Isaya 2 – NEN & KJV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Isaya 2:1-22

Mlima Wa Bwana

(Mika 4:1-3)

12:1 Isa 1:1Hili ndilo aliloliona Isaya mwana wa Amozi kuhusu Yuda na Yerusalemu:

22:2 Dan 2:35; 11:45; Yoe 3:17; Mdo 2:17; Isa 11:9; 65:9; Zek 14:10; Yer 16:19Katika siku za mwisho

mlima wa Hekalu la Bwana utaimarishwa

kama mlima mkuu miongoni mwa milima yote,

utainuliwa juu ya vilima,

na mataifa yote yatamiminika huko.

32:3 Zek 8:21; Lk 24:47; Yn 4:22; Isa 33:22; 45:23; Yer 3:17; Kum 33:19Mataifa mengi yatakuja na kusema,

“Njooni, twendeni mlimani mwa Bwana,

kwenye nyumba ya Mungu wa Yakobo.

Atatufundisha njia zake,

ili tuweze kuenenda katika mapito yake.”

Sheria itatoka Sayuni,

neno la Bwana litatoka Yerusalemu.

42:4 Hos 2:18; Yer 30:11; Za 96:13; 51:4; 46:9; Yoe 3:10; Mwa 49:10; Zek 9:10Atahukumu kati ya mataifa

na ataamua migogoro ya mataifa mengi.

Watafua panga zao ziwe majembe,

na mikuki yao kuwa miundu ya kukata matawi.

Taifa halitainua upanga dhidi ya taifa jingine,

wala hawatajifunza vita tena.

52:5 Isa 60:19-20; 1Yn 1:5-7; Isa 58:1; 60:1Njooni, enyi nyumba ya Yakobo,

tutembeeni katika nuru ya Bwana.

Siku Ya Bwana

62:6 Kum 18:10, 14; 31:17; Yer 12:7; 2Nya 16:7; Isa 44:25; 2Fal 16:7; Kum 31:17Umewatelekeza watu wako,

nyumba ya Yakobo.

Wamejaa ushirikina utokao Mashariki,

wanapiga ramli kama Wafilisti

na wanashikana mikono na wapagani.

72:7 Mwa 41:43; Kum 17:16; Mik 5:10; Za 17:14; Isa 31:1; Kum 17:17Nchi yao imejaa fedha na dhahabu,

hakuna mwisho wa hazina zao.

Nchi yao imejaa farasi,

hakuna mwisho wa magari yao.

82:8 Isa 10:9-11; 17:8; 44:17; Ufu 9:20; 2Nya 32:19; Mik 5:13; Isa 44:17; Za 135:15Nchi yao imejaa sanamu,

wanasujudia kazi za mikono yao,

vitu vile vidole vyao vimevitengeneza.

92:9 Za 62:9; Isa 13:11; 5:15; 2:11, 17; Hes 4:5; Neh 4:5Kwa hiyo mwanadamu atashushwa

na binadamu atanyenyekezwa:

usiwasamehe.

102:10 Ufu 6:15-16; Nah 3:11; Za 145:12; Isa 2:19; 2The 1:9Ingieni kwenye miamba,

jificheni ardhini

kutokana na utisho wa Bwana

na utukufu wa enzi yake!

112:11 Isa 24:21-23; 37:23; 10:12; 5:15; Eze 31:10; Oba 1:8; Neh 9:29; Ay 40:11; Za 46:10; Hab 2:5Macho ya mtu mwenye majivuno yatanyenyekezwa

na kiburi cha wanadamu kitashushwa,

Bwana peke yake ndiye atakayetukuzwa siku hiyo.

122:12 Za 76:12; 59:12; Eze 7:7; Ay 40:11; Isa 13:6-9; 34:8; Yer 30:7; Mao 1:12; 2Sam 22:28; Yoe 1:15; Amo 5:18Bwana Mwenye Nguvu Zote anayo siku aliyoiweka akiba

kwa wote wenye kujivuna na wenye kiburi,

kwa wote wanaojikweza

(nao watanyenyekezwa),

132:13 Amu 9:15; Isa 10:33, 34; 29:17; Eze 27:5; Za 22:12; Zek 11:2kwa mierezi yote ya Lebanoni iliyo mirefu sana,

na mialoni yote ya Bashani,

142:14 Isa 30:25; 40:4kwa milima yote mirefu

na vilima vyote vilivyoinuka,

152:15 Isa 25:2, 12; 30:25; 32:14; 33:18; Sef 1:16kwa kila mnara ulio mrefu sana

na kila ukuta wenye ngome,

162:16 Mwa 10:4; 1Fal 10:22; 9:26kwa kila meli ya biashara,2:16 Au: ya Tarshishi (ona pia 1Fal 10:22; 22:48; 2Nya 9:21; 20:36; Isa 60:9.)

na kila chombo cha baharini cha fahari.

