Isaya 23 – NEN & HTB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Isaya 23:1-18

Unabii Kuhusu Tiro

123:1 Zek 9:2-4; Amo 1:9-10; Eze 26:1-21; Mwa 10:4; 1Fal 10:22; Yos 19:29; Yer 47:4Neno kuhusu Tiro:

Ombolezeni, enyi meli za Tarshishi!

Kwa kuwa Tiro imeangamizwa,

imeachwa bila nyumba wala bandari.

Kuanzia nchi ya Kitimu23:1 Kitimu hapa ni Kipro, kisiwa katika Bahari ya Mediterania.

neno limewajia.

223:2 Ay 2:13; Eze 27:1-24; Amu 1:31Nyamazeni kimya, enyi watu wa kisiwani,

pia ninyi wafanyabiashara wa Sidoni,

ambao mabaharia wamewatajirisha.

323:3 Isa 19:7; Za 83:7; Eze 27:3; Mwa 41:5Kwenye maji makuu

nafaka za Shihori zilikuja;

mavuno ya Naili yalikuwa mapato ya Tiro,

naye akawa soko la mataifa.

423:4 Mwa 10:15, 19Uaibishwe ee Sidoni, nawe ee ngome la bahari,

kwa kuwa bahari imesema:

“Sijapata kuwa na uchungu wa kuzaa wala sijapata kuzaa,

wala sijapata kulea wana wala kutunza mabinti.”

523:5 Eze 30:9; 26:17-18Habari ifikapo Misri,

watakuwa katika maumivu makuu kwa ajili ya taarifa kutoka Tiro.

623:6 Mwa 10:4Vukeni mpaka Tarshishi,

ombolezeni, enyi watu wa kisiwani.

723:7 Isa 5:14; 32:13; 22:2; Eze 26:13; Isa 23:12Je, huu ndio mji wenu uliojaa sherehe,

mji wa zamani, zamani kabisa

ambao miguu yake imeuchukua

kufanya makao nchi za mbali sana?

823:8 Isa 2:12; Eze 28:2; 1Tim 3:4; Nah 3:16; Eze 28:5; Ufu 18:23Ni nani amepanga hili dhidi ya Tiro,

mji utoao mataji,

ambao wafanyabiashara wake ni wana wa mfalme

na wachuuzi wake ni watu mashuhuri wa dunia?

923:9 Ay 40:11; Isa 13:11; 5:13; Eze 27:3; Isa 14:24; 9:15Bwana Mwenye Nguvu Zote ndiye alipanga jambo hili,

ili kukishusha kiburi cha utukufu wote

na kuwanyenyekesha wale wote

ambao ni mashuhuri duniani.

10Ee Binti Tarshishi,

pita katika nchi yako kama vile Mto Naili

kwa kuwa huna tena bandari.

1123:11 Kut 14:21; Eze 26:4; Zek 9:3-4; Za 46:6Bwana amenyoosha mkono wake juu ya bahari

na kuzifanya falme zake zitetemeke.

Ametoa amri kuhusu Kanaani

kwamba ngome zake ziangamizwe.

1223:12 Ufu 18:22; Sef 3:14; Zek 2:10; Isa 37:22; Yer 14:17; Mao 2:13; Mwa 10:4Alisema, “Usizidi kufurahi,

ee Bikira Binti Sidoni, sasa umepondwa!

“Simama, vuka uende Kitimu;

hata huko hutapata pumziko.”

1323:13 Isa 43:14; Yer 51:12; Za 74:14; Isa 18:6Tazama katika nchi ya Wakaldayo,

watu hawa ambao sasa hawaonekani kama wapo!

Waashuru wameifanya nchi hiyo

kuwa mahali pa viumbe wa jangwani.

Wamesimamisha minara yao ya vita kuuzunguka,

wameziteka ngome zake na kuziacha tupu

na kuufanya kuwa magofu.

1423:14 Mwa 10:4; Isa 2:16; Eze 27:25; 1Fal 10:22Ombolezeni, enyi meli za Tarshishi;

ngome yenu imeangamizwa!

