Unabii Dhidi Ya Moabu
115:1 Hes 21:28; 22:3-6; Kum 23:6; Hes 17:12; Yer 51:58; 48:24; 2Fal 3:25Neno kuhusu Moabu:
Ari iliyo Moabu imeangamizwa:
imeharibiwa kwa usiku mmoja!
Kiri iliyo Moabu imeangamizwa,
imeharibiwa kwa usiku mmoja!
215:2 Yer 48:35; Law 21:5; Ay 1:20; Hes 21:20; Isa 16:12; 2Sam 10:4; Law 13:40Diboni anakwea hadi kwenye hekalu lake,
mpaka mahali pake pa juu ili walie,
Moabu anaombolezea Nebo na Medeba.
Kila kichwa kimenyolewa
na kila ndevu limeondolewa.
315:3 Mao 2:11; Mik 1:8; Isa 3:24; Yos 2:8; Yer 48:38; Isa 14:31; Eze 7:18; Yer 47:2Wamevaa nguo za magunia barabarani,
juu ya mapaa na kwenye viwanja
wote wanaomboleza,
wamelala kifudifudi kwa kulia.
415:4 Hes 32:3; 21:23-25; Yos 13:26Heshboni na Eleale wanalia,
sauti zao zinasikika hadi Yahazi.
Kwa hiyo watu wenye silaha wa Moabu wanapiga kelele,
nayo mioyo yao imezimia.
515:5 Isa 16:11; Yer 48:31; 48:3-5; 4:20; Mwa 13:10; Hes 21:29Moyo wangu unamlilia Moabu;
wakimbizi wake wanakimbilia Soari,
hadi Eglath-Shelishiya.
Wanapanda njia ya kwenda Luhithi,
wanakwenda huku wanalia;
barabarani iendayo Horonaimu
wanaombolezea maangamizi yao.
615:6 Isa 19:5-7; Za 37:2; Hos 4:3; Yer 48:34; Isa 16:8; 33:9; 14:17; Yer 14:5Maji ya Nimrimu yamekauka
na majani yamenyauka;
mimea imekauka wala hakuna
kitu chochote kibichi kilichobaki.
715:7 Isa 30:6; Yer 48:36Kwa hiyo mali waliyoipata na kujiwekea akiba
wamezichukua na kuvuka Bonde la Mierebi.
815:8 Hes 21:16Mwangwi wa kilio chao umefika hadi mpakani mwa Moabu,
kilio chao cha huzuni kimefika hadi Eglaimu,
maombolezo yao hadi Beer-Elimu.
915:9 2Fal 17:25; Eze 25:8-11Maji ya Dimoni yamejaa damu,
lakini bado nitaleta pigo jingine juu ya Dimoni:
simba juu ya wakimbizi wa Moabu
na juu ya wale wanaobaki katika nchi.
关于摩押的预言
1以下是关于摩押的预言:
摩押的亚珥城必在一夜之间被摧毁,沦为废墟;
摩押的基珥城必在一夜之间被摧毁,沦为废墟。
2底本城的人上到神庙,
到他们的丘坛痛哭。
摩押人都剃光头发,
刮掉胡须,
为尼波和米底巴城哀号。
3他们身披麻衣走在街上,
房顶和广场上都传出号啕大哭的声音。
4希实本人和以利亚利人都哭喊,
声音一直传到雅杂,
因此摩押的战士大声喊叫,
胆战心惊。
5我为摩押感到悲哀。
她的人民逃难到琐珥和伊基拉·施利施亚。
他们上到鲁希斜坡,边走边哭,
在去何罗念的路上为自己的不幸哀哭。
6宁林的河道干涸,
青草枯萎,植被消失,毫无绿色。
7因此,摩押人把自己积存的财物都运过柳树河。
8摩押境内哀声四起,
号啕声传到以基莲,
传到比珥·以琳。
9底门的河里流的都是血,
但我还要降更多灾难给底门:
狮子必吞噬逃出摩押的人和那里的余民。