Isaya 15 – NEN & OL

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Isaya 15:1-9

Unabii Dhidi Ya Moabu

115:1 Hes 21:28; 22:3-6; Kum 23:6; Hes 17:12; Yer 51:58; 48:24; 2Fal 3:25Neno kuhusu Moabu:

Ari iliyo Moabu imeangamizwa:

imeharibiwa kwa usiku mmoja!

Kiri iliyo Moabu imeangamizwa,

imeharibiwa kwa usiku mmoja!

215:2 Yer 48:35; Law 21:5; Ay 1:20; Hes 21:20; Isa 16:12; 2Sam 10:4; Law 13:40Diboni anakwea hadi kwenye hekalu lake,

mpaka mahali pake pa juu ili walie,

Moabu anaombolezea Nebo na Medeba.

Kila kichwa kimenyolewa

na kila ndevu limeondolewa.

315:3 Mao 2:11; Mik 1:8; Isa 3:24; Yos 2:8; Yer 48:38; Isa 14:31; Eze 7:18; Yer 47:2Wamevaa nguo za magunia barabarani,

juu ya mapaa na kwenye viwanja

wote wanaomboleza,

wamelala kifudifudi kwa kulia.

415:4 Hes 32:3; 21:23-25; Yos 13:26Heshboni na Eleale wanalia,

sauti zao zinasikika hadi Yahazi.

Kwa hiyo watu wenye silaha wa Moabu wanapiga kelele,

nayo mioyo yao imezimia.

515:5 Isa 16:11; Yer 48:31; 48:3-5; 4:20; Mwa 13:10; Hes 21:29Moyo wangu unamlilia Moabu;

wakimbizi wake wanakimbilia Soari,

hadi Eglath-Shelishiya.

Wanapanda njia ya kwenda Luhithi,

wanakwenda huku wanalia;

barabarani iendayo Horonaimu

wanaombolezea maangamizi yao.

615:6 Isa 19:5-7; Za 37:2; Hos 4:3; Yer 48:34; Isa 16:8; 33:9; 14:17; Yer 14:5Maji ya Nimrimu yamekauka

na majani yamenyauka;

mimea imekauka wala hakuna

kitu chochote kibichi kilichobaki.

715:7 Isa 30:6; Yer 48:36Kwa hiyo mali waliyoipata na kujiwekea akiba

wamezichukua na kuvuka Bonde la Mierebi.

815:8 Hes 21:16Mwangwi wa kilio chao umefika hadi mpakani mwa Moabu,

kilio chao cha huzuni kimefika hadi Eglaimu,

maombolezo yao hadi Beer-Elimu.

915:9 2Fal 17:25; Eze 25:8-11Maji ya Dimoni yamejaa damu,

lakini bado nitaleta pigo jingine juu ya Dimoni:

simba juu ya wakimbizi wa Moabu

na juu ya wale wanaobaki katika nchi.

O Livro

Isaías 15:1-9

Profecia contra Moabe

1Eis a mensagem de Deus sobre Moabe: Numa só noite as tuas cidades de Ar e de Quir de Moabe serão destruídas. 2O teu povo em Dibom vai-se lamentando; vão para os santuários pagãos lamentando-se pelo destino que Nebo e Medeba vão ter; rapam as cabeças de tristeza e cortam as barbas. 3Andam vestidos de saco pelas ruas e de cada casa saem clamores de lamentações. 4Os choros, nas cidades de Hesbom e de Eleale, até de longe se ouvem, até mesmo em Jaaz! Os mais valentes dos combatentes de Moabe gritam de terror.

5O meu coração chora por causa de Moabe! O seu povo foge para Zoar e para Eglate-Selichia. Vão subindo a ladeira até Luite, a chorar, e os seus prantos ouvem-se por todo o caminho de Horonaim. 6Até o ribeiro de Nimrim se tornou num sítio desolado; as suas verdes margens secaram; desapareceu toda a sua vegetação. 7Os que fogem, desesperados, levam apenas o que podem transportar consigo e atravessam o ribeiro dos Salgueiros. 8A terra toda de Moabe está em pranto, duma ponta à outra; as suas lamentações chegam até Eglaim, fazem-se ouvir até Beer-Elim. 9A torrente que passa em Dibom ficará vermelha, por causa do sangue, mas isto não será tudo quanto a Dibom. Por fim, andarão leões atrás dos sobreviventes, daqueles que escaparam e ficaram na terra.