Isaya 18 – NEN & KJV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Isaya 18:1-7

Unabii Dhidi Ya Kushi

118:1 Mwa 10:6; Sef 2:12; Isa 5:8; Za 68:31; Eze 29:10; Oba 1:1Ole kwa nchi ya mvumo wa mabawa,18:1 Au: wa nzige.

kando ya mito ya Kushi,

218:2 Mwa 10:8-9; 2Nya 12:3; Kut 2:3; Ay 9:26; Mwa 41:14iwapelekayo wajumbe wake kwa njia ya bahari

kwa mashua za mafunjo juu ya maji.

Nendeni, wajumbe wepesi,

kwa taifa la watu warefu wenye ngozi nyororo,

kwa taifa linaloogopwa mbali na karibu,

taifa gomvi lenye lugha ngeni,

ambalo nchi yao imegawanywa kwa mito.

318:3 Za 60:4; Yer 4:21; Za 33:8; Isa 5:26; 5:26; 31:9; Yos 6:21; Amu 3:27Enyi mataifa yote ya ulimwengu,

ninyi mnaoishi duniani

wakati bendera itakapoinuliwa milimani,

mtaiona,

nayo tarumbeta itakapolia,

mtaisikia.

418:4 Hos 5:15; 2Sam 1:21; Za 133:3; Isa 64:12; 26:21; Amu 5:31; Za 18:12; Isa 26:19Hili ndilo Bwana aliloniambia:

“Nitatulia kimya na kutazama

kutoka maskani yangu,

kama joto linalometameta katika mwanga wa jua,

kama wingu la umande

katika joto la wakati wa mavuno.”

518:5 Isa 17:10-11; Eze 17:6; Isa 10:33Kwa maana, kabla ya mavuno,

wakati wa kuchanua ukishapita

na maua yakawa zabibu zinazoiva,

atayakata machipukizi kwa mundu wa kupogolea matawi,

naye atakata na kuyaondoa matawi yaliyopanuka.

618:6 Yer 7:33; Eze 32:4; 39:17; Isa 37:36; 8:8; 56:9Yote yataachwa kwa ajili ya ndege wawindao wa mlimani

na wanyama pori,

ndege watajilisha juu yake wakati wote wa kiangazi,

nao wanyama pori wakati wote wa masika.

718:7 Sef 3:10; Za 68:31; 2Nya 9:24; Isa 60:7; Mwa 41:4; 41:14Wakati huo matoleo yataletwa kwa Bwana Mwenye Nguvu Zote

kutoka kwa taifa la watu warefu wenye ngozi nyororo,

kutoka kwa taifa linaloogopwa mbali na karibu,

kutoka taifa gomvi lenye lugha ngeni,

ambalo nchi yao imegawanywa kwa mito,

matoleo yataletwa katika Mlima Sayuni, mahali pa Jina la Bwana Mwenye Nguvu Zote.

King James Version

Isaiah 18:1-7

1Woe to the land shadowing with wings, which is beyond the rivers of Ethiopia: 2That sendeth ambassadors by the sea, even in vessels of bulrushes upon the waters, saying, Go, ye swift messengers, to a nation scattered and peeled, to a people terrible from their beginning hitherto; a nation meted out and trodden down, whose land the rivers have spoiled!18.2 scattered…: or, outspread and polished18.2 meted…: or, that meteth out and treadeth down: Heb. of line, line, and treading under foot18.2 have…: or, despise 3All ye inhabitants of the world, and dwellers on the earth, see ye, when he lifteth up an ensign on the mountains; and when he bloweth a trumpet, hear ye. 4For so the LORD said unto me, I will take my rest, and I will consider in my dwelling place like a clear heat upon herbs, and like a cloud of dew in the heat of harvest.18.4 consider…: or, regard my set dwelling18.4 upon…: or, after rain 5For afore the harvest, when the bud is perfect, and the sour grape is ripening in the flower, he shall both cut off the sprigs with pruning hooks, and take away and cut down the branches. 6They shall be left together unto the fowls of the mountains, and to the beasts of the earth: and the fowls shall summer upon them, and all the beasts of the earth shall winter upon them.

7¶ In that time shall the present be brought unto the LORD of hosts of a people scattered and peeled, and from a people terrible from their beginning hitherto; a nation meted out and trodden under foot, whose land the rivers have spoiled, to the place of the name of the LORD of hosts, the mount Zion.18.7 scattered…: or, outspread and polished