1523:15 Yer 25:22; Za 90:10Wakati huo Tiro utasahauliwa kwa miaka sabini, muda wa maisha ya mfalme. Lakini mwisho wa miaka hiyo sabini, itakuwa kwa Tiro kama ilivyo katika wimbo wa kahaba:

1623:16 Mit 7:10“Twaa kinubi, tembea mjini kote,

ewe kahaba uliyesahauliwa;

piga kinubi vizuri, imba nyimbo nyingi,

ili upate kukumbukwa.”

1723:17 Kum 23:17-18; Mwa 10:15-19; Ufu 17:1; 18:3-9; Eze 16:26; Yer 25:26; Nah 3:4Mwishoni mwa miaka sabini, Bwana atashughulika na Tiro. Naye atarudia ajira yake ya ukahaba, na atafanya biashara yake na falme zote juu ya uso wa dunia. 1823:18 Yos 6:17-19; Za 72:10; Zek 14:20-21; Isa 61:6; Mik 4:13; Kut 28:36; Isa 18:7; 60:5-9; Amo 1:9-10Lakini faida na mapato yake yatawekwa wakfu kwa Bwana; hayatahifadhiwa wala kufichwa. Faida zake zitakwenda kwa wale wakaao mbele za Bwana kwa ajili ya chakula tele na mavazi mazuri.

Het Boek

Jesaja 23:1-18

Gods profetie over Tyrus

1Dit is Gods profetie over Tyrus.

Huil, schepen van Tyrus, die vanuit verre landen op de thuisreis zijn! Huil om uw haven, want hij is verdwenen! De geruchten die u op Cyprus hoorde, zijn waar. 2-3 Overal heerst een doodse stilte. De geluiden van de rumoerige haven, vol schepen uit Sidon die koopwaar van over de zee uit Egypte en het gebied langs de Nijl aanvoeren, zijn verstomd. U was de grootste handelsmarkt ter wereld.

4Schaam u, Sidon, bolwerk van de zee. Want nu bent u kinderloos! 5Als dit nieuws Egypte bereikt, zal het veel angst veroorzaken. 6Vlucht naar Tarsis, mannen van Tyrus, en huil onderweg. 7Deze verlaten ruïne is alles wat overbleef van uw eens zo luisterrijke stad. Het einde van een roemruchte geschiedenis. Denk eens aan alle kolonisten die u naar verre landen stuurde!

8Wie heeft deze ramp over Tyrus gebracht? Over dit land dat koninkrijken schiep en wiens inwoners de belangrijkste kooplieden ter wereld waren? 9De Here van de hemelse legers heeft dit gedaan, om uw trots te vernietigen en zijn verachting te tonen over de hooggeplaatsten onder de mensen. 10Zeil maar verder, schepen van Tarsis, want uw haven is er niet meer. 11De Here strekt zijn hand uit over de zee, Hij doet de koninkrijken van deze aarde beven, Hij geeft bevel de vestingen in Kanaän te verwoesten. 12Hij zegt: ‘U, onteerde maagd, dochter van Sidon, zult nooit meer blij of sterk zijn. Zelfs als u naar Cyprus vlucht, zult u geen rust vinden.’ 13Want het zullen de Babyloniërs en niet de Assyriërs zijn die Tyrus aanvallen. Zij zullen het belegeren, de paleizen met de grond gelijk maken en het herscheppen in een ruïne. 14Huil maar, schepen van Tarsis, want uw thuishaven is verdwenen!

15-16 Zeventig jaar lang zal Tyrus worden vergeten. Dan, onder een andere koning, zal de stad weer tot leven komen, zij zal mooie liederen spelen als een prostituee die lange tijd vergeten was. Nu loopt zij weer door de straten op zoek naar minnaars en wordt weer herkend. 17Ja, na zeventig jaar zal de Here Tyrus weer laten opleven, maar zij zal niet anders zijn dan vroeger, zij zal weer terugkeren op haar slechte wegen en hoererij bedrijven met de koninkrijken van de wereld. 18Maar de winst van haar handelstransacties zal aan de Here gewijd worden. Zij zal geen voorraad kunnen opslaan, maar het zal tot voedsel en kleding dienen voor hen die bij de Here wonen.