172:17 2Sam 22:28; Ay 40:112:17 Nah 3:13; Ebr 10:31; Kum 2:25; Isa 11:10, 15Majivuno ya mwanadamu yatashushwa,

na kiburi cha wanadamu kitanyenyekezwa,

Bwana peke yake ndiye atatukuzwa siku hiyo,

182:18 Kum 9:21; Mik 5:13; Eze 36:25; Isa 21:9; Yer 10:11; 1Sam 5:2nazo sanamu zitatoweka kabisa.

192:19 Hos 10:8; Nah 1:3-6; Ay 9:6; 30:9; Ebr 12:26; Hab 3:6; Amu 6:2; Isa 7:19; 14:16; Ay 30:6; Lk 23:30; Ufu 6:15Watu watakimbilia kwenye mapango ndani ya miamba,

na kwenye mahandaki ardhini

kutokana na utisho wa Bwana

na utukufu wa enzi yake,

ainukapo kuitikisa dunia.

202:20 Law 11:19; Eze 36:25; 7:19-20; 14:6; Ufu 9:20; Isa 2:11; Ay 22:24Siku ile, watu watawatupia

panya na popo

sanamu zao za fedha na za dhahabu,

walizozitengeneza ili waziabudu.

212:21 Kut 33:22; Za 145:12; Isa 33:10; 2:19Watakimbilia kwenye mapango miambani

na kwenye nyufa za miamba

kutokana na utisho wa Bwana

na utukufu wa enzi yake,

ainukapo kuitikisa dunia.

222:22 Mit 23:4; Yer 17:5; Yak 4:14; Ay 12:19; Za 119:8-9; Isa 51:12; 40:15; Za 18:42; 118:6, 8; 146:3Acheni kumtumainia mwanadamu,

ambaye hana kitu ila pumzi katika pua zake.

Yeye ana thamani gani?

King James Version

Isaiah 2:1-22

1The word that Isaiah the son of Amoz saw concerning Judah and Jerusalem. 2And it shall come to pass in the last days, that the mountain of the LORD’s house shall be established in the top of the mountains, and shall be exalted above the hills; and all nations shall flow unto it.2.2 established: or, prepared 3And many people shall go and say, Come ye, and let us go up to the mountain of the LORD, to the house of the God of Jacob; and he will teach us of his ways, and we will walk in his paths: for out of Zion shall go forth the law, and the word of the LORD from Jerusalem. 4And he shall judge among the nations, and shall rebuke many people: and they shall beat their swords into plowshares, and their spears into pruninghooks: nation shall not lift up sword against nation, neither shall they learn war any more.2.4 pruninghooks: or, scythes 5O house of Jacob, come ye, and let us walk in the light of the LORD.

6¶ Therefore thou hast forsaken thy people the house of Jacob, because they be replenished from the east, and are soothsayers like the Philistines, and they please themselves in the children of strangers.2.6 from…: or, more than the2.6 please…: or, abound with the 7Their land also is full of silver and gold, neither is there any end of their treasures; their land is also full of horses, neither is there any end of their chariots: 8Their land also is full of idols; they worship the work of their own hands, that which their own fingers have made: 9And the mean man boweth down, and the great man humbleth himself: therefore forgive them not.

10¶ Enter into the rock, and hide thee in the dust, for fear of the LORD, and for the glory of his majesty. 11The lofty looks of man shall be humbled, and the haughtiness of men shall be bowed down, and the LORD alone shall be exalted in that day. 12For the day of the LORD of hosts shall be upon every one that is proud and lofty, and upon every one that is lifted up; and he shall be brought low: 13And upon all the cedars of Lebanon, that are high and lifted up, and upon all the oaks of Bashan, 14And upon all the high mountains, and upon all the hills that are lifted up, 15And upon every high tower, and upon every fenced wall, 16And upon all the ships of Tarshish, and upon all pleasant pictures.2.16 pleasant…: Heb. pictures of desire 17And the loftiness of man shall be bowed down, and the haughtiness of men shall be made low: and the LORD alone shall be exalted in that day. 18And the idols he shall utterly abolish.2.18 he…: or, shall utterly pass away 19And they shall go into the holes of the rocks, and into the caves of the earth, for fear of the LORD, and for the glory of his majesty, when he ariseth to shake terribly the earth.2.19 of the earth: Heb. of the dust 20In that day a man shall cast his idols of silver, and his idols of gold, which they made each one for himself to worship, to the moles and to the bats;2.20 his idols of silver…: Heb. the idols of his silver, etc2.20 each…: or, for him 21To go into the clefts of the rocks, and into the tops of the ragged rocks, for fear of the LORD, and for the glory of his majesty, when he ariseth to shake terribly the earth. 22Cease ye from man, whose breath is in his nostrils: for wherein is he to be accounted of?