Isaya 16 – NEN & CCB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Isaya 16:1-14

Hali Ya Kukata Tamaa Ya Moabu

116:1 Isa 10:32; Amu 1:36; 2Fal 14:7; 2Nya 32:23; 2Fal 3:4; Oba 1:3Pelekeni wana-kondoo kama ushuru

kwa mtawala wa nchi,

Kutoka Sela, kupitia jangwani,

hadi mlima wa Binti Sayuni.

216:2 Mit 27:8; Hes 21:13-14; Yer 48:40; Hes 21:29Kama ndege wanaopapatika

waliofukuzwa kutoka kwenye kiota,

ndivyo walivyo wanawake wa Moabu

kwenye vivuko vya Arnoni.

316:3 1Fal 18:4“Tupeni shauri,

toeni uamuzi.

Wakati wa adhuhuri,

fanyeni kivuli chenu kama usiku.

Waficheni watoro,

msisaliti wakimbizi.

416:4 Isa 55:7; 9:4; 2:2-4Waacheni watoro wa Moabu wakae pamoja nanyi;

kuweni mahali pao pa salama ili kuepuka mharabu.”

Mtesi atafikia mwisho na maangamizi yatakoma,

aletaye vita atatoweka kutoka nchi.

516:5 1Sam 13:14; Mik 4:7; Isa 7:2; Dan 7:14; Mit 20:28; Isa 9:7; Lk 1:32Kwa upendo kiti cha enzi kitaimarishwa,

kwa uaminifu mtu ataketi juu yake,

yeye atokaye nyumba ya Daudi:

yeye ambaye katika kuhukumu hutafuta haki,

na huhimiza njia ya haki.

616:6 Eze 25:8; Yer 25:21; Law 26:19; Ay 20:6; Sef 2:8; Yer 49:16; Amo 2:1Tumesikia juu ya kiburi cha Moabu:

kiburi chake cha kujivuna na udanganyifu,

kiburi chake na ufidhuli wake,

lakini majivuno yake si kitu.

716:7 1Nya 16:3; 2Fal 3:25; Yer 48:20; 49:3; Isa 13:6Kwa hiyo Wamoabu wanaomboleza,

wanaiombolezea Moabu kwa pamoja.

Wanaomboleza na kuhuzunika

kwa ajili ya watu wa Kir-Haresethi.

816:8 Ay 8:16; Hes 21:32; 21:25; Isa 15:6; 5:2; Ay 8:16; Za 80:11Mashamba ya Heshboni yananyauka,

pia na mizabibu ya Sibma.

Watawala wa mataifa

wamekanyaga mizabibu iliyo mizuri sana,

ambayo ilipata kufika Yazeri

na kuenea kuelekea jangwani.

Machipukizi yake yalienea

yakafika hadi baharini.

916:9 Isa 15:3; Eze 27:31; Yer 40:12; Ay 7:3; Hes 32:3; Ezr 3:13Hivyo ninalia kama Yazeri aliavyo,

kwa ajili ya mizabibu ya Sibma.

Ee Heshboni, ee Eleale,

ninakulowesha kwa machozi!

Kelele za furaha kwa ajili ya tunda lako lililoiva

na kwa ajili ya mavuno zimekomeshwa.

1016:10 Isa 24:7-8; Amu 9:27; Ay 24:11; Yer 25:30; Isa 5:2Furaha na shangwe zimeondolewa

kutoka mashamba ya matunda;

hakuna yeyote aimbaye wala apazaye sauti

katika mashamba ya mizabibu;

hakuna yeyote akanyagaye zabibu shinikizoni,

kwa kuwa nimekomesha makelele.

1116:11 Isa 15:5; Hos 11:8; Flp 2:1; Ay 30:31; Isa 63:15Moyo wangu unaomboleza kwa ajili ya Moabu kama kinubi,

nafsi yangu yote kwa ajili ya Kir-Haresethi.

1216:12 Za 115:4-7; 1Kor 8:4; Hes 22:4; Isa 15:2; 1Fal 11:7; 18:29Wakati Moabu anapojitokeza mahali pake pa juu,

anajichosha mwenyewe tu;

anapokwenda mahali pake pa kuabudia miungu ili kuomba,

haitamfaidi lolote.

13Hili ndilo neno ambalo Bwana ameshasema kuhusu Moabu. 1416:14 Isa 25:10; Yer 48:42; Kum 15:18; 13:16; Isa 20:3; 37:30; Law 19:13Lakini sasa Bwana anasema: “Katika miaka mitatu, kama vile mtumishi aliyefungwa na mkataba angeihesabu, fahari ya Moabu na watu wake wengi watadharauliwa, nao walionusurika watakuwa wachache sana, tena wanyonge.”

Chinese Contemporary Bible (Simplified)

以赛亚书 16:1-14

1摩押人从西拉穿过旷野,来到锡安城的山,

把羊羔献给那里的掌权者。

2亚嫩河渡口,

摩押16:2 摩押人”希伯来文是“摩押的女子”。如同被赶离巢穴的飞鸟。

3他们对犹大人说:“给我们出个主意,伸张正义吧!

请让你们的影子在正午如黑夜,

遮盖逃难的人,

不要出卖逃亡者。

4让我们这些逃难的摩押人留在你们那里,

好躲避毁灭者。”

欺压和毁灭之事终必停止,

入侵者终必从地上消失。

5那时,必有一个宝座在爱中坚立,

大卫家的人必坐在上面以信实治国,

秉公审判,速行公义。

6我们听说摩押人心骄气傲、狂妄自大,

然而他们所夸耀的都是虚假的。

7他们必为摩押哀哭,

人人都必哀哭,

为不再有吉珥·哈列设的美味葡萄饼而哀叹、悲伤。

8因为希实本的农田荒废,

西比玛的葡萄树枯萎。

各国的君王都来践踏这些上好的葡萄树。

它们的枝子曾经伸展到雅谢和旷野,

嫩枝一直蔓延到海。

9因此,我像雅谢人一样为西比玛的葡萄树哀哭。

希实本以利亚利啊,

我用眼泪来浇灌你们,

因为再无人为你们的果品和庄稼而欢呼了。

10肥美的田园里听不到快乐的声音,

葡萄园里也无人歌唱欢呼,

榨酒池里无人榨酒。

我已经使欢呼声止息。

11我的内心为摩押

吉珥·哈列设哀鸣,

好像凄凉的琴声。

12摩押人上丘坛祭拜,

却落得筋疲力尽;

在庙宇里祷告,

却毫无用处。

13以上是耶和华所说有关摩押的预言。 14现在,耶和华说:“正如一个雇工的工作年限是三年,摩押的荣耀也必在三年之内消失,那里的人民必遭藐视,残存的人必寥寥无几、软弱无力。”