Isaya 15 – NEN & NIV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Isaya 15:1-9

Unabii Dhidi Ya Moabu

115:1 Hes 21:28; 22:3-6; Kum 23:6; Hes 17:12; Yer 51:58; 48:24; 2Fal 3:25Neno kuhusu Moabu:

Ari iliyo Moabu imeangamizwa:

imeharibiwa kwa usiku mmoja!

Kiri iliyo Moabu imeangamizwa,

imeharibiwa kwa usiku mmoja!

215:2 Yer 48:35; Law 21:5; Ay 1:20; Hes 21:20; Isa 16:12; 2Sam 10:4; Law 13:40Diboni anakwea hadi kwenye hekalu lake,

mpaka mahali pake pa juu ili walie,

Moabu anaombolezea Nebo na Medeba.

Kila kichwa kimenyolewa

na kila ndevu limeondolewa.

315:3 Mao 2:11; Mik 1:8; Isa 3:24; Yos 2:8; Yer 48:38; Isa 14:31; Eze 7:18; Yer 47:2Wamevaa nguo za magunia barabarani,

juu ya mapaa na kwenye viwanja

wote wanaomboleza,

wamelala kifudifudi kwa kulia.

415:4 Hes 32:3; 21:23-25; Yos 13:26Heshboni na Eleale wanalia,

sauti zao zinasikika hadi Yahazi.

Kwa hiyo watu wenye silaha wa Moabu wanapiga kelele,

nayo mioyo yao imezimia.

515:5 Isa 16:11; Yer 48:31; 48:3-5; 4:20; Mwa 13:10; Hes 21:29Moyo wangu unamlilia Moabu;

wakimbizi wake wanakimbilia Soari,

hadi Eglath-Shelishiya.

Wanapanda njia ya kwenda Luhithi,

wanakwenda huku wanalia;

barabarani iendayo Horonaimu

wanaombolezea maangamizi yao.

615:6 Isa 19:5-7; Za 37:2; Hos 4:3; Yer 48:34; Isa 16:8; 33:9; 14:17; Yer 14:5Maji ya Nimrimu yamekauka

na majani yamenyauka;

mimea imekauka wala hakuna

kitu chochote kibichi kilichobaki.

715:7 Isa 30:6; Yer 48:36Kwa hiyo mali waliyoipata na kujiwekea akiba

wamezichukua na kuvuka Bonde la Mierebi.

815:8 Hes 21:16Mwangwi wa kilio chao umefika hadi mpakani mwa Moabu,

kilio chao cha huzuni kimefika hadi Eglaimu,

maombolezo yao hadi Beer-Elimu.

915:9 2Fal 17:25; Eze 25:8-11Maji ya Dimoni yamejaa damu,

lakini bado nitaleta pigo jingine juu ya Dimoni:

simba juu ya wakimbizi wa Moabu

na juu ya wale wanaobaki katika nchi.

New International Version

Isaiah 15:1-9

A Prophecy Against Moab

1A prophecy against Moab:

Ar in Moab is ruined,

destroyed in a night!

Kir in Moab is ruined,

destroyed in a night!

2Dibon goes up to its temple,

to its high places to weep;

Moab wails over Nebo and Medeba.

Every head is shaved

and every beard cut off.

3In the streets they wear sackcloth;

on the roofs and in the public squares

they all wail,

prostrate with weeping.

4Heshbon and Elealeh cry out,

their voices are heard all the way to Jahaz.

Therefore the armed men of Moab cry out,

and their hearts are faint.

5My heart cries out over Moab;

her fugitives flee as far as Zoar,

as far as Eglath Shelishiyah.

They go up the hill to Luhith,

weeping as they go;

on the road to Horonaim

they lament their destruction.

6The waters of Nimrim are dried up

and the grass is withered;

the vegetation is gone

and nothing green is left.

7So the wealth they have acquired and stored up

they carry away over the Ravine of the Poplars.

8Their outcry echoes along the border of Moab;

their wailing reaches as far as Eglaim,

their lamentation as far as Beer Elim.

9The waters of Dimon15:9 Dimon, a wordplay on Dibon (see verse 2), sounds like the Hebrew for blood. are full of blood,

but I will bring still more upon Dimon15:9 Dimon, a wordplay on Dibon (see verse 2), sounds like the Hebrew for blood.

a lion upon the fugitives of Moab

and upon those who remain in the land.