Isaya 22 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Isaya 22:1-25

Unabii Kuhusu Yerusalemu

122:1 Za 125:2; Yoe 3:2-14; Yos 2:8; Isa 13:1; Yer 48:38; 21:13Neno kuhusu Bonde la Maono:

Nini kinachokutaabisha sasa,

kwamba ninyi nyote mmepanda juu ya mapaa?

222:2 Isa 5:14; 32:13; Eze 22:5; Isa 21:5; 10:4; 2Fal 25:3Ewe mji uliojaa ghasia,

ewe mji wa makelele na sherehe!

Watu wenu waliokufa hawakuuawa kwa upanga,

wala hawakufa vitani.

322:3 Isa 13:14; 2Fal 25:6Viongozi wako wote wamekimbia pamoja,

wamekamatwa bila kutumia upinde.

Ninyi nyote mliokamatwa mlichukuliwa wafungwa pamoja,

mlikimbia wakati adui alipokuwa bado mbali.

422:4 Mao 1:16; Lk 19:41; Yer 9:1; Eze 21:6; Isa 15:3; Lk 19:41Kwa hiyo nilisema, “Geukia mbali nami,

niache nilie kwa uchungu.

Usijaribu kunifariji

juu ya maangamizi ya watu wangu.”

522:5 Amo 5:18-20; Es 3:15; Sef 1:15; Isa 2:12; Ay 40:12; 2Sam 22:43; Eze 8:17-18; 13:14; Mao 1:5Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, anayo siku

ya ghasia, ya kukanyaga, na ya kuogofya

katika Bonde la Maono,

siku ya kuangusha kuta

na ya kupiga kelele mpaka milimani.

622:6 Isa 21:2; 2Fal 16:9; Yer 51:56; 49:35; Za 46:9Elamu analichukua podo,

pamoja na waendesha magari ya vita na farasi.

Kiri anaifungua ngao.

722:7 Yos 15:18; 2Nya 32:1-2Mabonde yako yaliyo mazuri sana yamejaa magari ya vita,

nao wapanda farasi wamewekwa kwenye malango ya mji;

822:8 2Nya 32:5; 1Fal 7:2; Isa 2:12ulinzi wa Yuda umeondolewa.

Nawe ulitazama siku ile

silaha katika Jumba la Kifalme la Mwituni,

922:9 2Fal 18:17; 2Nya 32:4-5; Wim 4:4; 2Fal 20:20mkaona kuwa Mji wa Daudi

una matundu mengi katika ulinzi wake,

mkaweka akiba ya maji

kwenye Bwawa la Chini.

1022:10 Yer 33:4; 2Nya 32:15; 32:5; Yer 33:4Mlihesabu majengo katika Yerusalemu

nanyi mkabomoa nyumba ili kuimarisha ukuta.

1122:11 Yer 39:4; Neh 3:16; 2Fal 25:4; 19:25; 1Sam 12:24Mlijenga bwawa la maji katikati ya kuta mbili

kwa ajili ya maji ya Bwawa la Zamani,

lakini hamkumtazama Yule aliyelitengeneza,

au kuwa na heshima kwa Yule aliyeubuni tangu zamani za kale.

1222:12 Yoe 2:17; Law 13:40; Mik 1:16; Isa 3:24; Yoe 1:9-13Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote,

aliwaita siku ile

ili kulia na kuomboleza,

kungʼoa nywele zenu na kuvaa nguo ya gunia.

1322:13 Mhu 8:15; Isa 5:12; 21:5; Lk 17:26-29; 1Kor 15:32; 1Sam 25:36; Isa 28:7-8Lakini tazama, kuna furaha na sherehe,

kuchinja ngʼombe na kuchinja kondoo,

kula nyama na kunywa mvinyo!

Mnasema, “Tuleni na kunywa,

kwa kuwa kesho tutakufa!”

1422:14 Eze 24:13; Isa 5:9; 1Sam 2:25; Isa 13:11; 30:13-14; 1Sam 3:14Bwana Mwenye Nguvu Zote amelifunua hili nikiwa ninasikia: Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, asema: “Mpaka siku ya kufa kwenu, dhambi hii haitafanyiwa upatanisho.”

1522:15 2Fal 6:30; 18:18; Mwa 41:40; Isa 36:3; 1Fal 4:6Hili ndilo Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, asemalo:

“Nenda ukamwambie huyu wakili Shebna,

ambaye ni msimamizi wa jumba la kifalme:

1622:16 Mt 27:60; Hes 32:42Unafanya nini hapa, na ni nani aliyekupa ruhusa

kujikatia kaburi lako mwenyewe,

ukichonga kaburi lako mahali palipo juu,

na kutoboa kwa patasi mahali pako pa kupumzikia katika mwamba?

1722:17 Yer 10:18; 13:18; 22:26“Jihadhari, Bwana yu karibu kukukamata thabiti,

na kukutupa mbali, ewe mtu mwenye nguvu.

1822:18 Ay 18:11; Isa 14:19; Mwa 41:43Atakuvingirisha uwe kama mpira

na kukutupa katika nchi kubwa.

