

na kuzifanya falme zake zitetemeke.

Ametoa amri kuhusu Kanaani

kwamba ngome zake ziangamizwe.

1223:12 Ufu 18:22; Sef 3:14; Zek 2:10; Isa 37:22; Yer 14:17; Mao 2:13; Mwa 10:4Alisema, “Usizidi kufurahi,

ee Bikira Binti Sidoni, sasa umepondwa!

“Simama, vuka uende Kitimu;

hata huko hutapata pumziko.”

1323:13 Isa 43:14; Yer 51:12; Za 74:14; Isa 18:6Tazama katika nchi ya Wakaldayo,

watu hawa ambao sasa hawaonekani kama wapo!

Waashuru wameifanya nchi hiyo

kuwa mahali pa viumbe wa jangwani.

Wamesimamisha minara yao ya vita kuuzunguka,

wameziteka ngome zake na kuziacha tupu

na kuufanya kuwa magofu.

1423:14 Mwa 10:4; Isa 2:16; Eze 27:25; 1Fal 10:22Ombolezeni, enyi meli za Tarshishi;

ngome yenu imeangamizwa!

1523:15 Yer 25:22; Za 90:10Wakati huo Tiro utasahauliwa kwa miaka sabini, muda wa maisha ya mfalme. Lakini mwisho wa miaka hiyo sabini, itakuwa kwa Tiro kama ilivyo katika wimbo wa kahaba:

1623:16 Mit 7:10“Twaa kinubi, tembea mjini kote,

ewe kahaba uliyesahauliwa;

piga kinubi vizuri, imba nyimbo nyingi,

ili upate kukumbukwa.”

1723:17 Kum 23:17-18; Mwa 10:15-19; Ufu 17:1; 18:3-9; Eze 16:26; Yer 25:26; Nah 3:4Mwishoni mwa miaka sabini, Bwana atashughulika na Tiro. Naye atarudia ajira yake ya ukahaba, na atafanya biashara yake na falme zote juu ya uso wa dunia. 1823:18 Yos 6:17-19; Za 72:10; Zek 14:20-21; Isa 61:6; Mik 4:13; Kut 28:36; Isa 18:7; 60:5-9; Amo 1:9-10Lakini faida na mapato yake yatawekwa wakfu kwa Bwana; hayatahifadhiwa wala kufichwa. Faida zake zitakwenda kwa wale wakaao mbele za Bwana kwa ajili ya chakula tele na mavazi mazuri.

Japanese Contemporary Bible

イザヤ書 23:1-18

23

ツロについての預言

1これは、ツロへの神のことばです。

「遠い国から来るタルシシュの船よ、

なくなった母港のために泣きなさい。

キプロスで聞いたうわさは全部ほんとうだったのです。

2-3どこも死の静寂が覆っています。

海の向こうから、

また、エジプトとナイル川沿いの地から

品々を運んで来たシドンの船でいっぱいになり、

にぎわっていたかつての貿易中心地は、

今ではひっそり静まり返っています。

4海の要塞であるシドンよ、

今はもう子(ツロ。シドンの植民地)がいないのだから

恥じなさい。

5エジプトがこのことを聞いたら、

悲しみにくれるでしょう。

6ツロの人たちよ、泣きながらタルシシュへ逃げなさい。

7もの言わぬ廃墟が、

かつては喜びにあふれていた地の、

ただ一つの名残りです。

輝かしい歴史を振り返り、

遠くにあった植民地の一つ一つを思い出しなさい。

8だれが、大帝国を築き上げて

世界貿易の王者にのし上がったツロを、

こんな悲惨な目に会わせたのでしょう。

9天の軍勢に命令を下す主が、

その思い上がりをたたきのめし、

人間の偉大さなど取るに足りないことを示そうと、

このようにしたのです。

10タルシシュの船よ、

母港がなくなってしまったのだから、

あてもなく航海を続けなさい。

11-12主は海の上に御手を伸ばし、

地上の国々を縮み上がらせます。

この偉大な商都を滅ぼせと命じた神は、

こう語りします。

『ああ、名誉を傷つけられたシドンの娘よ、

二度と小躍りして喜ぶな。

おまえはたといキプロスに逃げ伸びても、

休むことはできない。』

13見なさい。

バビロンもアッシリヤ人に滅ぼされ、

野獣の住みかになっています。

彼らはしつこく攻撃して宮殿を壊し、

瓦礫の山にしました。

14大洋をわがもの顔で走る船よ、

母港は無残に壊されたのだから泣き叫びなさい。

15-16ツロは七十年の間忘れられます。そのあと別の王が治めるようになって、町は息を吹き返し、娼婦が久しく会わない恋人を捜して、甘い歌を歌いながら通りを歩くように恋の歌を歌います。

17七十年たって、主がツロを生き返らせても、ツロは昔のままです。世界中で同じ悪事を重ねるのです。 18ところが、ずっとのちになって、その利益は主のために使われるようになり、祭司の食卓を潤し、上等の服で着飾らせるようになります。