Huko ndiko utakakofia,

na huko ndiko magari yako ya vita ya fahari yatabakia,

wewe unayeifedhehesha nyumba ya bwana wako!

1922:19 Za 52:5; Lk 16:3Nitakuondoa kutoka kazi yako,

nawe utaondoshwa kutoka nafasi yako.

2022:20 2Fal 18:18“Katika siku ile, nitamwita mtumishi wangu, Eliakimu mwana wa Hilkia. 2122:21 Ay 29:16Nitamvika joho lako, nami nitamfunga mshipi wako kiunoni mwake, na kumkabidhi mamlaka yako. Yeye atakuwa baba kwa wale wanaoishi Yerusalemu na kwa nyumba ya Yuda. 2222:22 1Nya 9:27; Mt 16:19; Ay 12:14; Ufu 3:7; Isa 7:2Nitaweka mabegani mwake ufunguo wa nyumba ya Daudi. Kile afunguacho hakuna awezaye kufunga, na kile afungacho hakuna awezaye kufungua. 2322:23 Eze 15:3; Zek 10:4; Ezr 9:8; Ay 6:25; 1Sam 2:7-8; Ay 36:7Nitamgongomea kama kigingi kilicho mahali palipo imara, naye atakuwa kiti cha enzi cha heshima kwa ajili ya nyumba ya baba yake. 24Utukufu wote wa jamaa yake utakuwa juu yake: Watoto wa jamaa hiyo na machipukizi yake, vyombo vyake vyote vidogo, tangu bakuli hadi magudulia yote.”

2522:25 Isa 46:11; Mik 4:4Bwana Mwenye Nguvu Zote asema, “Katika siku ile, kigingi kilichogongomewa mahali imara kitaachia njia. Kitakatwa, nacho kitaanguka na mzigo ulioningʼinia juu yake utaanguka chini.” Bwana amesema.

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

以賽亞書 22:1-25

關於耶路撒冷的預言

1以下是關於異象谷22·1 異象谷」指耶路撒冷。的預言。

為什麼你們全城的人都上到房頂呢?

2你們這座充滿喧鬧、騷動和歡樂的城啊,

你們中間被殺的人既非喪身刀下,

也非死於戰場。

3你們的官長一起逃跑,

一箭未發便束手就縛,

逃到遠方的也一同被擒。

4所以,我說:「你們不要管我,

讓我痛哭一場吧!

不要安慰我,

我的同胞都被毀滅了。」

5主——萬軍之耶和華已經定了日子,

要使耶路撒冷飽受恐慌、

失敗和混亂,

城牆被攻破,

哭喊聲響徹山間。

6以攔人帶著箭袋,

率領戰車和騎兵前來,

吉珥人也亮出盾牌。

7你們佳美的山谷中佈滿戰車,

騎兵在你們的城門前列陣。

8猶大毫無防衛之力。

那時,你們依靠藏在林宮裡的兵器。 9你們看見大衛城破口纍纍,你們儲存下池的水, 10數點耶路撒冷城的房屋,把房屋拆掉修補城牆。 11又在兩道城牆之間建造新的蓄水池,用來盛舊池的水。耶和華從古時已定了這一切,要使這一切發生,但你們既不仰望祂,也不理會祂。

12那日,萬軍之耶和華呼召你們哭泣哀號,

剃光頭髮,身披麻衣。

13但你們還是歡喜作樂,

宰牛殺羊,喝酒吃肉,說:

「讓我們吃喝吧!

因為明天我們就死了。」

14萬軍之耶和華啟示我說:

「你們這罪到死也得不到赦免。

這是主——萬軍之耶和華說的。」

15主——萬軍之耶和華吩咐我去見宮廷總管舍伯那,對他說: 16「你在這裡做什麼?你憑什麼在這裡為自己挖墳墓,在高處為自己挖墳墓,在磐石上為自己鑿安息之所? 17看啊,你這有權有勢的人,耶和華必緊緊抓住你,把你猛力拋開。 18祂必把你揉作一團,像球一樣扔到寬闊之地。在那裡,你必死亡,你華美的戰車也必遭毀滅,你是你主人家的羞辱。」 19耶和華對舍伯那說:「我必解除你的官職,把你從高位上拉下來。

20「到那日,我必召來我的僕人——希勒迦的兒子以利亞敬21給他穿上你的朝服,繫上你的腰帶,把你的權柄交給他。他必像父親一樣保護耶路撒冷猶大的人民。 22我必把大衛家的鑰匙交給他。他開啟的,沒有人能關;他關閉的,沒有人能開。 23我要使他像深嵌在堅固之處的橛子一樣穩固,他必給他的家族帶來尊榮。 24他所有的親屬都靠他得榮耀,如同杯子和酒瓶等小器皿掛在一個橛子上。」

25萬軍之耶和華說:「到那日,牢牢釘在堅固之處的釘子必鬆動,被砍落在地上,掛在上面的東西必被除掉。這是耶和華說的。」